Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JA LIFUNZU 42

Kamulana na Kweli Konigubi nu Usadikishu Thabiti

Kamulana na Kweli Konigubi nu Usadikishu Thabiti

“Nhakikisa mambu goa; kamulana na gagabi gasapi.”​—1 BAT. 5:21.

NHAMBU 142 Kushikilia Tumaini Letu

MUHTASARI *

1. Ndaba jaki bandu bingi atei kuchanganyikiwa?

 KUNA maelfu ya dini zinazodai kuwa za Kikristo, zinazosema zinamwabudu Mungu kwa njia anayoikubali. Hivyo, haishangazi kwamba watu wengi wamechanganyikiwa! Wanajiuliza hivi, “Je, kuna dini moja tu ya kweli au dini zote zinampendeza Mungu?” Je, tuna usadikisho thabiti katika akili zetu kwamba tunachofundisha ni kweli, na kwamba utaratibu wa ibada unaofuatwa na Mashahidi wa Yehova leo ndio ambao Yehova anaukubali? Je, kweli inawezekana kuwa na usadikisho wa aina hiyo? Acheni tuchunguze uthibitisho uliopo.

2. Kulengana na 1 Wathesalonike 1:5, ndaba jaki ntumi Paulo jukabi nu usadikishu kuhusu kweli?

2 Mtume Paulo alikuwa na usadikisho thabiti kuhusu kweli. (Soma 1 Wathesalonike 1:5.) Usadikisho huo haukutegemea hisia. Paulo alikuwa mwanafunzi mwenye bidii wa Neno la Mungu. Aliamini kwamba, “kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Tim. 3:16) Alijifunza mambo gani? Kwenye Maandiko, Paulo alipata uthibitisho usiopingika kwamba Yesu alikuwa Masihi aliyeahidiwa—uthibitisho ambao viongozi wa dini ya Kiyahudi walichagua kuupuuza. Viongozi hao wanafiki wa kidini walidai kumwakilisha Mungu, lakini walimkana kwa matendo yao. (Tito 1:16) Tofauti nao, Paulo hakuchagua mambo ambayo angekubali kuamini na yale ambayo angekataa kuamini katika Neno la Mungu. Alikuwa tayari kufundisha na kutumia “mashauri yote ya Mungu.”​—Mdo. 20:27.

3. Ili tuba nu usadikishu thabiti, bo, kubi lazima tuba ni majibu gi maswali gitu goa? (Linga kabe lisanduku “ Kasi ni Mawasu Gika Yehova Gabi ‘Gingi Ngani Kwitu Kusimuli.’”)

3 Baadhi ya watu wanahisi kwamba dini ya kweli inapaswa kujibu maswali yao yote, hata maswali ambayo hayajibiwi kihususa katika Biblia. Je, hayo ni matarajio yanayofaa? Fikiria mfano wa Paulo. Aliwatia moyo waamini wenzake ‘wahakikishe mambo yote,’ lakini pia alikiri kwamba kulikuwa na mambo mengi ambayo hakuyaelewa. (1 The. 5:21) Aliandika hivi: “Tuna ujuzi usio kamili,” na akaongezea hivi: “Tunaona kwa njia isiyo ya waziwazi kupitia kioo cha chuma.” (1 Kor. 13:9, 12) Paulo hakuelewa kila kitu; ni hivyo kwetu pia. Lakini, Paulo aliona au kuelewa kweli za msingi kumhusu Yehova. Alijua mambo yaliyotosha kumsadikisha kwamba alikuwa amepata kweli!

4. Tuwesa kuimalisha bo usadikishu gwitu kwamba tujipatiki kweli, na msitusungusa ki kuhusu Akristo ba sakaka?

4 Njia moja tunayoweza kuimarisha usadikisho wetu kwamba tumeipata kweli ni kwa kulinganisha utaratibu wa ibada uliowekwa na Yesu na ule ambao Mashahidi wa Yehova wanafuata leo. Katika makala hii, tutaona kwamba Wakristo wa kweli (1) wanakataa ibada ya sanamu, (2) wanaliheshimu jina la Yehova, (3) wanaipenda kweli, na (4) wanapendana sana.

TUKANA IBADA JA SANAMU

5. Tulibola ki kuhuma kuka Yesu kuhusu indela jejifaa jukunhabudu Mungu, nu tuwesa kutumi bo mambu gajwapundisaje?

5 Akichochewa na upendo wenye kina kwa Mungu, Yesu alimwabudu Yehova peke yake alipokuwa mbinguni na alipokuwa hapa duniani. (Luka 4:8) Aliwafundisha wanafunzi wake wafanye vivyo hivyo. Yesu na wanafunzi wake waaminifu hawakutumia kamwe sanamu katika ibada. Kwa kuwa Mungu ni Roho, hakuna kitu ambacho mwanadamu anaweza kutengeneza kinachoweza hata kukaribia utukufu wa Yehova! (Isa. 46:5) Lakini namna gani kuhusu kutengeneza sanamu za wale wanaoitwa watakatifu na kusali kwao? Katika amri ya pili ya zile Amri Kumi, Yehova alisema hivi: “Usijitengenezee sanamu ya kuchongwa au mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni au kilicho chini duniani . . . Usiviinamie.” (Kut. 20:4, 5) Maneno hayo yako wazi kwa wale wanaotamani kumpendeza Mungu.

6. Mashahidi baka Yehova apwata utalatibu bo gwi ibada leleno?

6 Wanahistoria wamekiri kwamba Wakristo wa mapema walimwabudu Mungu peke yake. Kwa mfano, kitabu History of the Christian church kinasema kwamba Wakristo wa mapema “wangeshtushwa sana” na wazo la kuweka sanamu katika sehemu za ibada. Leo, Mashahidi wa Yehova wanafuata kielelezo kilichowekwa na Wakristo wa karne ya kwanza. Hatusali kwa sanamu za “watakatifu” au malaika; wala hatusali hata kwa Yesu. Na hatufanyii nembo za kitaifa matendo ya ibada. Liwalo na liwe, tumeazimia kutii maneno haya ya Yesu: “Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu.”​—Mt. 4:10.

7. Ibi tofauti bo yeibi wazi kati jaka Mashahidi bika Yehova na dini yenge?

7 Leo, watu wengi ni wafuasi wa viongozi mashuhuri wa kidini. Wanawapenda sana viongozi hao hivi kwamba nyakati nyingine ni kana kwamba wanawaabudu. Watu wengi hujaa kwenye makanisa yao, kununua vitabu vyao, na kuwatolea michango mingi, au mashirika wanayoyaunga mkono. Baadhi yao, wanaamini kila neno ambalo viongozi hao wanasema. Wanasisimka sana kuwaona viongozi hao, kana kwamba wamemwona Yesu mwenyewe! Tofauti nao, waabudu wa kweli wa Yehova hawana makasisi. Ingawa tunawaheshimu wale wanaoongoza, tunakubali fundisho hili lililo wazi la Yesu: “Nanyi nyote ni ndugu.” (Mt. 23:8-10) Hatuabudu watu, iwe ni viongozi wa kidini au viongozi wa kisiasa. Na hatuwaungi mkono katika malengo yao. Hatuungi mkono upande wowote katika ulimwengu huu na tunajitenga nao. Kwa njia hizo, sisi ni tofauti sana na vikundi vingi vinavyodai kuwa vya Kikristo.​—Yoh. 18:36.

TUHESHIMU LIHINA LIKA YEHOVA

Wakristo wa kweli wanajivunia kuwaambia wengine kumhusu Yehova (Tazama fungu la 8 hadi 10) *

8. Tumanya bo kwamba Yehova jupala lihina laki litukuzwa nu kumanyikana kuka kila mundo?

8 Pindi moja, Yesu alisali hivi: “Baba, litukuze jina lako.” Yehova mwenyewe alijibu sala hiyo kwa sauti kubwa kutoka mbinguni akiahidi kwamba angelitukuza jina lake. (Yoh. 12:28) Katika kipindi chote cha huduma yake, Yesu alilitukuza jina la Baba yake. (Yoh. 17:26) Hivyo, ni jambo linalopatana na akili kwamba Wakristo wa kweli wangejivunia kulitumia jina la Mungu na kulifanya lijulikane kwa wengine.

9. Akristo ba karne ja kwanza basibitisha bo kwamba biliheshimua lihina lika Mungu?

9 Katika karne ya kwanza W.K., muda mfupi baada ya kutaniko la Kikristo kuanzishwa, Yehova ‘alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.’ (Mdo. 15:14) Wakristo hao wa karne ya kwanza walijivunia kulitumia jina la Mungu na kulifanya lijulikane kwa wengine. Walilitumia sana jina la Mungu katika huduma na walipoandika vitabu vya Biblia. * Walijithibitisha wenyewe kuwa watu kwa ajili ya jina la Mungu.—Mdo. 2:14, 21.

10. Gubi usibitishu bo kwamba aka Mashahidi bika Yehova ndo bandu kwa ajili ji lihina lika Yehova?

10 Je, Mashahidi wa Yehova ni watu kwa ajili ya jina la Yehova? Fikiria uthibitisho ufuatao. Leo, viongozi wengi wa kidini wamefanya kila wanaloweza ili kuficha ukweli wa kwamba Mungu ana jina la kibinafsi. Wameliondoa katika tafsiri zao za Biblia, na katika baadhi ya visa, wamepiga marufuku matumizi ya jina hilo katika ibada zao. * Je, kuna mtu anayeweza kupinga kwamba Mashahidi wa Yehova pekee ndio wanaolipa jina la Yehova heshima na utukufu kama linavyostahili? Tunalifanya jina la kibinafsi la Mungu lijulikane na kila mtu kuliko kikundi kingine chochote cha kidini! Kwa njia hiyo, tunafanya kila tunaloweza kuishi kulingana na jina letu, Mashahidi wa Yehova. (Isa. 43:10-12) Tumechapisha nakala zaidi ya milioni 240 za Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya, inayotumia jina la Yehova mahali ambapo limeondolewa na watafsiri wengine wa Biblia. Na tunatayarisha machapisho mengine yanayotegemea Biblia ambayo yanatumia jina la Yehova katika lugha zaidi ya 1,000!

TUJIPAI KWELI

11. Akristo bi mapema balangia bo kwamba bijipala kweli?

11 Yesu aliipenda kweli, yaani, kweli kumhusu Mungu na makusudi Yake. Yesu aliishi kupatana na kweli hiyo, na aliifanya ijulikane kwa wengine. (Yoh. 18:37) Wafuasi wa kweli wa Yesu pia waliipenda sana kweli. (Yoh. 4:23, 24) Isitoshe, mtume Petro aliurejelea Ukristo kuwa “ile njia ya kweli.” (2 Pet. 2:2) Kwa sababu waliipenda sana kweli, Wakristo wa mapema walikataa mawazo ya kidini, utamaduni, na maoni ya kibinafsi ambayo hayakupatana na kweli. (Kol. 2:8) Vivyo hivyo leo, Wakristo wa kweli wanajitahidi kuendelea “kutembea katika kweli” kwa kuhakikisha kwamba mambo yote wanayoamini na njia yao ya maisha inategemea kabisa Neno la Yehova.​—3 Yoh. 3, 4.

12. Baalongo bala pamanya kwamba uelewaji gwitu guhitaji malekebishu ahenga ki, na ndaba jaki ahenga hela?

12 Watu wa Mungu leo, hawadai kwamba wana ujuzi kamilifu au kamili kuhusu kweli. Nyakati nyingine, wamefanya makosa yanayohusu mafundisho na miongozo ya tengenezo. Hatupaswi kushangazwa na hilo. Maandiko yanataja wazi kwamba ujuzi sahihi unaongezeka kadiri wakati unavyopita. (Kol. 1:9, 10) Yehova hufunua kweli hatua kwa hatua, na ni lazima tuwe tayari kungoja kwa subira hadi nuru ya kweli ing’ae zaidi. (Met. 4:18) Wale wanaoongoza wanapotambua kwamba uelewaji fulani wa kweli unahitaji kurekebishwa, hawasiti kufanya marekebisho yanayohitajika. Wakati dini nyingi zinazodai kuwa za Kikristo zinafanya mabadiliko ili kuwapendeza waumini wao au kuwa karibu zaidi na ulimwengu, mabadiliko yanayofanywa na tengenezo la Yehova yamekusudiwa kutusaidia kumkaribia zaidi Mungu na kufuata utaratibu wa ibada ulioanzishwa na Yesu. (Yak. 4:4) Mabadiliko tunayofanya hayaongozwi na mielekeo ya kisasa au maoni yanayopendwa na wengi, bali yanaongozwa na uelewaji ulio wazi zaidi wa Maandiko. Sisi tunaipenda kweli!​—1 The. 2:3, 4.

TUPALINI NGAMAA

13. Jibi sifa bo jejibi muhimu ngani jeajilangi Akristo ba kweli, naka Mashahidi bika Yehova ajilangi bo leleno?

13 Kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza lilikuwa na sifa nyingi nzuri, lakini sifa muhimu zaidi iliyolitambulisha ilikuwa upendo. Yesu alisema hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu—mkiwa na upendo miongoni mwenu.” (Yoh. 13:34, 35) Leo, Mashahidi wa Yehova wanafurahia upendo wa kweli na umoja ulimwenguni pote. Tofauti kabisa na mashirika mengine, undugu wetu unatuunganisha kama familia licha ya kutoka katika mataifa, jamii, na utamaduni mbalimbali. Tunajionea uthibitisho wa upendo wa kweli kwenye mikutano na makusanyiko yetu. Uthibitisho huo unaimarisha usadikisho wetu kwamba njia yetu ya ibada ni ile inayokubaliwa na Yehova.

14. Kulengana na Wakolosai 3:12-14, kwi indela bo muhimu tuwesa kulangi kwamba tupalini ngane?

14 Maandiko yanatuhimiza ‘tupendane sana.’ (1 Pet. 4:8) Njia moja tunayoonyesha upendo huo ni kwa kusameheana na kuvumiliana inapohusu udhaifu wetu mbalimbali. Pia, tunatafuta fursa za kuwa wakarimu na kuonyesha ukaribishaji wageni kwa wote kutanikoni, hata wale ambao huenda wametukosea. (Soma Wakolosai 3:12-14.) Kwa kweli, kifungo hicho cha upendo ni sifa kuu inayowatambulisha Wakristo wa kweli.

“IMANI JIMWA”

15. Kwi indela bo jengi tupwata utalatibu gu ibada gobabeka Akristo ba karne ja kwanza?

15 Tunafuata utaratibu wa ibada uliowekwa na kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza kwa njia nyingine pia. Kwa mfano, muundo wa tengenezo letu​—unaotia ndani waangalizi wanaosafiri, wazee wa makutaniko, na watumishi wa huduma—unafuata mpango ulioanzishwa na mitume katika karne ya kwanza. (Flp. 1:1; Tito 1:5) Maoni yetu kuhusu ngono na ndoa, jinsi tunavyoheshimu utakatifu wa damu, na tamaa yetu ya kulilinda kutaniko kutokana na watenda dhambi wasiotubu, yanategemea utaratibu uliowekwa katika karne ya kwanza.​—Mdo. 15:28, 29; 1 Kor. 5:11-13; 6:9, 10; Ebr. 13:4.

16. Tulibola ki kubokana ni malobi gagapatikana mu Waefeso 4:4-6?

16 Yesu alisema kwamba wengi wangedai kuwa wanafunzi wake, lakini si wote wangekuwa wa kweli. (Mt. 7:21-23) Pia, Maandiko yalitabiri kwamba katika siku za mwisho, wengi ‘wangeonekana kama watu wanaomwogopa Mungu.’ (2 Tim. 3:1, 5) Hata hivyo, Biblia inatuambia waziwazi kwamba kuna “imani moja” ambayo Mungu anaikubali.—Soma Waefeso 4:4-6.

17. Akanya lelenu babumpwata Yesu na baabi ni imani jimu ja kweli jela?

17 Ni nani wanaofuata ile imani moja ya kweli leo? Tumechunguza uthibitisho. Tumeona utaratibu wa ibada ambao Yesu alifundisha na uliofuatwa na Wakristo wa karne ya kwanza. Jibu ni moja tu—Mashahidi wa Yehova. Ni pendeleo kubwa sana kuwa miongoni mwa watu wa Yehova na kujua ukweli kumhusu Yehova na makusudi yake! Acheni tuendelee kushikamana na kweli tukiwa na usadikisho thabiti.

NHAMBU 3 Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu

^ ekichweka 5 Katika makala hii, tutazungumzia utaratibu wa ibada ya kweli uliowekwa na Yesu na tutachunguza jinsi wanafunzi wake wa mapema walivyofuata utaratibu huo. Pia, tutathibitisha kwamba leo, Mashahidi wa Yehova wanafuata utaratibu huo wa ibada ya kweli.

^ ekichweka 9 Tazama sanduku “Je, Wakristo wa Karne ya Kwanza Walitumia Jina la Mungu?” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 2010, ukurasa 6.

^ ekichweka 10 Kwa mfano, mwaka 2008 Papa Benedict wa 16 aliamuru kwamba jina la Mungu “lisitumiwe au kutajwa” katika ibada, nyimbo, au sala za Kikatoliki.

^ ekichweka 63 MAELEZO YA PICHA: Tengenezo la Yehova limetoa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika lugha zaidi ya 200 ili watu waweze kusoma Biblia yenye jina la Mungu katika lugha yao wenyewe.