Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 43

Tusiache!

Tusiache!

“Tusiache kufanya mema.”​—GAL. 6:9.

WIMBO 68 Tupande Mbegu ya Ufalme

KIFUPI YA HABARI *

1. Tuko na furaha na pendeleo gani?

 TUKO na furaha sana na pendeleo ya kuwa Mashahidi wa Yehova! Tuko watu wa Yehova na tunaonyesha kama tuko mashahidi wake wakati tunahubiri na kufanya wanafunzi. Tuko wenye furaha wakati tunasaidia wengine wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele” juu wafikie kuwa waamini. (Mdo. 13:48) Tunajisikia sawa vile Yesu mwenye “alikuwa na furaha kubwa kupitia roho takatifu” wakati wanafunzi wake walimuambia matokeo ya muzuri yenye walipata mu mahubiri.​—Lu. 10:1, 17, 21.

2. Namna gani tunaweza kuonyesha kama kazi yetu ya kuhubiri ni ya maana sana?

2 Kazi yetu ya kuhubiri ni ya maana sana. Mutume Paulo alimuambia Timoteo hivi: “Endelea kuwa muangalifu juu yako mwenyewe na kuhusu kufundisha kwako.” Kisha aliongezea hivi: “Kwa kufanya vile utajiokoa wewe mwenyewe na utaokoa pia wale wenye wanakusikiliza.” (1 Ti. 4:16) Kwa hiyo, kazi yetu ya kuhubiri inaokoa uzima. Njo maana tunapaswa kuendelea kuwa waangalifu juu tuko raia wa Ufalme wa Mungu. Kila mara tunapenda kutenda mu njia yenye inamuletea Yehova utukufu na kutenda kulingana na mambo yenye tunahubiri. (Flp. 1:27) Tunaonyesha kama ‘tuko waangalifu kuhusu kufundisha kwetu’ kwa kujitayarisha muzuri mbele ya kuenda ku mahubiri na kwa kumuomba Yehova atusaidie mbele ya kuhubiria wengine.

3. Je, ni kila mutu njo atapendezwa na ujumbe wa Ufalme? Leta mufano.

3 Hata wakati tunafanya yetu yote ili kuhubiria wengine, watu wengi mu eneo yetu pengine hawapendezwe na habari njema ya Ufalme. Fikiria mufano ya Ndugu Georg Lindal, mwenye alihubiri yeye peke mu Islande kuanzia 1929 mupaka 1947. Aliangushia watu vitabu mingi sana lakini hakuna mwenye alifikia kuwa Shahidi wa Yehova. Aliandika hivi: “Watu fulani walionekana sawa vile walipinga ujumbe wa Biblia lakini wengi kati yao hawakupendezwa tu na ile ujumbe.” Wamisionere wenye walipata diplome yao ku masomo ya Gileadi walienda kule ili kusaidia lakini wao pia walihubiri kwa miaka mingi bila kupata mwenye anapendezwa. Ku mwisho, kisha miaka kenda wakaaji fulani wa inchi ya Islande walitoa maisha yao kwa Yehova na kubatizwa. *

4. Tunaweza kujisikia namna gani wakati watu wanakatala ujumbe wetu?

4 Tunajisikiaka mubaya wakati watu wanakatala kujifunza Biblia. Pengine tunaweza kujisikia sawa vile Paulo mwenye alikuwa na “huzuni kubwa na maumivu yenye hayaishe” juu Wayahudi wengi walikatala kama Yesu alikuwa Masiya mwenye aliahidiwa. (Ro. 9:1-3) Pengine uko unajifunza Biblia na mutu fulani, unajikaza kuwa mwalimu muzuri na unasali sana kwa ajili ya ule mwanafunzi lakini hatumikishe mambo yenye iko anajifunza na unapaswa kuacha kujifunza pamoja naye. Ao pengine hauyasaidiaka mutu mupaka afikie kubatizwa. Ile inaonyesha kama ni kosa yako na kama Yehova hapendezwe na utumishi wako? Mu hii habari tutajibia maulizo mbili: (1) Nini itaonyesha kama kazi yetu ya kuhubiri haiko ya bure? (2) Tunapaswa kutazamia nini wakati tunahubiria wengine?

NINI ITAONYESHA KAMA KAZI YETU YA KUHUBIRI HAIKO YA BURE?

5. Pengine ni juu ya nini sikuzote kazi yetu ya kuhubiri haikuwake na matokeo yenye tulitazamia?

5 Biblia inasema hivi kuhusu mutu mwenye anafanya mapenzi ya Mungu: “Kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.” (Zb. 1:3) Lakini, ile haimaanishe kama, kila jambo yenye tunafanya kwa ajili ya Yehova itatimia sawa vile tunapenda. Maisha ya wanadamu ‘inajaa na taabu’ juu ya kutokamilika, ni kusema, kutokamilika kwetu na kwa wengine. (Yob. 14:1) Pia, wale wenye wanatupinga pengine wakati fulani wanaweza kutufanya tuache kuhubiri kama kawaida. (1 Ko. 16:9; 1 Te. 2:18) Sasa, nini njo inafanya Yehova aone kama kazi yetu ya kuhubiri haiko ya bure? Fikiria kanuni fulani za Biblia zenye zitatusaidia kupata jibu ya ile ulizo.

Yehova anasamini bidii yetu, ikuwe tunahubiria watu uso kwa uso, kupitia barua ao kupitia telefone (Ona fungu ya 6)

6. Nini njo inamufurahisha Yehova kuhusu kazi yenye tunamutolea?

6 Yehova anaona bidii yetu na uvumilivu wetu. Tunamufurahisha Yehova wakati tunahubiri kwa bidii juu tunamupenda hata kama watu hawapendi kutusikiliza. Paulo aliandika hivi: “Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu na upendo wenye mulionyesha kwa ajili ya jina lake kwa kutumikia na kuendelea kutumikia watakatifu.” (Ebr. 6:10) Yehova anakumbuka bidii na upendo wetu hata kama bidii yenye tunaonyesha hailete matokeo ya muzuri. Njo maana pengine unaweza kutumikisha mambo yenye Paulo aliambia Wakristo Wakorinto wakati alisema: “Kazi yenu haiko ya bure kuhusiana na Bwana,” hata kama kazi yenye mulifanya kwa bidii hailete matokeo yenye mulitazamia.​—1 Ko. 15:58.

7. Mambo yenye mutume Paulo alisema kuhusu utumishi wake inaweza kutufundisha nini?

7 Mutume Paulo alikuwa misionere muzuri zaidi mwenye alianzisha makutaniko mbalimbali. Lakini wakati watu fulani walianza kumusema mubaya Paulo kwa kusema kama hakukuwa mwalimu muzuri, hakuzungumuzia namna alikuwa tayari ameshasaidia watu wengi wafikie kuwa Wakristo. Kuliko kujitetea Paulo aliandika hivi: “Nimefanya kazi nyingi zaidi.” (2 Ko. 11:23) Sawa vile Paulo, tusisahau kama bidii na uvumilivu njo mambo yenye Yehova anaona kuwa ya maana sana.

8. Tunapaswa kukumbuka nini kuhusu utumishi wetu?

8 Utumishi wetu unamupendeza Yehova. Yesu alituma wanafunzi wake 70 ili wahubiri ujumbe wa Ufalme na kisha wao kumaliza kuhubiri “wakarudia wakiwa na furaha.” Juu ya nini walikuwa na furaha sana? Walisema hivi: “Hata pepo wachafu wanatutii wakati tunatumia jina lako.” Lakini, Yesu alirekebisha mawazo yao kwa kuwaambia hivi: “Musifurahi kwa sababu roho waovu wanawatii, lakini mufurahi kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.” (Lu. 10:17-20) Yesu alijua kama kila mara wanafunzi wake hawangepata ile matokeo ya muzuri mu utumishi wao. Kusema kweli, hatujue ni watu ngapi wenye wanafunzi wa Yesu walizungumuza nao wenye walifikia kuwa Wakristo. Wanafunzi walipaswa kuelewa kama haiko tu mambo yenye walitimiza njo ingewaletea furaha lakini ya maana zaidi ni kujua kama Yehova alipendezwa na bidii yenye walionyesha ili kutimiza ile kazi.

9. Kulingana na Wagalatia 6:7-9, tutapata nini kama tunahubiri kwa uvumilivu?

9 Kama tunahubiri kwa uvumilivu tutapata uzima wa milele. Wakati tunafanya yetu yote ili kuhubiri na kufundisha habari njema, tuko pia ‘tunapanda kwa roho’ kwa kuacha roho takatifu ya Mungu itende mu maisha yetu. Kama ‘hatuache’ ao “hatuchoke,” Yehova anatuhakikishia kama atatupatia uzima wa milele ikuwe tumesaidia mwanafunzi wa Biblia atoe maisha yake kwa Mungu ao hapana.​—Soma Wagalatia 6:7-9.

TUNAPASWA KUTAZAMIA NINI WAKATI TUNAHUBIRIA WENGINE?

10. Juu ya nini watu fulani wanaitika ao kukatala wakati tunawahubiria?

10 Kuitika ao kukatala kweli kunategemea kwanza hali ya moyo ya wasikilizaji wetu. Yesu alifasiria ile kweli katika mufano wake wa mupandaji mwenye alipanda mbegu katika udongo mbalimbali. Lakini mbegu moja tu njo ilitoa matunda. (Lu. 8:5-8) Yesu alisema kama zile udongo mbalimbali zinafananisha watu wenye kukubali “neno la Mungu” mu njia mbalimbali. (Lu. 8:11-15) Sawa vile mupandaji, hatuna uwezo wa kukomalisha kweli mu moyo ya wenye tulihubiria juu ile inategemea hali ya moyo yao. Daraka yetu ni kuendelea kupanda mbegu ya muzuri ya ujumbe wa Ufalme. Kama vile mutume Paulo alisema, “kila mutu atapokea zawabu yake mwenyewe kulingana na kazi yake mwenyewe,” hapana kulingana na matokeo ya kazi yake.​—1 Ko. 3:8.

Hata kama Noa alihubiri kwa uaminifu kwa miaka mingi, hakuna mutu aliingia naye mu safina isipokuwa tu bibi yake, wana wake, na bibi za wana wake. Hata vile, Noa alitii kwa kutimiza kazi yenye Mungu alimupatia! (Ona fungu ya 11)

11. Juu ya nini Yehova alipendezwa na Noa mwenye alikuwa “muhubiri wa haki”? (Ona picha kwenye jalada.)

11 Zamani watumishi wengi wa Yehova walihubiria watu wenye hawakupenda kuwasikiliza. Kwa mufano, Noa alikuwa “muhubiri wa haki,” pengine kwa miaka 40 ao 50 hivi. (2 Pe. 2:5) Bila shaka, Noa alitazamia kama watu wenye angehubiria wangemusikiliza lakini Yehova hakumuambiaka uhakikisho wowote juu ya ile. Wakati alimuambia Noa ajenge safina Mungu alisema hivi: “Unapaswa kuingia ndani ya safina, wewe, wana wako, bibi yako, na bibi za wana wako.” (Mwa. 6:18) Na wakati Yehova alimuambia ukubwa wa safina yenye angepaswa kujenga, pengine Noa alitambua kama watu wengi hawangemusikiliza juu safina haingekuwa ya munene sana ili kuenea watu wengi. (Mwa. 6:15) Kama vile tunajua hakuna hata mutu moja mwenye alimusikiliza Noa. (Mwa. 7:7) Je, Yehova aliwaza kama Noa hakuhubiri kabisa vile inastahili? Hapana! Yehova alipendezwa sana na Noa juu alifanya kwa uaminifu mambo yote yenye Yehova alimuambia afanye.​—Mwa. 6:22.

12. Namna gani nabii Yeremia alipata furaha mu utumishi wake hata kama watu walimupinga na kukatala kumusikiliza?

12 Nabii Yeremia yeye pia alihubiri zaidi ya miaka 40 hata kama watu walimupinga na walikatala kumusikiliza. Alivunjika moyo sana juu ya “kutukanwa na kuchekwa” na wapinzani wake, ile ilimufanya aanze kuwaza kuacha mugao wake. (Yer. 20:8, 9) Lakini Yeremia hakuacha! Nini njo ilimusaidia aachane na mawazo yake ya mubaya na aendelee kuwa na furaha mu utumishi wake? Alikazia uangalifu mambo mbili ya maana. Kwanza, ujumbe wa Mungu wenye aliambia watu ungewaletea “wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini.” (Yer. 29:11) Pili, Yehova alimuchagua juu aambie watu ujumbe wake. (Yer. 15:16) Siye pia tunaambia watu ujumbe wenye kuwa na tumaini na tunabeba jina Yehova. Wakati tunakaza akili yetu juu ya hii mambo mbili ya maana sana tunaweza kuwa na furaha hata kama watu wanakatala ao wanakubali ujumbe wetu.

13. Tunajifunza nini kupitia mufano wa Yesu wenye kuwa mu Marko 4:26-29?

13 Maendeleo ya kiroho inafanyikaka hatua kwa hatua. Yesu alifundisha ile kweli katika mufano wake wa mupandaji mwenye analala kisha kufanya kazi yake. (Soma Marko 4:26-29.) Kisha ule mupandaji kupanda mbegu, zilikomala polepole na ule mupandaji hangeweza kufanya jambo yoyote juu zikomale haraka. Na weye pia, pengine hautaona matokeo ya kufanya wanafunzi kwa wakati fulani juu maendeleo ya kiroho inafanyikaka hatua kwa hatua. Sawa vile tu mupandaji hawezi kufanya mimea ikomale haraka kama vile anapenda ni vile pia na siye hatuwezi kukaza wanafunzi wetu wa Biblia wafanye maendeleo ya kiroho sawa vile tunapenda. Njo maana kama wanafunzi wetu wanakawia kufanya maendeleo hatupaswe kuvunjika moyo wala kuacha. Sawa vile kazi ya kulima, kazi ya kufanya wanafunzi pia inaomba uvumilivu.​—Yak. 5:7, 8.

14. Ni mufano gani unaonyesha kama inaomba wakati mingi mbele watu waanze kutusikiliza?

14 Mu maeneo fulani, inachukua muda murefu sana juu mutu afikie kubatizwa. Ona mufano wa Gladys na Ruby Allen, dada wa tumbo moja wenye mu 1959 walitumwa kama mapainia wa kawaida mu Inchi ya Kanada, katika jimbo ya Québec. * Juu watu walikuwa wanaogopa mambo yenye majirani wao na mapadri wangefanya ao kusema kama wanazungumuza na Mashahidi, watu walikatala kuzungumuza na siye. Gladys anakumbuka hivi: “Tulikuwa tunatumia saa munane kila siku ili kuhubiri nyumba kwa nyumba na tulifanya vile kwa miaka mbili bila hata kupata mutu moja mwenye anakubali ujumbe wetu! Wakati watu walikuwa wanafika ku milango yao na wanatuona, walikuwa tu wanajirudilia yao mu nyumba. Lakini hatukuacha.” Pole kwa pole watu walibadilisha mawazo yao na wamoja walianza kutusikiliza. Sasa kuko makutaniko tatu mu ile muji.​—Isa. 60:22.

15. 1 Wakorinto 3:6, 7 inatufundisha nini kuhusu kazi ya kufanya wanafunzi?

15 Kazi ya kufanya wanafunzi haiko kazi ya mutu moja. Kila mutu mu kutaniko anaweza kusaidia mutu fulani afikie kubatizwa. (Soma 1 Wakorinto 3:6, 7.) Kwa mufano, ndugu moja anaachia mutu fulani mwenye kupendezwa trakte ao gazeti. Ule ndugu anafikia kuona kama programu yake haitamuruhusu kumurudilia ule mutu mwenye kupendezwa, njo maana anaomba muhubiri mwingine amurudilie ule mutu. Ule muhubiri anaanzisha naye funzo ya Biblia. Kisha anaomba ndugu na dada fulani wamusindikize ku ile funzo, na kila mumoja wao anatia moyo ule mwanafunzi mu njia mbalimbali. Kila ndugu ao dada mwenye ule mwanafunzi anakutana naye atasaidia kumwangia mbegu ya kweli maji. Ni mu ile njia njo Yesu alisema kama, mupandaji na muvunaji wanaweza kufurahi pamoja wakati wa mavuno ya kiroho.​—Yoh. 4:35-38.

16. Juu ya nini unaweza kupata furaha mu utumishi wako hata kama hali yako ya afya haiko muzuri ao hauna uwezo mingi?

16 Pengine hauweze tena kuhubiri na kufundisha sawa vile zamani juu ya hali yako ya afya ao juu hauna tena uwezo mingi. Unaweza kuendelea kuwa na furaha juu ya mambo yenye unaweza kufanya katika kazi ya kufanya wanafunzi. Ona mufano wa Daudi, mwenye yeye na watu wake, waliokoa familia zao na vitu vyao kutoka kwa Waamaleki. Watu mia mbili walikuwa wamechoka sana juu ya kupigana vita, kwa hiyo walibakia nyuma ili kuchunga mizigo. Kisha kupata ushindi, Daudi aliomba wagawanye kati yao sawasawa vitu vyenye vilichukuliwa mu vita. (1 Sa. 30:21-25) Hii habari inatufundisha jambo fulani kuhusu kazi yetu ya kufanya wanafunzi. Kila mutu mwenye anafanya yake yote mu kazi ya kufanya wanafunzi anaweza kila mara kuwa na furaha sana wakati mutu anafikia kumujua Yehova na kubatizwa.

17. Tunapaswa kumushukuru Yehova juu ya mambo gani?

17 Tuko wenye shukrani sana kuona vile Yehova anasamini utumishi wenye tunamutolea. Anajua kama hatuwezi kukaza mutu atusikilize ao aanze kumuabudu. Hata vile, anaona bidii yetu na nia yetu ya muzuri na anatubariki. Anatufundisha pia namna ya kupata furaha kuhusu mambo yenye tuko na uwezo wa kufanya katika kazi ya kuhubiri. (Yoh. 14:12) Tunaweza kuwa hakika kama tutamupendeza Yehova kama hatuache!

WIMBO 67 “Hubiri Neno”

^ Tuko wenye furaha wakati watu wanakubali habari njema yenye tunawaletea, na tunaweza kusikia mubaya wakati wanakatala ile habari njema. Pengine uko unajifunza Biblia na mutu mwenye hafanye maendeleo ao pengine hauyasaidiaka mutu mupaka afikie kubatizwa. Ile inaonyesha kabisa kama kazi ya kuhubiri na ya kufanya wanafunzi inakushinda? Mu hii habari, tutaona ni juu ya nini utumishi wetu hauko wa bure na tunaweza kuendelea kuwa na furaha ikuwe watu wanatusikiliza ao hapana.

^ Ona Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2005 uku. 205-211.

^ Ona habari juu ya maisha ya watu, “Siwezi Kubadili Kitu Ng’o!” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Tarehe 1 Mwezi wa 9, 2002.