Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

1921—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja

1921—Kumepita Sasa Miaka Mia Moja

GAZETI Munara wa Mulinzi wa Tarehe 1 Mwezi wa 1, 1921 iliuliza hii ulizo wanafunzi wa Biblia: “Ni kazi gani tunaweza kutazamia hii mwaka?” Kisha ikaleta jibu kwa kutaja Isaya 61:1, 2, yenye iliwakumbusha kazi ya kuhubiri yenye walipewa. Inasema hivi: “Yehova alinitia mafuta ili nitangazie wapole habari njema . . . , kutangaza mwaka wa nia njema ya Yehova na siku ya kisasi ya Mungu wetu.”

WAHUBIRI WENYE UHODARI

Ili kutimiza kazi yao ya kuhubiri, wanafunzi wa Biblia walipaswa kuwa na sifa ya uhodari. Walipaswa pia kuwa na lazima ya kutangazia “habari njema” wapole, lakini pia kutangazia waovu “siku ya kisasi.”

Ndugu J. H. Hoskin, mwenye aliishi Kanada, alitoa ushahidi kwa uhodari ijapokuwa upinzani. Mu mwaka wa 1921, alikutana na pastere moja wa kanisa ya Metodiste. Ndugu Hoskin alianza mazungumuzo kwa kusema hivi: “Tunapaswa kuwa na mazungumuzo ya muzuri kuhusu Biblia, na hata kama hatukubaliane kuhusu mambo fulani, tunaweza kumalizia mazungumuzo yetu kwa amani na kuendelea kuwa marafiki.” Lakini mambo haikufanyika vile. Ndugu Hoskin anakumbuka hivi: “Kisha tu kuzungumuza na ule pastere kwa dakika kidogo, akapiga mulango nguvu sana na nikawaza kama kioo ya ile mulango itapasuka.”

Kisha ule pastere akatomboka kwa kusema hivi: “Juu ya nini hauende kuongea na wenye hawako Wakristo?” Ndugu Hoskin hakumujibia kitu, kisha akaondoka na wakati alikuwa mu njia akawaza hivi, ‘Niliwaza nilikuwa naongea na mwenye haiko Mukristo. Kumbe alikuwa Mukristo!’

Siku ya kufuata ule pastere alikuwa mu kanisa yake. Kisha akasema mambo ya mubaya kuhusu ndugu Hoskin. Ndugu Hoskin anakumbuka hivi: “Aliambia watu kama hakuna mutu muongo sawa miye mwenye alishakafika mu ile muji na kama nilipaswa kuuawa.” Lakini ile haikumufanya aache, aliendelea kuhubiri na kuzungumuza na watu wengi. Anasema hivi: “Nafurahiaka kuhubiri sana. Watu fulani walishangazwa na hata walisema hivi, ‘tunajua kama uko mutu wa Mungu!’ Na waliniuliza kama wanaweza kunisaidia ikiwa nilikosewa jambo fulani.”

IBADA YA FAMILIA NA YA KIPEKEE

Ili kusaidia watu waelewe Biblia muzuri zaidi, kila mara Wanafunzi wa Biblia walitoa maulizo fulani kuhusu Biblia na majibu mu gazeti L’Âge d’Or. * Kulikuwa maulizo fulani ya Biblia kwa ajili ya vijana na yenye wazazi wangezungumuza pamoja na watoto wao. Wazazi wangeuliza watoto wao maulizo na kuwasaidia kupata majibu mu Biblia. Maulizo kama vile, “Biblia iko na vitabu ngapi?” ilifundisha mambo ya musingi ya maana. Ulizo ingine kama vile, “Je, kila Mukristo wa kweli anapaswa kutazamia mateso?” ilitayarisha vijana ili wakuwe wahubiri wenye uhodari.

Kulikuwa pia maulizo fulani ya Biblia na majibu kwa ajili ya wenye tayari walikuwa wanajua mambo mingi kuhusu Biblia. Majibu fulani ingeweza kupatikana mu buku ya kwanza ya kitabu Études des Écritures. Wasomaji wengi walijfunza mambo mingi kupitia ile maulizo. Lakini kisha pale, L’Âge d’Or ya tarehe 1 Mwezi wa 12, 1921, ilitangaza kama ile maulizo haingetolewa tena. Juu ya nini kulikuwa ile mabadiliko yenye haikutazamiwa?

KITABU YA MUPYA!

Kitabu La Harpe de Dieu

Karte yenye kuwa na mugao wa kusoma

Karte yenye kuwa na maulizo

Wale wenye walikuwa wanaongoza waliona kama wanafunzi wapya wa Biblia walipaswa kujifunza kweli za musingi mu njia yenye kupangwa muzuri zaidi. Juu ya kufikia ile kusudi, kitabu La Harpe de Dieu ilitolewa mu Mwezi wa 11, 1921. Wale wenye walikubali ile kitabu waliandikishwa ku masomo fulani. Ile masomo ya kipekee ilisaidia wasomaji “kutambua kusudi ya Mungu ya kupatia wanadamu uzima wa milele.” Ile masomo ilikuwa inafanywa namna gani?

Wakati mutu alikubali ile kitabu, walikuwa wanamupatia karte fulani ya kidogo yenye ilimuambia ni ukurasa gani alipaswa kusoma mu ile kitabu. Juma yenye ilifuata, alipata karte ingine yenye ilikuwa na maulizo mingi kuhusu mambo yenye alikuwa amesoma. Ku mwisho ya ile karte kulikuwa pia mugao wa kusoma kwa ajili ya juma yenye ilifuata.

Kila juma na kwa muda wa majuma 12, mwanafunzi alipata karte ya mupya kutoka kwa kutaniko. Mara mingi, ni wale wenye walikuwa wazee-wazee mu kutaniko ao wale wenye hawangeweza kuenda kuhubiri nyumba kwa nyumba njo walikuwa wanatuma zile karte. Kwa mufano, Anna K. Gardner, wa Millvale, mu Pennsylvanie, Inchi ya Amerika, alisema hivi: “Wakati kitabu La Harpe de Dieu ilitolewa, ilipatia dada yangu mwenye alikuwa na magumu ya kutembea, mwenye aliitwa Thayle, kazi mingi yenye angeweza kufanya, ni kusema, kutuma kila juma karte za maulizo.” Wakati mutu alimaliza ile masomo, mutu fulani wa mu kutaniko alimutembelea ili kumusaidia ajifunze mambo mingi zaidi juu ya Biblia.

Thayle Gardner akiwa mu kiti yake ya vilema

KULIKUWA KUNGALI KAZI

Ku mwisho wa mwaka, Ndugu Joseph Rutherford alitumia makutaniko yote barua. Na alionyesha kama “ushahidi wenye ulitolewa hii mwaka kuhusu Ufalme ulifikia kusaidia watu wengi zaidi kuliko miaka yenye ilipita.” Kisha aliongezea hivi: “Kungali kazi mingi ya kufanya. Muendelee kutia wengine moyo ili wajiunge mu hii utumishi yenye imebarikiwa.” Wanafunzi wa Biblia walifuata kabisa mambo yenye alisema. Mu mwaka wa 1922 wahubiri, walihubiri kwa uhodari kuhusu Ufalme mu njia ya kushangaza sana.

^ L’Âge d’Or ilibadilishwa na kuitwa Consolation mu 1937 na kisha ikaitwa Amuka! mu 1946.