Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JA LIFUNZU 44

Upalani Nkamulani Guka Yehova Gumaanisha ki Kwako?

Upalani Nkamulani Guka Yehova Gumaanisha ki Kwako?

“Upalani nkamulani [guka Yehova] gudumu milele.”​—ZAB. 136:1.

NHAMBU 108 Upendo Mshikamanifu wa Mungu

MUHTASARI *

1. Yehova jutujege mwoju tuhenga kike?

 YEHOVA anapendezwa na upendo mshikamanifu. (Hos. 6:6) Anawatia moyo watumishi wake wafanye vivyo hivyo pia. Kupitia nabii Mika, Mungu anatuhimiza ‘tuupende upendo mshikamanifu.’ (Mika 6:8, maelezo ya chini.) Ni wazi kwamba kabla ya kufanya hivyo tunahitaji kujua upendo mshikamanifu ni nini.

2. Upalani nkamulani ndo kike?

2 Upendo mshikamanifu ni nini? Msemo “upendo mshikamanifu” unapatikana mara 230 hivi katika Biblia TakatifuTafsiri ya Ulimwengu Mpya. Unamaanisha nini? Kulingana na “Kamusi ya Maneno ya Biblia” inayopatikana katika tafsiri hiyo, unamaanisha “upendo unaochochewa na uwajibikaji au ujitoaji, utimilifu, ushikamanifu, na kufungamana kwa dhati. Mara nyingi usemi huu unatumiwa kurejelea upendo wa Mungu kwa wanadamu, lakini pia wanadamu wanaweza kuwa na upendo huo kati yao.” Yehova ni mfano bora zaidi wa upendo mshikamanifu. Katika makala hii, tutachunguza jinsi Yehova anavyowaonyesha wanadamu upendo mshikamanifu. Katika makala inayofuata, tutazungumzia jinsi ambavyo tukiwa watumishi wa Mungu, tunaweza kumwiga Yehova kwa kuonyeshana upendo mshikamanifu.

YEHOVA JUBI NU “UPALANI GWINGI NKAMULANI”

3. Yehova jwayekula utu gwaki kuka Musa jinsi bole?

3 Muda mfupi baada ya Waisraeli kutoka Misri, Yehova alifunua utu wake kwa Musa, kwa kumtangazia Musa jina Lake na sifa zake. Alisema hivi: “Mimi Yehova, Yehova, ni Mungu mwenye rehema na huruma, si mwepesi wa hasira, nina upendo mwingi mshikamanifu na kweli, ninawatendea maelfu kwa upendo mshikamanifu, ninasamehe makosa na uovu na dhambi.” (Kut. 34:6, 7) Kwa kusema maneno hayo yenye kutia moyo kuhusu sifa Zake, Yehova alimfunulia Musa jambo la pekee kuhusu upendo wake mshikamanifu. Ni jambo gani hilo?

4-5. (a) Yehova julifafunua bole? (b) Musitusungusa maswali bole?

4 Yehova hakusema tu kwamba ana upendo mshikamanifu bali alisema ana “upendo mwingi mshikamanifu.” Ufafanuzi huo unapatikana mara 6 zaidi katika Biblia. (Hes. 14:18; Neh. 9:17; Zab. 86:15; 103:8; Yoe. 2:13; Yona 4:2) Katika visa hivyo vyote, ufafanuzi huo unamhusu Yehova peke yake, na si wanadamu. Je, si ni jambo linalopendeza kwamba Yehova mwenyewe anakazia sana sifa yake ya upendo mshikamanifu? Bila shaka, upendo mshikamanifu ni sifa muhimu kwake. * Hivyo, haishangazi kwamba Mfalme Daudi alichochewa kusema hivi: “Ee Yehova, upendo wako mshikamanifu unafika mpaka mbinguni . . . Jinsi upendo wako mshikamanifu ulivyo na thamani sana, Ee Mungu! Katika kivuli cha mabawa yako, wanadamu hukimbilia.” (Zab. 36:5, 7) Kama Daudi, je, tunathamini sana upendo mshikamanifu wa Mungu?

5 Ili kuelewa zaidi upendo mshikamanifu unamaanisha nini, acheni tuchunguze maswali mawili: Yehova anawaonyesha nani upendo mshikamanifu? Na tunaweza kunufaikaje kutokana na matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu?

YEHOVA JWAALANGI UPALANI NKAMULANI AKANYANE?

6. Yehova jwaalangi upalani nkamulani akanyane?

6 Yehova anawaonyesha nani upendo mshikamanifu? Biblia inataja kwamba tunaweza kupenda vitu vingi, kama vile “kilimo,” “divai na mafuta,” “nidhamu,” “ujuzi,” “hekima” na kadhalika. (2 Nya. 26:10; Met. 12:1; 21:17; 29:3) Hata hivyo, upendo mshikamanifu hauonyeshwi kuelekea vitu au dhana fulani; unaonyeshwa kwa watu. Lakini Yehova haonyeshi upendo mshikamanifu kwa mtu yeyote tu. Anawaonyesha wale walio katika uhusiano wa pekee pamoja naye. Mungu wetu ni mshikamanifu kwa rafiki zake. Ana kusudi la pekee kuwaelekea, naye hatakata tamaa juu yao.

Yehova anaiandalia familia nzima ya wanadamu vitu vizuri, hata wale ambao hawamwabudu (Tazama fungu la 7) *

7. Yehova jwalangi bo bandu upalani kuujumla?

7 Yehova amewaonyesha upendo wanadamu kwa ujumla. Yesu alimwambia hivi mwanamume aliyeitwa Nikodemo: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.”​—Yoh. 3:1, 16; Mt. 5:44, 45.

Kutokana na maneno ya Mfalme Daudi na nabii Danieli, Yehova huwaonyesha upendo mshikamanifu wale wanaomjua, wanaomwogopa, wanaompenda, na kushika amri zake (Tazama fungu la 8 na 9)

8-9. (a) Kwa sabu bo Yehova jwaalangi upalani nkamulani atumishi bake? (b) Musitusungusa ki sajeno?

8 Kama ilivyotajwa awali, Yehova anawaonyesha upendo wake mshikamanifu wale tu walio na uhusiano mzuri pamoja naye, yaani, watumishi wake. Hilo linaonekana wazi kupitia maneno ya Mfalme Daudi na nabii Danieli. Kwa mfano, Daudi alisema hivi: “Endelea kuwatendea kwa upendo wako mshikamanifu wale wanaokujua.” “Upendo mshikamanifu wa Yehova ni wa milele na milele kuelekea wale wanaomwogopa.” Na Danieli alisema hivi: “Ee Yehova Mungu wa kweli, [unayewatendea] kwa upendo mshikamanifu wale wanaokupenda na kushika amri zako.” (Zab. 36:10; 103:17; Dan. 9:4) Kulingana na maneno hayo yaliyoongozwa na roho, Yehova huwaonyesha upendo mshikamanifu watumishi wake kwa sababu wanamjua, wanamwogopa, wanampenda, na kushika amri zake. Yehova anawaonyesha upendo mshikamanifu watu wake tu, waabudu wake wa kweli.

9 Kabla hatujaanza kumtumikia Yehova, tulionyeshwa upendo ambao Mungu huwaonyesha wanadamu kwa ujumla. (Zab. 104:14) Hata hivyo, tukiwa waabudu wake tunanufaika pia kutokana na upendo wake mshikamanifu. Isitoshe, Yehova anawahakikishia hivi watumishi wake: “Upendo wangu mshikamanifu hautaondolewa kwako.” (Isa. 54:10) Kwa kweli, kama Daudi alivyojionea, “Yehova atamtendea mshikamanifu wake kwa njia ya pekee.” (Zab. 4:3) Tunapaswa kuitikiaje Yehova anapotutunza kwa njia hiyo ya pekee? Mtunga zaburi alisema hivi: “Yeyote aliye na hekima atayachunguza mambo hayo naye atatafakari kwa makini matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu.” (Zab. 107:43) Tukiwa na ushauri huo ulioongozwa na roho akilini mwetu, acheni tuchunguze njia tatu ambazo watumishi wa Yehova wananufaika kutokana na matendo yake ya upendo mshikamanifu.

TUWESA KUNUFAIKA BO KUBOKANA NA MATENDU GIKA YEHOVA GUUPALANI NKAMULANE?

Yehova huwapatia baraka nyingine zaidi wale wanaomwabudu (Tazama fungu la 10 hadi 16) *

10. Kumanya kwamba upalani nkamulani guka Mungu gudumu mileli kutujangati bole? (Zaburi 31:7)

10 Upendo mshikamanifu wa Mungu unadumu milele. Jambo hilo la muhimu kuhusu upendo mshikamanifu linatajwa mara 26 katika Zaburi ya 136. Katika mstari wa kwanza tunasoma hivi: “Mshukuruni Yehova, kwa maana ni mwema; upendo wake mshikamanifu unadumu milele.” (Zab. 136:1) Katika mstari wa 2 hadi wa 26, tunaona maneno “kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele” yakijirudia. Tunaposoma sehemu zinazobaki za zaburi hiyo, hatuna budi kuvutiwa na njia ambazo Yehova anaonyesha upendo wake mshikamanifu bila kuacha. Maneno “kwa maana upendo wake mshikamanifu unadumu milele” yanatuhakikishia kwamba upendo wa Mungu kwa watu wake haubadiliki-badiliki. Inatia moyo sana kujua kwamba Yehova hakati tamaa haraka inapohusu watumishi wake! Badala yake, yeye hufungamana na wale wanaomtumikia na kushikamana nao, hasa nyakati za taabu. Jinsi tunavyonufaika: Kujua kwamba Yehova anashikamana nasi kunatupatia shangwe na nguvu tunazohitaji ili kukabiliana na taabu zetu na kuendelea kutembea katika njia ya uzima.​—Soma Zaburi 31:7.

11. Kulengana na Zaburi 86:5, kibi ki sesunchoche Yehova kuba jojusamehe?

11 Upendo mshikamanifu wa Mungu unamchochea awe mwenye kusamehe. Yehova anapomwona mtenda dhambi aliyetubu na kuikataa njia yake ya dhambi, upendo mshikamanifu unamchochea kuwa mwenye kusamehe. Mtunga zaburi Daudi alisema hivi kumhusu Yehova: “Hajatutendea kulingana na dhambi zetu, wala hajatupa adhabu tuliyostahili kulingana na makosa yetu.” (Zab. 103:8-11) Kutokana na mambo yenye kuumiza aliyopitia, Daudi alielewa kibinafsi mtu anavyoweza kulemewa na mzigo wa dhamiri yenye hatia. Lakini pia, alijifunza kwamba Yehova yuko “tayari kusamehe.” Ni nini kinachomchochea Yehova kuwa mwenye kusamehe? Jibu linapatikana kwenye Zaburi 86:5. (Soma.) Naam, kama Daudi alivyosema kwenye sala, Yehova husamehe kwa sababu ana upendo mwingi mshikamanifu kwa wale wote wanaomwitia.

12-13. Kibi ki sesatujangatya anatulemiwi na hatia kwa sabu ja zambi ya wakati gogupetike?

12 Tunapotenda dhambi, ni jambo linalofaa, na hata zuri kiafya, kujutia kosa letu. Kufanya hivyo kunaweza kutochochea tutubu na tuchukue hatua ya kurekebisha makosa yetu. Hata hivyo, baadhi ya watumishi wa Mungu wamelemewa na hatia kwa sababu ya makosa ya wakati uliopita. Moyo wao unaowahukumu unawasadikisha kwamba Yehova hataweza kuwasemehe kamwe—haidhuru wametubu kadiri gani. Ikiwa unakabiliana na hisia hizo, kujifunza kuhusu utayari wa Mungu wa kuwaonyesha upendo mshikamanifu watumishi wake kutakusaidia.

13 Jinsi tunavyonufaika: Licha ya kutokamilika kwetu, tunaweza kumtumikia Yehova kwa shangwe tukiwa na dhamiri safi. Hilo linawezekana kwa sababu “damu ya Yesu Mwana wake hutusafisha kutoka katika dhambi yote.” (1 Yoh. 1:7) Unapovunjika moyo kwa sababu ya udhaifu fulani, kumbuka kwamba Yehova yuko tayari, naam, anatamani kumsamehe mtenda dhambi anayetubu. Ona uhusiano ambao Daudi alionyesha kati ya upendo mshikamanifu na msamaha wa Yehova. Aliandika hivi: “Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia, ndivyo upendo wake mshikamanifu ulivyo mkubwa kuelekea wale wanaomwogopa. Kama mashariki ilivyo mbali sana na magharibi, ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali sana na sisi.” (Zab. 103:11, 12) Kwa kweli, Yehova yuko tayari ‘kusamehe kwa njia kubwa.’​—Isa. 55:7.

14. Daudi jwafafunua bo indela ambaju upalani nkamulani guka Mungu gutulenda?

14 Upendo mshikamanifu wa Mungu hutupatia ulinzi wa kiroho. Katika sala yake kwa Yehova, Daudi alisema hivi: “Wewe ni mahali pangu pa kujificha; utanilinda nisipatwe na taabu. Utanizunguka kwa kelele za shangwe za ukombozi. . . . Mtu anayemtumaini Yehova amezungukwa na upendo Wake mshikamanifu.” (Zab. 32:7, 10) Kama tu kuta zilizozunguka jiji la kale zilivyowalinda watu wake, ndivyo matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu yanavyotuzunguka kwa kutupatia ulinzi wa kiroho kutokana na hatari zinazoweza kujaribu utimilifu wetu. Zaidi ya hayo, upendo mshikamanifu wa Yehova unamchochea atuvute kwake.—Yer. 31:3.

15. Gubi uhusianu bo kati juupalani nkamulani guka Yehova nu ulinzi gogupatikana mulikimbiliu na ngome?

15 Daudi alitumia lugha nyingine ya picha kufafanua ulinzi ambao watu wa Mungu wanapata. Aliandika hivi: “Mungu ni kimbilio langu salama, Mungu unayenitendea kwa upendo mshikamanifu.” Daudi alisema hivi pia kumhusu Yehova: “Yeye ni upendo wangu mshikamanifu na ngome yangu, kimbilio langu salama na mwokozi wangu, ngao yangu na Yule ambaye nimejificha ndani yake.” (Zab. 59:17; 144:2) Kwa nini Daudi alilinganisha upendo mshikamanifu wa Yehova na kimbilio na ngome? Haidhuru tunaishi wapi duniani, maadamu sisi ni watumishi wake, Yehova atatupatia ulinzi wote tunaohitaji ili kulinda uhusiano wetu wenye thamani pamoja naye. Uhakikisho kama huo, unapatikana katika Zaburi 91. Mwandikaji wa zaburi hiyo alisema hivi: “Nitamwambia Yehova: ‘Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu.’” (Zab. 91:1-3, 9, 14) Musa alitumia lugha hiyo ya picha kuhusu ulinzi wa kimbilio. (Zab. 90:1, maelezo ya chini.) Zaidi ya hayo, karibu na mwisho wa maisha yake, Musa alikazia ulinganifu mwingine wenye kutia moyo. Aliandika hivi: “Mungu ni kimbilio tangu nyakati za kale, mikono yake ya milele iko chini yako.” (Kum. 33:27) Maneno “mikono yake ya milele iko chini yako” yanatuambia nini kumhusu Yehova?

16. Tubalikiwi katika indela bo ibele? (Zaburi 136:23)

16 Yehova anapokuwa Kimbilio letu, tunahisi tukiwa salama. Hata hivyo, kuna siku ambazo huenda tukahisi tumevunjika moyo, tupo chini na tunashindwa kunyanyuka. Katika siku hizo, Yehova atafanya nini kwa ajili yetu? (Soma Zaburi 136:23.) Ataiweka mikono yake chini yetu akitunyanyua kwa wororo na kutusaidia kusimama tena kwa miguu yetu. (Zab. 28:9; 94:18) Jinsi tunavyonufaika: Kujua kwamba sikuzote tunaweza kuutumaini utegemezo wa Mungu kunatusaidia kukumbuka kwamba tumebarikiwa kwa njia mbili. Kwanza, tuna mahali salama pa kimbilio haidhuru tunaishi wapi. Pili, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo anatujali sana.

KWA NDABA JAKI UPALANI NKAMULANI GUKA MUNGU GUTUPEKE UHAKIKA KWAMBA JWATUTEGIMIZAJE?

17. Kwa sabu juupalani nkamulani guka Yehova, tuwesa kuba nuuhakika bole? (Zaburi 33:18-22)

17 Kama tulivyozungumzia, tunapokabiliana na majaribu, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atatenda kwa niaba yetu kwa kutupatia utegemezo tunaohitaji ili tudumishe utimilifu wetu. (2 Kor. 4:7-9) Nabii Yeremia alisema hivi: “Hatujaangamia kwa sababu ya upendo mshikamanifu wa Yehova, kwa maana rehema zake hazikomi kamwe.” (Omb. 3:22) Tuna uhakika kwamba bila shaka, Yehova ataendelea kutuonyesha upendo wake mshikamanifu kwa sababu kama mtunga zaburi anavyotuhakikishia, “jicho la Yehova linawalinda wale wanaomwogopa, wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu.”​—Soma Zaburi 33:18-22.

18-19. (a) Tupai kukomboka kike? (b) Twilongalya ki mumakala jejipwata?

18 Tungependa kukumbuka nini? Kabla ya kuanza kumtumikia Yehova, tulipokea upendo ambao Mungu huwaonyesha wanadamu kwa ujumla. Hata hivyo, tukiwa waabudu wake, tunanufaika pia kutokana na upendo wake mshikamanifu. Akichochewa na upendo huo, Yehova anatukumbatia kwa mikono yake yenye kutulinda. Sikuzote Yehova atatuweka karibu naye, na atatimiza kusudi lake kutuhusu. Anataka tufanikiwe! (Zab. 46:1, 2, 7) Hivyo, haidhuru tutakabili jaribu gani, Yehova atatupatia nguvu tunazohitaji ili kudumisha utimilifu wetu.

19 Tumeona jinsi Yehova anavyowaonyesha upendo mshikamanifu watumishi wake. Anatarajia sisi pia tuonyeshane vivyo hivyo upendo mshikamanifu. Tunaweza kufanyaje hivyo? Makala inayofuata itazungumzia jambo hilo muhimu.

NHAMBU 136 “Malipo Kamili” Kutoka kwa Yehova

[Maelezo ya Chini]

^ ekichweka 5 Upendo mshikamanifu ni nini? Yehova anawaonyesha nani upendo mshikamanifu, nao hunufaikaje na upendo huo mshikamanifu? Majibu ya maswali hayo yatajibiwa katika makala ya kwanza kati ya makala mbili zinazozungumzia sifa hii ya pekee.

^ ekichweka 4 Wazo la kwamba upendo mshikamanifu wa Mungu ni mwingi linatajwa pia katika mistari mingine ya Biblia​—Tazama Nehemia 13:22; Zaburi 69:13; 106:7; na Maombolezo 3:32.

^ ekichweka 54 MAELEZO YA PICHA: Yehova anawaonyesha upendo wanadamu kwa ujumla, kutia ndani watumishi wake. Picha ndogo-ndogo zilizo juu ya kikundi cha watu zinaonyesha baadhi ya njia ambazo Mungu anatuonyesha upendo wake. Njia kubwa zaidi ni fursa ya kunufaika kutokana na mpango wa fidia.

^ ekichweka 62 MAELEZO YA PICHA: Wale wanaokuwa watumishi wa Yehova na kuweka imani katika mpango wa fidia wanatendewa na Yehova kwa njia ya pekee. Zaidi ya kupokea upendo ambao Mungu anawaonyesha wanadamu kwa ujumla, watumishi wa Yehova wanapokea upendo mshikamanifu ambao Yehova anawaonyesha watumishi wake tu. Baadhi ya njia anazofanya hivyo zinaonyeshwa katika picha ndogo-ndogo.