Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 48

“No Mwanka Bwejage Baatheru”

“No Mwanka Bwejage Baatheru”

“Karageni buri baatheru mikarirene yenu yonthe.”​—1 PET. 1:15.

RWĨMBO 34 Kutembea kwa Utimilifu

MUHTASARI *

1. Mũtũmwa Petero aaere ũtaaro bũrĩkũ Akristũ barĩa betĩkĩtie ũmwe nawe, na nĩkĩ no bwoneke bũrĩ ũntũ bũbũũmũ kũthingata ũtaaro bwawe?

 IWE tuna tumaini la kuishi mbinguni au duniani, tunaweza kunufaika kwa kuchunguza shauri ambalo mtume Petro aliwapatia Wakristo watiwa-mafuta katika karne ya kwanza. Petro aliandika hivi: “Iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote kama Yule Mtakatifu aliyewaita ninyi, kwa maana imeandikwa: ‘Lazima muwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.’” (1 Pet. 1:15, 16) Kutokana na maneno hayo, tunajifunza kwamba tunaweza kumwiga Yehova ambaye ni mfano bora zaidi wa utakatifu. Tunaweza, na ni lazima tuwe watakatifu katika mwenendo wetu. Huenda hilo likaonekana haliwezekani kwa sababu sisi si wakamilifu. Hata Petro mwenyewe alifanya makosa kadhaa; lakini mfano wake unaonyesha kwamba tunaweza ‘kuwa watakatifu.’

2. Nĩ biũria birĩkũ tũgacũnkũũna kĩthoomone gĩkĩ?

2 Katika makala hii, tutachunguza maswali yafuatayo: Utakatifu ni nini? Biblia inatufundisha nini kuhusu utakatifu wa Yehova? Tunaweza kuwa watakatifu katika mwenendo wetu jinsi gani? Na kuna uhusiano gani kati ya kuwa watakatifu na uhusiano wetu pamoja na Yehova?

ŨTHERU NĨMBI?

3. WAntũ babaingĩ barĩ na mwonere jũrĩkũ jwegie ũtheru, ĩndĩ nĩkũ tũũmba kwona nteto cia mma?

3 Watu wengi wanafikiri kwamba mtu mtakatifu ni mtu ambaye hatabasamu, anavaa mavazi ya kidini, na sikuzote hapendi ucheshi. Lakini hilo si sahihi. Yehova, ambaye ni mtakatifu, anafafanuliwa kuwa “Mungu mwenye furaha.” (1 Tim. 1:11) Wale wanaomwabudu wanaitwa “wenye furaha.” (Zab. 144:15) Yesu aliwashutumu wale waliovaa mavazi yaliyowatofautisha na wengine na kuonyesha uadilifu wao mbele ya watu. (Mt. 6:1; Marko 12:38) Tukiwa Wakristo, maoni yetu kuhusu utakatifu yanategemea mambo tunayojifunza katika Biblia. Tunasadiki kwamba Mungu wetu mtakatifu na mwenye upendo hawezi kamwe kutupatia amri ambayo hatuwezi kuitii. Hivyo, Yehova anapotuambia: “Lazima muwe watakatifu,” tuna hakika kwamba jambo hilo linawezekana. Bila shaka, ili tuwe watakatifu katika mwenendo wetu, tunapaswa kuelewa kwanza maana ya utakatifu.

4. Biugo “utheru” na “umutheru” nĩ kuuga atĩa?

4 Utakatifu ni nini? Katika Biblia maneno “takatifu” na “utakatifu” kimsingi yanarejelea usafi wa kimaadili na kidini. Maneno hayo yanaweza pia kuleta wazo la kuwekwa kando kwa ajili ya utumishi wa Mungu. Kwa maneno mengine, tutaonwa kuwa watakatifu ikiwa sisi ni safi kimaadili, tunamwabudu Yehova kwa njia anayoikubali, na ikiwa tuna uhusiano wa kibinafsi pamoja naye. Wazo tu la kwamba tunaweza kuwa na uhusiano wa kibinafsi pamoja na Mungu wetu mtakatifu, linatustaajabisha hasa kwa sababu ya yale ambayo Biblia inatufundisha kuhusu utakatifu wa Yehova.

“MUTHERU, MUTHERU, MUTHERU NI MWATHANI [JEHOVA, NWT]”

5. Nĩmbi tũũmba kwiritana bwegie Jehova kuumania na araĩka etĩkua?

5 Yehova ni safi katika kila njia. Tunajifunza jambo hilo kutokana na ufafanuzi uliotolewa kumhusu na maserafi, ambao ni malaika wanaotumikia karibu na kiti chake cha ufalme. Baadhi yao walitangaza hivi: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova wa majeshi.” (Isa. 6:3) Bila shaka, ili wawe na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu wao mtakatifu, ni lazima pia malaika wawe watakatifu, na kwa kweli ni watakatifu. Isitoshe, ndiyo sababu kuwepo tu kwa malaika wa Yehova mahali fulani duniani, kunaweza kupafanya pawe patakatifu. Hivyo ndivyo ilivyotokea Musa alipokuwa kwenye kichaka cha miiba kilichokuwa kikiwaka moto.​—Kut. 3:2-5; Yos. 5:15.

Maneno “Utakatifu ni wa Yehova” yaliandikwa katika bamba la dhahabu lililokuwa kwenye kilemba cha kuhani mkuu. (Tazama fungu la 6 na 7)

6-7. (a) Kũringana na Kuuma 15:1, 11, nĩatĩa Musa ainyĩrĩrie ũtheru bwa Mũrungu? (b) Nĩmbi biarikanagia Aisiraeli bonthe ũtheru bwa Mũrungu? (Tega mbica karatacine ka mbere.

6 Baada ya Musa kuwaongoza Waisraeli kuvuka Bahari Nyekundu, aliwasisitizia kwamba Mungu wao Yehova, ni mtakatifu. (Soma Kutoka 15:1, 11.) Mwenendo wa waabudu wa miungu ya Misri haukuwa mtakatifu hata kidogo. Ilikuwa hivyo pia kwa waabudu wa miungu ya Wakanaani. Ibada yao ilitia ndani kuwatoa dhabihu watoto na matendo yenye kuchukiza ya ngono. (Law. 18:3, 4, 21-24; Kum. 18:9, 10) Tofauti na hilo, Yehova hangewataka kamwe waabudu wake wafanye jambo lolote ovu. Yeye ni mtakatifu kabisa. Hilo lilionyeshwa wazi kupitia maandishi yaliyokuwa kwenye bamba la dhahabu katika kilemba cha kuhani mkuu. Bamba hilo lilikuwa na maneno haya: “Utakatifu ni wa Yehova.”​—Kut. 28:36-38.

7 Ujumbe uliokuwa kwenye bamba hilo ungemwonyesha wazi kila mtu kwamba kwa kweli Yehova ni mtakatifu. Hata hivyo, namna gani kuhusu Mwisraeli ambaye hangeweza kuliona bamba hilo kwa sababu hakuweza kumkaribia kuhani mkuu? Je, hangepata ujumbe huo muhimu? La! Kila Mwisraeli alisikia ujumbe huo kwa kuwa Sheria ilisomwa mbele ya wanaume, wanawake, na watoto. (Kum. 31:9-12) Ikiwa ungekuwa hapo, ungesikia maneno haya: “Mimi ni Yehova Mungu wenu . . . nanyi ni lazima muwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu.” “Ni lazima muwe watakatifu mbele zangu, kwa sababu mimi, Yehova, ni mtakatifu.”​—Law. 11:44, 45; 20:7, 26.

8. Nĩmbi tũkwiritana kuumania na Mantu ja Alawi 19:2 na M1 Petero 1:14-​16?

8 Acheni tukazie maneno yanayopatikana kwenye Mambo ya Walawi 19:2, ambayo yalisomwa mbele ya Waisraeli wote. Yehova alimwambia hivi Musa: “Waambie hivi Waisraeli wote: ‘Mnapaswa kuwa watakatifu, kwa sababu mimi, Yehova Mungu wenu, ni mtakatifu.’ ” Huenda Petro alikuwa akinukuu maneno hayo alipowahimiza Wakristo ‘wawe watakatifu.’ (Soma 1 Petro 1:14-16.) Bila shaka, hatupo chini ya Sheria ya Musa. Hata hivyo, mambo ambayo Petro aliandika yanaunga mkono masomo tunayojifunza katika kitabu cha Mambo ya Walawi 19:2, kwamba Yehova ni mtakatifu na wale wanaompenda wanapaswa kujitahidi kuwa watakatifu. Hilo ni kweli, iwe tuna tumaini la kuishi mbinguni au katika dunia paradiso.​—1 Pet. 1:4; 2 Pet. 3:13.

“KARAGENI BURI BAATHERU. . .MIKARIRENE YENU YONTHE”

9. Nĩatĩa tũkagunĩka twacũnkũũna iuku rĩa Mantu ja Alawi 19?

9 Kwa sababu tunataka kumfurahisha Mungu wetu mtakatifu, tunatamani kujifunza jinsi tunavyoweza kuwa watakatifu. Yehova ametuandalia ushauri hususa wa jinsi tunavyoweza kufanya hivyo. Mfano mzuri wa ushauri huo unapatikana kwenye Mambo ya Walawi sura ya 19. Msomi wa Kiebrania, Marcus Kalisch, aliandika hivi: “Sura hii ya pekee huenda ndiyo yenye habari nyingi zaidi kuhusu hali mbalimbali, na kwa njia fulani ndiyo sura muhimu zaidi katika kitabu cha Mambo ya Walawi au katika vitabu vitano vya kwanza vya Biblia.” Acheni tuzungumzie baadhi ya mistari katika sura hii iliyo na masomo muhimu kuhusu hali mbalimbali katika maisha yetu ya kila siku. Tunapofanya hivyo, kumbuka kwamba masomo hayo yanafuata maneno haya ya utangulizi: “Mnapaswa kuwa watakatifu.”

Sheria kuhusu wazazi inayopatikana kwenye Mambo ya Walawi 19:3, inapaswa kuwachochea Wakristo kufikiria jambo gani? (Tazama fungu la 10 hadi 12) *

10-11. Ĩandĩko rĩa Mantu ja Alawi 19:3, rĩriuga tũrĩbatara kũthithia atĩa na nĩatĩa tũbuĩrĩte kwona ũtongeeria bũu?

10 Baada ya kusema kwamba Waisraeli walipaswa kuwa watakatifu, Yehova aliongeza hivi: “Kila mmoja wenu anapaswa kumheshimu mama yake na baba yake . . . Mimi ni Yehova Mungu wenu.”​—Law. 19:2, 3.

11 Ni wazi kwamba tunapaswa kuchukua kwa uzito mwongozo wa Mungu wa kuwaheshimu wazazi wetu. Kumbuka jambo ambalo Yesu alisema, mwanamume fulani alipomuuliza hivi: “Ninapaswa kufanya mambo gani mema ili nipate uzima wa milele?” Jibu la Yesu kwa mwanamume huyo lilitia ndani agizo la kumheshimu baba na mama yake. (Mt. 19:16-19) Yesu hata aliwashutumu Mafarisayo na waandishi kwa kutumia hila ili kuepuka jukumu la kuwaheshimu wazazi. Hivyo ‘walilibatilisha neno la Mungu.’ (Mt. 15:3-6) “Neno la Mungu” lilitia ndani amri ya tano kati ya zile Amri Kumi na pia jambo tunalosoma kwenye Mambo ya Walawi 19:3. (Kut. 20:12) Kwa mara nyingine tena, kumbuka kwamba mwongozo unaopatikana kwenye Mambo ya Walawi 19:3—wa kuwaheshimu mama na baba​—unatolewa baada tu ya maneno: “Mnapaswa kuwa watakatifu, kwa sababu mimi, Yehova Mungu wenu, ni mtakatifu.”

12. Kupatana na shauri linalopatikana katika andiko la Mambo ya Walawi 19:3, tunapaswa kujiuliza swali gani?

12 Kupatana na shauri la Yehova la kuwaheshimu wazazi wetu, tunapaswa kujiuliza, ‘Je, ninawaheshimu wazazi wangu?’ Ikiwa unahisi kwamba hukuwa unafanya hivyo kikamili wakati uliopita, unaweza kuamua kurekebisha hali hiyo sasa. Huwezi kubadili mambo ya wakati uliopita, lakini unaweza kuazimia kuanzia sasa kufanya mengi zaidi kwa ajili ya wazazi wako. Labda unaweza kufanya mipango ili utumie muda zaidi pamoja nao. Je, tunaweza kuwasaidia zaidi kimwili, kiroho, au kihisia? Tukifanya hivyo tutakuwa tukitii andiko la Mambo ya Walawi 19:3.

13. (a) Kũgwatanĩra na ũtaaro bũrĩa bũkwonora kĩrĩ ĩandĩko rĩa Mantu ja Alawi 19:3, nĩ kĩũria kĩrĩkũ tũkũbatara gũciũria?

13 Andiko la Mambo ya Walawi 19:3 linatufundisha jambo lingine kuhusu kuwa watakatifu. Linataja kuhusu kushika Sabato. Wakristo hawako chini ya Sheria, hivyo hatuhitaji kushika Sabato ya kila juma. Hata hivyo, tunaweza kujifunza mambo mengi kutokana na jinsi Waisraeli walivyoshika Sabato na jinsi walivyonufaika kwa kufanya hivyo. Sabato ilikuwa siku ya kupumzika kutokana na kazi na kukazia uangalifu mambo ya kiroho. * Ndiyo sababu siku ya Sabato, Yesu alikuwa akienda kwenye sinagogi katika mji wake wa nyumbani na kusoma Neno la Mungu. (Kut. 31:12-15; soma Luka 4:16-18.) Amri ya Mungu ya “kushika sabato [zake]” kwenye Mambo ya Walawi 19:3, inapaswa kutuchochea kutenga wakati kutoka kwenye shughuli zetu za kila siku ili tukazie fikira zaidi mambo ya kiroho. Je, unahisi kwamba unahitaji kufanya marekebisho fulani kuhusiana na jambo hilo? Ikiwa utatenga kwa ukawaida muda wa kukazia mambo ya kiroho, utasitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Yehova, ambao ni muhimu ili kuwa watakatifu.

RIKIA NGWATANĨRO YAAKU AMWE NA JEHOVA

14. Kĩrĩ ĩandĩko rĩa Mantu ja Alawi 19 nĩ ũmma bũrĩkũ bwa bata bũkwinyĩ ĩrua kaĩrĩ na kaĩrĩ?

14 Andiko la Mambo ya Walawi sura ya 19 linataja tena na tena kweli muhimu ambayo inaweza kutusaidia tuendelee kuwa watakatifu. Mstari wa 4 unamalizia kwa maneno haya: “Mimi ni Yehova Mungu wenu.” Maneno hayo au yanayofanana na hayo yanapatikana mara 16 katika sura hiyo. Hilo linatukumbusha amri ya kwanza: “Mimi ni Yehova Mungu wako . . . Usiwe na miungu mingine yoyote ila mimi.” (Kut. 20:2, 3) Kila Mkristo anayetaka kuwa mtakatifu anapaswa kuhakikisha kwamba uhusiano wake pamoja na Mungu ndilo jambo muhimu kuliko kitu au mtu yeyote. Na kwa kuwa tunaitwa Mashahidi wa Yehova, tumeazimia kuepuka matendo yoyote yanayoweza kulichafua au kuliletea suto jina lake takatifu.​—Law. 19:12; Isa. 57:15.

15. Mĩstaarĩ ya ĩandĩko rĩa Mantu ja Alawi 19 yegie igogwana, ĩbuĩrĩte gũtuurutĩ ĩra kũthithia atĩa?

15 Waisraeli walionyesha kwamba wanamkubali Yehova kuwa Mungu wao kwa kutii sheria zake. Andiko la Mambo ya Walawi 18:4 linasema: “Mnapaswa kutekeleza sheria zangu, nanyi mnapaswa kutii amri zangu na kuzifuata. Mimi ni Yehova Mungu wenu.” Sura ya 19 ina baadhi ya “amri” ambazo Waisraeli walipewa. Kwa mfano, mistari ya 5-8, 21, 22 inataja dhabihu za wanyama. Dhabihu hizo zilipaswa kutolewa kwa njia ambayo ‘haingechafua kitu kitakatifu cha Yehova.’ Kusoma mistari hiyo kunapaswa kutuchochea kumfurahisha Yehova na kumtolea dhabihu za sifa zinazokubalika, kama andiko la Waebrania 13:15 linavyotuhimiza tufanye.

16. Nĩmbi biũmba gũtũriikania mwanya jũrĩa jũrĩo gatĩgatĩ ka barĩa batumĩkagĩra Mũrungu na barĩa batĩmũtumĩkagĩra?

16 Ili tuwe watakatifu ni lazima tuwe tayari kuwa tofauti na watu wengine. Kufanya hivyo kunaweza kuwa changamoto. Nyakati nyingine wanafunzi wenzetu, wafanyakazi wenzetu, watu wa ukoo wasio waamini, na wengine huenda wakatushinikiza tufanye mambo ambayo yatachafua ibada yetu kwa Yehova. Wanapofanya hivyo, tunahitaji kufanya uamuzi muhimu. Ni nini kinachoweza kutusaidia kufanya uamuzi sahihi? Fikiria kanuni hii inayopatikana kwenye andiko la Mambo ya Walawi 19:19, ambayo kwa sehemu inasema hivi: “Usivae vazi lililoshonwa kwa nyuzi za aina mbili.” Sheria hiyo iliwatofautisha Waisraeli na mataifa yaliyowazunguka. Leo, kwa kuwa hatuko chini ya Sheria si vibaya kwa Mkristo kuvaa mavazi yaliyoshonwa kwa nyuzi za aina mbalimbali, kama mchanganyiko wa pamba na poliesta. Lakini tunaepuka kuwa kama watu ambao imani na matendo yao yanapingana na mafundisho ya Biblia, hata ikiwa watu hao ni wanafunzi wenzetu, wafanyakazi wenzetu, au watu wetu wa ukoo. Bila shaka, kiasili tunawapenda watu wetu wa ukoo na tunawaonyesha upendo jirani zetu pia. Hata hivyo, maamuzi tunayofanya maishani, yanapaswa kuonyesha kwamba tunamtii Yehova hata ikiwa tutaonekana kuwa tofauti. Kumbuka kwamba kuwa watakatifu kunahusisha kuwekwa kando kwa ajili ya Mungu. Hilo ni muhimu ili tuwe watakatifu.​—2 Kor. 6:14-16; 1 Pet. 4:3, 4.

Watu wa Mungu walipaswa kujifunza jambo gani kutokana na Mambo ya Walawi 19:23-25, na unajifunza nini kutokana na mistari hiyo? (Tazama fungu la 17 na 18) *

17-18. Nĩ kĩthoomo kĩrĩkũ kĩa bata tũũmba kwiritana kuumania na ĩandĩko rĩa Mantu ja Alawi 19:23-25?

17 Maneno, “Mimi ni Yehova Mungu wenu” yalipaswa kuwakumbusha Waisraeli watangulize maishani uhusiano wao pamoja na Yehova. Jinsi gani? Andiko la Mambo ya Walawi 19:23-25 linaonyesha njia moja. (Soma.) Fikiria maneno hayo yangemaanisha nini kwa Waisraeli walipoingia katika Nchi ya Ahadi. Ikiwa mwanamume angepanda miti kwa ajili ya chakula, hakupaswa kula matunda ya miti hiyo kwa miaka mitatu. Katika mwaka wa nne, matunda hayo yaliwekwa kando kwa ajili ya kutumiwa katika patakatifu pa Mungu. Ni katika mwaka wa tano tu ndipo mmiliki wa miti hiyo angekula matunda yake. Sheria hiyo ilipaswa kuwasaidia Waisraeli waelewe kwamba hawakupaswa kutanguliza mapendezi yao. Walipaswa kutumaini kwamba Yehova angewaandalia mahitaji yao, na kuitegemeza kwanza ibada yake. Angehakikisha kwamba wana chakula cha kutosha. Na Mungu aliwatia moyo watoe matoleo kwa ukarimu katika patakatifu, mahali ambapo walimwabudu.

18 Sheria inayopatikana kwenye andiko la Mambo ya Walawi 19:23-25 inatukumbusha maneno ya Yesu kwenye Mahubiri ya Mlimani. Alisema hivi: “Acheni kuhangaikia kuhusu . . . kile mtakachokula au kunywa.” Yesu aliongezea hivi: “Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivi vyote.” Mungu atatuandalia mahitaji yetu, kama pia anavyowaandalia ndege. (Mt. 6:25, 26, 32) Tuna hakika kwamba Yehova atatuandalia mahitaji yetu. Na bila kujionyesha, tunatoa “zawadi za rehema” ili kuwasaidia wenye uhitaji. Pia, tunafurahia kuchangia gharama za kutaniko. Yehova anaona ukarimu wa aina hiyo naye atatulipa. (Mt. 6:2-4) Hivyo, tunapokuwa wakarimu tunaonyesha kwamba tunaelewa masomo tunayopata kwenye Mambo ya Walawi 19:23-25.

19. Nĩatĩa wagunĩka tontũ bwa gũcũnkũũna gĩcuncĩ gĩkĩ kĩa iuku rĩa Mantu ja Alawi?

19 Tumechunguza mistari michache katika Mambo ya Walawi sura ya 19, na tumeona jinsi tunavyoweza kumwiga Mungu wetu mtakatifu. Na tunapomwiga, tunaonyesha kwamba tunajitahidi ‘kuwa watakatifu katika mwenendo wetu wote.’ (1 Pet. 1:15) Watu wengi ambao hawamwabudu Yehova wamejionea mwenendo huo mzuri. Isitoshe, wengine wamechochewa kumtukuza Yehova. (1 Pet. 2:12) Hata hivyo, kuna mambo mengi zaidi tunayoweza kujifunza katika Mambo ya Walawi sura ya 19. Makala inayofuata itazungumzia mistari mingine katika sura hiyo na itatusaidia kutambua maeneo mengine katika maisha yetu ambayo tunaweza ‘kuwa watakatifu’ kama Petro anavyotuhimiza.

RWĨMBO 80 “Onjeni Mwone Kwamba Yehova Ni Mwema”

^ Tunampenda sana Yehova, na tunataka kumfurahisha. Yehova ni mtakatifu na anatarajia waabudu wake wawe watakatifu. Je, kweli hilo linawezekana kwa wanadamu wasio wakamilifu? Ndiyo, linawezekana. Kuchunguza kwa makini shauri la mtume Petro kwa Wakristo wenzake, na maagizo ya Yehova kwa Waisraeli wa kale, kutatusaidia kujifunza jinsi tunavyoweza kuwa watakatifu katika mwenendo wetu wote.

^ Kwa habari zaidi kuhusu Sabato na masomo tunayoweza kujifunza, tazama makala “‘Kuna Wakati Uliowekwa’ wa Kufanya Kazi na Kupumzika” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 2019.

^ MAELEZO YA PICHA: Mwana ambaye ni mtu mzima anatumia muda pamoja na wazazi wake, anampeleka mke na mtoto wake wakawatembelee, na anahakikisha kwamba anawasiliana nao kwa ukawaida.

^ MAELEZO YA PICHA: Mkulima Mwisraeli anachunguza baadhi ya matunda kwenye mti ambao alipanda.