Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JI LIFUNZU 49

Setulibola Mmambu ga Walawi Kuhusu Jinsi Jakwahenge Bangi

Setulibola Mmambu ga Walawi Kuhusu Jinsi Jakwahenge Bangi

“Lasima gumpala nnzaku kama egulipai gwamwe.”​—LAW. 19:18.

NHAMBU 109 Pendaneni Sana Kutoka Moyoni

MUHTASARI *

1-2. Twasungusa ki mumakala jejilonguli, na musitusungusa ki mu makala jenzeno?

 KATIKA makala iliyotangulia, tulichunguza ushauri hususa unaopatikana katika Mambo ya Walawi sura ya 19. Kwa mfano, kwenye mstari wa 3, Yehova aliwaambia Waisraeli wawaheshimu wazazi wao. Tulizungumzia jinsi ambavyo leo tunaweza kutumia ushauri huo kushughulikia mahitaji ya kimwili, kihisia, na kiroho ya wazazi wetu. Katika mstari huohuo, watu wa Mungu walikumbushwa umuhimu wa kushika Sabato. Tulijifunza kwamba ingawa hatuko chini ya sheria ya Sabato leo, tunaweza kutumia kanuni hiyo kwa kutenga wakati kwa ukawaida ili kushughulikia mambo yanayohusiana na ibada yetu. Kwa kufanya hivyo, tutaonyesha kwamba tunajitahidi kuwa watakatifu kama tunavyoagizwa kwenye Mambo ya Walawi 19:2 na 1 Petro 1:15.

2 Katika makala hii, tutaendelea kuchunguza Mambo ya Walawi sura ya 19. Sura hii inatufundisha nini kuhusu kuwaonyesha ufikirio watu wenye matatizo ya kiafya, kuwa wanyoofu katika masuala ya kibiashara, na kuwaonyesha wengine upendo? Tunataka kuwa watakatifu kama Mungu alivyo mtakatifu, basi acheni tuone mambo tunayoweza kujifunza.

KWALANGI UFIKILIU BAABI NA MATATISU GIKIAFYA

Andiko la Mambo ya Walawi 19:14, linatutia moyo tuwatendeeje viziwi na vipofu? (Tazama fungu la 3 hadi 5) *

3-4. Kulengana niliandiku la Mambu ga Walawi 19:14, aka viziwi na aka vipofu bapaswa kwahenge bole?

3 Soma Mambo ya Walawi 19:14. Yehova alitarajia watu wake wawaonyeshe ufikirio wale waliokuwa na matatizo ya kiafya. Kwa mfano, Waisraeli hawakupaswa kumtukana kiziwi. Kumtukana kulihusisha kumtisha au kumlaani. Kumtendea hivyo kiziwi kulikuwa jambo baya sana! Hangesikia mambo yaliyosemwa kumhusu, basi hangeweza kujitetea.

4 Zaidi ya hayo, katika mstari wa 14 tunajifunza kwamba watumishi wa Mungu hawakupaswa “kuweka kizuizi mbele ya kipofu.” Kitabu kimoja cha marejeo kinaeleza hivi kuhusu watu walio na matatizo ya kiafya: “Katika Mashariki ya Karibu ya kale [watu hao] walitendewa vibaya na bila haki.” Huenda baadhi ya watu ambao hawakuwa na ufikirio waliweka kizuizi mbele ya kipofu ili kumuumiza kimakusudi au ili kumcheka. Hilo linasikitisha sana! Kupitia amri hiyo, Yehova aliwasaidia watu wake waone kwamba walipaswa kuwahurumia wale waliokuwa na matatizo ya kiafya.

5. Tuwesa kwalangi bo huluma baabi na matatisu gikiafya?

5 Yesu aliwaonyesha huruma wale waliokuwa na matatizo ya kiafya. Kumbuka ujumbe ambao Yesu alimtumia Yohana Mbatizaji: “Vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, [na] wafu wanafufuliwa.” Walipoona miujiza ya Yesu, ‘watu wote walimsifu Mungu.’ (Luka 7:20-22; 18:43) Wakristo wanafurahia kuiga mtazamo wa Yesu wa kuwaonyesha huruma wale walio na matatizo ya kiafya. Hivyo tunawatendea kwa fadhili, ufikirio, na subira watu hao. Ni kweli kwamba Yehova hajatupatia uwezo wa kufanya miujiza. Hata hivyo, tuna pendeleo la kuwaambia walio vipofu kimwili au kiroho habari njema kuhusu paradiso ambayo wanadamu wataponywa kabisa kimwili na kiroho. (Luka 4:18) Tayari habari njema hizo zinawafanya wengi wamtukuze Mungu.

KUBA TWANYOOFU MUSHUGULI IKIBIASHALA

6. Mambu ga Walawi sula ja 19 jutujangati bo kuelewa Amuli Komi yela?

6 Baadhi ya mistari katika Mambo ya Walawi sura ya 19 inafafanua mambo yaliyotajwa katika zile Amri Kumi. Kwa mfano, amri ya nane ilisema hivi: “Usiibe.” (Kut. 20:15) Huenda mtu akafikiri kwamba maadamu anajitahidi kuepuka kuchukua kitu ambacho si chake, basi anatii amri hiyo. Hata hivyo, inawezekana kwamba anaiba kwa njia nyingine.

7. Pangi mfanyabiashala jwivunja bo amli ja nani kuhusu kujiba?

7 Huenda mfanyabiashara akajivunia kwamba hajawahi kuchukua kitu ambacho si chake. Lakini namna gani kuhusu jinsi anavyofanya biashara yake? Kama inavyoonyeshwa kwenye Mambo ya Walawi 19:35, 36, Yehova alisema hivi: “Msitumie vipimo vya uwongo kupima urefu, uzito, au ujazo. Mnapaswa kutumia mizani sahihi, vipimo sahihi, kipimo sahihi cha vitu vikavu, na kipimo sahihi cha vitu vya majimaji.” Mfanyabiashara aliyetumia kipimo kisicho sahihi ili kuwadanganya wateja wake alikuwa akiwaibia. Kuchunguza zaidi Mambo ya Walawi sura ya 19 kunaweka wazi jambo hilo.

Kulingana na Mambo ya Walawi 19:11-13, Mkristo anaweza kujiuliza maswali gani kuhusu jinsi anavyofanya biashara? (Tazama fungu la 8 hadi 10) *

8. Abali yeipatikana mulianduku la Mambu ga Walawi 19:11-13 yajangatya bo Ayahudi kutii amli ja nani, natwe tunufaika bole?

8 Soma Mambo ya Walawi 19:11-13. Andiko la mambo ya Walawi 19:11 linaanza kwa neno: “Msiibe.” Mstari wa 13 unahusianisha kuiba na kutokuwa wanyoofu katika biashara, unaposema: “Usimlaghai mwenzako.” Hivyo, ulaghai kwenye biashara unahusianishwa na wizi na unyang’anyi. Ingawa amri ya nane ilitoa sheria kuhusu kuiba, habari hususa zinazopatikana katika Mambo ya Walawi zingewasaidia Wayahudi kuelewa jinsi ambavyo wangetumia kanuni inayopatikana kwenye sheria hiyo. Tunanufaika kwa kutafakari maoni ya Yehova kuhusu ukosefu wa unyoofu na kuiba. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Kulingana na Mambo ya Walawi 19:11-13, je, kuna jambo fulani maishani mwangu ambalo ninahitaji kulifanyia kazi? Je, ninahitaji kufanya mabadiliko katika mazoea yangu kwenye biashara au kazi yangu?’

9. Shelia jejipatikana mu Mambu ga Walawi 19:13 jaboa ulinzi bole?

9 Kuna jambo lingine kuhusu unyoofu ambalo Mkristo aliyewaajiri wafanyakazi anapaswa kuzingatia. Andiko la Mambo ya Walawi 19:13, linamalizia hivi: “Usikae na mshahara wa kibarua usiku kucha mpaka asubuhi.” Katika jamii ya wakulima huko Israeli, wafanyakazi vibarua walipaswa kulipwa kila siku baada ya kazi. Ikiwa mfanyakazi huyo angekosa kulipwa, hangekuwa na pesa za kununulia familia yake chakula siku hiyo. Yehova alieleza hivi: “Uhitaji na uhai wake unategemea mshahara wake.”​—Kum. 14:14, 15; Mt. 20:8.

10. Tulibola ki mu Mambu ga Walawi 19:13?

10 Leo, wafanyakazi wengi wanalipwa mara moja au mbili kwa mwezi, na si kila siku. Hata hivyo, kanuni inayopatikana kwenye Mambo ya Walawi 19:13 bado inatumika. Baadhi ya waajiri hawawatendei kwa haki wafanyakazi wao kwa sababu wanawalipa mshahara mdogo kuliko wanavyostahili. Wanajua kwamba huenda wafanyakazi hao hawana tumaini lingine isipokuwa kuendelea kufanya kazi ili wasife njaa. Tunaweza kusema waajiri hao ‘wanakaa na mshahara wa kibarua.’ Mkristo ambaye amewaajiri wafanyakazi anapaswa kukumbuka kanuni hiyo. Sasa acheni tuone jambo lingine tunaloweza kujifunza kwenye Mambo ya Walawi sura ya 19.

MPALA NNZAKU KAMA EGULIPALA GWAMWE

11-12. Yesu jwakazila ki kukunukuu Mambu ga Walawi 19:17, 18?

11 Tunaposhughulika na wengine, Mungu anatarajia tufanye mengi zaidi ya kuepuka tu kuwaumiza. Tunaona jambo hilo kwenye Mambo ya Walawi 19:17, 18. (Soma.) Ona amri hii iliyo wazi: “Ni lazima umpende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe.” Mkristo anapaswa kufanya hivyo ikiwa anataka kumfurahisha Mungu.

12 Fikiria jinsi Yesu alivyokazia umuhimu wa amri inayopatikana kwenye Mambo ya Walawi 19:18. Farisayo fulani alimuuliza hivi: “Ni amri gani iliyo kuu zaidi katika Sheria?” Yesu alijibu kwamba “amri ya kwanza na iliyo kuu zaidi” ni kumpenda Yehova kwa moyo wetu wote, nafsi yetu yote, na akili yetu yote. Kisha Yesu akanukuu Mambo ya Walawi 19:18, akisema: “Ya pili, kama hiyo, ni hii, ‘Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’” (Mt. 22:35-40) Kuna njia nyingi za kuwaonyesha upendo jirani zetu, na tunajifunza mengi zaidi kwenye Mambo ya Walawi sura ya 19.

13. Lisimulizi la Bibilia kunhusu Yosefu lutujangati bo kuelewa lijambu ambalu pa baadai biliandika mu Mambu ga Walawi 19:18?

13 Njia moja ya kuwaonyesha upendo jirani zetu ni kwa kutumia shauri linalopatikana kwenye andiko la Mambo ya Walawi 19:18. Linasema hivi: “Usilipize kisasi wala usiwe na kinyongo.” Wengi wetu tunawafahamu watu ambao wameweka kinyongo kumwelekea mfanyakazi mwenzao, mwanafunzi mwenzao, mtu wa ukoo, au mshiriki wa familia—labda kwa miaka mingi! Kumbuka kwamba ndugu nusu kumi wa Yosefu walimwekea kinyongo, jambo ambalo hatimaye lilisababisha wamtendee kwa chuki. (Mwa. 37:2-8, 25-28) Hata hivyo, Yosefu aliwatendea kwa njia tofauti kabisa! Alipopata mamlaka angeweza kulipiza kisasi dhidi ya ndugu zake, lakini aliwaonyesha rehema. Yosefu hakuweka kinyongo. Badala yake, alitenda kupatana na shauri ambalo baadaye liliandikwa kwenye Mambo ya Walawi 19:18.​—Mwa. 50:19-21.

14. Ndo ki sekilangi kwamba twakali tukapaswa kutii kanuni yeibi mu Mambu ga Walawi 19:18?

14 Wakristo wanaotaka kumfurahisha Mungu wanapaswa kuiga kielelezo cha Yosefu cha kusamehe badala ya kuweka kinyongo au kulipiza kisasi. Pia, jambo hilo linapatana na sala ya kielelezo, kwa kuwa Yesu alituhimiza tuwasamehe wale wanaotukosea. (Mt. 6:9, 12) Pia, mtume Paulo aliwashauri Wakristo wenzake hivi: “Wapendwa, msijilipizie kisasi.” (Rom. 12:9) Na aliwatia moyo hivi: “Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari hata ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine.” (Kol. 3:13) Kanuni za Yehova hazibadiliki. Leo, bado tunapaswa kutii kanuni zilizo kwenye Mambo ya Walawi 19:18.

Kama vile tunavyoepuka kuchokonoa kidonda halisi, hatupaswi kuendelea kufikiria makosa tuliyotendewa na wengine. Tunapaswa kujitahidi kuyasahau (Tazama fungu la 15) *

15. Gubi mfanu bo gogutujangati kuelegwa ndaba jaki tupaswa kwasame bangi nukujegwa?

15 Fikiria mfano ufuatao. Kuumizwa kihisia kunaweza kulinganishwa na vidonda halisi. Vidonda vingine ni vidogo na vingine ni vikubwa. Kwa mfano, unapopika huenda ukajikata kidogo na kisu. Jeraha hilo linaweza kutusababishia maumivu lakini baada ya muda mfupi linapona. Baada ya siku moja au mbili hata tunasahau mahali tulipokuwa tumejikata. Vivyo hivyo, baadhi ya makosa ambayo watu hututendea ni madogo. Kwa mfano, huenda rafiki yetu akasema au kufanya jambo fulani bila kufikiri na kutuumiza, lakini tunaweza kumsamehe kwa urahisi. Hata hivyo, unapopata jeraha kubwa huenda daktari akahitaji kushona kidonda hicho na kukifunga bendeji. Lakini ikiwa tutaendelea kukigusa-gusa au kukichokonoa, huenda hakitapona na tutajiumiza. Inasikitisha kwamba mtu anaweza kufanya jambo kama hilo anapoumizwa sana na makosa ya wengine. Huenda akaendelea kufikiria jinsi alivyoumizwa hisia na matendo ya mtu huyo. Lakini wale wanaoweka kinyongo wanajiumiza wenyewe. Ni jambo bora zaidi kutii shauri linalopatikana kwenye Mambo ya Walawi 19:18!

16. Kulengana na Mambu ga Walawi 19:33, 34, bapaswa kwahenge bo ageni, na twe tulibola kike?

16 Yehova alipowaamuru Waisraeli wawapende wenzao, hakumaanisha kwamba walipaswa kuwapenda tu watu wa jamii au taifa lao. Waliambiwa pia walipaswa kuwapenda wageni miongoni mwao. Ujumbe huo ulio wazi unapatikana kwenye Mambo ya Walawi 19:33, 34. (Soma.) Mgeni alipaswa kutendewa “kama mwenyeji,” na Waisraeli walipaswa ‘kumpenda’ kama wanavyojipenda wenyewe. Kwa mfano, Waisraeli walipaswa kuwaruhusu wageni na maskini wanufaike na mpango wa kuokota masalio. (Law. 19:9, 10) Kanuni ya kuwapenda wageni inawahusu Wakristo leo. (Luka 10:30-37) Jinsi gani? Kuna mamilioni ya wahamiaji na huenda baadhi yao wanaishi karibu nawe. Tunapaswa kuwatendea wanaume, wanawake, na watoto hao kwa heshima na staha.

KASI MUHIMU AMBAJU NGASEAJILOGWI MU MAMBU GA WALAWI SULA JA 19

17-18. (a) Kulengana niliandiku la Mambu ga Walawi 19:2 na 1 Petro 1:15, atujege mwoju tuhenga kike? (b) Mtumi Petro jutujegala mwoju tuhenga kasi bo jumuhimo?

17 Kwenye andiko la Mambo ya Walawi 19:2 na 1 Petro 1:15, watu wa Mungu wanahimizwa kuwa watakatifu. Mistari mingine mingi katika Mambo ya Walawi sura ya 19 inatusaidia kuona mambo tunayoweza kufanya ili kupata kibali cha Yehova. Tumezungumzia mistari ambayo inaonyesha baadhi ya mambo tunayopaswa kufanya na mambo tunayopaswa kuepuka. * Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanaonyesha kwamba Yehova anataka tuendelee kutumia kanuni hizo. Lakini mtume Petro anaongezea jambo lingine.

18 Huenda tunashiriki katika shughuli nyingi za kiroho na kufanya mambo mengi mema, hata hivyo, Petro anakazia jambo moja hususa. Kabla ya kututia moyo tuwe watakatifu katika mwenendo wetu wote, Petro anatuhimiza hivi: “Kazeni akili zenu kwa ajili ya utendaji.” (1 Pet. 1:13, 15) Utendaji huo unahusisha nini? Petro alisema kwamba ndugu za Kristo waliotiwa mafuta ‘wangetangaza kotekote sifa bora za Yule aliyewaita.’ (1 Pet. 2:9) Leo, Wakristo wote wana pendeleo la kufanya kazi hiyo muhimu zaidi ambayo inawanufaisha watu kuliko kazi nyingine yoyote. Tukiwa kikundi cha watu watakatifu tuna pendeleo kubwa sana la kushiriki kwa bidii na kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri na kufundisha! (Marko 13:10) Tunapojitahidi kabisa kufuata kanuni zinazopatikana kwenye Mambo ya Walawi sura ya 19, tunathibitisha kwamba tunampenda Mungu wetu na jirani zetu. Na tunaonyesha kwamba tunataka ‘kuwa watakatifu’ katika mwenendo wetu wote.

NHAMBU 111 Sababu za Kuwa na Shangwe

[Maelezo ya Chini]

^ ekichweka 5 Wakristo hawako chini ya Sheria ya Musa, lakini Sheria hiyo inataja mambo mengi ambayo tunapaswa kufanya au kuyaepuka. Kujifunza mambo hayo kunaweza kutusaidia kuwaonyesha wengine upendo na kumfurahisha Mungu. Makala hii inazungumzia jinsi tunavyoweza kunufaika kutokana na baadhi ya masomo kwenye Mambo ya Walawi sura ya 19.

^ ekichweka 17 Mistari ambayo haijazungumziwa katika makala hizi inakazia kuepuka ubaguzi, uchongezi, kutokula damu, na pia kuwasiliana na roho waovu, kubashiri, na uasherati.​—Law. 19:15, 16, 26-29, 31.​—Tazama “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika toleo hili.

^ ekichweka 52 MAELEZO YA PICHA: Shahidi akimsaidia ndugu kiziwi kuwasiliana na daktari.

^ ekichweka 54 MAELEZO YA PICHA: Ndugu anayemiliki biashara ya kupaka rangi anampatia mfanyakazi wake mshahara.

^ ekichweka 56 MAELEZO YA PICHA: Ni rahisi kwa dada huyu kusahau jeraha dogo. Je, atachagua kufanya hivyo inapohusu jeraha kubwa zaidi?