Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unakuwaka Mufanyakazi Muzuri?

Unakuwaka Mufanyakazi Muzuri?

“NILIKUWA pembeni yake nikiwa fundi wa kazi. . . . Nilifurahi mbele yake wakati wote.” (Mez. 8:30) Hii andiko inaonyesha namna Mwana wa Mungu alitumika pamoja na Baba yake kwa miaka mingi mbele akuye hapa ku dunia. Pia mu hii andiko, tunajifunza kama Yesu ‘alifurahi’ wakati alikuwa anatumika pamoja na Baba yake.

Mbinguni, Yesu alijifunza sifa zenye zilimufanya akuwe mufanyakazi muzuri. Kisha, wakati alikuwa hapa ku dunia alikuwa mufano muzuri zaidi wa mutu mwenye alitumika muzuri pamoja na watu wengine. Namna gani mufano wa Yesu unaweza kutusaidia? Kwa kujifunza mufano wake, tunaweza kupata kanuni tatu zenye zinaweza kutusaidia kutumika muzuri pamoja na wengine. Zile kanuni zitatusaidia tukuwe na umoja pamoja na ndugu zetu.

Usisahau mufano wa Yehova na wa Yesu wa kuwa tayari kuambia wanafanyakazi wenzako mambo yenye unajua na uzoefu wako

KANUNI YA 1: ‘MUONYESHANE HESHIMA’

Kwa unyenyekevu, mufanyakazi muzuri anaona wafanyakazi wenzake kuwa wa maana na hajionyeshe kama yeye ni wa maana sana kuwashinda. Yesu alijifunza ile sifa ya unyenyekevu kwa Baba yake. Hata kama Baba yake yeye peke njo anastahili kuitwa Muumbaji, alipenda watu wengine wajue kazi ya maana sana yenye Mwana wake alifanya pamoja na wafanyakazi wenzake. Tunaelewa ile muzuri zaidi kupitia mambo yenye Mungu alisema: “Tufanye mutu kwa mufano wetu.” (Mwa. 1:26) Wakati Yehova alisema ile maneno, Yesu alijua kama Yehova ni munyenyekevu sana.​—Zb. 18:35.

Wakati alikuwa hapa ku dunia, Yesu pia alikuwa munyenyekevu. Wakati watu walimusifu juu ya mambo yenye alikuwa amefanya, alimutukuza Mungu. (Mk. 10:17, 18; Yoh. 7:15, 16) Yesu alifanya yake yote juu kukuwe hali ya amani kati yake na wanafunzi wake, na aliwatendea sawa vile marafiki hapana sawa watumwa. (Yoh. 15:15) Aliwanawisha hata miguu juu ya kuwafundisha sifa ya unyenyekevu. (Yoh. 13:5, 12-14) Sawa vile Yesu, tunapaswa kuheshimia wafanyakazi wenzetu kuliko kutia faida zetu pa nafasi ya kwanza. Tunaweza kufanya mambo mingi zaidi wakati tunaheshimia wengine na wakati kila mara hatutazamie wengine watusifu juu ya mambo yenye tulifanya.​—Ro. 12:10.

Mutu munyenyekevu anajua kama “mambo yanatimizwa kupitia washauri wengi.” (Mez. 15:22) Ikuwe tuko na uzoefu ao tuko na uwezo wa namna gani, tunapaswa kukumbuka kama hakuna mutu mwenye anajuaka mambo yote. Hata Yesu alijua kama kulikuwa mambo fulani yenye hakujua. (Mt. 24:36) Pia alipenda kujua mawazo ya wanafunzi wake wenye hawakamilike. (Mt. 16:13-16) Njo maana, wafanyakazi wenzake walijisikia muzuri kuwa pamoja naye! Vilevile, wakati tuko wanyenyekevu tutakumbuka kama hatujue mambo yote, na wakati tunasikiliza mawazo ya wengine tutakuwa na amani pamoja nao, na pamoja tutaweza ‘kutimiza mambo fulani.’

Ni jambo ya maana, zaidi sana kwa wazee, kuiga unyenyekevu wa Yesu wakati wanatumika pamoja. Wanapaswa kukumbuka kama roho takatifu inaweza kuongoza muzee yeyote ili alete mawazo yenye itasaidia baraza ya wazee kukamata maamuzi ya muzuri. Kama mu mikutano yao, wazee wanajikaza kutia hali yenye itafanya kila mutu ajisikie huru kutoa mawazo yake, pamoja watakamata maamuzi yenye italetea faida kutaniko yote.

KANUNI YA 2: “USAWAZIKO WENU UJULIKANE”

Mufanyakazi muzuri anatumikaka kwa usawaziko pamoja na wengine. Iko tayari kubadilika na kuachilia mambo fulani. Kusema kweli, Yesu alikuwa na nafasi mingi ya kuona namna Baba yake alikuwa na usawaziko. Kwa mufano, Yehova alimutumia aokoe wanadamu kutoka katika hukumu ya kifo.​—Yoh. 3:16.

Yesu alikuwa tayari kuachilia mambo kama inafaa na kama iliomba kufanya vile. Kumbuka namna alimusaidia mwanamuke mumoja Mufoinike, hata kama Yesu alitumwa ku watu wa nyumba ya Israeli. (Mt. 15:22-28) Yesu alikuwa pia na usawaziko kuhusu mambo yenye alitazamia kutoka kwa wanafunzi wake. Kisha rafiki yake Petro kumukana mbele ya watu, Yesu alikuwa tayari kumusaheme. Kisha, alimupatia Petro madaraka ya maana sana. (Lu. 22:32; Yoh. 21:17; Mdo. 2:14; 8:14-17; 10:44, 45) Juu “usawaziko [wetu] ujulikane kwa watu wote,” tunapaswa kuwa tayari kuachilia mambo fulani. Ile njo mufano wa Yesu unatufundisha.​—Flp. 4:5.

Kuwa na usawaziko kutatuchochea pia kujipatanisha na hali ili kutumika kwa amani pamoja na watu wa namna zote. Yesu alitendea muzuri wale wenye aliishi pamoja nao, na hata maadui wake wenye walikuwa na wivu walisema kama ni “rafiki ya wakusanya-kodi na watenda-zambi” wenye walikubali ujumbe wake. (Mt. 11:19) Sawa vile Yesu, je, na siye tunaweza kutumika muzuri pamoja na wengine? Ndugu Louis, mwenye alipitisha wakati mingi mu muzunguko na mwenye alitumika ku Beteli na watu wa desturi mbalimbali, anasema hivi: “Kutumika pamoja na watu wenye hawakamilike iko sawa vile kujenga ukuta na ma brike yenye kuwa na ukubwa tofauti. Juu ma brike iko tofauti, inaomba kujikaza sana juu ukuta unyooke muzuri. Nilijikaza sana kufanya mabadiliko ili kutumika kwa amani na wengine juu tufikie kufanya kazi fulani.” Ile ni roho ya muzuri kabisa!

Mufanyakazi muzuri hajizuiake kuambia wengine mambo yenye anajua

Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko na usawaziko wakati tuko pamoja na ndugu na dada zetu mu kutaniko? Tunaweza kufanya vile wakati tuko mu kikundi yetu ya mahubiri. Pengine tunaweza kutumika pamoja na wahubiri wenye kuwa na madaraka ya familia tofauti na yetu ao wenye kuwa na miaka tofauti na yetu. Tunaweza kupunguza hatua yetu ao kufanya aina fulani ya mahubiri yenye wao wanapenda juu wafurahie utumishi zaidi.

KANUNI YA 3: UKUWE “TAYARI KUSHIRIKI NA WENGINE”

Mufanyakazi muzuri anakuwaka “tayari kushiriki na wengine.” (1 Ti. 6:18) Wakati alikuwa anatumika pamoja na Baba yake, Yesu aliona kama Yehova hakukuwa anamuficha mambo fulani. Wakati Yehova “alitayarisha mbingu,” Yesu ‘alikuwa pale’ na angeweza kujifunza mambo fulani kutoka kwake. (Mez. 8:27) Kisha, Yesu yeye mwenyewe aliambia wanafunzi wake “mambo yote yenye [alisikia]” kutoka kwa Baba yake. (Yoh. 15:15) Na siye pia tunaweza kuiga mufano wa Yehova kwa kuwa tayari kuambia ndugu na dada zetu mambo yenye tunajua na uzoefu wetu. Mufanyakazi muzuri hajizuie kuambia wengine mambo yenye wanapenda kujua ao mambo yenye inaweza kuwasaidia. Lakini anafurahia kuambia wengine mambo ya muzuri yenye amejifunza.

Tunaweza pia kuambia wafanyakazi wenzetu maneno yenye kutia moyo. Wakati mutu fulani anaona bidii yetu na anatushukuru, je, ile haitutiake moyo? Yesu alikamata wakati wa kuambia wafanyakazi wenzake mambo ya muzuri yenye aliona kwao. (Linganisha na Matayo 25:19-23; Luka 10:17-20.) Hata aliwaambia kama watafanya “kazi kubwa” kuliko yenye yeye alifanya. (Yoh. 14:12) Usiku mbele akufe, alipongeza mitume wake waaminifu. Aliwaambia hivi: “Ninyi ndio mumeshikamana na mimi katika majaribu yangu.” (Lu. 22:28) Waza kidogo namna ile maneno iliwatia moyo na iliwachochea kufanya mambo ya muzuri! Na siye pia, kama tunakamata wakati wa kupongeza wafanyakazi wenzetu, kusema kweli, watafurahi na watajikaza kufanya muzuri zaidi.

UNAWEZA KUWA MUFANYAKAZI MUZURI

Ndugu Kayode anasema hivi: “Haiko lazima mutu akuwe mukamilifu juu akuwe mufanyakazi muzuri. Lakini, mufanyakazi muzuri anafanya watu wengine wafurahi na anafanya kazi ikuwe mwepesi.” Uko mufanyakazi wa vile? Pengine unaweza kuuliza ndugu ao dada fulani akuambie anawazaka uko mufanyakazi wa namna gani. Kama wanafurahiaka kutumika pamoja na weye, sawa vile wanafunzi wa Yesu walikuwa wanafurahi kutumika pamoja naye, unaweza kusema hivi sawa vile mutume Paulo: “Tuko wafanyakazi wenzenu kwa ajili ya furaha yenu.”​—2 Ko. 1:24.