Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JI LIFUNZU 51

Nhendalya ‘Kumpelakane’

Nhendalya ‘Kumpelakane’

“Jonzo ndo Mwanajwa, mpendwa, jonunzetaki. Mumpelakania.”​—MT. 17:5.

NHAMBU 54 “Hii Ndiyo Njia”

MUHTASARI *

1-2. (a) Akamitumi atatu bika Yesu baamuliwa ahenga ki, na bombi bahenga bole? (b) Musitusungusa ki mu makala jenzeno?

 BAADA ya Pasaka ya mwaka wa 32 W.K., mtume Petro, Yakobo, na Yohana waliona maono ya kustaajabisha. Wakiwa kwenye mlima mrefu, labda Mlima Hermoni, Yesu aligeuka sura mbele yao. “Uso wake ukang’aa kama jua, na mavazi yake ya nje yakang’aa kama nuru.” (Mt. 17:1-4) Mwishoni mwa maono hayo, mitume hao walimsikia Mungu akisema: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nimemkubali. Msikilizeni.” (Mt. 17:5) Baadaye, maisha ya mitume hao watatu yalithibitisha kwamba kwa kweli walimsikiliza Yesu. Tunapaswa kuiga mfano wao.

2 Katika makala iliyotangulia, tulijifunza kwamba kusikiliza sauti ya Yesu kunamaanisha kuacha kufanya mambo fulani. Katika makala hii, tutachunguza mambo mawili ambayo Yesu alisema kwamba tunapaswa kufanya.

“NNZINGALA KUPETE UNDYANGU MWEMBAMBA”

3. Kulengana na Mathayo 7:13, 14, tupaswa kuhenga kike?

3 Soma Mathayo 7:13, 14. Ona kwamba Yesu alitaja malango mawili tofauti yanayoongoza kwenye barabara mbili tofauti, barabara yenye “nafasi kubwa” na barabara yenye “nafasi ndogo.” Hakuna barabara ya tatu. Ni lazima tujiamulie wenyewe tutatembea kwenye barabara ipi. Huo ndio uamuzi muhimu zaidi ambao tunahitaji kufanya, kwa sababu uzima wetu wa milele unategemea uamuzi huo.

4. Guwesa kujifafanu bo balabala jejibi na “nafasi ngolongo”?

4 Tunapaswa kukumbuka tofauti kati ya barabara hizo mbili. Barabara yenye “nafasi kubwa” ina watu wengi kwa sababu ni rahisi kuifuata. Inasikitisha kwamba watu wengi wanachagua kubaki kwenye barabara hiyo na kutenda kama watu wanaotembea humo. Hawatambui kwamba Shetani Ibilisi ndiye anayewachochea watu watembee kwenye barabara hiyo, na kwamba barabara yake inaongoza kwenye kifo.​—1 Kor. 6:9, 10; 1 Yoh. 5:19.

5. Baazi ja bandu ahengiki jitihada bo ili kujipata balabala jejibi na “nafasi nzoku” nu kuanza kujipwata?

5 Tofauti na barabara yenye “nafasi kubwa,” ile barabara nyingine ina “nafasi ndogo,” na Yesu alisema kwamba watu wachache ndio wanaweza kuipata. Kwa nini? Ona kwamba katika mstari unaofuata, Yesu aliwaonya wafuasi wake dhidi ya manabii wa uwongo. (Mt. 7:15) Inakadiriwa kwamba kuna maelfu ya dini, na nyingi zinadai kuwa zinafundisha ukweli. Mamilioni ya watu wamevunjwa moyo sana na wamechanganyikiwa na kuwepo kwa dini hizo nyingi, hivi kwamba hata hawajitahidi kutafuta barabara inayoongoza kwenye uzima. Lakini barabara hiyo inaweza kupatikana. Yesu alisema: “Mkikaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, nanyi mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.” (Yoh. 8:31, 32) Tunakupongeza kwa sababu wewe hukufuata umati; badala yake ulitafuta kweli. Ulianza kuchunguza kwa makini Neno la Mungu ili ujifunze mambo ambayo anataka tufanye, na ulisikiliza mafundisho ya Yesu. Kati ya mambo uliyojifunza ni kwamba Yehova anatarajia tuyakatae mafundisho ya dini za uwongo na kuacha kusherehekea sikukuu ambazo chanzo chake ni cha kipagani. Pia, ulijifunza kwamba si rahisi kufanya mambo ambayo Yehova anataka tufanye na kuacha mazoea ambayo hayampendezi. (Mt. 10:34-36) Huenda ilikuwa vigumu kwako kufanya mabadiliko yaliyohitajika. Hata hivyo, uliendelea kujitahidi kwa sababu unampenda Baba yako wa mbinguni na unataka kupata kibali chake. Bila shaka, unamfurahisha sana!​—Met. 27:11.

JINSI JUKUHIGALI MMBALABALA JEJIBI NA NAFASI NZOKU

Shauri na viwango vya Mungu vinatusaidia kuendelea kubaki kwenye barabara yenye “nafasi ndogo” (Tazama fungu la 6 hadi 8) *

6. Kulengana na Zaburi 119:9, 10, 45, 133, kibi ki sekiwesa kutujangati tuendalya kuhigali mmbalabala jejibi na nafasi nzoko?

6 Tunapoanza kutembea kwenye barabara yenye nafasi ndogo, nini kinachoweza kutusaidia tuendelee kubaki katika barabara hiyo? Fikiria mfano huu. Ukingo uliojengwa kando ya barabara nyembamba iliyo kwenye mlima unasaidia kumlinda dereva na gari lake. Ukingo huo umekusudiwa kuwasaidia madereva wawe salama, yaani, kuwasaidia wasiache njia na kuanguka. Hakuna dereva anayeweza kulalamika kwamba ukingo huo unamnyima uhuru! Viwango vya Yehova vinavyopatikana katika Biblia ni kama ukingo huo. Viwango vyake vinatusaidia kuendelea kubaki katika barabara yenye nafasi ndogo.​—Soma Zaburi 119:9, 10, 45, 133.

7. Akakombu apaswa kujibona bo balabala jejibi na nafasi nzoko?

7 Enyi vijana, je, nyakati nyingine mnahisi kwamba viwango vya Yehova vinawanyima uhuru? Shetani anataka mfikiri hivyo. Anataka mkazie fikira mambo ambayo watu wanaotembea katika barabara yenye nafasi kubwa wanafanya, kwa sababu wanaonekana kana kwamba wanafurahia maisha. Anaweza kutumia mambo ambayo wanafunzi wenzako wanafanya au mambo unayoona kwenye Intaneti yakufanye uhisi kwamba unakosa mambo mazuri wanayofurahia. Shetani anataka ufikiri kwamba viwango vya Yehova vinakuzuia kufurahia maisha kikamili. * Lakini kumbuka hili: Shetani hataki wale wanaotembea katika barabara yake waone kile kitakachowapata mwisho wa safari yao. Hata hivyo, Yehova amekuonyesha wazi maisha mazuri ambayo utafurahia ikiwa utabaki kwenye barabara ya uzima.​—Zab. 37:29; Isa. 35:5, 6; 65:21-23.

8. Akakombu awesa kulibola ki kubokana nu mfanu guka Olaf?

8 Fikiria mambo unayoweza kujifunza kutokana na simulizi la ndugu kijana anayeitwa Olaf. * Wanafunzi wenzake walimshinikiza ajihusishe katika uasherati. Alipowaeleza kwamba Mashahidi wa Yehova wanaishi kulingana na viwango vya juu vya maadili vilivyo katika Biblia, baadhi ya wasichana katika darasa lake walijitahidi hata zaidi kumshawishi afanye nao ngono. Lakini Olaf alibaki imara. Hata hivyo, alikabili changamoto nyingine pia. Olaf anasema hivi: “Walimu wangu walijaribu kunisadikisha kwamba nilipaswa kufuatilia elimu ya juu kwa sababu nitaheshimika. Waliniambia kwamba bila elimu ya juu sitafanikiwa maishani.” Ni nini kilichomsaidia Olaf kukabiliana na changamoto hizo? Anasema hivi: “Nilisitawisha uhusiano wa karibu na ndugu na dada katika kutaniko letu. Walikuwa kama familia kwangu. Pia, nilianza kujifunza Biblia kwa bidii zaidi. Kadiri nilivyojifunza zaidi, ndivyo nilivyosadiki kwamba hii ndiyo kweli. Nami nikaazimia kumtumikia Yehova.”

9. Baapala kuhigali mbalabala jejibi na nafasi nzoku hahitaji kuhenga kike?

9 Shetani angependa uiache barabara inayoongoza kwenye uzima. Anataka ujiunge na watu wengi walio katika barabara yenye nafasi kubwa “inayoongoza kwenye uharibifu.” (Mt. 7:13) Hata hivyo, tutaendelea kubaki katika barabara yenye nafasi ndogo, ikiwa tutaendelea kumsikiliza Yesu na kuiona barabara hiyo kama ulinzi. Sasa acheni tuchunguze jambo lingine ambalo Yesu alisema tunapaswa kufanya.

HENGA AMANI NUNDONGU JWAKU

10. Kulengana na Mathayo 5:23, 24, Yesu jwapwaga tupaswa kuhenga kike?

10 Soma Mathayo 5:23, 24. Yesu alizungumzia pindi ambayo ilikuwa muhimu sana kwa waabudu Wayahudi waliokuwa wakimsikiliza. Mwazie mtu fulani hekaluni aliye tayari kumpatia kuhani mnyama kwa ajili ya dhabihu. Ikiwa pindi hiyo mtu anakumbuka kwamba ndugu yake ana jambo fulani dhidi yake, alipaswa kuiacha dhabihu na ‘kwenda zake.’ Kwa nini? Ni jambo gani ambalo lingekuwa muhimu zaidi kuliko kumtolea Yehova dhabihu? Yesu alieleza wazi hivi: “Kwanza fanya amani na ndugu yako.”

Je, utaiga mfano wa Yakobo, ambaye kwa unyenyekevu alifanya amani pamoja na ndugu yake? (Tazama fungu la 11 na 12) *

11. Yakobo jwahenga jitihada bo ili kuhenga amani na Esau.

11 Tunaweza kujifunza masomo muhimu kuhusu kufanya amani kwa kuchunguza tukio fulani katika maisha ya mzee wa ukoo Yakobo. Baada ya Yakobo kuwa mbali na nchi aliyozaliwa kwa zaidi ya miaka 20, Mungu alimtuma malaika amwamuru arudi huko. (Mwa. 31:11, 13, 38) Lakini kulikuwa na tatizo. Esau, ndugu yake mkubwa, alikuwa anataka kumuua. (Mwa. 27:41) Yakobo “[aliogopa] sana na kushikwa na wasiwasi” kwamba huenda bado ndugu yake alikuwa na kinyongo dhidi yake. (Mwa. 32:7) Yakobo alichukua hatua gani ili kufanya amani na ndugu yake? Kwanza, alisali kwa bidii kwa Yehova kuhusu jambo hilo. Kisha, akamtumia Esau zawadi kubwa. (Mwa. 32:9-15) Mwishowe, ndugu hao waliokuwa wametengana walipokutana uso kwa uso, Yakobo alichukua hatua ya kwanza kumwonyesha heshima Esau. Akiwa mbele ya Esau, aliinama mpaka chini, si mara moja au mbili, bali mara saba! Kwa unyenyekevu na heshima, Yakobo alifanya amani pamoja na ndugu yake.​—Mwa. 33:3, 4.

12. Tulibola ki kubokana nu mfanu guka Yakobo?

12 Tunaweza kujifunza kutokana na jinsi Yakobo alivyojitayarisha ili kukutana na ndugu yake na jinsi alivyomfikia Esau. Kwa unyenyekevu, Yakobo alimwomba Yehova msaada. Kisha, akatenda kulingana na sala yake, kwa kuchukua hatua ili atakapokutana na ndugu yake mambo yaende vizuri kadiri inavyowezekana. Ndugu hao walipokutana, Yakobo hakubishana na Esau kuhusu ni nani aliyekuwa na makosa. Lengo la Yakobo lilikuwa kufanya amani na ndugu yake. Tunaweza kuigaje mfano wa Yakobo?

JINSI JUKUHENGA AMANI NA BANGI

13-14. Anatunkosi mwamini nnzitu, tupaswa kuhenga kike?

13 Tunapoendelea kutembea katika barabara inayoongoza kwenye uzima, tunapaswa kudumisha amani pamoja na ndugu zetu. (Rom. 12:18) Tunapaswa kufanya nini tunapotambua kwamba tumemkosea mwamini mwenzetu? Kama Yakobo, tunapaswa kusali kwa Yehova kutoka moyoni. Tunaweza kumwomba abariki jitihada zetu za kufanya amani na ndugu yetu.

14 Pia, tunapaswa kutumia muda ili kujichunguza. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, niko tayari kukubali makosa, kuomba msamaha kwa unyenyekevu, na kufanya amani? Yehova na Yesu watahisije ikiwa nitachukua hatua ya kwanza ya kufanya amani pamoja na ndugu au dada yangu?’ Majibu yetu yanaweza kutuchochea tumsikilize Yesu na kwa unyenyekevu tumfikie mwamini mwenzetu ili kufanya amani. Kwa kufanya hivyo, tutakuwa tukiiga mfano wa Yakobo.

15. Kanuni jejipatikana mu Waefeso 4:2, 3 jiwesa kutujangati bo kuhenga amani nundongu jwito?

15 Hali ingekuwaje ikiwa Yakobo angeanza kubishana kwa kiburi alipokutana na ndugu yake! Huenda matokeo yangekuwa tofauti kabisa. Tunapoenda kufanya amani pamoja na ndugu yetu, tunahitaji kufanya hivyo kwa roho ya unyenyekevu. (Soma Waefeso 4:2, 3.) Methali 18:19 inasema hivi: “Ndugu aliyekosewa ni mgumu kuliko jiji lenye ngome, na kuna mizozo ambayo ni kama makomeo ya ngome.” Kuomba msamaha kwa unyenyekevu kunaweza kutusaidia tufaulu kuingia kwenye “ngome” hiyo.

16. Tupaswa kuholale ki, na kwa ndaba jakike?

16 Pia, tunahitaji kufikiria kwa makini mambo tutakayosema na jinsi tutakavyoyasema kwa ndugu yetu. Tunapokuwa tayari, tunapaswa kumfikia ndugu yetu tuliyemkosea tukiwa na lengo la kuondoa maumivu moyoni mwake. Huenda mwanzoni akasema mambo yanayoumiza. Inaweza kuwa rahisi kukasirika au kujaribu kujitetea, lakini je, kufanya hivyo kunaweza kuleta amani? Bila shaka, la! Kumbuka kwamba kufanya amani na ndugu yako ni muhimu zaidi kuliko kutafuta ni nani mwenye makosa.​—1 Kor. 6:7.

17. Guwesa kulibola ki kubokana nu mfanu guka Gilbert?

17 Ndugu anayeitwa Gilbert alijitahidi sana kufanya amani. Anasema hivi: “Sikuwa na uhusiano mzuri na mshiriki wa karibu wa familia. Kwa zaidi ya miaka miwili, nilijitahidi kuzungumza kwa unyoofu na kwa utulivu ili kurudisha tena uhusiano wetu mzuri.” Gilbert alifanya jambo gani lingine? Anasema hivi: “Kabla ya kuzungumza naye, nilisali na kujitayarisha kiakili ili nisikasirike ikiwa atasema maneno yasiyo ya fadhili. Nilihitaji kuwa tayari kusamehe. Nilijifunza kutosisitiza kwamba sina makosa, na nilielewa lengo langu lilikuwa kufanya amani.” Matokeo yalikuwa nini? Gilbert anasema hivi: “Leo, nina amani ya akili kwa sababu nina uhusiano mzuri na watu wote katika familia yangu.”

18-19. Anatunkosi mundu fulani, tupaswa kuazimi kuhenga ki, na kwa ndaba jakike?

18 Hivyo, unapaswa kuazimia kufanya nini unapotambua kwamba umemkosea Mkristo mwenzako? Fuata mwongozo wa Yesu wa kufanya amani. Sali kwa Yehova kuhusu jambo hilo, na utegemee roho yake takatifu ikusaidie kufanya amani. Kwa kufanya hivyo, utakuwa na furaha, na utathibitisha kwamba unamsikiliza Yesu.—Mt. 5:9.

19 Tunashukuru kwamba Yehova anatoa mwongozo wenye upendo kupitia “kichwa cha kutaniko,” Yesu Kristo. (Efe. 5:23) Acheni tuazimie ‘kumsikiliza’ Yesu, kama mtume Petro, Yakobo, na Yohana walivyofanya. (Mt. 17:5) Tumechunguza jinsi tunavyoweza kufanya hivyo kwa kufanya amani pamoja na Mkristo mwenzetu ambaye tumemkosea. Kwa kufanya hivyo na kuendelea kubaki katika barabara yenye nafasi ndogo inayoongoza kwenye uzima, tutapata baraka nyingi sasa na furaha ya kudumu wakati ujao.

NHAMBU 130 Uwe Mwenye Kusamehe

^ ekichweka 5 Yesu anatuhimiza tuingie kupitia lango jembamba linaloongoza kwenye barabara ya uzima. Pia, anatuamuru tufanye amani pamoja na waamini wenzetu. Huenda tukakabili changamoto gani tunapojitahidi kutumia shauri hilo, na tunaweza kuzishindaje changamoto hizo?

^ ekichweka 7 Tazama broshua Majibu ya Maswali 10 Ambayo Vijana Huuliza, swali la 6: “Nifanye Nini Ninaposhinikizwa na Vijana Wenzangu?” na kibonzo kwenye ubao Simama Imara Unaposhinikizwa na Marafiki! kwenye www.pr418.com/sw. (Tafuta kwenye MAFUNDISHO YA BIBLIA > MATINEJA.)

^ ekichweka 8 Baadhi ya majina yamebadilishwa.

^ ekichweka 56 MAELEZO YA PICHA: Kwa kuendelea kubaki katika barabara yenye “nafasi ndogo” iliyo na ulinzi wa ukingo ambao Mungu huandaa, tunaepuka hatari kama ponografia, kushirikiana na watu walio na maadili mapotovu, na kushinikizwa kutanguliza elimu ya juu maishani.

^ ekichweka 58 MAELEZO YA PICHA: Ili kufanya amani, Yakobo aliinama tena na tena mbele ya Esau, ndugu yake.