Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 51

Muendelee ‘Kumusikiliza’

Muendelee ‘Kumusikiliza’

“Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali. Mumusikilize.”​—MT. 17:5.

WIMBO 54 “Hii Ndiyo Njia”

KIFUPI YA HABARI *

1-2. (a) Mitume tatu fulani wa Yesu waliamuriwa kufanya nini, na walitenda namna gani? (b) Ni nini tutazungumuzia mu hii habari?

 KISHA pasaka ya mwaka wa 32 K.K.Y., mutume Petro, Yakobo, na Yohana waliona maono yenye kushangaza sana. Siku moja, ku mulima moja murefu, inawezekana ku chongo ya mulima Hermoni, Yesu aligeuzwa sura mbele yao. Biblia inasema hivi: “Uso wake ukangaa kama jua, na nguo zake za inje zikangaa kama mwangaza.” (Mt. 17:1-4) Karibu na mwisho wa ile maono, mitume wake walisikia sauti ya Mungu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali. Mumusikilize.” (Mt. 17:5) Maisha ya wale mitume tatu inaonyesha kama walimusikiliza Yesu. Na siye tunapenda kufuata mufano wao.

2 Mu habari yenye ilitangulia, tulijifunza kama kusikiliza sauti ya Yesu, kunamaanisha kama tunapaswa kuacha kufanya mambo fulani. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo mbili yenye Yesu alisema yenye tunapaswa kufanya.

“MUINGIE KUPITIA MULANGO MWEMBAMBA”

3. Kulingana na Matayo 7:13, 14, tunapaswa kufanya nini?

3 Soma Matayo 7:13, 14. Mu ile andiko, Yesu alionyesha kama kuko milango mbili yenye inaongoza katika barabara mbili tofauti, barabara “kubwa” na barabara ya “kidogo.” Hakuna barabara ya tatu. Tunapaswa kujichagulia siye wenyewe ni barabara gani tutapita ndani. Ile ni uamuzi wa maana sana wenye tunapaswa kukamata juu unaweza kutusaidia kupata uzima wa milele.

4. Barabara “kubwa” njo nini?

4 Hatupaswe kusahau hata kidogo tofauti zenye kuwa kati ya zile barabara mbili. Ile barabara “kubwa” iko na watu wengi juu ni mwepesi kutembea ndani. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, watu wengi wanachagua kubakia mu ile barabara na wanafuata wengine wengi wenye kutembea mu ile barabara. Wanashindwa kutambua kama ni Shetani njo iko anajaribu kukokota watu waingie mu ile barabara, barabara yenye inaongoza ku kifo.​—1 Ko. 6:9, 10; 1 Yoh. 5:19.

5. Watu fulani walifanya nini ili kupata barabara ya “kidogo” na kuanza kutembea ndani yake?

5 Tofauti na ile barabara “kubwa,” ile barabara ingine iko ya “kidogo,” na Yesu alisema kama ni watu kidogo tu njo wanaipata. Juu ya nini? Mu mustari wenye kufuata, Yesu alionya wafuasi wake juu ya manabii wa uongo. (Mt. 7:15) Kulingana na hesabu fulani, kuko maelfu ya dini, na mingi kati ya zile dini, zinasema kama zinafundishaka kweli. Juu kuko dini mingi, watu wengi wanavunjika moyo ao kuvurugika, na ile inafanya hata wasitafute barabara yenye inaongoza kwenye uzima. Lakini kusema kweli, mutu anaweza kupata ile barabara. Yesu alisemaa hivi: “Kama munakaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, na mutajua kweli, na kweli itawaweka ninyi huru.” (Yoh. 8:31, 32) Tunafurahi kuona kama weye haukufuata wale watu wengi, lakini ulitafuta njo kweli. Ulianza kujifunza sana Neno ya Mungu ili kujua mambo yenye unapaswa kufanya, na ulisikiliza mafundisho ya Yesu. Kati ya ile mambo yenye ulisikiliza, ulijifunza kama Yehova anatazamia tukatale mafundisho ya dini ya uongo na kuacha kusherehekea sikukuu zao zenye ni za kipagani na hata kufanya matendo yao ya mubaya. Tena, ulijifunza kama haiko mwepesi kufanya mambo yenye Yehova anatuomba tufanye na kuachana kabisa na matendo yote yenye inapingana na sheria yake. (Mt. 10:34-36) Pengine haikukuwa mwepesi kwako kuachana na ile mambo yote ya mubaya. Hata vile, ulivumilia juu unamupenda baba yako wa mbinguni, na unapenda kukubaliwa naye. Anapaswa kufurahi sana juu ya ile!​—Mez. 27:11.

NAMNA UNAWEZA KUBAKIA MU BARABARA YA KIDOGO

Mashauri ya Mungu na kanuni zake zinatusaidia kubakia katika barabara ya “kidogo” (Ona fungu ya 6-8) *

6. Kulingana na Zaburi ya 119:9, 10, 45, 133, ni nini inaweza kusaidia mutu abakie mu barabara ya kidogo?

6 Kama tu mutu anaanza kutembea ndani ya barabara ya kidogo, ni nini inaweza kumusaidia abakie mule? Fikiria mufano wenye kufuata. Mu inchi fulani, kunakuwaka kitu fulani yenye kufanana na lupango yenye inakuwaka pembeni-pembeni ya barabara yenye kuwa chini ya mulima. Ile lupango inalinda shofere na gari. Ile lupango inatayarishwa ili kulinda shofere wasikuwe karibu-karibu sana na barabara ao wasitoke inje ya barabara. Shorefe wengi hawakuwake wanasema-sema kama ile lupango iko ya mubaya ao inawafunga-funga, hapana! Kanuni za Yehova zenye kuwa mu Biblia ziko kama ile lupango. Kanuni zake zinatusaidia kubakia mu barabara ya kidogo.​—Soma Zaburi 119:9, 10, 45, 133.

7. Vijana wanapaswa kuona namna gani barabara ya kidogo?

7 Vijana, wakati fulani munawazaka kama kanuni za Yehova zinawafunga-funga? Njo vile Shetani anapenda muwaze. Anapenda mukaze akili yenu juu ya mambo yenye wale wenye kuwa mu barabara kubwa wako wanafanya na juu ya wakati wa muzuri wenye inaonekana wako wanapitisha. Anaweza kutumia mambo yenye wanafunzi wenzenu wako wanafanya ku masomo, ao mambo yenye munaangalia ku Enternete, juu ya kufanya muwaze kama kuko kitu fulani ya muzuri munakosa. Shetani anapenda muwaze kama kanuni za Yehova ziko zinawafunga-funga ili musifurahie kabisa maisha. * Lakini musisahau hii jambo: Shetani hapendi wale wenye wako mu barabara yake wajue mambo yenye inawachunga kule mwisho. Lakini Yehova yeye, anapenda mujue kama kuko maisha ya muzuri sana yenye iko nawachunga kule mbele, kama munabakia mu barabara ya uzima.​—Zb. 37:29; Isa. 35:5, 6; 65:21-23.

8. Vijana wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wa Olaf?

8 Ona mambo yenye unaweza kujifunza kupitia mufano wa kijana mwenye kuitwa Olaf. * Marafiki wake walimukaza afanye ngono pamoja nao. Wakati aliwafasiria kama Mashahidi wa Yehova wanaishi kulingana na kanuni za juu za mwenendo, vijana fulani wanamuke wa ku masomo yao walitumia ile nafasi ili kumusadikisha alale nao. Lakini Olaf alishikamana na mambo yenye kuwa sawa. Na haiko ile tu njo jaribu alipata. Olaf anasema hivi: “Walimu wangu walijaribu kunifanya niamini kama kusoma masomo ya juu njo itafanya watu waniheshimie. Waliniambia kama ikiwa sifanye vile, singekuwa na furaha mu maisha.” Ni nini ilimusaidia Olaf apambane na ile majaribu? Anasema tena hivi: “Nilijikaza ili nikuwe na urafiki wa karibu sana na ndugu na dada wa mu kutaniko yangu. Walikuwa kama familia yangu. Tena nilianza kujifunza Biblia sana. Kadiri nilijifunza sana, ni vile nilifikia kuanza kuamini kama ile njo kweli. Na ile ilinisaidia nibatizwe na kuendelea kumutumikia Yehova.”

9. Ni nini inaombwa kwa wale wenye wanapenda kubakia mu barabara ya kidogo?

9 Shetani anapenda weye utoke mu barabara yenye inaongoza kwenye uzima. Anapenda uunge mukono wale watu wengi wenye kuwa mu ile barabara kubwa “yenye kuongoza kwenye uharibifu.” (Mt. 7:13) Lakini, kama tunaendelea kumusikiliza Yesu na kuona ile barabara ya kidogo kuwa ulinzi, ile itatusaidia kubakia kabisa mu ile barabara ya kidogo. Sasa, muache tuzungumuzie jambo ingine yenye Yesu alisema yenye tunapaswa kufanya.

FANYA AMANI PAMOJA NA NDUGU YAKO

10. Kulingana na Matayo 5:23, 24, Yesu alisema tunapaswa kufanya jambo gani?

10 Soma Matayo 5:23, 24. Yesu alizungumuzia hali moja, yenye ilikuwa ya maana sana kwa waabudu Wayahudi, wenye walikuwa wanamusikiliza. Waza, mutu fulani iko ku hekalu na iko karibu kutoa zabihu ya munyama kwa kuhani. Sasa kama ile wakati anakumbuka kama kuko ndugu yake mwenye iko na jambo fulani juu yake, alipaswa kuacha ile zabihu yake pale na ‘kuenda.’ Juu ya nini? Kuko kitu ya maana zaidi kuliko kumutolea Yehova zabihu? Yesu alisema waziwazi hivi: “Fanya kwanza amani na ndugu yako.”

Je, uko tayari kuiga mufano wa Yakobo, mwenye alijikaza kwa unyenyekevu wote kufanya amani pamoja na ndugu yake? (Ona fungu ya 11-12) *

11. Fasiria mambo yenye Yakobo alifanya ili kufanya amani na Esau.

11 Tunaweza kujifunza somo za muzuri sana kuhusu namna ya kufanya amani kwa kuchunguza mambo yenye ilitokea mu maisha ya Yakobo. Kisha kufanya miaka 20 hivi inje ya inchi yao ya kizalikio, Mungu alimuamuru Yakobo kupitia malaika, arudie kwao. (Mwa. 31:11, 13, 38) Lakini kulikuwa tatizo. Ndugu yake mukubwa, Esau, alikuwa anapenda kumuua. (Mwa. 27:41) Yakobo ‘aliogopa sana na alikuwa na wasiwasi’ juu pengine ndugu yake alikuwa angali na kinyongo kumuelekea yeye. (Mwa. 32:7) Yakobo alifanya nini ili kufanya amani pamoja na ndugu yake? Kwanza, alisali sana kwa Yehova juu ya ile jambo. Kisha, alimutumia Esau zawadi moja ya muzuri. (Mwa. 32:9-15) Ku mwisho, wakati walionana uso kwa uso, Yakobo alikamata hatua ya kumuonyesha heshima Esau. Aliinama mbele yake, hapana tu mara moja ao mara mbili, lakini mara saba! Juu Yakobo alionyesha kuwa alikuwa munyenyekevu na mwenye heshima, ile ilisaidia afanye amani na ndugu yake.​—Mwa. 33:3, 4.

12. Mufano wa Yakobo unatufundisha nini?

12 Namna Yakobo alijitayarisha ili kukutana na ndugu yake Esau inaweza kutufundisha jambo fulani. Kwa unyenyekevu wote, Yakobo alimuomba Yehova musaada. Kisha kutoa sala, alitenda kulingana na sala yake, kwa kufanya yake yote ili kufanya amani pamoja na ndugu yake. Wakati wote wawili walikutana, Yakobo hakubishana-bishana na Esau juu ya kujua mwenye alikuwa na kosa na mwenye hakukuwa na kosa. Kusudi ya Yakobo ilikuwa kufanya amani na ndugu yake. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Yakobo?

NAMNA YA KUFANYA AMANI NA WENGINE

13-14. Tunapaswa kufanya nini kama tunakosea muamini mwenzetu?

13 Siye wenye tuko tunatembea mu barabara yenye kuongoza kwenye uzima, tunapenda kuishi kwa amani pamoja na ndugu zetu. (Ro. 12:18) Tunaweza kufanya nini wakati tunatambua kama tulikosea muamini mwenzetu? Sawa vile Yakobo, tunapaswa kusali kwa Yehova. Tunaweza kumuomba abariki bidii yenye tutaonyesha ili kufanya amani pamoja na ndugu yetu.

14 Tena, tunapaswa kukamata wakati wa kujichunguza siye wenyewe. Tunaweza kujiuliza maulizo sawa vile: ‘Je, niko tayari kutia kiburi yangu pembeni, kuomba musamaha kwa unyenyekevu, na kufanya amani? Yehova na Yesu, watasikia namna gani wakati nakamata hatua ya kufanya amani pamoja na ndugu ao dada yangu?’ Majibu yetu ku ile maulizo, inaweza kutuchochea kumusikiliza Yesu na kumukaribia muamini mwenzetu kwa unyenyekevu wote, ili tu kufanya amani. Kuhusu ile jambo, Yakobo ni mufano muzuri wenye tunaweza kufuata.

15. Namna gani kutumikisha kanuni yenye kuwa mu Waefeso 4:2, 3 inaweza kutusaidia kufanya amani pamoja na ndugu ao dada yetu?

15 Waza, kama Yakobo angeonyesha kiburi wakati alikutana na ndugu yake! Mambo ingekuwa mubaya sana, haiko vile? Wakati tunaenda kumuona ndugu ao dada yetu juu ya kuzungumuzia tatizo yenye ilitokea kati yake na siye, tunapaswa kuwa na roho ya unyenyekevu. (Soma Waefeso 4:2, 3.) Mezali 18:19 inasema: “Ndugu mwenye wamekosea ni mugumu kuliko muji wenye ngome, na kuko mabishano yenye kuwa kama mapingo ya ngome.” Ndugu mwenye wamekosea iko sawa ile “ngome.” Lakini wakati tunaomba musamaha, ile inaweza kumusaidia akuwe tayari kufanya amani pamoja na siye.

16. Ni jambo gani tunapaswa kufikiria kwa uzito, na juu ya nini?

16 Tunapaswa pia kufikiria kwa uzito mambo tutasema na ndugu yetu na namna tutaisema. Wakati tuko tayari, tunapaswa kumuona mwenye tulikosea, lakini tukiwa na kusudi ya kumaliza ile tatizo yenye kuwa kati yake na siye. Pengine ku mwanzo anaweza kusema maneno yenye itafanya tujisikie mubaya. Inaweza kuwa mwepesi kukasirika ao kujaribu kujitetea. Lakini kufanya vile kutatusaidia kabisa kurudisha amani? Hapana. Tusisahau kama kurudisha amani kati yetu na ndugu yetu, njo jambo ya maana sana kuliko kujaribu kujua nani njo iko na kosa na nani njo hana kosa.​—1 Ko. 6:7.

17. Mufano wa Gilbert unaweza kutufundisha nini?

17 Ndugu Gilbert alifanya yake yote ili kuwa mufanya-amani. Anasema hivi: “Sikuanza kupatana kabisa na mutu fulani wa familia yangu ya karibu. Kwa zaidi ya miaka mbili, nilifanya yangu yote ili kuongea naye waziwazi na kwa utulivu juu ya kurudisha uhusiano wangu pamoja naye.” Lakini Gilbert alifanya nini ingine? Anasema hivi: “Mbele ya kuzungumuza na ule mutu wa familia yangu, nilisali na kujitayarisha kiakili juu nisikasirike kama anasema jambo fulani ya mubaya kunihusu. Nilipaswa kuwa tayari kusamehe. Nilijifunza kupigania hapana haki zangu, na nilielewa kama daraka yangu ni kufanya amani.” Ile ilikuwa na matokeo gani? Gilbert anasema tena hivi: “Leo, niko na amani ya akili, juu niko na uhusiano wa muzuri pamoja na watu wote wa familia yangu.”

18-19. Kama tulikosea mutu fulani, tunapaswa kuwa na azimio gani, na juu ya nini?

18 Sasa, tunapaswa kuwa na azimio gani wakati tunatambua kama tulikosea ndugu yetu Mukristo? Tunapaswa kufuata muongozo wa Yesu kuhusu kufanya amani. Tunapaswa kuzungumuza na Yehova juu ya ile jambo, na kutegemea roho yake takatifu ili itusaidie tukuwe wafanya-amani. Kama tunafanya vile, tutakuwa na furaha, na ile itaonyesha pia kama tuko tunamusikiliza Yesu.​—Mt. 5:9.

19 Tuko wenye shukrani sana kwa Yehova juu anatupatia muongozo wa upendo kupitia “kichwa cha kutaniko,” ni kusema, Yesu kristo. (Efe. 5:23) Muache tuazimie ‘kumusikiliza Yesu’ sawa tu vile Petro, Yakobo, na Yohana walifanya. (Mt. 17:5) Tumezungumuzia namna tunaweza kufanya ili kurudisha amani kati yetu na ndugu yetu Mukristo mwenye tulikosea. Kama tunafuata ile mashauri na tunabakia katika barabara ya kidogo yenye kuongoza kwenye uzima, tutapata baraka mingi tangu sasa na furaha ya milele na milele wakati wenye kuja.

WIMBO 130 Tusameheane

^ Yesu anatuomba kupitia kwenye mulango mwembamba wenye unaongoza kwenye barabara ya uzima. Tena, anatuomba tufanye amani pamoja na waamini wenzetu. Ni magumu gani tunaweza kupata wakati tuko tunajikaza kufuata ile shauri, na namna gani tunaweza kushinda ile magumu?

^ Ona ulizo ya 6 ya broshua Majibu ya Maulizo 10 Yenye Vijana Wanajiulizaka,Nifanye Nini Kama Wenzangu Wananikaza Kufanya Jambo Fulani?” na picha kwenye ubao Usikubali Marafiki Wakudanganye! yenye kuwa ku www.pr418.com. (Ona sehemu MAFUNDISHO YA BIBLIA > VIJANA.)

^ Majina fulani imebadilishwa.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Kama tunabakia katika barabara ya “kidogo” yenye kulindwa na lupango ya mufano yenye Mungu anatoa, tutaepuka hatari mbalimbali, sawa vile pornografia, marafiki wabaya, na mikazo ya watu wengine wenye kutuchochea kusoma sana katika maisha.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Juu alipenda kufanya amani, Yakobo aliinama mara mingi mbele ya ndugu yake Esau.