Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JI LIFUNZU 7

“Pelakania Malobi ga Babi na Hekima”

“Pelakania Malobi ga Babi na Hekima”

“Tega likutu laku gupelakania malobi ga babi na hekima.”​—MET. 22:17.

NHAMBU 123 Kutii Utaratibu wa Kitheokrasi kwa Ushikamanifu

MUHTASARI *

1. Tuwesa kushauliwa kwi indela bole, na kwa ndaba jaki twe twaboa tuhitaji kushauliwa?

 PINDI kwa pindi, sisi sote tunahitaji shauri. Nyakati fulani huenda sisi wenyewe tukachukua hatua ya kwanza ili kuomba ushauri kwa mtu fulani tunayemheshimu. Katika visa vingine, huenda ndugu anayetujali akatufikia na kutuambia kwamba tunakaribia kuchukua “hatua isiyofaa” ambayo tutaijutia. (Gal. 6:1) Pia, huenda tukapata shauri mtu fulani anapoturekebisha baada ya kufanya kosa zito. Haidhuru njia tunayopata shauri, tunapaswa kusikiliza. Tukifanya hivyo tutanufaika na tunaweza kuokoa uhai wetu!​—Met. 6:23.

2. Kulengana na Methali 12:15 na maelesu ga pai, kwa ndaba jaki tupaswa kupelakane lishaule?

2 Andiko letu la msingi linatutia moyo ‘tusikilize maneno ya wenye hekima.’ (Met. 22:17) Hakuna mwanadamu anayejua kila kitu; sikuzote kuna mtu ambaye ana ujuzi au uzoefu mwingi kuliko sisi. (Soma Methali 12:15 na maelezo ya chini.) Hivyo, tunaposikiliza ushauri tunaonyesha kwamba sisi ni wanyenyekevu. Kufanya hivyo kunaonyesha tunatambua kwamba tumepungukiwa; na kwamba tunahitaji msaada ili kufikia malengo yetu. Mfalme Sulemani mwenye hekima aliandika hivi kwa mwongozo wa roho: “Mambo hufanikiwa kupitia washauri wengi.”​—Met.  15:22.

Ni njia ipi kati ya njia hizi mbili za kushauriwa ambayo ni ngumu zaidi kwako kukubali? (Tazama fungu la 3 na 4)

3. Pangi tuwesa kujopa lishauli kupete indela bole?

3 Huenda tukashauriwa moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja. Tunamaanisha nini tunaposema kwa njia isiyo ya moja kwa moja? Huenda tukasoma jambo fulani kwenye Biblia au mojawapo ya machapisho yetu, linaloweza kutufanya tutue na kufikiria kuhusu hatua fulani tunayotaka kuchukua, na kutuchochea kurekebisha mwenendo wetu. (Ebr. 4:12) Hilo ni shauri lisilo la moja kwa moja. Tunamaanisha nini tunaposema shauri la moja kwa moja? Mzee wa kutaniko au ndugu mwingine anayestahili anaweza kutuambia jambo fulani tunalohitaji kufanyia kazi. Hilo ni shauri la moja kwa moja. Ikiwa mtu anatupenda sana hivi kwamba anatupatia shauri linalotegemea Biblia, tunapaswa kuonyesha uthamini kwa kusikiliza jambo analotuambia na kutumia shauri hilo.

4. Kulengana na Muhubiri 7:9, tupaswa kuhenga ki patupata lishaule?

4 Ukweli ni kwamba huenda ikawa vigumu hasa kukubali shauri la moja kwa moja. Hata tunaweza kukasirika. Kwa nini? Ingawa tunakubali kwamba sisi si wakamilifu, huenda ikawa changamoto kukubali shauri mtu anapotaja kihususa udhaifu fulani tulio nao. (Soma Mhubiri 7:9.) Tunaweza kujitetea, kutilia shaka nia ya mtu anayetushauri, au kukasirishwa na njia aliyotupatia shauri. Hata tunaweza kumchambua mtu aliyetushauri kwa kujiambia: ‘Ana haki gani ya kunishauri mimi? Yeye pia ana mapungufu yake!’ Mwishowe, ikiwa hatukubaliani na shauri, huenda tukalipuuza au kutafuta shauri lingine tunalokubaliana nalo.

5. Musitusungusa ki mumakala jenzeno?

5 Katika makala hii, tutazungumzia mifano ya Kimaandiko ya wale waliokataa shauri na wale waliokubali shauri. Pia, tutachunguza mambo yanayoweza kutusaidia kukubali shauri na kunufaika nalo.

BA AKANAJE LISHAULI

6. Tulibola ki kubokana na jinsi Mfalme Rehoboamu ejwajetakya lishaule?

6 Fikiria mfano wa Rehoboamu. Alipoanza kutawala akiwa mfalme wa Israeli, watu wake walienda kumwomba jambo fulani. Walimwomba awapunguzie masharti mazito ambayo Sulemani, baba yake, alikuwa amewawekea. Inapendeza kwamba Rehoboamu alishauriana na wanaume wazee wa Israeli ili kuona jinsi ambavyo angewajibu watu hao. Wanaume wazee walimshauri mfalme kwamba ikiwa angefanya jambo ambalo watu walikuwa wamemwomba, sikuzote wangemuunga mkono. (1 Fal. 12:3-7) Rehoboamu hakuridhika na ushauri huo aliopewa, hivyo alitafuta ushauri kutoka kwa wanaume wa rika lake. Inaelekea wanaume hao walikuwa na umri wa miaka 40 hivi, hivyo walikuwa na kiasi fulani cha uzoefu maishani. (2 Nya. 12:13) Lakini katika pindi hiyo, walimpa Rehoboamu ushauri mbaya. Walimshauri awaongezee watu masharti mazito zaidi. (2 Fal. 12:8-11) Kwa kuwa Rehoboamu alikuwa amepata maoni kutoka vyanzo viwili tofauti, angeweza kusali kwa Yehova na kumuuliza afuate ushauri gani. Badala yake, aliamua kukubali ushauri uliokuwa unamfurahisha yeye na akawasikiliza wanaume vijana. Matokeo yalikuwa mabaya sana kwa Rehoboamu na watu wa Israeli. Sisi pia, nyakati fulani huenda tusikubaliane na ushauri tunaopewa. Hata hivyo, ikiwa ushauri huo unategemea Neno la Mungu tunapaswa kuukubali.

7. Mfanu guka Mfalme Uzia gutupundisa kike?

7 Mfalme Uzia alikataa kusikiliza shauri. Aliingia sehemu ya hekalu ambayo makuhani pekee ndio walioruhusiwa kuingia, naye akajaribu kufukiza uvumba. Makuhani wa Yehova walimwambia hivi: “Si vyema kwako, Uzia, kumfukizia Yehova uvumba! Ni makuhani tu wanaopaswa kufukiza uvumba.” Uzia aliitikiaje? Ikiwa angekubali shauri kwa unyenyekevu na kuondoka haraka hekaluni, huenda Yehova angemsamehe. Badala yake, “Uzia . . . akawaka hasira.” Kwa nini alikataa kusikiliza shauri hilo? Inaonekana alihisi kwamba kwa kuwa yeye ni mfalme, angeweza kufanya chochote alichotaka. Lakini Yehova hakuhisi hivyo. Kwa sababu ya kimbelembele chake, Uzia alipigwa na ukoma naye “[akaendelea] kuwa na ukoma mpaka siku aliyokufa.” (2 Nya. 26:16-21) Mfano wa Uzia unatufundisha kwamba haidhuru sisi ni nani, ikiwa tutakataa shauri linalotegemea Biblia, tutapoteza kibali cha Yehova.

BAJETAKYA LISHAULI

8. Ayubu jwajetakya bo lishaule?

8 Tofauti na mifano ya kuonya ambayo tumetoka tu kuzungumzia, Biblia ina mifano mizuri ya wale ambao walibarikiwa kwa sababu walisikiliza shauri. Mfikirie Ayubu. Ingawa alikuwa anamwogopa Mungu, hakuwa mkamilifu. Kwa sababu ya mkazo mkali, alisema maneno yasiyo sahihi. Matokeo ni kwamba alipewa shauri la moja kwa moja, kutoka kwa Elihu na kutoka kwa Yehova. Ayubu aliitikiaje? Kwa unyenyekevu, alisikiliza ushauri. Alisema hivi: “[Nilizungumza], lakini sikuwa na uelewaji . . . ninabatilisha niliyosema, nami ninatubu katika mavumbi na majivu.” Yehova alimbariki Ayubu kwa sababu alikuwa mnyenyekevu.​—Ayu. 42:3-6, 12-17.

9. Musa jutubekila mfanu bo gwasapi pakuhusu kujetake lishaule?

9 Musa ni mfano mzuri wa mtu ambaye alikubali kurekebishwa baada ya kufanya kosa zito. Pindi moja, alilemewa na hasira naye akakosa kumpa heshima Yehova. Kwa sababu hiyo, Musa alipoteza pendeleo la kuingia katika Nchi ya Ahadi. (Hes. 20:1-13) Musa alipoeleza jinsi alivyovunjika moyo kwa sababu ya uamuzi huo, Yehova alimwambia hivi: “Usizungumze nami tena kamwe kuhusu jambo hili.” (Kum. 3:23-27) Musa hakukasirika. Badala yake, alikubaliana na uamuzi wa Yehova, naye Yehova akaendelea kumtumia kuwaongoza Waisraeli. (Kum. 4:1) Ayubu na Musa walituwekea mfano mzuri ambao tunapaswa kuiga kuhusu kusikiliza shauri. Ayubu alirekebisha maoni yake, hakujitetea. Musa alionyesha kwamba alikubali shauri la Yehova kwa kuendelea kuwa mwaminifu hata baada ya kupoteza pendeleo alilothamini sana.

10. (a) Methali 4:10-13 jipwaga ki kuhusu faida jukujetake lishaule? (b) Baazi jaka ndugu na dada awesiki bo kulangi ntazamu gwasapi kuhusu lishaule leapatike?

10 Tunanufaika tunapoiga mifano iliyowekwa na wanaume waaminifu kama vile Ayubu na Musa. (Soma Methali 4:10-13.) Ndugu na dada zetu wengi wamefanya hivyo. Fikiria kile ambacho ndugu anayeitwa Emmanuel, anayeishi nchini Kongo, anasema kuhusu onyo alilopewa: “Ndugu wakomavu katika kutaniko letu waliona kwamba nilikuwa karibu kuharibu uhusiano wangu pamoja na Yehova, nao wakaja kunisaidia. Nilitumia shauri lao na kufanya hivyo kulinisaidia kuepuka matatizo mengi.” * Painia anayeitwa Megan, kutoka Kanada, anasema hivi kuhusu shauri: “Mara nyingine si jambo ninalotaka kusikia, lakini ndilo jambo ninalohitaji kusikia.” Na ndugu kutoka Kroatia anayeitwa Marko anasema hivi: “Nilipoteza pendeleo langu, lakini ninapokumbuka wakati huo, ninatambua kwamba shauri nililopata lilinisaidia kuimarisha tena hali yangu ya kiroho.”

11. Ndugu Karl Klein jwapwaga ki kuhusu kujetake lishaule?

11 Mfano mwingine wa mtu aliyenufaika kwa sababu ya kukubali shauri ni Ndugu Karl Klein, ambaye alitumikia akiwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza. Katika simulizi lake la maisha, Ndugu Klein alisimulia kuhusu pindi ambayo alipewa shauri zito na Joseph F. Rutherford aliyekuwa rafiki yake wa karibu. Ndugu Klein anakiri kwamba mwanzoni hakuitikia vizuri shauri hilo. Alisema hivi: “Tulipoonana tena, [Ndugu Rutherford] alinisalimia hivi kwa shauku, ‘Hujambo Karl!’ Kwa kuwa bado nilikuwa na uchungu, nilimjibu kwa sauti ya chini. Akaniambia hivi: ‘Karl uwe mwangalifu! Ibilisi anakuwinda!’ Nikiwa nimeaibika, nilijibu hivi: ‘Ah, hakuna tatizo Ndugu Rutherford.’ Lakini alijua nimekasirika, basi akarudia tena onyo lake, ‘Ni sawa. Lakini uwe mwangalifu. Ibilisi anakuwinda.’ Alikuwa sahihi kabisa! Tukiwa na kinyongo kumwelekea ndugu yetu, hasa anaposema jambo analopaswa kusema . . . , inakuwa rahisi kwa Ibilisi kutunasa.” * (Efe. 4:25-27) Ndugu Klein alikubali shauri la Ndugu Rutherford, na wakaendelea kuwa marafiki wa karibu.

KI SEKIWESA KUTUJANGATI KUJETAKE LISHAULE?

12. Unyenyekevu guwesa kutujangatibo kujetake lishaule? (Zaburi 141:5)

12 Ni nini kinachoweza kutusaidia kukubali shauri? Tunahitaji kuwa wanyenyekevu na kukumbuka kwamba sisi si wakamilifu na nyakati nyingine tunaweza kutenda kipumbavu. Kama tulivyozungumzia katika mafungu yaliyotangulia, Ayubu alikuwa na maoni yasiyo sahihi. Lakini baadaye, alirekebisha njia yake ya kufikiri na Yehova alimbariki kwa kufanya hivyo. Kwa nini? Kwa sababu Ayubu alikuwa mnyenyekevu. Alithibitisha unyenyekevu wake kwa kukubali shauri ambalo alipewa na Elihu, hata ingawa Elihu alikuwa na umri mdogo sana kuliko Ayubu. (Ayu. 32:6, 7) Unyenyekevu utatusaidia sisi pia kukubali shauri, hata tunapohisi kwamba hatukustahili kupewa shauri hilo au ikiwa yule anayetushauri ana umri mdogo kuliko sisi. Mzee fulani wa kutaniko kutoka Kanada anasema hivi: “Kwa kuwa hatujioni kama wengine wanavyotuona, tunawezaje kufanya maendeleo ikiwa hakuna mtu anayetushauri?” Ni nani miongoni mwetu ambaye hahitaji kufanya maendeleo katika kusitawisha sifa za tunda la roho na katika kutimiza huduma yetu ya Kikristo?​—Soma Zaburi 141:5.

13. Tupaswa kulibonabo lishauli letupata?

13 Ona shauri kuwa wonyesho wa upendo wa Mungu. Yehova anatutakia mema. (Met. 4:20-22) Anapotushauri kupitia Neno lake, machapisho yanayotegemea Biblia, au mwamini mwenzetu mkomavu, anatuonyesha kwamba anatupenda. Andiko la Waebrania 12:9, 10 linasema: “Yeye hufanya hivyo kwa faida yetu.”

14. Tupaswa kukazi fikila ki patupata lishaule?

14 Kazia fikira shauri, si jinsi linavyotolewa. Nyakati nyingine, huenda tukahisi kwamba shauri tulilopewa halikutolewa kwa njia nzuri. Bila shaka, yule anayetoa shauri anapaswa kujitahidi kulitoa kwa njia ambayo itakuwa rahisi kwa mtu mwingine kulikubali. * (Gal. 6:1) Lakini ikiwa sisi ndio tunaoshauriwa, tunapaswa kukazia fikira ujumbe ulio katika shauri hilo, hata ikiwa tunahisi kwamba lingetolewa kwa njia bora zaidi. Huenda tukajiuliza: ‘Hata ikiwa sikubaliani na njia ambayo shauri hilo lilitolewa, je, kuna ukweli wowote katika mambo yaliyosemwa? Je, ninaweza kuepuka kukazia fikira udhaifu wa yule anayenishauri ili ninufaike na shauri hilo?’ Tutakuwa wenye hekima ikiwa tutafikiria jinsi tunavyoweza kunufaika kutokana na shauri lolote tunalopewa.​—Met. 15:31.

LOBA USHAULI NA NDO PAGWINUFAIKA

15. Kwa ndaba jaki tupaswa kuloba ushaule?

15 Biblia inatuhimiza tuombe ushauri. Methali 13:10 inasema: “Hekima ni ya wale wanaotafuta ushauri.” Maneno hayo ni ya kweli kabisa! Wale wanaoomba ushauri badala ya kusubiri mtu fulani aje kuwashauri, mara nyingi wanafanya maendeleo makubwa zaidi ya kiroho kuliko wale ambao hawatafuti ushauri. Hivyo, chukua hatua ya kwanza ya kuomba ushauri.

Kwa nini dada huyu kijana anamwomba dada mkomavu ushauri? (Tazama fungu la 16)

16. Tuwesa kuloba ushauli patukuba katika hali bole?

16 Ni pindi gani ambazo huenda tukaomba ushauri kutoka kwa mwamini mwenzetu? Fikiria hali hizi. (1) Dada fulani anamwomba mhubiri mwenye uzoefu ajiunge naye anapoongoza funzo la Biblia na baadaye anamwomba amshauri jinsi anavyoweza kuboresha njia yake ya kufundisha. (2) Dada mseja anataka kununua suruali ndefu, hivyo anamwomba dada mkomavu atoe maoni yake kuhusu suruali hiyo. (3) Ndugu amepewa mgawo wake wa kwanza wa kutoa hotuba ya watu wote. Anamwomba msemaji mzoefu asikilize kwa makini hotuba yake na ampe ushauri hususa wa jinsi anavyoweza kuiboresha. Ni vizuri hata kwa ndugu ambao wametoa hotuba kwa miaka mingi kuomba ushauri kama huo kutoka kwa wasemaji wenye uzoefu na kisha kutumia ushauri huo.

17. Tuwesa kunufaikabo kutokana nilishaule?

17 Katika majuma au miezi ijayo, sisi sote tutapata shauri iwe ni la moja kwa moja, au lisilo la moja kwa moja. Hilo likitokea, kumbuka mambo ambayo tumezungumzia. Endelea kuwa mnyenyekevu. Kazia fikira ujumbe ulio katika shauri, na si jinsi shauri lilivyotolewa. Na utumie shauri ulilopewa. Hakuna yeyote miongoni mwetu anayezaliwa akiwa na hekima. Lakini ‘tunaposikiliza mashauri na kukubali nidhamu,’ Neno la Mungu linatuahidi kwamba ‘tutakuwa na hekima.’​—Met. 19:20.

NHAMBU 124 Washikamanifu Sikuzote

^ Watu wa Yehova wanatambua umuhimu wa kusikiliza shauri linalotegemea Biblia. Wakati huohuo si rahisi sikuzote kukubali shauri. Kwa nini? Na ni nini kitakachotusaidia tunufaike kutokana na ushauri tunaopata?

^ Baadhi ya majina yamebadilishwa.

^ Katika makala inayofuata, tutazungumzia jinsi wale wanaotoa shauri wanavyoweza kufanya hivyo kwa njia ya busara.