Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 9

Uige Yesu kwa Kuwa Tayari Kutumikia Wengine

Uige Yesu kwa Kuwa Tayari Kutumikia Wengine

“Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”​—MDO. 20:35.

WIMBO 17 “Ninataka”

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni roho gani ya muzuri tunaona kati ya watu wa Yehova?

TANGU zamani, Biblia ilitabiri kama watu wa Mungu ‘wangejitoa kwa kujipendea’ mu utumishi wa Yehova chini ya muongozo wa Mwana wake. (Zb. 110:3) Ile unabii iko inatimia kabisa leo. Kila mwaka, watumishi wa Yehova wako wanapitisha mamilioni ya saa mu kazi ya kuhubiri. Wanafanya vile kwa kujipendea bila kulipwa. Wanakamata pia wakati ili kusaidia ndugu zao wapate mambo yenye wako nayo lazima, kuwatia moyo, na ili kutia nguvu imani yao katika Yehova. Wazee na watumishi wa huduma wanapitisha saa ya mingi ili kutayarisha sehemu mbalimbali za mikutano na ili kufanya kazi ya uchungaji. Juu ya nini watu wa Yehova wanafanya ile kazi yote? Ni juu wanamupenda Yehova na wanapenda majirani wao.​—Mt. 22:37-39.

2. Sawa vile inaonyeshwa mu Waroma 15:1-3, Yesu alituwekea mufano gani?

2 Yesu alionyesha kama alihangaikia sana mahitaji ya wengine kuliko yake. Tuko tunajikaza kufanya yetu yote ili kufuata hatua zake. (Soma Waroma 15:1-3.) Wale wenye kufuata mufano wake watapata faida mingi. Yesu alisema: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”​—Mdo. 20:35.

3. Tutazungumuzia mambo gani mu hii habari?

3 Mu hii habari, tutajikumbusha mambo fulani yenye Yesu alifanya ili kutumikia wengine na tutazungumuzia namna tunaweza kuiga mufano wake. Tutazungumuzia pia namna tunaweza kuwa kabisa tayari ili kutumikia wengine.

UIGE MUFANO WA YESU

Hata kama alikuwa alishachoka, Yesu alifanya nini wakati watu wengi walikuya kumuona? (Ona fungu ya 4)

4. Namna gani Yesu alihangaikia mahitaji ya wengine kuliko yake?

4Yesu alisaidia wengine hata kama alikuwa mwenye kuchoka. Fikiria mambo yenye Yesu alifanya wakati watu wengi walikuya kumuona ku mulima, inawezekana karibu na Kapernaumu. Yesu alikuwa amepitisha usiku wote na iko anasali. Yesu alipaswa kuwa mwenye kuchoka sana. Lakini wakati aliona watu wengi wanakuya kumuona, alisikilia huruma maskini na wagonjwa wenye walikuwa kati yao. Hakuponyesha tu wagonjwa, lakini pia alitoa moya kati ya hotuba zenye kutia moyo sana: Mahubiri ya kwenye Mulima.​—Lu. 6:12-20.

Ni mu njia gani tunaweza kuiga roho ya Yesu ya kujitolea mu maisha yetu? (Ona fungu ya 5)

5. Namna gani vichwa ya familia wanaiga Yesu wakati walishachoka?

5Namna vichwa ya familia wanaiga Yesu. Fikiria hii mufano: Kisha kutumika muchana yote muzima, kichwa ya familia anarudia ku nyumba na anachoka sana. Yeye na familia yake wako na programu ya kufanya ibada ya familia ile mangaribi. Pengine anapenda waifanye siku ingine, lakini anamuomba Yehova amupatie nguvu ya kuongoza ile ibada. Yehova anajibia sala yake na funzo inafanyika kama kawaida. Watoto wanajifunza jambo moya ya maana sana ile mangaribi: Kwa wazazi wao, mambo ya kiroho njo ya maana sana kuliko mambo yote.

6. Leta mufano wenye kuonyesha namna Yesu alitumia wakati wake ili kusaidia wengine.

6Yesu alipitisha wakati na wengine hata saa alipenda kuwa yeye peke. Unaweza kufikiria namna Yesu alijisikia wakati alipata habari kama rafiki yake Yohana Mubatizaji aliuawa? Yesu alipaswa kuhuzunika sana. Biblia inasema: “Wakati Yesu alisikia habari [kuhusu kifo ya Yohana], akaenda mahali kwenye hakuna watu ili akuwe peke yake.” (Mt. 14:10-13) Tunaweza kuelewa juu ya nini alipenda kuwa yeye peke. Watu fulani wanapendaka kulia na wako fasi yao, wao peke. Lakini Yesu yeye, hakuweza kufanya vile juu alipata kizuizi. Tayari watu wengi walikuwa walishafika fasi kwenye angekuwa yeye peke. Alifanya nini? Alihangaikia mahitaji ya wale watu wengi, na “akawasikilia huruma.” Yesu aliona kama walikuwa na lazima ya musaada na kitulizo kutoka kwa Mungu. Njo maana aliwasaidia mara moya. Kwa kweli, “akaanza kuwafundisha [hapana mambo kidogo, lakini] mambo mengi.”​—Mk. 6:31-34; Lu. 9:10, 11.

7-8. Leta mufano wenye kuonyesha namna wazee wenye upendo wanaiga Yesu wakati inaomba kusaidia.

7Namna wazee wenye upendo wanaiga Yesu. Tunasamini sana kazi ya kujitolea yenye wazee wanafanya kwa ajili yetu! Ndugu na dada wengi mu kutaniko hawajuake kazi mingi yenye wazee wanafanyaka. Kwa mufano, wakati kuko mambo fulani ya haraka yenye inatokea kuhusu matunzo, ndugu wa Halmashauri ya Uhusiano na Hopitale wanakuwaka tayari kusaidia ndugu zao bila kukawia. Mara mingi mambo ya vile inatokeaka katikati ya usiku! Lakini juu wako na huruma kwa ajili ya ndugu na dada zao wapendwa, wale wazee pamoya na familia zao, wanatia mahitaji ya ndugu zao pa nafasi ya kwanza.

8 Wazee wanasaidia pia mu kazi ya kujenga Majumba yetu ya Ufalme na majengo ingine ya tengenezo, na pia wanasaidia hata mu kazi ya kutoa misaada. Na mu makutaniko yetu wazee wanapitisha saa za mingi ili kutufundisha, kututia moyo, na kututegemeza. Hauone kama wale wazee na familia zao wanastahili kabisa pongezi zetu? Yehova aendelee kuwabariki juu ya roho ya muzuri yenye wako wanaonyesha! Lakini, sawa vile tu siye wote, wazee wanapaswa kuwa na usawaziko. Hawapaswe kupitisha wakati mingi sana mu zile kazi mbalimbali za kiroho mupaka wakose wakati wa kuhangaikia mahitaji ya familia zao.

NAMNA YA KUONYESHA ROHO YA KUJITOLEA

9. Kulingana na Wafilipi 2:4, 5, ni mutazamo gani wa akili Wakristo wote wanapaswa kuonyesha?

9 Soma Wafilipi 2:4, 5. Hata kama siye wote hatuko wazee, tunaweza kuiga roho ya kujitolea yenye Yesu alikuwa nayo. Biblia inasema kama ‘alichukua umbo ya mutumwa.’ (Flp. 2:7) Fikiria mambo yenye tunaweza kujifunza mu ile andiko. Mutumwa ao mutumishi muzuri, anafanyaka yake yote ili kumufurahisha bwana wake. Juu tuko watumwa wa Yehova na tunatumikia ndugu zetu, tunapenda kutumikia Yehova zaidi na kutumikia ndugu zetu. Tunaweza kufanya vile kwa kufikiria mapendekezo yenye kufuata.

10. Ni maulizo gani tunaweza kujiuliza?

10Uchunguze mutazamo wako. Ujiulize maulizo sawa hii: ‘Ni kwa kiasi gani nakuwaka tayari kutoa wakati na nguvu yangu ili kusaidia wengine? Kwa mufano, nitafanya nini wakati wananiomba kuenda kutembelea ndugu fulani muzee mwenye kuwa ku hopitale ao kuenda kamata dada fulani muzee ili kuenda naye ku mikutano? Nakuwaka tayari kusaidia wakati kuko lazima ya wajitoleaji ili kusafisha fasi ya kufanyia mikusanyiko ya eneo ao kusafisha Jumba ya Ufalme?’ Wakati tunajitoa kwa Yehova, tunamuahidi kama tutatumia mambo yote yenye tuko nayo ili kumutumikia. Anapenda tutumie wakati wetu, nguvu yetu, na vitu vya kimwili vyenye tuko navyo ili kusaidia wengine. Na Yehova anafurahiaka sana wakati tunajitolea kwa kupenda.

11. Namna gani sala inaweza kukusaidia kuonyesha roho ya kujitolea zaidi?

11Usali kwa Yehova kutoka ku moyo. Waza unatambua kama uko na lazima ya kuwa na roho ya kujitolea zaidi lakini haujisikie kufanya mabadiliko yoyote. Mu ile hali, usali kwa Yehova kutoka ku moyo, bila kumufichika kitu. Umuambie Yehova namna unajisikia na umuombe akupatie “hamu na pia nguvu za kutenda.”​—Flp. 2:13.

12. Namna gani ndugu vijana wenye kubatizwa wanaweza kusaidia tengenezo?

12 Kama uko ndugu kijana mwenye kubatizwa, umuombe Yehova akusaidie ukuwe na hamu ya kutumikia zaidi ndugu na dada zako mu kutaniko. Mu ma inchi fulani, kuko wazee wengi kuliko watumishi wa huduma, na wengi kati ya wale watumishi wa huduma hawako vijana sana na hawako wenye kuzeeka. Kadiri mu tengenezo ya Yehova munaendelea kuwa ongezeko kubwa, tuko na lazima ya ndugu vijana ili kuhangaikia ndugu na dada mu kutaniko. Kama uko tayari kutumikia fasi kwenye kuko uhitaji utapata furaha sana. Juu ya nini? Juu utamufurahisha Yehova, ndugu na dada wataona kama uko tayari kusaidia wengine na utakuwa mwenye kutosheka juu ulisaidia wengine.

Wakristo wa Yudea wanakimbia kupitia Muto Yordani na kuenda katika muji wa Pela. Wale wenye walifika mbele mu ile muji wako wanapatia chakula ndugu zao Wakristo wenye wametoka tu kufika (Ona fungu ya 13)

13-14. Tunawea kufanya nini ili kusaidia ndugu na dada zetu? (Ona picha ku jalada.)

13Ukuwe mutazamaji na uone ni nani iko na lazima ya musaada. Mutume Paulo aliambia hivi Wakristo wenye walikuwa wanaisha Yudea: “Musisahau kutenda mema na kushiriki pamoja na wengine vile vyenye muko navyo, kwa maana Mungu anapendezwa na zabihu za namna hiyo.” (Ebr. 13:16) Ile ilikuwa shauri ya muzuri kabisa! Wakati kidogo kisha kupokea ile barua, wale Wakristo walipaswa kuacha nyumba zao, biashara yao, na watu wa familia zao wenye hawakukuwa Wakristo, na walipaswa ‘kuanza kukimbilia kwenye milima.’ (Mt. 24:16) Ile wakati, ilikuwa jambo ya maana sana kwao kusaidiana. Kama wangekuwa wako wanatumikisha ile shauri ya Paulo mbele ile hali itokee, ingekuwa mwepesi sana kwao kuishi na vitu kidogo mu makao yao ya mupya.

14 Haiko kila mara njo ndugu na dada zetu watakuwa wanatuambia mambo yenye wako nayo lazima. Kwa mufano, dada anaweza kufa na anaacha bwana yake. Ule ndugu iko na lazima ya chakula, transport, ao kumusaidia kufanya ma kazi fulani ya nyumba? Pengine hawezi kutuambia juu asionekane kuwa muzigo kwa wengine. Lakini anaweza kuwa mwenye shukrani wakati tunamusaidia hata mbele aombe musaada. Hatupaswe kufikiri kama mutu mwingine atamusaidia ao kama iko na lazima ya musaada, atatuambia tu. Unaweza kujiuliza hivi: ‘Kama miye njo ningekuwa mu ile hali, ni musaada gani ningependa wanipatie?’

15. Tunapaswa kufanya nini kama tunapenda kusaidia watu wengine?

15Ufanye ikuwe mwepesi kwa wengine kukukaribia. Bila shaka, unajua mu kutaniko yenu ndugu na dada wenye wanakuwaka tayari kusaidia wengine. Hawafanyake tujisikie sawa vile tunakuwaka tunawazuru. Tunajua kama tunaweza kuwategemea wakati tunakuwa mu uhitaji, na siye tunapenda kuiga mufano wao muzuri! Alan, mwenye ni muzee na mwenye iko na miaka 40 hivi, anapendaka wengine wamukaribie kwa wepesi. Alan anasema hivi kuhusu mufano wa Yesu: “Yesu alikuwa na mambo mingi sana ya kufanya, lakini watu wa miaka mbalimbali walimukaribia kwa wepesi na hawakuogopa kumuomba musaada. Walijua muzuri kama alikuwa anawahangaikia. Napenda kuonyesha mutazamo sawa ule wa Yesu na kujulikana kama mutu mwenye wengine wanaweza kukaribia kwa wepesi, mutu muchangamufu, na mwenye kuwahangaikia.”

16. Namna gani kutumikisha Zaburi 119:59, 60 kunaweza kutusaidia kufuata mufano wa Yesu kwa ukaribu?

16 Hatupaswe kuvunjika moyo kama tunashindwa kumuiga Yesu kwa ukamilifu. (Yak. 3:2) Mwanafunzi hawezi kupita mwalimu wake kwa ukamilifu. Lakini wakati anajifunza kupitia makosa yake na anajikaza kuiga mwalimu wake, kadiri inawezekana, ule mwanafunzi ataendelea kufanya maendeleo zaidi. Ni vile pia kama tunatumikisha mambo yenye tunajifunza kupitia funzo yetu ya kipekee na kujikaza kurekebisha makosa yenye pengine tunaweza kuwa nayo, ile itatusaidia kufuata mufano wa Yesu kwa ukaribu.​—Soma Zaburi 119:59, 60.

FAIDA ZA KUWA NA ROHO YA KUJITOLEA

Kama wanaiga roho ya Yesu ya kujitolea, wazee wanawekea mufano muzuri vijana (Ona fungu ya 17) *

17-18. Kuiga roho ya kujitolea ya Yesu kutaleta faida gani?

17 Kama tuko tayari kusaidia, ile inaweza kuchochea wengine pia wafanye vile. Muzee moya mwenye kuitwa Tim anasema hivi: “Ndugu fulani vijana walifikia kuwa watumishi wa huduma. Sababu moya ni kwamba waliona namna wengine walikuwa tayari kusaidia na walipenda kuiga mufano wao. Hawa ndugu vijana wanasaidia sana kutaniko yetu na wanategemeza sana wazee.”

18 Watu wengi mu dunia leo wanajipendaka tu wenyewe. Lakini watumishi wa Yehova wako tofauti kabisa. Roho yenye Yesu alikuwa nayo ya kusaidia wengine inagusa sana moyo na tumeazimia kufuata mufano wake. Kwa kweli, hatuwezi kufuata hatua zake kwa ukamili, lakini tunaweza ‘kufuata hatua zake kwa ukaribu.’ (1 Pe. 2:21) Kama tunajikaza kumuiga Yesu, siye pia tutapata furaha ya kukubaliwa na Yehova.

WIMBO 13 Kristo Ni Mufano Muzuri

^ fu. 5 Kila mara Yesu alihangaikia sana mahitaji ya wengine kuliko mahitaji yake. Mu hii habari, tutaona ni mu njia gani mbalimbali tunaweza kuiga mufano wake. Tutaona pia namna kuiga sifa yake ya kuwa tayari kutumikia wengine kutatuletea faida.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu moya kijana mwenye kuitwa Dan, iko anaangalia namna wazee wawili wamekuya kuona baba yake ku hopitale. Mufano wenye upendo wenye wale wazee wanaonyesha inamugusa sana Dan. Naye pia anachochewa kusaidia wengine mu kutaniko. Ndugu mwingine kijana mwenye kuitwa Ben anaangalia namna Dan iko anaonyesha kuwa anahangaikia wengine. Mufano wa Dan unatia moyo Ben kusaidia mu kazi ya kusafisha Jumba ya Ufalme.