Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI JUU YA MAISHA YA WATU

Nilipata Jambo ya Muzuri Zaidi Kuliko Kazi ya Kutunza Watu

Nilipata Jambo ya Muzuri Zaidi Kuliko Kazi ya Kutunza Watu

“MAMBO yenye muko munaniambia njo ilikuwaka ndoto yangu wakati nilikuwa mutoto!” Njo maneno niliambiaka bibi na bwana fulani mu 1971. Ile wakati njo nilianza kutumika mu clinic yangu na niko doktere. Wale bibi na bwana walikuwaka nani, na nini njo ilikuwaka ndoto yangu? Muache niwaelezee namna ile mazungumuzo ilibadilisha mambo yenye nilikuwa ninatanguliza mu maisha yangu na juu ya nini niliamini kama ile ndoto yangu ya tangu utoto ilikuwa karibu kutimia.

Nilizaliwa mu 1941, mu muji wa Paris, katika inchi ya Ufaransa. Familia yetu haikukuwa na makuta mingi. Nilipenda sana kusoma. Sasa waza vile nilijisikia mubaya sana wakati nilikuwa na miaka 10 na wakanipata na ugonjwa wa tuberculose. Ile ilinilazimisha nisimamishe masomo! Wadoktere waliniomba nibakie mu kitanda juu ya kuepuka kuchokesha mapafu ao ma poumons yangu. Kwa hiyo, kwa miezi fulani nilipitisha wakati wangu na niko nasoma diksionere na kusikiliza programu mbalimbali za Radio Sorbonne ya université ya Paris. Siku yenye doktere aliniambia kama napona na kama naweza kurudia ku masomo, nilifurahi sana. Nilijiambia hivi: ‘Kazi yenye wadoktere wanafanyaka ni ya muzuri sana!’ Kuanzia ile siku, ndogo yangu ikakuwa kuponyesha wagonjwa. Kila mara, wakati baba alikuwa ananiuliza nini njo ningefanya mu maisha yangu, jibu yangu ilikuwa tu ileile, “Napenda kuwa doktere.” Njo vile kutunza ilifikia kuwa jambo yenye nilipenda sana mu maisha yangu.

SAYANSI ILIFANYA NIMUKARIBIE MUNGU ZAIDI

Familia yetu ilikuwa ya Wakatoliki. Lakini sikukuwa najua mambo mingi sana juu ya Mungu, na nilikuwa na maulizo mingi sana yenye nilikuwa siyapata majibu. Ni kisha tu kuanza kujifunza masomo ya kuwa doktere ku université njo nilifikia kuamini kabisa kama vitu vyote viliumbwa.

Nakumbuka wakati niliangaliaka ku mikroskope kwa mara ya kwanza chembe yenye inaitwa chembe ya tulipe. Nilishangaa sana kuona namna vitu mbalimbali vyenye kufanyiza ile chembe vilikuwa vinatumika wakati vinawekwa fasi ya joto na fasi ya baridi. Nilishangaa pia wakati nilichunguza namna cytoplasme (ni kusema umaji-maji fulani wenye kuwa ndani ya ile chembe) ilikuwa inajikokota wakati ilichangwa na chumvi na namna ilikuwa inasambaa wakati iliwekwa ndani ya maji safi. Juu ya ile uwezo na pia uwezo ingine mbalimbali, ile inawezesha viumbe vidogo vyenye kuishi vijipatanishe na hali zenye zinajikuta ndani. Kusema kweli, wakati nilichunguza maajabu ya kila chembe, nilifikia kuamini kama uzima haukujitokeza wenyewe.

Mu mwaka wa pili wa masomo yangu ya kinganga, nilifikia kupata uhakikisho tena zaidi wenye kuonyesha kama Mungu iko. Mu somo za Anatomie, tulijifunza kama, namna sehemu ya mbele ya mukono wa mwanadamu ilifanywa inasaidia vidole vyetu vijikunje ao vijinyooshe. Kwa kweli, namna mishipa inaungana na mifupa na namna kila kitu kinatumika muzuri pamoya, ni maajabu kabisa. Nilijifunza kama kuko kamba moya yenye inaunganisha moya kati ya mishipa ya sehemu ya mbele ya mukono wetu mupaka ku mufupa wa pili wa kidole yetu. Kamba inagawanywa mu sehemu mbili ili kufanyiza vitu sawa vile vilalo. Ile makamba inapita sasa chini ya vile vilalo na inaenda mupaka ku mwisho wa vidole, kwenye inaingia muzuri juu ikuwe fasi yake. Vitu fulani vya nguvu vyenye vinaitwa tissus njo vinakamatisha mifupa ya vidole. Kama haikufanyizwa vile, makamba yenye kuwa mu mikono ingekuwa yenye kuonekana na yenye kukokotika na ile ingefanya vidole visitumike muzuri.

Niliojionea waziwazi kama mwenye aliumba mwili wa mwanadamu iko na akili sana, sana kabisa. Nilishangazwa hata zaidi kuhusu kazi ya Muumbaji wakati nilijifunza namna mutoto anaanzaka kupumua kisha kuzaliwa. Nilijifunza kama, wakati mutoto alikuwa mu tumbo, hakukuwa na lazima ya kupumua juu alikuwa anapata oksijeni kwa mama yake kupitia kamba yenye inaunganisha mama na mutoto. Ile kamba inaitwa cordon ombilical. Njo maana alvéoles, vitu vidogo vyenye kuwa sawa ballons, vinakuwaka ndani ya mapafu na haviyajazwa hewa. Majuma fulani mbele mutoto azaliwe, njia za alvéoles zinakuwaka na umaji-maji wenye kujulikana kuwa surfactant. Kisha mutoto kuzaliwa na wakati ananyonya kwa mara ya kwanza, mambo fulani ya kushangaza inatokeaka: Tundu yenye kuwa mu moyo wa mutoto inajifunga. Ile inasaidia damu ishuke muzuri. Ile wakati surfactant inazuia alvéoles zisibanane saa yenye zinajazwa hewa na mara moya mutoto anakuwa na uwezo wa kupumua yeye mwenyewe.

Nilipenda kujua ule mwenye aliumbaka ile mambo yote yenye kushangaza. Njo maana nilianza kukamata kwa uzito usomaji wangu wa Biblia. Nilishangazwa sana na sheria za Mungu kuhusu usafi zenye alipatia Waisraeli kumepita miaka 3 000 hivi. Mungu aliomba Waisraeli kufunika mavi yao, kunawa na maji kila mara, na kutenga mutu yeyote mwenye kuonyesha alama fulani za ugonjwa wenye kuambukiza na wengine. (Law. 13:50; 15:11; Kum. 23:13) Biblia inazungumuzia namna magonjwa inaweza kuenea. Ni vile pia wanasayansi wamevumbula mu miaka ya hivi karibuni. Na nimefikia kutambua kama sheria zenye zinahusu ngono zenye kuzungumuziwa mu kitabu ya Walawi zililinda taifa nzima ya Israeli. (Law. 12:1-6; 15:16-24) Nilifikia kuona kama Muumbaji alipatia Waisraeli zile sheria kwa faida yao na kama anakuwaka anabariki wale wenye wanatii amri zake. Nilifikia kuwa hakika kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu, Mungu mwenye sikujua jina ile wakati.

NAMNA NILIKUTANA NA BIBI YANGU NA NAMNA NILIMUJUA YEHOVA

Miye na Lydie siku ya ndoa yetu, tarehe 3 Mwezi wa 4, 1965

Wakati nilikuwa nasoma masomo ya kuwa doktere, nilikutana na kijana moya mwanamuke. Jina yake Lydie, mwenye nilipenda sana. Tulioana mu 1965 wakati nilikuwa karibu kumaliza masomo. Mu 1971, miye na Lydie tayari tulikuwa na watoto watatu, lakini sasa tuko na watoto sita. Lydie amekuwa akinitegemeza mu kazi yangu ya kinganga na hata mu familia yetu.

Nilitumika miaka tatu mu hopitale mbele ya kufungula clinic yangu. Kisha wakati fulani, bibi na bwana fulani wenye nilizungumuzia mbele, wakakuya juu ya matunzo. Nilikuwa karibu kumuandikia bwana yake madawa yenye angetumia, kisha bibi akaniambia hivi: “Doktere tafazali, hapana mambo ya damu mu matunzo.” Nilishituka na kisha nikamuuliza: “Kweli? Juu ya nini?” Akaniambia: “Tuko Mashahidi wa Yehova.” Nilikuwaka siyasikia juu ya Mashahidi wa Yehova ao mambo yenye wanafundisha kuhusu damu. Ule mwanamuke alikamata Biblia yake na kunionyesha andiko yenye inaonyesha juu ya nini wanakatala kutiwa damu. (Mdo. 15:28, 29) Yeye na bwana yake walinionyesha mambo yenye Ufalme wa Mungu utatimiza; ni kusema utatosha mateso, magonjwa, na kifo. (Ufu. 21:3, 4) Nilisema hivi kwa kushangaa: “Mambo yenye muko munaniambia njo ilikuwaka ndoto yangu wakati nilikuwa mutoto! Nilifikia kuwa doktere juu ya kusaidia watu wasiteseke.” Nilipenda sana ile mazungumuzo, njo maana tuliifanya kwa saa moya na nusu. Wakati ule bibi na bwana walienda, mu moyo wangu sikukuwa tena Mukatoliki na nilifikia kujifunza kama Muumbaji mwenye nilikuwa napenda sana anakuwaka na jina, Yehova!

Nilikutana na ule bibi na bwana yake, wenye walikuwa Mashahidi, mara tatu mu clinic yangu. Na kila mara, tulikuwa tunazungumuza kwa zaidi ya saa moya. Niliwaalika kwangu juu ya kuwa na wakati mingi zaidi wa kuzungumuza nao kuhusu Biblia. Hata kama Lydie alikubali kuwa ku funzo ya Biblia, ilikuwa nguvu sana kwake kukubali kama mafundisho fulani yenye tulifundishwa mu kanisa ya Katoliki ilikuwa ya bongo. Njo maana nilialika padri moya kwetu. Tulizungumuzia sana mambo ya dini mupaka usiku sana, na tulitumia tu Biblia. Ile mazungumuzo ilimusaidia Lydie kuwa hakika kama Mashahidi wa Yehova wanafundishaka kweli. Kwa hiyo, upendo wetu kwa Yehova Mungu uliongezeka sana mupaka siye wote wawili tukabatizwa mu 1974.

TULIMUTIA YEHOVA PA NAFASI YA KWANZA

Mambo yenye nilijifunza juu ya kusudi ya Mungu kwa ajili ya wanadamu ilifanya nione jambo ingine ya maana sana mu maisha yangu. Kwangu na kwa Lydie, kumutumikia Yehova njo ilifikia kuwa jambo ya maana sana mu maisha yetu. Tuliazimia kukomalisha watoto wetu kulingana na kanuni za Biblia. Tulifundisha watoto wetu kumupenda Mungu na watu. Ile ilifanya tukaribiane zaidi​—Mt. 22:37-39.

Wakati fulani, miye na Lydie tunakuwaka tunacheka saa yenye tunakumbuka vile watoto wetu walikuwa walishajua kama miye na Lydie tunakuwa tunakubaliana mu maamuzi yetu. Walijua kama maneno yenye Yesu alisemaka, “muache neno lenu ‘Ndiyo’ limaanishe ndiyo, na ‘Hapana’ yenu imaanishe hapana,” njo ilikuwa kanuni ya mu nyumba yetu. (Mt. 5:37) Kwa mufano, siku moya Lydie alikataza mutoto yetu mwanamuke wa miaka 17 asiende na kikundi fulani ya vijana wenzake. Mumoya mu ile kikundi akaambia mutoto yetu, “Kama mama yako anakukatalia usiende, umuambie baba yako!” Lakini mutoto yetu akasema: “Bote ni bamoya tu. Banakubalianaka tu.” Watoto wetu wote sita walijua kama tulikuwa na umoja mu kutumikisha kanuni za Biblia. Tunamushukuru sana Yehova, kuona vile leo watu wengi wa familia yetu ni Mashahidi wa Yehova.

Hata kama kweli ilibadilisha mambo yenye nilikuwa naona kuwa ya lazima sana, nilipenda kutumikisha ufundi wangu kwa kinganga juu ya kusaidia watu wa Mungu. Njo maana, nilijitolea sawa vile doktere ili kusaidia ku Beteli yenye ilikuwa mu muji wa Paris na kisha tena mu makao ya mupya ya Beteli yenye ilikuwa mu muji wa Louviers. Ni karibu miaka 50 sasa na niko nasaidia ku Beteli. Mu hii kipindi yote nimepata marafiki wazuri sana kati ya washiriki wa Beteli, wamoya kati yao wako sasa na miaka 90 hivi. Siku moya, nilishangala sana wakati nilikutana na Mwanabeteli moya wa mupya. Nilivumbula kama miye njo doktere mwenye nilisaidiaka kuzalisha mama yake kumepita miaka 20 hivi. Na ule mutoto mwenye ule mama alizalaka njo ule mwenye anakuwa sasa Mwanabeteli!

NIMEONA VILE YEHOVA ANAHANGAIKIAKA SANA WATU WAKE

Mu hii miaka yote, upendo wangu kwa Yehova umeongezeka sana kadiri nimechunguza namna iko anaongoza na kulinda watu wake kupitia tengenezo yake. Ku mwanzo-mwanzo ya miaka ya 1980, Baraza Yenye Kuongoza ilikamata mupango fulani mu Amerika ili kusaidia wanganga kwa ujumla waelewe muzuri uamuzi wa Mashahidi wa Yehova wenye wako wagonjwa kuhusu mambo ya damu.

Kisha mu 1988, Baraza Yenye Kuongoza iliweka idara ya mupya ku Beteli yenye iliitwa Idara ya Habari za Hopitale. Ku mwanzo, ile idara ilikuwa inasimamia Halmashauri za Uhusiano na Hopitale (CLH) zenye zilikuwa zimeanzishwa mu Amerika ili kusaidia Mashahidi wa Yehova wenye ni wagonjwa wapate wanganga wenye kuheshimia musimamo wao kuhusu damu. Wakati ile mupango ilianzishwa mu dunia yote, CLH ziliwekwa pia mu inchi ya Ufaransa. Ninafurahi kuona vile tengenezo ya Yehova iko inategemeza kwa upendo ndugu na dada wenye ni wagonjwa wakati wako na lazima ya musaada!

NDOTO YANGU INATIMIA

Tunaendelea kufurahia kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu

Kutunza wengine njo jambo yenye nilipenda sana. Wakati nilichunguza mambo yenye nilikuwa ninatanguliza mu maisha, nilifikia kuelewa kama jambo ya maana zaidi ni kusaidia watu wamujue na wamutumikia Yehova Mungu, mwenye ni Chanzo ya uzima kuliko kuwatunza. Muda kidogo kisha kueneza miaka ya kuacha kazi, miye na Lydie tulipitisha sasa saa mingi kila mwezi ili kuhubiri habari njema juu ya Ufalme wa Mungu tukiwa mapainia wa kawaida. Tungali tunajikaza kufanya hii kazi yenye kuokoa uzima.

Pamoya na Lydie, mu 2021

Niko ninajikaza kutunza wale wenye ni wagonjwa. Lakini kusema kweli, ile matunzo ni ya muda kidogo tu. Nimeelewa kama hata doktere wa hali ya juu sana hawezi kutunza magonjwa yote wala kuzuia kifo. Nachunga kwa hamu sana wakati wenye maumivu, magonjwa, na kifo haitakuwa tena. Mu dunia mupya yenye iko karibu sana, nitakuwa na nafasi ya kujifunza milele uumbaji wa Mungu na pia kuhusu namna mwili wa mwanadamu ulifanywa kwa njia ya ajabu sana. Ndoto yangu ya wakati nilikuwa mutoto imetimia kwa sehemu tu. Niko hakika kama mambo ingine ya muzuri zaidi iko inanichunga kule mbele!