Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Yehova alikubali Waisraeli watoe njiwa-tetere na njiwa kama zabihu. Ile ilikuwa na faida gani?

CHINI ya sheria ya Musa, Yehova alikubali njiwa-tetere na njiwa watolewe kama zabihu. Kila mara, wale ndege wawili walitajwa pamoya katika sheria kuhusu zabihu na mumoja angeweza kutolewa ku fasi ya mwingine. (Law. 1:14; 12:8; 14:30) lle ilikuwa na faida gani? Sababu moya ni kwamba njiwa-tetere hawakukuwa wanapatikana kila mara. Juu ya nini?

Njiwa-tetere

Njiwa-tetere ni ndege wenye wanapendaka kufanya safari na wanaishi mu inchi ya Israeli mu miezi ya kifukutu zaidi. Kila mwaka mu Mwezi wa 10, wanaenda kusini mu ma inchi yenye kuwa na kifukutu zaidi na wanarudia mu Israeli mu kipindi ya mvua ya mwisho. (Wim. 2:11, 12; Yer. 8:7) Mu Israeli ya zamani ile ilifanya ikuwe nguvu sana kwa Waisraeli kutoa njiwa-tetere kama zabihu mu kipindi ya baridi.

Njiwa mwenye kuitwa Biset

Tofauti na ile, kwa ujumla njiwa hawafanyake safari, njo maana wanakuwaka mu Israeli kila mwaka. Zaidi ya ile, njiwa walikuwa wanafugwa. (Linganisha na Yohana 2:14, 16.) Kitabu moya inasema hivi: “Mu vijiji na miji yote ya Palestina watu walikuwa wanafuga njiwa. Kila mwenye-nyumba alikuwa na nyumba yake ya njiwa, ao tundu mu ukuta, kwenye ndege wangeweza kuishi.” (Bible Plants and Animals)​—Linganisha na Isaya 60:8.

Njiwa mwenye kuwa mu nyumba yake

Kwa hiyo, Yehova alionyesha kama alikuwa mwenye upendo na mwenye usawaziko kwa kukubali Waisraeli watoe ndege zenye zilipatikana mu mwaka.