Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JI LIFUNZU 10

Guwesa “Kuguhula Utu gwa Zamani”

Guwesa “Kuguhula Utu gwa Zamani”

“Guhula utu gwa zamani pamu ni mazoea gaki.”​—KOL. 3:9.

NHAMBU 29 Kuishi Kulingana na Jina Letu

MUHTASARI *

1. Maisha gaku gikabibo kabula ja kulibola Bibilia?

 MAISHA yako yalikuwaje kabla hujaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova? Wengi wetu hatupendi hata kufikiria jambo hilo. Inaelekea mtazamo na utu wetu ulikuwa umefinyangwa na viwango vya mfumo huu wa mambo, yaani, viwango vya ulimwengu kuhusu yaliyo sawa na yaliyo mabaya. Ikiwa ndivyo, ‘hatukuwa na tumaini na tulikuwa bila Mungu katika ulimwengu.’ (Efe. 2:12) Lakini hayo yote yalibadilika ulipoanza kujifunza Biblia!

2. Gukimanya sindubo pagwaanza kulibola Bibilia?

2 Ulipojifunza Biblia uligundua kwamba una Baba wa mbinguni anayekupenda sana. Ulitambua kwamba ikiwa unataka kumfurahisha Yehova na kuwa sehemu ya familia ya waabudu wake, ungehitaji kufanya mabadiliko makubwa katika njia yako ya maisha, mtazamo, na njia ya kufikiri. Ulihitaji kujifunza kuishi kulingana na viwango vyake vya juu.​—Efe. 5:3-5.

3. Kulengana na Wakolosai 3:9, 10, Yehova jupala tuhenga ki, na mututulongalya ki mu makala jenzeno?

3 Muumba na Baba yetu wa mbinguni, Yehova, ana haki ya kuamua jinsi washiriki wa familia yake wanavyopaswa kujiendesha. Na anataka kabla hatujabatizwa, tujitahidi ‘kuvua utu wa zamani pamoja na mazoea yake.’ * (Soma Wakolosai 3:9, 10.) Makala hii, itawasaidia wale wanaotaka kubatizwa wajibu maswali haya matatu: (1) “Utu wa zamani” ni nini? (2) Kwa nini Yehova anatuhimiza tuuvue? (3) Tunaweza kufanya hivyo jinsi gani? Kwa wale ambao tayari tumebatizwa, makala hii itatusaidia kuepuka kurudia mazoea ya utu wa zamani.

“UTU GWA ZAMANI” NDO KIKE?

4. Mundu jojuongozwa na “utu gwa zamani” juhenga bole?

4 Kwa ujumla, mtu anayeongozwa na “utu wa zamani,” anaongozwa na kutenda kwa njia ya kimwili. Huenda akawa na ubinafsi, anakasirika upesi, hana shukrani, na ni mwenye kiburi. Huenda anafurahia kutazama ponografia na kutazama sinema zenye upotovu wa maadili au ukatili. Bila shaka, ana sifa fulani nzuri, na huenda akahisi hatia kuhusu mambo mabaya anayosema au kufanya. Lakini anakosa kichocheo cha kubadili njia yake ya kufikiri na mwenendo wake.​—Gal. 5:19-21; 2 Tim. 3:2-5.

Tunapovua “utu wa zamani,” hatuongozwi tena na mitazamo na mazoea ya kimwili (Tazama fungu la 5) *

5. Tupaswa kuba nu mtazamu bo gogubi nu usawaziku pakuhusu kuhula utu gwa zamane? (Matendo 3:19)

5 Sisi si wakamilifu, hivyo hatuwezi kuondoa kabisa mawazo na tamaa zote mbaya kutoka katika mioyo na akili zetu. Nyakati fulani huenda tutafanya au kusema jambo ambalo tutajutia. (Yer. 17:9; Yak. 3:2) Lakini tunapovua utu wa zamani, mitazamo na matendo ya kimwili hayatatudhibiti tena. Mambo hayo si sehemu ya utu wetu tena.​—Isa. 55:7; soma Matendo 3:19.

6. Ndaba jaki Yehova jutuhimiza tuhula mawasu na mazoea giliaha ga utu gwa zamane?

6 Yehova anatuhimiza tung’oe mawazo na mazoea mabaya kwa sababu anatupenda sana na anataka tufurahie maisha. (Isa. 48:17, 18) Anajua kwamba wale ambao hawapambani dhidi ya tamaa mbaya wanajiumiza wao wenyewe na wale wanaowazunguka. Anaumia tunapojiumiza na kuwaumiza wengine.

7. Kulengana na Waroma 12:1, 2, tupaswa kuhenga uamuzi bole?

7 Mwanzoni, huenda baadhi ya marafiki na watu wetu wa ukoo wakatudhihaki tunapojitahidi kufanya mabadiliko katika utu wetu. (1 Pet. 4:3, 4) Huenda wakasema kwamba tuna haki ya kufanya chochote tunachotaka na kwamba hatupaswi kuruhusu wengine watuambie mambo ya kufanya. Lakini wale ambao wanakataa viwango vya Yehova kihalisi hawako huru. Ukweli ni kwamba wanaruhusu ulimwengu unaotawaliwa na Shetani uwafinyange. (Soma Waroma 12:1, 2.) Sote tunapaswa kufanya uamuzi: tunaweza kuchagua kuendelea na utu wetu wa zamani, ambao unaongozwa na dhambi na ulimwengu wa Shetani, au kumruhusu Yehova atugeuze tuwe na utu bora kabisa ambao tunaweza kuwa nao sasa.​—Isa. 64:8.

JINZI EGUWESA “KUGUHULA” UTU GWA ZAMANI

8. Kike se satujangatya kujepa mawasu na mazoea giliaha?

8 Yehova anajua kwamba muda unahitajika ili kuepuka mawazo na mazoea mabaya. (Zab. 103:13, 14) Hata hivyo, kupitia Neno lake, roho yake, na tengenezo lake, Yehova anatupatia hekima, nguvu, na msaada tunaohitaji ili tufanye mabadiliko. Bila shaka, tayari amekusaidia. Acheni sasa tuchunguze baadhi ya hatua hususa tunazoweza kuchukua ambazo zitatusaidia kufanya maendeleo zaidi katika kuvua utu wa zamani na kustahili kubatizwa.

9. Lilobi lika Mungu liwesa kugujangati kuhenga kike?

9 Tumia Biblia ili kujichunguza kwa makini. Neno la Mungu ni kama kioo, linaweza kukusaidia kujichunguza jinsi unavyofikiri, kusema, na kutenda. (Yak. 1:22-25) Mwalimu wako wa Biblia na Wakristo wengine wakomavu, wanaweza kukupa ushauri. Kwa mfano, wanaweza kutumia Maandiko kukusaidia kutambua sifa zako nzuri na udhaifu wako. Wanaweza kukufundisha jinsi ya kutafuta habari zinazotegemea Biblia zinazotoa ushauri hususa kuhusu kushinda mazoea mabaya. Na sikuzote Yehova yuko tayari kukusaidia. Anajua njia bora ya kukusaidia; na anajua yaliyo moyoni mwako. (Met. 14:10; 15:11) Hivyo, uwe na mazoea ya kusali kwake na kujifunza Neno lake kila siku.

10. Guliboliki ki kubokana na kisa sika Eli?

10 Sadiki kwamba viwango vya Yehova ni bora. Tunaweza kunufaika na kila jambo ambalo Yehova anatuambia tufanye. Wale wanaoishi kulingana na viwango vyake wanajiheshimu, wana kusudi maishani, na furaha ya kweli. (Zab. 19:7-11) Kinyume chake, wale wanaopuuza viwango vya Yehova wanapata matokeo mabaya yanayosababishwa na matendo ya mwili. Ona kile ambacho mwanamume anayeitwa Eli, anasema kuhusu kukataa kufuata viwango vya Mungu. Alilelewa na wazazi wanaompenda Yehova. Lakini alipokuwa tineja, Eli alichagua kushirikiana na watu wabaya. Alianza kuishi maisha yaliyohusisha kutumia madawa ya kulevya, upotovu wa maadili, na wizi. Eli anasema kwamba alianza kuwa na hasira sana na jeuri. Anakiri hivi: “Kwa ufupi, nilifanya mambo yote ambayo nilikuwa nimefundishwa kwamba nikiwa Mkristo sikupaswa kufanya.” Hata hivyo, Eli hakusahau mambo aliyokuwa amejifunza alipokuwa kijana. Mwishowe, alianza kujifunza Biblia tena. Alijitahidi kung’oa mazoea yake mabaya naye akabatizwa mwaka wa 2000. Amenufaika jinsi gani kwa kuishi kulingana na viwango vya Yehova? Anasema hivi: “Sasa nina amani ya akili na dhamiri safi.” * Kama simulizi hili linavyoonyesha, wale wanaokataa viwango vya Yehova hujiumiza wenyewe. Hata hivyo, Yehova yuko tayari kuwasaidia wabadilike.

11. Yehova jusuki mambu bole?

11 Jifunze kuchukia mambo ambayo Yehova anachukia. (Zab. 97:10) Biblia inafunua kwamba Yehova anachukia “macho ya kiburi, ulimi wa uwongo, na mikono inayomwaga damu isiyo na hatia.” (Met. 6:16, 17) Pia, anawachukia kabisa “watu wakatili na wadanganyifu.” (Zab. 5:6) Yehova anachukia mitazamo na matendo hayo sana, hivi kwamba aliwaangamiza watu wote waovu katika siku za Noa kwa sababu walikuwa wameijaza dunia ukatili. (Mwa. 6:13) Fikiria mfano mwingine. Kupitia nabii Malaki, Yehova alisema kwamba anawachukia wale ambao kwa hila wanapanga njama ya kumtaliki mwenzi wao asiye na hatia. Yehova anakataa ibada yao naye atawatoza hesabu kwa matendo yao.​—Mal. 2:13-16; Ebr. 13:4.

Tunapaswa kuchukizwa sana na jambo ambalo Yehova anasema ni baya kama tunavyochukizwa na chakula kilichooza (Tazama fungu la 11 na 12)

12. Kumaanisha ki “kugasuki mambu maovu”?

12 Yehova anataka ‘tuchukie maovu.’ (Rom. 12:9) Neno ‘kuchukia’ linafafanua hisia kali; linamaanisha kuchukizwa sana na jambo au kitu fulani. Wazia hisia kali ambazo ungekuwa nazo ikiwa ungeambiwa ule chakula kilichooza. Kuwazia tu hilo kunaweza kukufanya uhisi kichefuchefu. Vivyo hivyo, tunapaswa kuchukizwa sana hata na wazo tu la kufanya jambo ambalo Yehova anasema ni baya.

13. Ndaba jaki ibi lasima tujilenda dhidi jimawasu giliaha?

13 Jilinde dhidi ya mawazo mabaya. Mawazo yetu huchochea matendo yetu. Hiyo ndiyo sababu Yesu alitufundisha tupinge mawazo yoyote yanayoweza kutuongoza kwenye kutenda dhambi nzito. (Mt. 5:21, 22, 28, 29) Bila shaka, tunapenda kumfurahisha Baba yetu wa mbinguni. Hivyo, ni muhimu sana tupinge haraka mawazo yoyote mabaya yanayoweza kuja akilini mwetu.

14. Gatukolabeka gayeku ki kutuhusu, na tupaswa kulilaluki maswali bole?

14 Dhibiti usemi wako. Yesu alisema hivi: “Mambo yanayotoka kinywani hutoka moyoni.” (Mt. 15:18) Naam, maneno yetu yanafunua mambo mengi kuhusu jinsi tulivyo moyoni. Hivyo, jiulize maswali haya: ‘Je, ninakataa kudanganya, hata ikiwa kusema ukweli kutaniletea matatizo? Ikiwa nimefunga ndoa, je, mimi ni mwangalifu ili nisiwachezee kimapenzi watu wa jinsia tofauti? Je, ninaepuka kabisa mazungumzo yaliyopotoka kimaadili? Je, ninajibu kwa utulivu mtu fulani anaponikasirisha?’ Utafaidika ikiwa utatafakari maswali hayo. Usemi wako unaweza kulinganishwa na mishono iliyo katika nguo. Kama tu mishono inavyoshikilia nguo, ndivyo usemi mbaya unavyoshikilia utu wa zamani. Ikiwa utajitahidi kadiri uwezavyo kuacha kutumia usemi uliopotoka kimaadili, uwongo, na matusi katika mazungumzo yako, itakuwa rahisi zaidi kwako kuvua utu wa zamani.

15. Imaanisha ki kugutundika utu gwa zamani “mu nkongo”?

15 Uwe tayari kuchukua hatua mara moja. Mtume Paulo alitumia lugha ya picha yenye nguvu kutufundisha umuhimu wa kuchukua kwa uzito himizo la kubadili njia yetu ya maisha. Aliandika kwamba ni lazima tuutundike utu wetu wa zamani “mtini.” (Rom. 6:6) Kwa maneno mengine, tunataka kufuata mfano wa Kristo. Tunahitaji kuua au kuondoa kabisa mitazamo na mazoea ambayo Yehova anayachukia. Baada ya kuchukua hatua hizo, ndipo tutakapojipatia dhamiri safi na kuwa na tumaini la kufurahia uzima wa milele. (Yoh. 17:3; 1 Pet. 3:21) Kumbuka kwamba Yehova hatabadili viwango vyake ili vitufae sisi. Badala yake, sisi tunahitaji kubadili utu wetu na kufuata viwango vyake.​—Isa. 1:16-18; 55:9.

16. Ndaba jaki lasima guazimia kuendale kupenga tamaa iliaha?

16 Endelea kupinga tamaa mbaya. Hata baada ya kubatizwa utahitaji kuendelea kupinga tamaa za mwili. Fikiria kisa cha mwanamume anayeitwa Maurício. Alipokuwa kijana alianza kuishi maisha ya ushoga. Hatimaye, alikutana na watu wa Yehova, naye akaanza kujifunza Biblia. Baada ya kufanya mabadiliko maishani mwake, alibatizwa mwaka wa 2002. Hata ingawa sasa amemtumikia Yehova kwa miaka mingi, Maurício anasema hivi: “Ninakubali kwamba nyakati nyingine nimelazimika kupambana na tamaa zisizofaa.” Lakini haruhusu jambo hilo limvunje moyo. Badala yake, anasema hivi: “Ninafarijika kujua kwamba kwa kuepuka kuongozwa na tamaa hizo, ninaweza kumfurahisha Yehova.” *

17. Libi lijambu bo leligujegi mwoju kuhusu kisa sika?

17 Sali kwa Yehova ili akusaidie, na utegemee roho yake, bali si uwezo wako mwenyewe. (Gal. 5:22; Flp. 4:6) Ni lazima tuazimie kujitahidi sana, ikiwa tunataka kuuvua utu wa zamani na kutouvaa tena. Fikiria kisa cha mwanamke anayeitwa Nabiha. Baba yake alimwacha alipokuwa na umri wa miaka sita tu. Anasema hivi: “Jambo hilo lilinisababishia uchungu mwingi wa kihisia.” Alipoendelea kukua, Nabiha akawa mwenye hasira sana na mjeuri. Akaanza kuuza dawa za kulevya, akakamatwa na polisi na kufungwa gerezani kwa miaka kadhaa. Mashahidi waliotembelea gereza alilokuwa amefungwa, walianza kujifunza Biblia pamoja naye. Nabiha alianza kufanya mabadiliko makubwa. Anasema hivi: “Ilikuwa rahisi kuacha baadhi ya mazoea yangu machafu. Lakini ilikuwa vigumu zaidi kuacha kuvuta sigara.” Nabiha alipambana kwa zaidi ya mwaka mmoja, na mwishowe alifaulu kuacha uraibu huo. Alifauluje? Anasema hivi: “Zaidi ya yote, kuendelea kusali kwa Yehova kulinisidia kuacha zoea hilo.” Sasa anawaambia wengine hivi: “Nina hakika kwamba ikiwa nilifanikiwa kufanya mabadiliko ili nimpendeze Yehova, basi mtu yeyote anaweza! *

GUWESA KUSTAHILI KUBATIZWA!

18. Kulengana na 1 Wakorinto 6:9-11, atumishi bingi bika Mungu awesiki kuhenga kike?

18 Katika karne ya kwanza, baadhi ya wanaume na wanawake ambao Yehova aliwachagua kuwa watawala pamoja na Kristo, walifanya mambo mabaya sana hapo awali. Kwa mfano, walikuwa wazinzi, wanaume waliofanya ngono na wanaume, na wezi. Hata hivyo, kwa msaada wa roho takatifu ya Mungu, walifaulu kubadili utu wao. (Soma 1 Wakorintho 6:9-11.) Vivyo hivyo leo, Biblia imewasaidia mamilioni ya watu kufanya mabadiliko katika maisha yao. * Wamefaulu kushinda mazoea mabaya yaliyokuwa yamekita mizizi. Mfano wao unathibitisha kwamba wewe pia unaweza kufanya mabadiliko katika utu wako na kushinda mazoea mabaya ili ustahili kubatizwa.

19. Musitulongalya kike mu makala jejipwata?

19 Zaidi ya kujitahidi kuuvua utu wa zamani, wale wanaotaka kubatizwa ni lazima wajitahidi kuvaa utu mpya. Katika makala inayofuata, tutazungumzia jinsi tunavyoweza kufanya hivyo na jinsi wengine wanavyoweza kutusaidia.

NHAMBU 41 Tafadhali Sikiliza Sala Yangu

^ Ili tustahili kubatizwa ni lazima tuwe tayari kufanya mabadiliko katika utu wetu. Makala hii, itatusaidia kuona ni tabia gani zinazofanyiza utu wa zamani, kwa nini tunahitaji kuzivua tabia hizo, na jinsi tunavyoweza kufanya hivyo. Makala inayofuata, itachunguza jinsi tunavyoweza kuendelea kuvaa utu mpya hata baada ya kubatizwa.

^ UFAFANUZI WA MANENO: “Kuvua utu wa zamani” kunamaanisha kung’oa mitazamo na mielekeo ambayo haimfurahishi Yehova. Tunapaswa kuanza kufanya hivyo kabla ya kubatizwa.​—Efe. 4:22.

^ Kwa habari zaidi, tazama makala “Biblia Inabadili Maisha​—‘Nilihitaji Kumrudia Yehova,’” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 2012.

^ Kwa habari zaidi, tazama makala “Biblia Inabadili Maisha​—‘Walinitendea kwa Fadhili Sana,’” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 2012.

^ Kwa habari zaidi, tazama makala “Biblia Inabadili Maisha​—‘Nikawa Msichana Mwenye Hasira,’” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 2012.

^ Tazama sanduku “Biblia Inabadili Maisha.”

^ MAELEZO YA PICHA: Kuondoa mitazamo na mazoea yasiyofaa ni kama kuvua vazi la zamani.