Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 10

Unaweza ‘Kuvua Utu wa Zamani’

Unaweza ‘Kuvua Utu wa Zamani’

“Muvue utu wa zamani pamoja na mazoea yake.”​—KOL. 3:9.

WIMBO 29 Tuishi Kulingana na Jina Yetu

KIFUPI YA HABARI *

1. Ulikuwa na maisha gani mbele ya kuanza kujifunza Biblia?

 ULIKUWA na maisha gani mbele ya kuanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova? Wengi kati yetu hawapendake kufikiri juu ya ile. Tabia yetu na utu wetu ulichochewa na mambo yenye ulimwengu unasema kama njo mambo ya muzuri na ya mubaya. Kama ni vile, ‘hatukukuwa na tumaini na tulikuwa bila Mungu katika ulimwengu.’ (Efe. 2:12) Lakini kisha kujifunza Biblia namna yetu ya kuishi ilibadilika!

2. Ulivumbula nini wakati ulianza kujifunza Biblia?

2 Wakati ulianza kujifunza Biblia, ulivumbula kama uko na Baba wa mbinguni mwenye anakupenda sana. Ulifikia kutambua kama ikiwa unapenda kumufurahisha Yehova na kuwa mu familia ya waabudu wake, unapaswa kufanya mabadiliko mu maisha yako, mu tabia yako na mu namna yako ya kufikiri. Ulijifunza kufanya mambo yenye Yehova anasema kuwa ni ya muzuri na kuepuka mambo yenye anasema kuwa ni ya mubaya.​—Efe. 5:3-5.

3. Kulingana na Wakolosai 3:9, 10, Yehova anapenda tufanye nini, na ni mambo gani tutazungumuzia mu hii habari?

3 Yehova ni Muumbaji wetu na Baba yetu wa mbinguni, kwa hiyo, iko na haki ya kuamua namna waabudu wa mu familia yake wanapaswa kutenda. Na ni vile anatuomba mbele ya kubatizwa, kujikaza ‘kuvua utu wa zamani pamoja na mazoea yake.’ * (Soma Wakolosai 3:9, 10.) Hii habari itasaidia wale wenye wanapenda kubatizwa kujibia hii maulizo tatu: (1) “Utu wa zamani” njo nini? (2) Juu ya nini Yehova anapenda tuvue utu wa zamani? (3) Namna gani tunaweza kufanya vile? Kwa siye wenye tayari tulishabatizwa, hii habari itatusaidia tusitende ao kufikiri mu njia yenye tulikuwa nafanya mbele tuvue utu wa zamani.

“UTU WA ZAMANI” NJO NINI?

4. Mutu mwenye kuongozwa na “utu wa zamani” anatendaka namna gani?

4 Mutu mwenye anaongozwa na “utu wa zamani” kwa kawaida anafikiri na kutenda mu njia ya kimwili. Pengine ni mwenye kujipenda yeye mwenyewe, mwenye kukasirika, mwenye kukosa shukrani, na mwenye kiburi. Pengine anafurahia kuangalia pornografia na kuangalia filme za jeuri ao zenye kuonyesha mambo ya uasherati. Bila shaka anaweza kuwa na sifa fulani za muzuri, na anaweza kujihukumu juu ya mambo ya mubaya yenye anasema ao kufanya. Lakini, anakosa jambo yenye itamusaidia kubadilisha namna yake ya kufikiri na matendo yake.​—Gal. 5:19-21; 2 Ti. 3:2-5.

Wakati tunavua “utu wa zamani,” tamaa zetu na matendo yetu haitatuongoza tena (Ona fungu ya 5) *

5. Tunaweza kabisa kuvua utu wa zamani? Fasiria. (Matendo 3:19)

5 Juu hatukamilike hakuna kabisa mutu mwenye anaweza kuondoa mawazo na tamaa za mubaya mu moyo na mu akili yetu. Wakati fulani, tunaweza kufanya ao kusema jambo fulani yenye tutahuzunikia kisha. (Yer. 17:9; Yak. 3:2) Lakini wakati tunavua utu wa zamani, tamaa zetu na matendo yetu haitatuongoza tena. Tutafikia kuwa tofauti.​—Isa. 55:7; soma Matendo 3:19.

6. Juu ya nini Yehova anapenda tuachane na mawazo na tabia za mubaya za utu wa zamani?

6 Yehova anapenda tuache kuwaza mambo ya mubaya na tabia za mubaya, juu anatupenda sana na anapenda tufurahie maisha. (Isa. 48:17, 18) Anajua kama, wale wenye hawapiganishe tamaa za mubaya wanajiumiza wao wenyewe na wanaumiza wenye kuwazunguka. Inamuumiza wakati anaona tunajiumiza siye wenyewe na tunaumiza wengine.

7. Kulingana na Waroma 12:1, 2, ni uhuru gani wenye tuko nao?

7 Marafiki wetu fulani na watu wa familia yetu, ku mwanzo wanaweza kutuchekelea juu tuko tunajikaza kufanya mabadiliko juu ya utu wetu. (1 Pe. 4:3, 4) Wanaweza kutuambia kama tuko na haki ya kufanya mambo yenye tunapenda na kama hatupaswe kuacha wengine watuambie mambo yenye tunapaswa kufanya. Lakini wale wenye wanakatala kanuni za Yehova hawakuwake kabisa huru. Kusema kweli, wanajiachaka njo wafinyangwe na ulimwengu wenye unatawaliwa na Shetani. (Soma Waroma 12:1, 2.) Siye wote tuko na uhuru wa kuchagula: Ikuwe tutabakia na utu wetu wa zamani, wenye umefanyizwa na zambi na ulimwengu wa Shetani, ao kama tutaacha Yehova atubadilishe juu tukuwe watu wazuri zaidi sasa.​—Isa. 64:8.

NAMNA GANI TUNAWEZA ‘KUVUA UTU WA ZAMANI’?

8. Nini njo itatusaidia kuepuka kuwa na mawazo ya mubaya na tabia za mubaya?

8 Yehova anajua kama itaomba wakati na nguvu juu tuepuke kuwa na mawazo na tabia za mubaya. (Zb. 103:13, 14) Hata vile, kupitia Neno yake, roho yake, na tengenezo yake, Yehova anatupatia hekima, nguvu, na musaada wenye tuko nao lazima ili kufanya mabadiliko. Bila shaka tayari alishakukusaidia. Muache basi tuzungumuzie mambo fulani yenye tunaweza kufanya ili kuvua utu wa zamani hata zaidi na kustahili kubatizwa.

9. Neno ya Mungu inaweza kukusaidia kufanya nini?

9 Utumie Biblia ili kujichunguza kwa ukaribu. Neno ya Mungu iko sawa vile kio yenye inaweza kutusaidia kuchunguza namna yetu ya kufikiri, kusema na ya kutenda. (Yak. 1:22-25) Mwalimu wako wa Biblia na Wakristo wengine wakomavu wanaweza kukupatia muongozo. Kwa mufano, wanaweza kutumia Maandiko ili kukusaidia kujua uwezo wako na uzaifu wako. Wanaweza kukufundisha namna ya kupata habari yenye inategemea Biblia yenye kutoa shauri juu ya namna ya kupambana na tabia za mubaya. Na siku zote Yehova iko tayari kukusaidia. Anajua muzuri namna anaweza kukusaidia juu anajua mambo yenye iko mu moyo wako. (Mez. 14:10; 15:11) Kwa hiyo, ukuwe na zoezi ya kusali kwake na kujifunza Neno yake kila siku.

10. Mufano wa Elie umekufundisha nini?

10 Ukuwe hakika kama kanuni za Yehova ni za muzuri zaidi. Tunaweza kupata faida kupitia mambo yote yenye Yehova anatuambia kufanya. Wale wenye wanaishi kulingana na kanuni zake wanajiheshimisha, wako na kusudi mu maisha na wako na furaha ya kweli. (Zb. 19:7-11) Lakini, wale wenye wanakatala kanuni za Yehova wanapata matokeo ya mubaya yenye inatokana na matendo ya mwili. Ona mambo yenye Elie alisema kuhusu kukatala kanuni za Mungu. Alikomalishwa na wazazi wenye wanamupenda Yehova. Lakini wakati Elie alianza kukomala alichagula marafiki wabaya. Alianza kutumia dawa za kulewesha, kuishi maisha mapotovu, na kuiba. Elie aliona kama kasirani yake iliongezeka na akakuwa mwenye kupenda vita sana. Anasema hivi: “Kwa kawaida, nilianza kufanya mambo yenye nilifundishwa kuwa Mukristo hapaswe kufanya.” Hata vile, Elie hakusahau mambo yenye alijifunza wakati alikuwa kijana. Ku mwisho alianza tena kujifunza Biblia. Alijikaza sana kuachana na tabia zake za mubaya na alibatizwa mu 2000. Namna gani kuishi kulingana na kanuni za Yehova kulimuletea faida? Elie anasema tena hivi: “Kwa sasa niko na amani ya akili na zamiri safi.” * Sawa vile ile mufano inaonyesha, wale wenye wanakatala kanuni za Yehova wanajiumizaka wao wenyewe. Hata vile, Yehova iko tayari kuwasaidia wabadilike.

11. Ni mambo gani Yehova anachukia?

11 Ujifunze kuchukia mambo yenye Yehova anachukia. (Zb. 97:10) Biblia inaonyesha kama Yehova anachukia “macho yenye majivuno, ulimi wa uongo, na mikono yenye kumwanga damu yenye haina kosa.” (Mez. 6:16, 17) Anachukia pia “watu wenye jeuri na wadanganyifu.” (Zb. 5:6) Yehova anachukia sana tabia na matendo ya vile na njo maana aliharibu waovu wote wa siku ya Noa, juu walikuwa walishajaza dunia na jeuri. (Mwa. 6:13) Fikiria mufano ingine. Kupitia nabii Malaki, Yehova alisema kama anachukia wale wenye kutenda kwa udanganyifu juu ya kuvunja ndoa. Mungu anakatala ibada yao na atawahukumu juu ya matendo yao.​—Mal. 2:13-16; Ebr. 13:4.

Kufanya jambo yenye Yehova anaona kuwa ya mubaya kunapaswa kutuchukiza sawa vile kula chakula ya kuoza (Ona fungu ya 11-12)

12. ‘Kuchukia sana mambo maovu’ inamaanisha nini?

12 Yehova anapenda ‘tuchukie sana mambo maovu.’ (Ro. 12:9) Maneno ‘kuchukia sana’ inaonyesha hisia kubwa sana. Inamaanisha kuchukizwa sana na jambo fulani. Unaweza kujisikia namna gani kama wanakuambia ukule chakula fulani yenye ilishaoza? Kuwaza tu juu ya ile kunaweza kufanya usikie sawa vile unataka tapika. Ni vile pia tunapaswa kujisikia wakati mawazo ya kufanya jambo yenye Yehova anasema ni ya mubaya inatukuya mu akili.

13. Juu ya nini tunapaswa kulinda mawazo yetu?

13 Ulinde mawazo yako. Mawazo yetu inakuwaka na matokeo fulani juu ya matendo yetu. Njo maana Yesu alitufundisha kama tunapaswa kuepuka mawazo ya mubaya yenye inaweza kufanya tuangukie mu zambi nzito. (Mt. 5:21, 22, 28, 29) Bila shaka, tunapendaka kufurahisha Baba yetu wa mbinguni. Njo maana ni jambo ya lazima sana kutosha mara moya mawazo ya mubaya yenye inakuya mu akili yetu!

14. Maneno yetu inaonyesha nini, na ni maulizo gani tunapaswa kufikiria?

14 Ukuwe muangalifu na maneno yenye unasema. Yesu alisema: “Mambo yenye yanatoka katika kinywa yanatoka katika moyo.” (Mt. 15:18) Maneno yetu inaonyeshaka vile tuko kabisa kwa ndani. Kwa hiyo, ujiulize hii maulizo: ‘Nakatalaka kusema uongo, hata kama kusema kweli itaniletea magumu? Tayari niko mu ndoa, lakini je, nakuwaka muangalifu juu nisichezee kimapenzi mwanaume ao mwanamuke fulani, ikuwe iko mu ndoa ao hapana? Najibiaka kwa upole wakati mutu fulani ananikwaza?’ Ni muzuri kufikiria sana ile maulizo. Maneno yako iko sawa mushono wenye unaunganishaka nguo. Kama tunafanya yetu yote juu mazungumuzo yetu isikuwe na maneno ya uongo, machafu, na yenye matusi, ile itafanya ikuwe mwepesi kwetu kuvua utu wa zamani.

15. Kupigilia misumari utu wetu “kwenye muti” kunamaanisha nini?

15 Ukuwe tayari kufanya mambo yenye inaomba kufanya. Mutume Paulo alitumia mufano ili kutufundisha kama ni jambo ya maana sana kubadilisha namna yetu ya kuishi. Aliandika kama tunapaswa kupigilia misumari utu wetu wa zamani “kwenye muti.” (Ro. 6:6) Yesu alikuwa tayari kupigiliwa misumari kwenye muti ili kumufurahisha Yehova. Vilevile, juu tumufurahishe Yehova tunapaswa kuwa tayari kuondoa matendo yenye anachukia. Ni kwa kufanya tu ile mambo njo tunaweza kuwa na zamiri safi na kuwa na tumaini ya kuishi milele. (Yoh. 17:3; 1 Pe. 3:21) Tusisahau kama Yehova hawezi kubadilisha kanuni zake juu tu ya kutufurahisha. Lakini, ni siye njo tunapaswa kubadilisha namna yetu ya kuwa na kujipatanisha na kanuni zake.​—Isa. 1:16-18; 55:9.

16. Juu ya nini unapaswa kuazimia kuendelea kupiganisha tamaa za mubaya?

16 Uendelee kupiganisha tamaa za mubaya. Hata kisha kubatizwa utaendelea kupiganisha tamaa za mwili. Fikiria mufano wa Maurício. Wakati alikuwa kijana alianza kuwa na mwenendo muchafu wa kulala na wanaume wenzake. Siku moya akakutana na Mashahidi wa Yehova na akaanza kujifunza Biblia. Kisha kufanya mabadiliko mu maisha yake, akabatizwa mu 2002. Hata kama ameshamutumikia Yehova kwa miaka mingi, Maurício anasema hivi: “Kusema kweli, nilipaswa kupiganisha tamaa zangu za mubaya wakati fulani.” Hakuacha ile imuvunje moyo. Lakini, anasema hivi: “Natiwaka moyo kujua kama wakati nachagula kutotenda kulingana na tamaa zangu ninamufurahisha Yehova.” *

17. Mu mufano wa Nabiha nini njo unaona kuwa yenye kutia moyo?

17 Usali kwa Yehova ili kupata musaada, na utegemee roho yake hapana nguvu yako. (Gal. 5:22; Flp. 4:6) Tunapaswa kujikaza sana kama tunapenda kuvua utu wetu wa zamani. Fikiria mufano wa Nabiha. Baba yake alimuachaka wakati alikuwa tu na miaka sita. Anasema hivi: “Ile ilinileteaka huzuni sana.” Wakati alikuwa anakomala, Nabiha alifikia kuwa mwenye kukasirika sana na mwenye kupenda kupigana. Akaanza kuuzisha dawa za kulewesha, akakamatwa na kisha akafungwa kwa miaka fulani mu gereza. Mashahidi wa Yehova wenye walienda tembelea gereza walianza kujifunza Biblia pamoya naye. Nabiha alianza kufanya mabadiliko makubwa. Anasema hivi: “Ilikuwa mwepesi kwangu kuachana na tabia fulani za mubaya. Lakini ilikuwa nguvu sana kwangu kuacha kuvuta tumbako.” Nabiha alipiganisha ile hali zaidi ya mwaka moya na kisha akaacha kuvuta tumbako. Nini njo ilimusaidia? Anasema hivi: “Kusali kikawaida njo kulinisaidia kuacha.” Kwa sasa anaambia wengine hivi: “Niko hakika kama, vile niliweza kufanya mabadiliko ili kumupendeza Yehova, kila mutu anaweza kufanya vile pia!” *

UNAWEZA KUSTAHILI KUBATIZWA!

18. Kulingana na 1 Wakorinto 6:9-11, watumishi wengi wa Mungu waliweza kufanya nini?

18 Mu karne ya kwanza, wanaume fulani na wanamuke fulani wenye Yehova alichagula ili kutawala pamoya na Kristo, walikuwa wanafanya matendo fulani ya mubaya zamani. Kwa mufano, walikuwa wazinifu, wezi, na wengine walikuwa wanafanya matendo ya kulala na wanaume wenzao ao na wanamuke wenzao. Lakini, kwa musaada wa roho takatifu ya Mungu walibadilisha utu wao. (Soma 1 Wakorinto 6:9-11.) Ni vile pia leo, Biblia imesaidia mamilioni ya watu kufanya mabadiliko mu maisha yao. * Wameachana kabisa na tabia za mubaya zenye haikukuwa kabisa mwepesi kuacha. Mufano wao unaonyesha kama na weye pia unaweza kufanya mabadiliko mu utu wako na kupiganisha tabia za mubaya juu ustahili kubatizwa.

19. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

19 Zaidi ya kujikaza sana ili kuvua utu wa zamani, wale wenye wanapenda kubatizwa wanapaswa kujikaza sana kuvaa utu mupya. Habari yenye kufuata itazungumuzia namna tunaweza kufanya vile na namna wengine wanaweza kutusaidia.

WIMBO 41 Tafazali, Sikia Sala Yangu

^ Juu tustahili kubatizwa tunapaswa kuwa tayari kufanya mabadiliko mu maisha yetu. Hii habari itatusaidia kujua utu wa zamani njo nini, juu ya nini tunapaswa kuvua utu wa zamani, na namna gani tunaweza kufanya vile. Habari yenye kufuata itazungumuzia namna tunaweza kuvaa utu mupya hata kisha kubatizwa.

^ MAFASIRIO YA MANENO FULANI: ‘Kuvua utu wa zamani’ kunamaanisha kuachana na matendo na muelekeo wowote wenye unamuchukiza Yehova. Tunapaswa kuanza kufanya vile mbele tubatizwe.​—Efe. 4:22.

^ Ili kujua mengi zaidi ona habari “Biblia Inabadili Maisha​—‘Nilihitaji kumrudia Yehova,’” ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 4, 2012.

^ Ili kujua mengi zaidi ona habari “Biblia Inabadili Maisha​—‘Walinitendea kwa Fadhili Sana,’” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 5, 2012.

^ Ili kujua mengi zaidi ona habari “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu​—‘Nilifikia Kuwa Kijana Mwanamuke Mwenye Kukasirika Haraka na Muchokozi,’” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 10, 2012.

^ Ona kisanduku “ Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu.”

^ MAFASIRIO YA PICHA: Kuvua tabia na matendo ya mubaya iko sawa vile kuvua nguo ya zamani.