Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 11

Endelea Kuvaa “Utu Mupya” Kisha Ubatizo

Endelea Kuvaa “Utu Mupya” Kisha Ubatizo

“Muvae utu mupya.”​—KOL. 3:10.

WIMBO 49 Tufurahishe Moyo wa Yehova

KIFUPI YA HABARI *

1. Mawazo yetu inakuwaka na matokeo gani juu ya utu wetu? Fasiria.

 IKUWE tumebatizwa kumepita tu masiku kidogo ao kwa miaka mingi, siye wote tunapenda kuwa na utu wenye Yehova anapenda. Juu tukuwe na ile utu tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu namna yetu ya kufikiri. Juu ya nini? Ni juu mambo yenye tunawazaka inakuwaka na matokeo fulani juu ya utu wetu. Kama kila mara tunakuwaka tunafikiri juu ya namna tunaweza kujifurahisha siye wenyewe ile itafanya tuseme na kufanya mambo ya mubaya. (Efe. 4:17-19) Lakini kama tunajaza akili yetu na mawazo ya muzuri ile itafanya tutende na tuseme mu njia yenye inamufurahisha Baba yetu Yehova.​—Gal. 5:16.

2. Ni maulizo gani tutazungumuzia mu hii habari?

2 Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia hatuwezi kuzuia mawazo yote ya mubaya iingie mu akili yetu. Lakini tunaweza kuchagula kutotenda kulingana na ile mawazo. Mbele tubatizwe tunapaswa kuacha kusema na kutenda mu njia yenye Yehova anachukia. Ile njo hatua ya kwanza na ya maana sana kama tunapenda kuvua utu wa zamani. Lakini, ili kumupendeza kabisa Yehova tunapaswa kutii hii amri: “Muvae utu mupya.” (Kol. 3:10) Mu hii habari tutajibia maulizo yenye kufuata: “Utu mupya” njo nini? Namna gani tunaweza kuvaa utu mupya na kuendelea kufanya vile?

“UTU MUPYA” NJO NINI?

3. Kulingana na Wagalatia 5:22, 23, “utu mupya” njo nini na namna gani mutu anaweza kuuvaa?

3 “Utu mupya” ni namna ya kuwaza na ya kutenda yenye inaonyesha utu wa Yehova. Mutu anavaa utu mupya kwa kuonyesha tunda ya roho ya Mungu, kwa kuacha roho takatifu iongoze mawazo yake, hisia zake na matendo yake. (Soma Wagalatia 5:22, 23.) Kwa mufano, anamupenda Yehova na watu wake. (Mt. 22:36-39) Tena mutu wa vile anaendelea kuwa na furaha hata kama iko anapambana na magumu. (Yak. 1:2-4) Ni mufanya-amani. (Mt. 5:9) Ni muvumilivu na anatendea wengine kwa upendo. (Kol. 3:13) Anapenda mambo ya muzuri na anaifanya. (Lu. 6:35) Anaonyesha kupitia matendo yake kama iko na imani ya nguvu katika Baba yake wa mbinguni. (Yak. 2:18) Anatulia wakati wanamuchokoza na anajizuia wakati anajaribiwa.​—1 Ko. 9:25, 27; Tit. 3:2.

4. Ili kuvaa utu mupya, juu ya nini tunapaswa kukomalisha sifa zote zenye kutajwa mu Wagalatia 5:22, 23 na mu maandiko ingine?

4 Juu ya kuvaa utu mupya tunapaswa kukomalisha sifa zote zenye kutajwa mu Wagalatia 5:22, 23 na mu maandiko ingine. * Sawa vile mutu anapaswa kuvaa kwa wakati moya nguo mbalimbali, ni vile pia tunapaswa kukomalisha zile sifa zote kwa wakati moya. Juu sifa mingi kati ya zile sifa ziko na uhusiano na sifa zingine. Kwa mufano, kama kweli unapenda jirani yako, utamutendea kwa uvumilivu na kwa wema. Na juu ya kuwa kabisa mutu muzuri, unapaswa kuwa mutulivu na mwenye kujizuia.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUVAA UTU MUPYA?

Kadiri tunajifunza kufikiri sawa Yesu, ni vile tutaweza kabisa kuonyesha utu wake (Ona fungu ya 5, 8, 10, 12, 14)

5. Inamaanisha nini kuwa na “akili ya Kristo,” na juu ya nini tunapaswa kujifunza maisha ya Yesu? (1 Wakorinto 2:16)

5 Soma 1 Wakorinto 2:16. Ili kuvaa utu mupya tunapaswa kuwa na “akili ya Kristo.” Mu maneno ingine, tunapaswa kujifunza namna Yesu anawaza na kisha tunamuiga. Yesu anaonyesha tunda ya roho ya Mungu kwa ukamilifu. Sawa vile kio fulani yenye haina kasoro, Yesu anaonyesha sifa za Yehova kwa ukamilifu. (Ebr. 1:3) Kadiri tunafikiri sawa Yesu, ni vile tutatenda kama yeye na tutapata faida kubwa sana kwa kuiga utu wake.​—Flp. 2:5.

6. Ni mambo gani hatupaswe kusahau wakati tuko tunajikaza kuvaa utu mupya?

6 Inawezekana kabisa kwetu kufuata mufano wa Yesu? Pengine tunaweza kuwaza hivi: ‘Yesu ni mukamilifu. Siwezi kabisa kuwa sawa yeye!’ Kama unawaza vile, kumbuka hii mambo. Kwanza, tuliumbwa juu tukuwe sawa Yehova na Yesu. Kwa hiyo, tunaweza kuchagula kuwaiga na tunaweza kuwa sawa vile wao kwa kiasi fulani. (Mwa. 1:26) Pili, roho takatifu ya Mungu njo nguvu kubwa sana mu ulimwengu wote. Kupitia ile nguvu unaweza kutimiza mambo yenye hauwezi kufanya kwa uwezo wako. Tatu, Yehova hatazamie kama unaweza kuonyesha sasa tunda yake ya roho kwa ukamilifu. Njo maana alishawekea wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi hapa ku dunia miaka 1 000 juu wakuwe wakamilifu. (Ufu. 20:1-3) Yehova anatazamia tufanye yote yenye tunaweza na kumutegemea juu tupate musaada.

7. Tutachunguza sasa mambo gani?

7 Namna gani tunaweza kabisa kumuiga Yesu? Tutachunguza kwa kifupi sifa ine za tunda ya roho ya Mungu. Wakati tutakuwa tunachunguza kila sifa tutaona ni somo gani tunajifunza kutoka kwa Yesu. Wakati tutakuwa tunafanya vile, tutaona maulizo fulani yenye itatusaidia kuchunguza ili kuona ikiwa tungali bado tunaendelea kuvaa utu mupya.

8. Namna gani Yesu alionyesha upendo?

8 Yesu alijitoa kwa ajili ya Baba yake na kwa ajili yetu juu alimupenda Baba yake sana. (Yoh. 14:31; 15:13) Namna ya kuishi ya Yesu hapa ku dunia inaonyesha kama alipenda watu. Kila siku alikuwa mwenye upendo na mwenye huruma, hata wakati wenye watu fulani walimupinga. Njia moya kubwa yenye alionyesha kama alipenda sana watu, ni kwa kuwafundisha juu ya Ufalme wa Mungu. (Lu. 4:43, 44) Yesu alionyesha pia kama alipenda Mungu na wanadamu kwa kuwa tayari kuteseka na kufa mu mikono ya watenda-zambi. Kwa kufanya vile, alitufungulia njia ya kupata uzima wa milele.

9. Namna gani tunaweza kumuiga Yesu katika kuonyesha upendo?

9 Tulijitoa kwa Yehova Baba yetu wa mbinguni na kubatizwa juu tunamupenda. Kwa hiyo, sawa vile Yesu, tunapaswa kuonyesha kama tunamupenda Yehova mu namna yenye tunatendea wengine. Mutume Yohana aliandika hivi: “Mwenye hamupendi ndugu yake mwenye amemuona, hawezi kumupenda Mungu mwenye hajaonaka.” (1 Yo. 4:20) Unaweza kujiuliza hivi: ‘Upendo wangu kwa wengine umeongezeka? Natendeaka wengine kwa huruma hata kama wao wananitendea kwa ukali? Je, upendo njo unanichocheaka kutumia wakati wangu na mali yangu ili kusaidia wengine wamujue Yehova? Nakuwaka tayari kufanya vile hata kama watu wengi hawafurahie bidii yenye ninaonyesha ao wakati wananipinga? Ninaweza kupata njia mbalimbali ili nipitishe wakati zaidi mu kazi ya kufanya wanafunzi?’​—Efe. 5:15, 16.

10. Nini inaonyesha kama Yesu alikuwa mufanya-amani?

10 Yesu alikuwa mufanya-amani. Wakati watu walimutendea mubaya hakurudisha ubaya kwa ubaya. Lakini alifanya zaidi ya ile. Yesu alikamata hatua ya kufanya amani na alitia moyo wengine wafanye vile wakati wanakosana. Kwa mufano, aliwafundisha kama ikiwa wanapenda Yehova akubali ibada yao, wanapaswa kufanya amani pamoya na ndugu zao. (Mt. 5:9, 23, 24) Na mara kwa mara alisaidia mitume wake kutatua mabishano yenye ilikuwa kati yao kuhusu nani alikuwa mukubwa kati yao.​—Lu. 9:46-48; 22:24-27.

11. Namna gani tunaweza kuwa wafanya-amani?

11 Juu ya kuwa mufanya-amani, haiombe tu kuepuka mambo yenye inaweza kufanya watu wasielewane. Inaomba pia kukamata hatua ya kufanya amani pamoya na wengine na kutia moyo ndugu na dada zetu wafanye amani wakati wanakosana. (Flp. 4:2, 3; Yak. 3:17, 18) Unaweza kujiuliza hii maulizo: ‘Niko tayari kufanya nini ili kufanya amani na wengine? Wakati ndugu ao dada ananikosea namuwekeaka kinyongo? Nachungaka yeye njo akamate hatua ya kwanza ya kuya kuniona ili kurudisha amani, ao miye njo nakamataka ile hatua hata kama inaonekana kuwa yeye njo alifanya ile jambo itokee? Wakati inafaa natiaka moyo wale wenye walikosana wafanye amani kati yao?’

12. Namna gani Yesu alionyesha fazili?

12 Yesu alikuwa mwenye fazili. (Mt. 11:28-30) Alionyesha fazili kwa kutendea wengine muzuri na kwa usawaziko, hata mu hali ya nguvu sana. Kwa mufano, wakati mwanamuke Mufoinike alimuomba aponyeshe mutoto wake, ku mwanzo Yesu hakufanya mambo yenye ule mwanamuke alimuomba. Lakini wakati alionyesha imani kubwa, kwa fazili, Yesu aliponyesha mutoto wake. (Mt. 15:22-28) Hata kama Yesu alikuwa mwenye fazili hakuepuka kupatia watu shauri. Wakati fulani alionyesha fazili kwa kuambia waziwazi watu wenye alipenda fasi kwenye walikosea. Kwa mufano, wakati Petro alijaribu kuvunja Yesu moyo juu asifanye mapenzi ya Yehova, alimurekebisha mbele ya wanafunzi wengine. (Mk. 8:32, 33) Alifanya vile haiko juu ya kumushushia Petro heshima, lakini juu ya kumuzoeza na kusaidia wanafunzi wengine wasikuwe na kimbelembele. Inawezekana Petro alijisikia mubaya lakini nizamu yenye alipata ilimuletea faida.

13. Namna gani tunaweza kuonyesha fazili ya kweli?

13 Juu ya kuonyesha kama tunapenda kutendea kwa fazili wale wenye tunapenda, wakati fulani inaomba kuwatolea shauri. Wakati unafanya vile, umuige Yesu kwa kufanya shauri yako itegemee kanuni zenye zinapatikana mu Neno ya Mungu. Zungumuza nao kwa heshima. Ukuwe hakika kama wanapenda kufanya mambo ya muzuri na utumainie kama wale wenye kumupenda Yehova na wenye kukupenda watakubali shauri yako ya upendo. Ujiulize hii maulizo: ‘Niko na uhodari wa kuambia waziwazi mutu mwenye napendaka kosa yenye alifanya? Kama inaomba kabisa nitoe shauri nasemaka kwa fazili, ao kwa ukali? Nini njo inanichochea nitoe shauri? Natoa shauri juu nilishamukasirikia ule mutu ao juu napenda kumusaidia?’

14. Namna gani Yesu alionyesha kama anapenda mambo ya muzuri?

14 Yesu hajue tu mambo ya muzuri lakini pia anaifanyaka. Yesu anapenda Baba yake, njo maana sikuzote anafanyaka mambo ya muzuri na nia ya muzuri. Mara mingi mutu muzuri anatafutaka njia mbalimbali ili kusaidia wengine na kuwafanyia mambo ya muzuri. Haitoshe tu kujua kama hii njo mambo ya muzuri ya kufanya, lakini tunapaswa njo kuifanya na nia ya muzuri. Mutu anaweza kujiuliza hivi, ‘Inawezekana kabisa kufanya mambo ya muzuri na nia ya mubaya?’ Ndiyo. Kwa mufano, Yesu alizungumuzia watu fulani wenye walipatia maskini zawadi, lakini walihakikisha kama wengine waliona mambo walifanya na kuwasifu. Hata kama zile zawadi zilikuwa za muzuri, Yehova hakuzifurahia.​—Mt. 6:1-4.

15. Namna gani tunaweza kuonyesha kabisa kama tuko watu wazuri?

15 Tunaweza kuwa watu wazuri kama tu tunafanya mambo ya muzuri na nia ya muzuri. Kwa hiyo, ujiulize hivi: ‘Nafanyaka kabisa mambo ya muzuri kuliko tu kuijua? Nini njo inanichocheaka kufanya mambo ya muzuri?’

NAMNA GANI TUNAWEZA KULINDA UTU MUPYA MU HALI YA MUZURI?

16. Kila siku tunapaswa kufanya nini na juu ya nini?

16 Hatupaswe kuwaza kama, ikiwa mutu anabatizwa hana tena lazima ya kuendelea kuvaa utu mupya. Utu mupya uko sawa vile “nguo ya mupya” yenye inapaswa kuwekwa mu hali ya muzuri. Njia moya yenye inaweza kutusaidia kulinda utu mupya ni kuonyesha tunda ya roho ya Mungu kila siku. Juu ya nini? Ni juu Yehova ni Mungu mwenye kutenda, na roho yake ni nguvu ya utendaji. (Mwa. 1:2) Kwa hiyo, kila sehemu ya tunda ya roho inaweza na inapaswa kutuchochea kutenda. Kwa mufano mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: “Imani bila matendo imekufa.” (Yak. 2:26) Tunaweza kusema pia vile kuhusu sifa zingine za tunda ya roho ya Mungu. Kila wakati tunaonyesha tunda ya roho, tunatoa ushuhuda kama roho ya Mungu iko inatenda ndani yetu.

17. Tunapaswa kutenda namna gani kama tunashindwa kuonyesha tunda ya roho?

17 Wakati fulani hata Wakristo wenye wamebatizwa kumepita miaka mingi wanaweza kushindwa kuonyesha tunda ya roho. Lakini jambo ya maana ni kujikaza kuendelea kuonyesha tunda ya roho. Fikiria hii mufano. Kama unapasula nguo yenye unapendaka sana, utaitupa mara moya? Hapana. Kwa kawaida utaitengeneza kama inawezekana. Na utajikaza kuwa muangalifu siku ingine. Vilevile, usivunjike moyo kama mu hali fulani unashindwa kutendea mutu fulani kwa fazili, uvumilivu ao kwa upendo. Kulomba musamaha kutoka ku moyo njo kutakusaidia ulinde urafiki wa muzuri pamoya na ule mutu. Na uazimie kufanya muzuri zaidi wakati wenye kuja.

18. Unaweza kuwa hakika na jambo gani?

18 Tuko wenye shukrani sana kwa ajili ya mufano muzuri wenye Yesu alituachia! Kadiri tunaiga namna yake ya kufikiri na namna yake ya kuwa, itakuwa mwepesi kwetu kutenda sawa yeye. Kadiri tutatenda sawa Yesu, ni vile tutaweza kuvaa muzuri zaidi utu wetu mupya. Mu hii habari tumezungumuzia tu sifa ine za tunda ya roho ya Mungu. Juu ya nini tusikamate wakati wa kuchunguza sifa zingine za tunda ya roho na kuona ni kwa kiasi gani tuko tunazitumikisha? Utapata habari za mingi kuhusu hii jambo mu kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova chini ya kichwa “Maisha ya Kikristo” kisha uende kwenye sehemu “Tunda la Roho.” Ukuwe hakika kama ikiwa unafanya sehemu yako, Yehova atakusaidia uvae utu mupya na uendelee kufanya vile.

WIMBO 127 Ninapaswa Kuwa Mutu wa Namna Gani?

^ Tunaweza kuvaa “utu mupya” hata kama tulikomalia wapi. Juu tuweze kufanya vile, tunapaswa kubadilisha namna yetu ya kufikiri na kujikaza kuwa kama Yesu. Mu hii habari, tutazungumuzia mifano fulani yenye kuonyesha namna Yesu alikuwa anatenda na kufikiri. Tutazungumuzia pia namna tunaweza kuendelea kumuiga kisha kubatizwa.

^ Wagalatia 5:22, 23 haionyeshe liste yote ya sifa za muzuri zenye roho takatifu ya Mungu inaweza kutusaidia kukomalisha. Ili kupata maelezo zaidi, ona sehemu “Maulizo ya Wasomaji Wetu” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 6, 2020.