Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 12

Unaona Mambo Yenye Zekaria Aliona?

Unaona Mambo Yenye Zekaria Aliona?

“‘Kwa roho yangu,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema.”​—ZEK. 4:6.

WIMBO 73 Utusaidie Tusiogope

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni jambo gani ya muzuri yenye ingepata Wayahudi wahamishwa?

 WAYAHUDI walikuwa na furaha sana. Yehova Mungu “alichochea roho ya Mufalme Koreshi wa Uajemi” juu aachilie Waisraeli wenye walikuwa walishapitisha miaka mingi mu Babiloni mu utumwa. Mufalme alitoa tangazo juu Wayahudi warudie kwao “na kujenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli.” (Ezr. 1:1, 3) Ile ilikuwa amri ya kufurahisha sana! Ilimaanisha kama Wayahudi wangeweza tena kuabudu Mungu wa kweli mu inchi yenye alikuwa amewapatia.

2. Wakati Wayahudi wahamishwa walirudia Yerusalemu walifanya nini kwanza?

2 Mu 537 M.K.Y., Wayahudi wa kwanza wahamishwa walifika mu Yerusalemu, yenye ilikuwa inchi kubwa ya ufalme wa kusini wa Yuda. Wayahudi wenye walirudia, mara moya walianza kujenga upya hekalu, na mu 536 hivi M.K.Y., walikuwa tayari walishamaliza musingi wa hekalu!

3. Nani njo alipinga Wayahudi na namna gani?

3 Wakati tu walianza kujenga upya hekalu, wale wahamishwa walianza kupambana na upinzani wa nguvu sana. Taifa zenye ziliwazunguka ‘zikaendelea kuwavunja moyo watu wa Yuda na kuwakatisha tamaa ili wasijenge.’ (Ezr. 4:4) Ilikuwa hali ya mubaya sana kwa Wayahudi na tena iliendelea kuharibika hata zaidi. Mu 522 M.K.Y., Artashasta alifikia kuwa mufalme mupya wa Uajemi. * Wale wapinzani waliwaza kama juu kulikuwa mufalme mupya wangeweza kuachisha kazi ya kujenga kwa ‘kutunga matatizo kwa kutumia sheria.’ (Zb. 94:20) Walituma barua kwa mufalme Artashasta na kusema kama Wayahudi walikuwa wanapanga kumuasi. (Ezr. 4:11-16) Mufalme aliamini uongo wao na akaamuru waache kazi ya kujenga hekalu. (Ezr. 4:17-23) Juu walikatazwa, Wayahudi walisimamisha kazi ya kujenga hekalu.​—Ezr. 4:24.

4. Yehova alifanya nini kisha kuona wapinzani wanasimamisha kazi ya hekalu? (Isaya 55:11)

4 Watu wa inchi fulani wenye hawakumuabudu Yehova na watu fulani wa utawala wa Uajemi waliazimia kabisa kuachisha kazi ya kujenga upya hekalu. Lakini Yehova alipenda Wayahudi wamalize kazi ya kujenga upya hekalu, na sikuzote anatimizaka kusudi yake. (Soma Isaya 55:11.) Yehova alichagula Zekaria ili kuwa nabii wake na alimupatia maono munane yenye kufurahisha, yenye alipaswa kuambia Wayahudi ili kuwatia moyo. Ile maono ilisaidia Wayahudi kuona kama haikuomba waogope wapinzani wao na iliwatia moyo waendelee na kazi yenye Yehova alipenda wafanye. Mu maono ya tano, Zekaria aliona kinara cha taa na mizeituni mbili.

5. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

5 Wakati fulani siye wote tunaweza kuvunjika moyo. Kwa hiyo, tunaweza kupata faida kupitia kitia moyo yenye Yehova alipatiaka Waisraeli kupitia maono ya tano ya Zekaria. Kuelewa ile maono kunaweza kutusaidia kumutumikia Yehova kwa uaminifu wakati watu wanatupinga, wakati hali yetu inabadilika, na wakati tunapata muongozo wenye hatuelewe.

WAKATI WATU WANATUPINGA

Zekaria aliona maono ya mizeituni mbili yenye kuwa ndani mafuta yenye kutumiwa mu kinara cha taa yenye ilikuwa na taa saba (Ona fungu ya 6)

6. Namna gani maono ya kinara cha taa na mizeituni mbili yenye kuzungumuziwa mu Zekaria 4:1-3 ilipatia Wayahudi uhodari? (Ona picha ku jalada.)

6 Soma Zekaria 4:1-3. Ile maono kuhusu kinara cha taa na mizeituni mbili ilipatia Wayahudi uhodari wa kupambana na upinzani. Namna gani? Uliona kama ile kinara cha taa iliendelea kuwa na mafuta? Mafuta yenye ilikuwa ndani ya mizeituni mbili ilikuwa inavuya mu bakuli, kisha mafuta yenye ilikuwa ndani ya ile bakuli ilikuwa inaenda mu taa saba za kinara cha taa. Ile mafuta ilisaidia zile taa ziendelee kuwaka bila kuzimika. Zekaria aliuliza hivi: “Vitu hivi vinamaanisha nini?” Malaika akamujibia kwa kumutolea hii ujumbe ya Yehova: “‘Hapana kwa nguvu za jeshi, wala kwa nguvu, lakini kwa roho yangu,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema.” (Zek. 4:4, 6) Mafuta yenye ilikuwa inatoka ndani ya ile miti ilifananisha roho takatifu ya Yehova yenye nguvu sana, nguvu yenye haiwezi kuisha. Roho takatifu ya Mungu ilikuwa yenye nguvu sana kuliko Utawala wote wa Uajemi. Juu Yehova alikuwa anategemeza wale wenye walikuwa wanajenga hekalu, ile ingefanya wamalize kazi yao ijapokuwa upinzani wowote. Ile ilikuwa ujumbe wenye kutia moyo sana. Wayahudi walikuwa tu na lazima ya kumutumainia Yehova na kuanza tena kujenga. Njo vile walifanya kabisa hata kama kazi ilikuwa ilishakatazwa.

7. Ni badiliko gani yenye ilitokea yenye ilitia moyo kwa kiasi fulani wale wenye walikuwa wanajenga hekalu ?

7 Badiliko fulani yenye ilitokea ilitia moyo kwa kiasi fulani wale wenye walikuwa wanajenga hekalu. Ni badiliko gani? Mu 520 M.K.Y., mufalme mupya, Dario wa kwanza alikuwa anatawala Uajemi. Mu mwaka wa pili wa utawala wake, alivumbula kama kazi ya kujenga hekalu ilikatazwa na ile haikupatana na sheria. Kisha Dario alitoa amri ili waendelee na kazi. (Ezr. 6:1-3) Ile tangazo ya mufalme ilishangaza kila mutu, lakini alifanya zaidi ya ile. Mufalme aliamuru watu wenye kuwazunguka waache kupinga Wayahudi na wawapatie makuta na kila kitu yenye walikuwa nayo lazima juu wamalize kazi ya kujenga upya hekalu! (Ezr. 6:7-12) Matokeo ilikuwa kwamba, Wayahudi walimaliza kazi ya kujenga hekalu kisha miaka ine hivi, mu 515 M.K.Y.​—Ezr. 6:15.

Utegemee nguvu ya Yehova wakati unapambana na upinzani fulani (Ona fungu ya 8)

8. Juu ya nini tunaweza kusema kama unaweza kuwa hodari wakati uko unapambana na upinzani?

8 Leo pia waabudu wengi wa Yehova wanapambana na upinzani. Kwa mufano, wamoja wanaishi mu mainchi kwenye kazi yetu inatiliwa vizuizi. Mu mainchi ya vile, ndugu zetu wanaweza kukamatwa na ‘kupelekwa mbele ya magavana na wafalme’ ili kuwatolea ushahidi. (Mt. 10:17, 18) Wakati fulani, kama kuko badiliko fulani mu utawala ile inaweza kusaidia kwa kiasi fulani. Ao muamuzi fulani mwenye kuwa na roho ya muzuri anaweza kamata uamuzi wenye unaweza kutusaidia tukuwe na uhuru zaidi. Mashahidi wengine wanapambana na upinzani wenye kuwa tofauti. Wanaishi mu inchi kwenye kuko uhuru wa kumuabudu Yehova, lakini wanaendelea kupambana na upinzani kutoka kwa watu wa familia yao wenye wanafanya yao yote ili kuwafanya waache kumutumikia Mungu wao. (Mt. 10:32-36) Mu hali za mingi watu wa familia, wanaacha kutupinga wakati wanatambua kama hawawezi kutukaza tuache kumutumikia Yehova. Na mu hali zingine, wale wenye ku mwanzo walikuwa wanatupinga sana wamefikia kuwa Mashahidi wenye bidii sana. Usiache kumutumikia Yehova wakati uko unapambana na upinzani. Ukuwe hodari. Usiogope kitu juu Yehova iko na weye na roho yake takatifu itakutegemeza!

WAKATI HALI YETU INABADILIKA

9. Juu ya nini Wayahudi fulani walivunjika moyo wakati waliona musingi wa hekalu ya mupya unawekwa?

9 Wakati musingi wa hekalu ya mupya uliwekwa, Wayahudi fulani wa zamani walilia. (Ezr. 3:12) Walionaka ile hekalu ya muzuri sana yenye Sulemani alijengaka, na waliwaza kama hii hekalu ya mupya ingekuwa ya “bure kwa kuilinganisha” na ile ya zamani. (Hag. 2:2, 3) Walivunjika moyo juu walilinganisha hekalu ya mupya na ile ya zamani. Maono ya Zekaria ingewasaidia wapate tena furaha yao. Namna gani?

10. Namna gani maneno ya malaika yenye kuwa mu Zekaria 4:8-10 ilisaidia Wayahudi wasiendelee kuvunjika moyo?

10 Soma Zekaria 4:8-10. Malaika alimaanisha nini wakati alisema kama Wayahudi ‘wangefurahi na kuona kamba ya kupima usawa katika mukono wa [gavana Muyahudi] Zerubabeli’? Kamba ya kupima usawa ni chombo yenye kuonyesha ikiwa kitu fulani iko yenye kunyooka ao kama iko sawa. Maneno ya malaika ilionyesha watu wa Mungu kama, hata kama hekalu ya mupya ilionekana kuwa tofauti na ile hekalu ya zamani yenye utukufu, ingemalizika na ingekuwa vile Yehova alipenda ikuwe. Yehova angeifurahia, sasa juu ya nini wao hawangeifurahia? Jambo yenye ilikuwa ya maana sana kwa Yehova ni wao wamuabudu mu hekalu mupya mu njia yenye Yeye alipenda. Kama Wayahudi wangemuabudu Yehova mu njia yenye anapenda na kutafuta kukubaliwa naye wangepata tena furaha yao.

Ukuwe na mutazamo muzuri wakati unapata mugao mupya (Ona fungu ya 11-12) *

11. Ni magumu gani yenye waabudu fulani wa Yehova wanapambana nayo leo?

11 Wakati hali inabadilika haiko mwepesi kwa wengi kati yetu. Wamoja kati ya wale wenye wamemutumikia Yehova mu utumishi wa wakati wote kwa muda murefu, wamepata mabadiliko fulani mu mugao wao. Wengine walilazimika kuacha mugao wenye walikuwa wanapenda juu ya miaka yao. Ni jambo ya kawaida kuwa na huzuni wakati mabadiliko sawa ile inatufikia. Ku mwanzo, pengine inaweza kuwa nguvu kuelewa ule uamuzi ao kukubaliana nao. Pengine, tunaweza kuwaza kama mbele ya pale mambo ilikuwa muzuri. Na pengine tunaweza kufikia kuvunjika moyo na kuwaza kama kwa sasa hatufanye mengi zaidi kwa ajili ya Yehova. (Mez. 24:10) Namna gani maono ya Zekaria inatusaidia kuendelea kujitolea zaidi kwa Mungu wetu?

12. Namna gani maono ya Zekaria inaweza kutusaidia tuendelee kuwa na furaha wakati hali yetu inabadilika?

12 Inaweza kuwa mwepesi kwetu kuzoea hali yetu ya mupya wakati tunajikaza kuona hali yetu sawa vile Yehova anaiona. Leo, iko anatimiza kazi ya maajabu sana na tuko na pendeleo kubwa sana ya kuwa wafanyakazi pamoya naye. (1 Ko. 3:9) Mugao wetu unaweza kubadilika, lakini upendo wa Yehova kwetu hauwezi. Njo maana, kama kuko badiliko fulani mu tengenezo yenye inakugusa weye kipekee, uepuke kujiuliza juu ya nini na nini njo ilifanya kukuwe ile badiliko. Kuliko kupenda maisha yako ikuwe sawa vile “siku za zamani,” muombe Yehova akusaidie uone mambo ya muzuri mu ile badiliko. (Muh. 7:10) Kuliko kuwaza juu ya mambo yenye hawezi tena kufanya, waza juu ya mambo yenye unaweza kufanya. Kupitia maono ya Zekaria, tunajifunza ulazima wa kuendelea kuwa na mutazamo muzuri. Ile njo itafanya tuendelee kuwa na furaha na waaminifu hata kama hali yetu inabadilika.

WAKATI NI NGUVU KUFUATA MUONGOZO FULANI

13. Pengine ni juu ya nini Waisraeli fulani waliwaza kama kuanza tena kujenga hekalu ilikuwa wazo ya mubaya?

13 Kazi ya kujenga upya hekalu ilikatazwa. Lakini Kuhani Mukubwa Yeshua (Yoshua) na Gavana Zerubabeli, wanaume wenye walichaguliwa ili kuongoza watu, “wakaanza kujenga upya nyumba ya Mungu.” (Ezr. 5:1, 2) Pengine Wayahudi fulani waliwaza kama ile ilikuwa uamuzi wa mubaya. Wayahudi hawangeweza kuficha kama walikuwa wanajenga hekalu na walijua kama maadui wao wangefanya yote yenye wangeweza ili kusimamisha kazi. Yoshua na Zerubabeli, wenye waliongoza kazi, walikuwa na lazima ya uhakikisho wenye kuonyesha kama Yehova alikuwa anawaunga mukono. Na waliupata. Namna gani?

14. Kulingana na Zekaria 4:12, 14, Kuhani Mukubwa Yoshua na Gavana Zerubabeli walipata uhakikisho gani?

14 Soma Zekaria 4:12, 14. Mu hii sehemu ya maono ya Zekaria, malaika anaonyesha nabii muaminifu wa Mungu kama, ile mizeituni mbili inafananisha “watiwa-mafuta wawili”, ni kusema, Yoshua na Zerubabeli. Malaika alisema kama ilikuwa sawa vile wale wanaume wawili walikuwa wenye ‘kusimama pembeni ya Bwana wa dunia yote,’ Yehova. Ile ilikuwa pendeleo kubwa sana! Yehova aliwatumainia. Kwa hiyo, Waisraeli wangeweza kutumainia jambo yoyote yenye wale wanaume waliwaambia wafanye juu Yehova aliwatumia wale wanaume ili kuongoza Waisraeli.

15. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunatii muongozo wa Yehova wenye kuwa mu Neno yake?

15 Njia moya yenye Yehova anaendelea kutumia leo ili kutolea watu wake muongozo ni Neno yake Biblia. Mu ile kitabu takatifu anatuambia namna ya kuabudu yenye Yeye anakubali. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunatii muongozo wenye tunapata mu Neno ya Mungu? Kwa kukazia uangalifu ule muongozo na kukamata wakati wa kuuelewa. Unaweza kujiuliza hivi: ‘Wakati nasoma Biblia ao moya kati ya vichapo vyetu nasimamaka kidogo ili kufikiri sana? Natafutaka kujua maana ya kweli fulani za Biblia zenye “ni nguvu kuelewa”? Ao nasomaka tu habari mbiombio?’ (2 Pe. 3:16) Kama tunakamata wakati wa kufikiri sana juu ya mambo yenye Yehova anatufundisha, tutaweza kufuata muongozo wake na kutimiza muzuri kazi yetu ya kuhubiri.​—1 Ti. 4:15, 16.

Utumainie muongozo wenye unapata kutoka kwa “mutumwa muaminifu na mwenye busara” (Ona fungu ya 16) *

16. Wakati hatuelewe kabisa muongozo wenye tunapata kutoka kwa “mutumwa muaminifu na mwenye busara” nini njo itatusaidia kuufuata?

16 Njia ingine yenye Yehova anatumia ili kututolea muongozo ni “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Wakati fulani, mutumwa muaminifu anaweza kututolea muongozo wenye hatuelewe kabisa. Kwa mufano, tunaweza kupewa maagizo fulani kuhusu namna ya kujitayarisha juu tuweze kupambana na musiba wa asili wenye pengine tunaweza kuwaza kama hautatokea mu eneo yetu. Ao pengine tunaweza kuwaza kama mutumwa muaminifu anapitisha mipaka wakati anatutolea maagizo fulani juu ya ugonjwa fulani wenye kuambukiza. Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunawaza kama maagizo yenye walitutolea haiko ya hekima? Tunaweza kupata faida kwa kufikiria namna Waisraeli walipata faida kwa kutenda kupatana na shauri yenye Yoshua na Zerubabeli waliwatolea. Tunaweza pia kufikiri juu ya habari za Biblia zenye tulishasoma. Wakati fulani, watu wa Mungu walitolewa muongozo wenye ulionekana sawa vile hauko wa muzuri ku macho ya wanadamu, lakini wenye ulifikia kuokoa uzima wao.​—Amu. 7:7; 8:10.

ONA MAMBO YENYE ZEKARIA ALIONA

17. Maono ya kinara cha taa na mizeituni mbili ilikuwa na matokeo gani juu ya Wayahudi?

17 Maono ya tano yenye Zekaria aliona pengine ilikuwa mufupi, lakini ilisaidia Wayahudi kuwa na mutazamo muzuri kuhusu kazi yao na ibada yao. Na wakati walitenda kulingana na mambo yenye Zekaria aliona, waliona namna Yehova aliwategemeza kwa upendo na kuwaongoza. Kupitia roho takatifu yake yenye nguvu, Yehova aliwasaidia waendelee na kazi yao na wapate tena furaha yao.​—Ezr. 6:16.

18. Maono ya Zekaria inaweza kuwa na matokeo gani mu maisha yako?

18 Maono ya Zekaria ya kinara cha taa na mizeituni mbili inaweza kuwa na matokeo ya muzuri mu maisha yako. Sawa vile tumetoka zungumuzia, inaweza kutusaidia kupata nguvu yenye tuko nayo lazima ili kupambana na wapinzani wetu, kuwa na furaha yenye tuko nayo lazima ili kupiganisha hali yetu kama hali inabadilika, na kutupatia tumaini yenye tuko nayo lazima ili kutii wakati tunapewa muongozo fulani wenye hatuelewe. Unapaswa kufanya nini wakati unapambana na magumu fulani mu maisha yako? Kwanza, ona mambo yenye Zekaria aliona, ni kusema, ushuhuda wenye kuonyesha kama Yehova anakuwaka anahangaikia watu wake. Kisha, tenda kulingana na mambo yenye unaona kwa kumutumainia Yehova na kuendelea kumuabudu kwa moyo wako wote. (Mt. 22:37) Kama unafanya vile, Yehova atakusaidia umutumikie milele kwa furaha.​—Kol. 1:10, 11.

WIMBO 7 Yehova Ni Nguvu Yangu

^ Yehova alimupatia nabii Zekaria maono mingi mbalimbali yenye kufurahisha. Mambo yenye Zekaria aliona ilimupatia yeye na watu wa Yehova nguvu ya kupambana na magumu yenye walikutana nayo wakati walikuwa wanapenda kurudisha ibada safi. Ile maono inaweza pia kutusaidia kumutumikia Yehova kwa uaminifu ijapokuwa magumu yetu. Mu hii habari, tutazungumuzia somo za maana sana zenye tunaweza kujifunza kupitia moya kati ya maono ya Zekaria yenye inatia ndani kinara cha taa na mizeituni.

^ Kisha miaka fulani mu siku za Gavana Nehemia, kulikuwa mufalme mwingine mwenye aliitwa Artashasta, mwenye alitendea muzuri sana Wayahudi.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu fulani anaona ulazima wa kuzoea mabadiliko yenye inatokana na miaka yake na matatizo yake ya afya.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Dada moya anafikiri juu ya namna Yehova iko anategemeza “mutumwa muaminifu na mwenye busara” sawa vile tu alitegemezaka Yoshua na Zerubabeli.