Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JI LIFUNZU 13

Ibada ja Sakaka Jijonzukya Laha Jako

Ibada ja Sakaka Jijonzukya Laha Jako

“Gusitahili, Ee Yehova gwa Mungu jwitu, kujopa utukufu na heshima na makili.”​—UFU. 4:11, NWT.

NHAMBU 31 Tembea Pamoja na Mungu!

MUHTASARI *

1-2. Ki sesifanya ibada jitu jujijetakya Mungo?

 UNAFIKIRIA nini unaposikia neno “ibada”? Labda unamwazia ndugu aliyepiga magoti kando ya kitanda chake akisali kwa hisia na kuumimina moyo wake. Au labda unafikiria familia yenye furaha ambayo inajifunza Biblia kwa makini pamoja.

2 Katika visa hivyo viwili, wahusika wote wanafanya matendo ya ibada. Je, Yehova atakubali ibada yao? Atakubali ikiwa wanafanya hivyo kupatana na mapenzi yake na wanafanya hivyo kwa sababu wanampenda na kumheshimu. Tunampenda sana Yehova. Tunajua kwamba anastahili kuabudiwa, na tunataka kumpa zawadi yetu ya ibada kwa njia bora kabisa.

3. Musitulongalya kya mu makala jenzeno?

3 Katika makala hii, tutazungumzia ibada ambayo Yehova aliikubali nyakati za kale na tutazungumzia mambo manane yanayohusu ibada inayokubalika leo. Tunapofanya hivyo, tunaweza kufikiria jinsi sisi wenyewe tunavyoweza kufanya ibada yetu iwe bora zaidi. Pia, tutazungumzia sababu zinazofanya ibada ya kweli itusaidie kuwa na furaha.

IBADA AMBAJU YEHOVA JUJIJETAKYA WAKATI GWA ZAMANI

4. Aabudu bika Yehova ba kabla ju Ukristo balangia bo kwamba babya bunheshimu Yehova nu kumpala?

4 Kabla ya Ukristo, wanaume waaminifu kama vile Abeli, Noa, Abrahamu, na Ayubu walionyesha kwamba walimheshimu na kumpenda Yehova. Jinsi gani? Kupitia utii, imani, na dhabihu zao. Biblia haitaji habari hususa kuhusu mambo yote waliyohitaji kufanya ili ibada yao ikubalike. Lakini ni wazi walifanya kila walichoweza ili wamheshimu Yehova, na ibada yao ilikubalika kwake. Kisha, Yehova aliwapatia wazao wa Abrahamu Sheria ya Musa. Sheria hizo zilitia ndani maagizo hususa kuhusu jinsi ya kumwabudu Yehova kwa njia anayoikubali.

5. Libi libadiliku bo lelabya mu ibada ja sakaka baada ja kuwa kuka Yesu nu kumfufua?

5 Baada ya Yesu kufa na kufufuliwa, Yehova hakuhitaji tena watu wamwabudu kwa kufuata Sheria ya Musa. (Rom. 10:4) Wakristo walihitaji kufuata sheria mpya, yaani, “sheria ya Kristo.” (Gal. 6:2) Wangetii “sheria” hiyo si kwa kuikariri na kufuata orodha ndefu ya mambo ya kufanya na mambo ambayo hawakupaswa kufanya, bali kwa kuiga mfano wa Yesu na kufuata mafundisho yake. Leo pia, Wakristo wanajitahidi kabisa kumfuata Kristo ili kumfurahisha Yehova na ‘kupata burudisho’ kwa ajili yao.​—Mt. 11:29.

6. Musitunufaika bo mu makala jenzeno?

6 Tunapochunguza kila jambo kuhusu ibada yetu, jiulize hivi, ‘Nimefanya maendeleo gani katika jambo hili?’ Huenda pia ukajiuliza, ‘Je, ninaweza kuboresha ibada yangu?’ Unapaswa kufurahia maendeleo uliyofanya lakini pia unapaswa kusali kwa Yehova ili akusaidie kuona mambo unayoweza kuboresha zaidi.

IBADA JITU JIHUSISHA KIKE?

7. Yehova juibona bo sala itu yu kuhuma kumwojo?

7 Tunamwabudu Yehova tunaposali kwake. Maandiko yanafananisha sala zetu zilizotayarishwa vizuri na uvumba uliotolewa kwenye hema la ibada na baadaye hekaluni. (Zab. 141:2) Uvumba huo ulitokeza harufu nzuri iliyomfurahisha Mungu. Vivyo hivyo, sala zetu za kutoka moyoni ‘zinampendeza,’ hata ikiwa tunatumia maneno rahisi sana. (Met. 15:8; Kum. 33:10) Tuna sababu nzuri za kuamini kwamba Yehova anapenda kutusikiliza tunapoonyesha upendo na shukrani zetu kwake. Anataka tumwambie mambo yanayotuhangaisha, mambo tunayotarajia, na mambo tunayotamani. Kabla ya kusali kwa Yehova, kwa nini usitenge muda wa kufikiria kwa makini mambo utakayosema? Kwa kufanya hivyo, utamtolea “uvumba” bora kabisa Baba yako wa mbinguni.

8. Tubi na fulsa bo ja sapi ju kunsifu Mungo?

8 Tunamwabudu Yehova tunapomsifu. (Zab. 34:1) Tunamsifu Yehova tunapowaambia wengine kuhusu sifa na kazi zake zenye kustaajabisha. Moyo wenye shukrani utatuchochea kumsifu Yehova. Tukitumia wakati kutafakari wema wa Yehova, yaani, mambo yote mazuri ambayo ametufanyia​—hatutakosa sababu za kumsifu. Kazi ya kuhubiri inatupatia fursa nzuri sana ya ‘kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani, tunda la midomo yetu.’ (Ebr. 13:15) Kama vile tunavyopaswa kufikiria kwa makini mambo tutakayosema kabla ya kusali kwa Yehova, ni vizuri kufikiria kwa makini kuhusu mambo tutakayowaambia wale tunaokutana nao katika huduma yetu. Tunataka ‘dhabihu yetu ya sifa’ iwe bora kabisa. Tunazungumza kutoka moyoni tunapowahubiria wengine.

9. Kama Aisraeli ba zamani, tupata faida bo etuketangana pamwa? Pwaga lijambu leguliboni.

9 Tunamwabudu Yehova tunapohudhuria mikutano. Waisraeli wa kale waliambiwa hivi: “Mara tatu kwa mwaka, wanaume wenu wote wanapaswa kwenda mbele za Yehova Mungu wenu mahali atakapochagua.” (Kum. 16:16) Waliacha nyumba na mashamba yao bila ulinzi. Lakini Yehova aliwaahidi hivi: “Hakuna mtu atakayetamani nchi yenu mtakapokuwa mkipanda kwenda mbele za Yehova Mungu wenu.” (Kut. 34:24) Kwa kumtumaini kabisa Yehova, Waisraeli hao waliomwogopa Mungu walihudhuria sherehe hizo za kila mwaka. Walibarikiwa sana kwa kufanya hivyo; waliongeza uelewaji wao wa Sheria ya Mungu, walitafakari wema wake, na kufurahia ushirika wenye kutia moyo pamoja na waamini wenzao. (Kum. 16:15) Tunapata faida kama hizo tunapojidhabihu ili kuhudhuria mikutano ya Kikristo. Na fikiria jinsi Yehova anavyofurahi tunapohudhuria mikutano tukiwa tumeandaa maelezo mafupi yaliyotayarishwa vizuri.

10. Ndaba jaki kujemba ndo sehemu muhimu ji ibada jito?

10 Tunamwabudu Yehova tunapoimba na ndugu na dada zetu. (Zab. 28:7) Waisraeli waliona kuimba kuwa sehemu muhimu ya ibada yao. Mfalme Daudi aliwapa Walawi 288 mgawo wa kuimba hekaluni. (1 Nya. 25:1, 6-8) Leo, tunaweza kuonyesha upendo wetu kwa Mungu tunapomwimbia nyimbo za sifa. Jambo muhimu si ubora wa sauti zetu. Fikiria ulinganisho huu: Tunapozungumza, “sisi sote hujikwaa mara nyingi,” lakini hilo halituzuii kuzungumza kutanikoni au katika huduma. (Yak. 3:2) Tunaweza kumwimbia Yehova sifa hata ikiwa tunafikiri kwamba sauti yetu si nzuri.

11. Kulengana nu ufafanuzi gwa Zaburi 48:13, ndabajaki tupaswa kutenga wakati ili kulibola Bibilia koni tubi pamwa mfamilia?

11 Tunamwabudu Yehova tunapojifunza Neno lake na kufundisha watoto wetu kumhusu. Sabato iliwapatia Waisraeli fursa ya kuacha shughuli zao za kila siku na kukazia fikira uhusiano wao pamoja na Yehova. (Kut. 31:16, 17) Waisraeli waaminifu waliwafundisha watoto wao kumhusu Yehova na wema wake. Leo, sisi pia ni lazima tutenge muda wa kujifunza na kusoma Neno la Mungu kibinafsi. Kufanya hivyo ni sehemu ya ibada yetu kwa Yehova, na kunatusaidia kumkaribia zaidi. (Zab. 73:28) Na tunapojifunza pamoja tukiwa familia tunaweza kukisaidia kizazi kipya, yaani, watoto wetu kusitawisha uhusiano wa karibu pamoja na Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo.​—Soma Zaburi 48:13.

12. Tulibola ki kubokana na jinsi Yehova ejujibona kasi ja baalenganakya yombu yi lihema li ibada?

12 Tunamwabudu Yehova tunapojenga na kudumisha sehemu za ibada. Biblia inasema kwamba kazi ya kutengeneza hema la ibada na vyombo vyake ilikuwa “kazi takatifu.” (Kut. 36:1, 4) Leo pia, Yehova anaiona kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme na majengo mengine ya kitheokrasi kuwa utumishi mtakatifu. Baadhi ya ndugu na dada wanatumia muda mwingi sana katika utendaji huo. Je, tunathamini mchango huo muhimu katika kazi ya Ufalme? Bila shaka, wanashiriki pia katika kazi ya kuhubiri. Baadhi yao huenda hata wakataka kuwa mapainia. Wazee wa kutaniko wanaweza kuonyesha kwamba wanaunga mkono kazi za ujenzi kwa kuwa tayari kuwaweka rasmi wanaume na wanawake hao wanaofanya kazi kwa bidii kuwa mapainia wanapostahili. Iwe tuna ustadi katika kazi ya ujenzi au la, sisi sote tunaweza kushiriki katika kudumisha usafi na kurekebisha majengo hayo.

13. Tupaswa kujibona bo misangu jetupiha ili kuunga nkonu kasi ju Ufalme?

13 Tunamwabudu Yehova tunapounga mkono kazi ya Ufalme kwa michango yetu. Waisraeli hawakupaswa kwenda mbele za Yehova mikono mitupu. (Kum. 16:16) Walipaswa kuleta zawadi kulingana na hali zao. Hivyo, walionyesha wanathamini mipango yote iliyokuwa imefanywa ili kuwanufaisha kiroho. Tunaweza kuonyeshaje upendo na shukrani zetu kwa Yehova kwa maandalizi ya kiroho tunayopata? Njia moja ni kwa kutoa michango yetu ya kifedha ili kutegemeza kutaniko letu na kazi ya ulimwenguni pote, kadiri hali zetu zinavyoruhusu. Mtume Paulo, anasema hivi: “Ikiwa utayari upo kwanza, hukubalika zaidi kulingana na kile ambacho mtu anacho, si kulingana na kile ambacho mtu hana.” (2 Kor. 8:4, 12) Yehova anathamini mchango wowote tunaotoa kutoka moyoni, hata kama ni kiwango kidogo.​—Marko 12:42-44; 2 Kor. 9:7.

14. Kulengana na Methali 19:17, Yehova jubona bo msaada gotwa apeke aka ndugu bitu baabi nu uhitaje?

14 Tunamwabudu Yehova tunapowasaidia Wakristo wenzetu walio na uhitaji. Yehova aliahidi kuwalipa Waisraeli waliowaonyesha kibali au kuwasaidia maskini. (Kum. 15:7, 10) Naam, kila wakati tunapowasaidia waamini wenzetu walio na uhitaji, Yehova anaona hilo kuwa zawadi kwake. (Soma Methali 19:17.) Kwa mfano, Wakristo kutoka Filipi walipomtumia Paulo zawadi akiwa gerezani, aliita “dhabihu yenye kukubalika inayompendeza Mungu vema.” (Flp. 4:18) Fikiria kuhusu kutaniko lenu na ujiulize, ‘Je, kuna mtu ninayeweza kumsaidia?’ Yehova anafurahi anapotuona tukitumia muda, nguvu, ustadi, na vitu vyetu vya kimwili kuwasaidia walio na uhitaji. Anaona kufanya hivyo kuwa sehemu ya ibada yetu.​—Yak. 1:27.

IBADA JA SAKAKA JUTUFANYA TUBYA NA LAHA

15. Ibada ja sakaka jihitaji wakati na makili, lakini ndaba jaki nga nsigu gogutopike?

15 Ibada ya kweli inahitaji muda na jitihada. Hata hivyo, si mzigo mzito. (1 Yoh. 5:3) Kwa nini? Kwa sababu ibada yetu inachochewa na upendo kwa Yehova. Fikiria mtoto mdogo anayetaka kumpa baba yake kitu fulani. Anaweza kutumia saa nyingi akichora picha ili ampe baba yake. Mtoto huyo hajutii muda aliotumia kuchora picha hiyo. Anampenda baba yake na anafurahi kumpatia picha hiyo. Vivyo hivyo, kwa sababu tunampenda Yehova, tunafurahi kutumia wakati na nguvu zetu ili kushiriki katika ibada ya kweli.

16. Kulengana na Waebrania 6:10, Yehova juibona bo jitihada yitu ikibinafsi yu kupala kumfulaisha?

16 Wazazi wenye upendo hawatarajii kupata zawadi ileile kutoka kwa kila mtoto. Wanatambua kwamba kila mtoto ni tofauti na hali zao zinatofautiana. Vivyo hivyo, Baba yetu wa mbinguni anaelewa hali zetu za kibinafsi. Huenda unaweza kufanya mengi zaidi kuliko ndugu na dada zako unaowajua na kuwapenda. Au huenda usiweze kufanya mengi kama wengine wanavyofanya, labda kwa sababu ya umri, afya, au majukumu yako ya kifamilia. Usivunjike moyo. (Gal. 6:4) Yehova hatasahau kazi yako. Maadamu unampatia Yehova kilicho bora kulingana na uwezo wako ukichochewa na nia nzuri, Yehova atafurahi. (Soma Waebrania 6:10.) Yehova anajua hata makusudio ya moyo wako. Anataka uwe na furaha na kuridhika na ibada unayomtolea.

17. (a) Ana kubi ngumu kutimisa sehemu fulani ji ibada jitu, tuwesa kujuku hatua bole? (b) Gunufaikibo na majawapu ja sehemu yeailangi mulisanduka “Jonzukya Laha Jako”?

17 Namna gani ikiwa tunaona ni vigumu kushiriki sehemu fulani ya ibada yetu, kama vile funzo la kibinafsi au huduma ya hadharani? Inaelekea tutagundua kwamba kadiri tunavyoshiriki mara nyingi katika utendaji huo, ndivyo tutakavyoufurahia zaidi na kunufaika nao. Tunaweza kuilinganisha ibada yetu na utendaji fulani, kama vile kufanya mazoezi au kujifunza kupiga chombo fulani cha muziki. Ikiwa tunafanya hivyo pindi chache tu, huenda tusifanye maendeleo makubwa. Lakini tuseme tunaamua kutenga wakati kila siku kwa ajili ya mazoezi hayo. Tunaweza kuanza kwa vipindi vifupi-vifupi, na kisha hatua kwa hatua kuvifanya viwe virefu zaidi. Tunapoona matokeo mazuri ya jitihada zetu, inaelekea tutatazamia kwa hamu vipindi hivyo na kuvifurahia sana. Je, unaweza kuona jinsi tunavyoweza kutumia mbinu hiyo katika ibada yetu?

18. Tutimisa bo, lijambu muhimu ngani mumaisha, nu kuhenga hela kuleta matokeu bole?

18 Tunapomwabudu Yehova kwa moyo wote tunatimiza jambo muhimu zaidi maishani. Matokeo ni kwamba tunafurahia maisha yenye shangwe na kusudi na tuna tumaini la kumwabudu Yehova milele. (Met. 10:22) Tayari tuna amani ya akili kwa sababu tunajua kwamba Yehova anawasaidia waabudu wake wanapokuwa na matatizo. (Isa. 41:9, 10) Bila shaka, tuna sababu nzuri za kuwa na furaha tunapomwabudu Baba yetu mwenye upendo, anayestahili “kupokea utukufu na heshima” kutoka kwa uumbaji wake wote!​—Ufu. 4:11.

NHAMBU 24 Njooni Kwenye Mlima wa Yehova

^ Yehova anastahili kuabudiwa kwa sababu yeye ndiye aliyeumba vitu vyote. Matendo yetu ya ibada yanakubalika kwake ikiwa tunatii amri zake na kuishi kulingana na kanuni zake. Katika makala hii, tutazungumzia mambo manane yanayohusu ibada yetu. Unapochunguza jinsi unavyoshiriki kufanya mambo hayo, ona jinsi yatakavyoongeza furaha yako.