Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 13

Ibada ya Kweli Itaongeza Furaha Yako

Ibada ya Kweli Itaongeza Furaha Yako

“Unastahili, Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu.”​—UFU. 4:11.

WIMBO 31 Utembee Pamoja na Mungu!

KIFUPI YA HABARI *

1-2. Nini njo itafanya Yehova akubali ibada yetu?

 NINI njo inakuya mu akili yako wakati unasikia neno “ibada”? Pengine unafikiri juu ya ndugu fulani mwenye anapiga magoti ili kusali na kumuomba Yehova kwa moyo wake wote mbele aende kulala. Ao pengine unafikiria familia yenye furaha yenye iko najifunza Biblia.

2 Ikuwe ni ule ndugu ao ile familia, wote wako wanamuabudu Yehova. Je, atakubali ibada yao? Ndiyo, kama tu wanamutolea ile ibada kulingana na mapenzi yake na wanafanya vile kwa upendo na kwa heshima. Tunamupendaka Yehova sana. Tunajua kama anastahili kuabudiwa, na tunapenda kumuabudu mu njia ya muzuri zaidi.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Mu hii habari, tutajifunza aina ya ibada yenye Yehova alikubali mu wakati wa zamani na tutazungumuzia njia munane ya ibada yenye Yehova anapenda tumuabudu leo. Wakati tutakuwa tunafanya vile, tutaona namna kila mumoja wetu kipekee anaweza kumutolea Yehova ibada mu njia ya muzuri zaidi. Tutaona pia sababu zenye zinafanya ibada ya kweli itupatie furaha.

AINA YA IBADA YENYE YEHOVA ALIKUBALI ZAMANI

4. Waabudu wa Yehova wa zamani walionyesha namna gani kama wanamuheshimia na kumupenda?

4 Zamani, wanaume waaminifu sawa vile Abeli, Noa, Abrahamu, na Yobu walionyesha kama wanamuheshimia na kumupenda Yehova. Namna gani? Kupitia utii wao, imani, na zabihu zenye walimutolea Yehova. Biblia haituonyeshe waziwazi kila kitu kuhusu aina ya ibada yenye wale wanaume walimutolea Yehova. Lakini ni wazi kuwa walifanya yao yote ili kumuabudu Yehova, na Yeye alikubali ibada yao. Kisha, Yehova alipatia wazao wa Abrahamu Sheria ya Musa. Zile sheria zilionyesha namna Yehova angeweza kuabudiwa mu njia yenye anakubali.

5. Kuhusu ibada ya kweli, ni mabadiliko gani ilitokea kisha kifo na ufufuo wa Yesu?

5 Kisha kifo ya Yesu na ufufuo wake, Yehova hakuomba tena watu wamutii kwa kufuata Sheria ya Musa. (Ro. 10:4) Wakristo walipaswa sasa kufuata sheria ya mupya, “Sheria ya Kristo.” (Gal. 6:2) Wangepaswa kutii ile “Sheria,” hapana kwa kuitia mu akili na kufuata liste ya mambo yenye walipaswa kufanya na yenye hawangepaswa kufanya, lakini kwa kuiga mufano wa Yesu na kufuata mafundisho yake. Leo pia, Wakristo wanafanya yao yote ili kufuata Kristo juu ya kumupendeza Yehova na ‘kupata pumuziko’ kwa ajili yao wenyewe.​—Mt. 11:29.

6. Namna gani hii habari inaweza kukuletea faida?

6 Wakati tutakuwa tunachungunza sehemu mbalimbali za ibada yetu, ujiulize hivi, ‘Ni maendeleo gani nimefanya kuhusu hii sehemu?’ Unaweza pia kujiuliza hivi, ‘Naweza kufanya nini juu ibada yangu ikuwe muzuri zaidi?’ Mambo yenye uko nafanya kwa sasa inaweza kukupatia furaha, lakini unapaswa kumuomba Yehova akusaidie uone mambo yenye unaweza kufanya ili ibada yako ikuwe muzuri zaidi.

IBADA YETU INATIA NDANI NINI?

7. Namna gani Yehova anaona sala zetu za kutoka ku moyo?

7 Tunamuabudu Yehova wakati tunasali kwake. Maandiko inalinganisha sala zetu na uvumba wenye ulitayarishwa kwa uangalifu, wenye ulikuwa unatolewa ku tabenakulo na kisha wakati fulani ku hekalu. (Zb. 141:2) Ile uvumba ilikuwa inatoa harufu ya muzuri yenye ilikuwa inamufuraisha Mungu. Vilevile, sala zetu ‘zinamufuraisha’ Yehova, hata kama tunatumia maneno ya mwepesi sana. (Mez. 15:8; Kum. 33:10) Tuko na sababu ya muzuri ya kuamini kama Yehova anafurahiaka kusikia wakati tunamuambia kama tunamupenda na kumushukuru. Anapenda tumuambie mahangaiko yetu, matumaini yetu, na tamaa zetu. Mbele ya kusali kwa Yehova, hauone kama ni muzuri kufikiri kwa uzito juu ya mambo yenye tunapenda kumuambia? Ukifanya vile, utamutolea Baba yako wa mbinguni “uvumba” wa muzuri zaidi.

8. Ni nafasi gani ya muzuri yenye tuko nayo ya kumusifu Yehova?

8 Tunamuabudu Yehova wakati tunamusifu. (Zb. 34:1) Tunamusifu Yehova kwa kuambia wengine juu ya sifa zake zenye kushangaza na kazi zake. Tutakuwa na mambo mingi ya muzuri ya kusema juu ya Yehova kama tuko wenye shukrani kwake. Kama tunakamata wakati wa kufikiri sana juu ya mambo yote ya muzuri yenye Yehova ametufanyia, hatutakosa hata jambo moya ya kumusifia ako. Kazi yetu ya kuhubiri inatutolea nafasi ya muzuri zaidi ya ‘kumutolea Mungu zabihu ya sifa, ni kusema, tunda la midomo yetu.’ (Ebr. 13:15) Sawa vile tunapaswa kufikiri kwa uzito juu ya mambo yenye tutasema mbele tusali kwa Yehova, ni vile pia tunapaswa kufikiri kwa uzito juu ya mambo yenye tutaambia watu mu mahubiri mbele tukutane nao. Tunapenda ‘zabihu zetu za sifa’ zikuwe za muzuri zaidi. Njo maana tunakuwaka tunahubiri kwa uchangamufu.

9. Sawa vile Waisraeli wa zamani, ni faida gani tunapataka kwa kukusanyika? Leta mufano fulani wenye kuonyesha namna mikutano imekusaidia.

9 Tunamuabudu Yehova wakati tunakusanyika. Waisraeli wa zamani waliambiwa hivi: “Mara tatu kwa mwaka, wanaume wako wote wataonekana mbele ya Yehova Mungu wako mahali kwenye atachagua.” (Kum. 16:16) Walipaswa kuacha nyumba zao na mashamba yao bila mutu wa kuilinda. Lakini Yehova aliwaahidi hivi: “Hakuna mutu mwenye atatamani inchi yako wakati utakuwa unapanda ili kuona uso wa Yehova Mungu wako.” (Kut. 34:24) Wakiwa na imani kabisa kwa Yehova, wale Waisraeli wenye kumuogopa walienda kusherehekea sikukuu za kila mwaka. Wangepata baraka mingi sana; kwa mufano, wangeelewa muzuri zaidi Sheria ya Mungu, wangefikiri sana juu ya uzuri wake, na wangefurahia kutiwa moyo na waamini wenzao. (Kum. 16:15) Na siye pia tunapataka baraka mingi wakati tunafanya yetu yote ili kukusanyika. Wazia namna Yehova anafurahiaka wakati tunakuya ku mukutano na tulishatayarisha maelezo ya mufupi na yenye kutia moyo.

10. Juu ya nini kuimba ni sehemu ya maana sana ya ibada yetu?

10 Tunamuabudu Yehova wakati tunaimba. (Zb. 28:7) Waisraeli waliona kuimba kuwa sehemu ya maana sana ya ibada yao. Mufalme Daudi alipatia Walawi 288 mugao wa kuwa waimbaji mu hekalu. (1 Ny. 25:1, 6-8) Leo, tunaweza kuonyesha kama tunamupenda Mungu wetu kwa kumuimbia nyimbo za sifa. Sauti yetu haiko njo ya maana sana. Fikiria hii jambo: Mu kuzungumuza “sisi sote tunajikwaa mara nyingi,” lakini ile haiko njo yenye inatuzuiaka kusema mu kutaniko na mu mahubiri. (Yak. 3:2) Vilevile, hata kama hatuna sauti ya muzuri, tusiache ile ituzuie kumuimbia Yehova nyimbo za sifa.

11. Sawa vile inaonyeshwa mu Zaburi 48:13, juu ya nini tunapaswa kupanga wakati wa kujifunza Biblia pamoya na familia?

11 Tunamuabudu Yehova wakati tunajifunza Neno yake na tunafundisha watoto wetu kumuhusu. Siku ya Sabato, Waisraeli hawakukuwa wanatumika na walitumia ile siku ili kutia nguvu uhusiano wao pamoya na Yehova. (Kut. 31:16, 17) Wazazi waaminifu walifundisha watoto wao kuhusu Yehova na uzuri wake. Leo pia, tunapaswa kukamata wakati wa kusoma na kujifunza Neno ya Mungu. Ile ni sehemu ya ibada yenye tunamutolea Yehova, na inatusaidia kumukaribia zaidi. (Zb. 73:28) Na wakati tunajifunza pamoya tukiwa familia, tunaweza kusaidia watoto wetu wakuwe na uhusiano wa karibu sana pamoya na Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo.​—Soma Zaburi 48:13.

12. Yehova alisamini sana wale wenye walijenga vitu vya tabenakulo. Ile inatufundisha nini?

12 Tunamuabudu Yehova wakati tunajenga na kutunza nafasi za ibada. Biblia inasema kama kazi ya kujenga tabenakulo na vitu vyake ilikuwa “kazi takatifu.” (Kut. 36:1, 4) Leo pia, Yehova anaona kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme na majengo ingine ya tengenezo kuwa sehemu ya ibada yenye tunamutolea. Ndugu na dada fulani wanatumia wakati wao mingi mu zile kazi. Tunasamini sana yote yenye wanafanya ili kutegemeza kazi ya Ufalme! Lakini, hawasahau pia kazi ya kuhubiri. Wamoja wanapenda kuwa hata mapainia. Wazee wa kutaniko wanaweza kuonyesha kama wanategemeza kazi ya ujenzi kwa kuruhusu wale ndugu na dada wenye bidii kuwa mapainia. Ikuwe tuko na uzoefu mu kazi ya ujenzi ao hapana, siye wote tunaweza kuungana mukono juu ile majengo iendelee kuwa safi na mu hali ya muzuri.

13. Namna gani tunapaswa kuona michango yenye tunatoa ili kutegemeza kazi ya Ufalme?

13 Tunamuabudu Yehova wakati tunategemeza kazi ya Ufalme kupitia michango yetu. Waisraeli hawakupaswa kuonekana mbele ya Yehova mikono wazi. (Kum. 16:16) Walipaswa kuleta zawadi kulingana na hali yao. Mu ile njia, walionyesha kama walikuwa wenye shukrani juu ya mambo yote ya kiroho yenye Yehova alikuwa amewafanyia. Namna gani tunaweza kuonyesha upendo wetu kwa Yehova na shukrani yetu kwa ajili ya chakula ya kiroho yenye tunapata? Njia moya ya kufanya vile, ni kutoa michango kwa ajili ya kutaniko yetu na juu ya kazi ya ulimwenguni pote kama hali yetu inaruhusu. Mutume Paulo alionyesha ile mu hii njia: “Kama utayari uko kwanza, unakubaliwa zaidi kulingana na kile chenye mutu iko nacho, haiko kulingana na kile chenye mutu hana.” (2 Ko. 8:4, 12) Yehova anasamini sana muchango wowote wenye tunatoa kutoka ku moyo hata ikuwe ngapi.​—Mk. 12:42-44; 2 Ko. 9:7.

14. Kulingana na Mezali 19:17, Yehova anaona namna gani musaada wenye tunatolea ndugu na dada zetu wenye kuwa mu uhitaji?

14 Tunamuabudu Yehova wakati tunasaidia Wakristo wenzetu wenye kuwa mu uhitaji. Yehova aliahidi kama atalipa Waisraeli wenye walionyesha ukarimu maskini. (Kum. 15:7, 10) Kila wakati tunasaidia muabudu mwenzetu mwenye kuwa mu uhitaji, Yehova anaona ile kuwa sawa vile zawadi yenye tunamupatia. (Soma Mezali 19:17.) Kwa mufano, wakati Wakristo wa Filipi walimutumia mufungwa Paulo zawadi, aliita ile zawadi kuwa “zabihu yenye kukubaliwa, yenye kumupendeza Mungu.” (Flp. 4:18) Fikiria wale wenye kuwa mu kutaniko yako na ujiulize hivi: ‘Kuko mutu mwenye naweza kusaidia?’ Yehova anafurahiaka wakati anatuona tunatumia wakati wetu, nguvu, uzoefu, na vitu vyetu vya kimwili ili kusaidia wale wenye kuwa mu uhitaji. Anaona ile kuwa sehemu ya ibada yenye tunamutolea.​—Yak. 1:27.

IBADA YA KWELI INAFANYA TUKUWE NA FURAHA

15. Ibada ya kweli inaomba wakati na bidii. Sasa juu ya nini ile haiko muzigo muzito?

15 Ibada ya kweli inaomba wakati na bidii. Lakini haiko muzigo muzito. (1 Yo. 5:3) Juu ya nini? Tunamuabudu Yehova juu tunamupenda. Wazia mutoto mudogo anapenda kupatia baba yake kitu fulani. Pengine anaweza kupitisha saa za mingi na iko anamuchapia picha fulani. Ule mutoto mwanaume hatahuzunikia wakati wenye alipitisha ili kuchapa ile picha. Anapenda baba yake, na anafurahi kumupatia ile zawadi. Vilevile, juu tunamupenda sana Yehova, tunafurahia kutumia wakati wetu na bidii yetu ili kuunga mukono ibada ya kweli.

16. Kulingana na Waebrania 6:10, Yehova anaona namna gani bidii yetu ya kupenda kumufurahisha?

16 Wazazi wenye upendo hawatazamie watoto wao wote wawapatie zawadi ileile. Wanaelewa kama kila mutoto iko tofauti mu mambo yenye anaweza kufanya. Vilevile, Baba yetu wa mbinguni anaelewa mambo yenye kila mumoja wetu iko na uwezo wa kufanya. Pengine unaweza kufanya mengi zaidi kuliko wale wenye unajua na kupenda. Ao pengine hauna uwezo wa kufanya mengi zaidi sawa vile wengine, pengine juu ya miaka yako, afya, ao juu ya madaraka yako ya familia. Kama ni vile, usivunjike moyo. (Gal. 6:4) Yehova hatasahau kazi yako. Kama uko namutolea yako yote na nia ya muzuri, atafurahi. (Soma Waebrania 6:10.) Yehova anajua hata mambo yenye ungependa kufanya. Anapenda ukuwe na furaha na utosheke na ibada yenye uko na uwezo wa kumutolea.

17. (a) Ikiwa tunaona kama sehemu fulani za ibada yetu kuwa nguvu ni hatua gani tunaweza kukamata? (b) Kati ya mambo yenye kuonyeshwa mu kisanduku “ Ongeza Furaha Yako” ni jambo gani yenye imekusaidia, na namna gani?

17 Tunaweza kufanya nini kama ni nguvu kwetu kufanya mambo fulani kati ya mambo yenye tumetoka tu kuzungumuzia, sawa vile kujifunza Biblia na kuhubiri? Inaonekana wakati tunafanya ile mambo mara mingi zaidi, ni vile tutapata furaha na faida mingi. Tunaweza kulinganisha ibada yetu na kazi fulani, sawa vile mazoezi fulani ao kujifunza chombo fulani ya muziki. Kama hatufanye vile mara kwa mara, inaweza kuwa nguvu kwetu kufanya maendeleo. Lakini nini njo inaweza kutokea kama tunaamua kufanya vile kila siku? Ku mwanzo, pengine tutafanya vile kwa muda mufupi tu, lakini polepole tutakuwa tunaongeza muda wenye tunatumia ili kufanya vile. Ni vile pia kuhusu ibada yetu. Wakati tunaona matokeo ya muzuri ya bidii yetu, tutapenda kufanya vile na kuifurahia kabisa.

18. Ni jambo gani njo ya maana sana yenye tunaweza kufanya, na kama tunafanya vile tutapata matokeo gani?

18 Kufanya yetu yote ili kumuabudu Yehova njo jambo ya maana sana yenye tunaweza kufanya. Ile itafanya tukuwe na maisha yenye furaha na yenye kutosheka na tutakuwa na tumaini ya kumuabudu Yehova milele. (Mez. 10:22) Tayari tuko na amani ya akili juu tunajua kama Yehova anasaidiaka waabudu wake wakati wanapambana na magumu fulani. (Isa. 41:9, 10) Kusema kweli, tuko na sababu ya kuwa na furaha wakati tunamuabudu Baba yetu mwenye upendo, mwenye anastahili “kupokea utukufu na heshima” kutoka kwa viumbe vyake vyote!​—Ufu. 4:11.

WIMBO 24 Tuende ku Mulima wa Yehova

^ Yehova anastahili kuabudiwa, juu yeye njo Muumbaji wa vitu vyote. Yehova anakubali mambo yenye tunafanya ili kumuabudu, lakini anaikubali tu kama tunatii sheria yake na kuishi kulingana na kanuni zake. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo munane yenye tunafanyaka wakati tuko naabudu Yehova. Tutajifunza namna tunaweza kufanya ile mambo munane muzuri zaidi, na namna inaweza kutupatia furaha zaidi.