Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Juu ya nini 2 Samweli 21:7-9 inasema kama Daudi “alimusikilia huruma Mefibosheti” lakini kisha akamutoa ili atundikwe?

Watu fulani wenye wamesoma ile habari wamejiuliza ile ulizo. Lakini mu ile mustari muko wanaume tofauti wenye walikuwa na jina Mefibosheti, na tunaweza kujifunza jambo fulani kwa kuchunguza mambo yenye ilitokea.

Mufalme Sauli wa Israeli alikuwa na watoto saba wanaume na watoto wawili wanamuke. Mutoto wa kwanza mwanaume wa Sauli alikuwa Yonatani. Kisha mufalme Sauli akapata mutoto mwanaume mwenye aliita Mefibosheti, ule mutoto alizaliwa na Rispa mwenye alikuwa suria wa Sauli. Jambo ya kushangaza, Yonatani pia alikuwa na mutoto mwanaume mwenye jina yake ilikuwa Mefibosheti. Kwa hiyo, Mufalme Sauli alikuwa na mutoto mwenye jina yake ilikuwa Mefibosheti, lakini pia mujukuu mwenye alikuwa na jina ileile.

Wakati fulani, Mufalme Sauli alianza kuchukia Wagibeoni na hata alijaribu kufanya yake yote ili wauawe. Inawezekana wengi kati yao waliuawa. Ni wazi kuwa kufanya vile ilikuwa mubaya. Juu ya nini? Juu mu wakati wa Yoshua, wakubwa Waisraeli walifanya agano ya amani pamoya na Wagibeoni.​—Yos. 9:3-27.

Ile agano ilikuwa ingali inatumika hata mu wakati wa Mufalme Sauli. Tofauti na ile agano, Mufalme Sauli alijaribu kuua Wagibeoni. Kufanya vile kulileta “hatia ya damu juu ya Sauli na juu ya nyumba yake.” (2 Sa. 21:1) Kisha Daudi alifikia kuwa mufalme. Wagibeoni wenye waliponaka walimuambia Daudi juu ya mauaji yenye ilipitikanaka. Daudi akawauliza nini njo angeweza kufanya ili kutengeneza ukosefu wa haki wenye Sauli alikuwa amefanya na juu Yehova abariki tena inchi. Kuliko kulomba makuta, wale Wagibeoni walilomba njo watoto wanaume saba wa ule mwanaume mwenye ‘alifanya mupango wa kuharibu’ waletwe na wauawe. (Hes. 35:30, 31) Daudi alikubali ombi yao.​—2 Sa. 21:2-6.

Ile wakati tayari Sauli na Yonatani walikuwa walishakufa mu vita, lakini mutoto mwanaume wa Yonatani, Mefibosheti alikuwa muzima. Alikuwa kilema juu ya aksida yenye alifanyaka akiwa mutoto na hakuungaka mukono tate yake ili kushambulia Wagibeoni. Daudi alifanyaka agano ya amani pamoya na Yonatani, ile ingeletea faida uzao wa Yonatani kutia ndani mwana wake, Mefibosheti. (1 Sa. 18:1; 20:42) Ile habari inaonyesha hivi: “Mufalme [Daudi] akamusikilia huruma Mefibosheti, mwana wa Yonatani mwana wa Sauli, kwa sababu ya kiapo chenye kilifanywa mbele ya Yehova.”​—2 Sa. 21:7.

Hata vile, Daudi alitimiza ombi ya Wagibeoni. Akawapatia watoto wanaume wawili wa Sauli, mumoja kati ya wale watoto jina yake ilikuwa Mefibosheti, na wajukuu tano wa Sauli. (2 Sa. 21:8, 9) Tendo yenye Daudi alifanyaka njo yenye ilimaliza hatia ya damu mu inchi.

Hii habari haiko tu historia. Sheria ya Mungu ilikuwa wazi. Ilisema: “Watoto hawapaswe kuuawa kwa sababu ya mambo yenye baba zao wanafanya.” (Kum. 24:16) Yehova hangekubali wale watoto wanaume wawili wa Sauli na wajukuu wake tano wauawe kama hawengekuwa na hatia fulani. Ile sheria iliongezea hivi: “Mutu anapaswa kuuawa kwa sababu tu ya zambi yake mwenyewe.” Inawezekana wale watoto saba wa Sauli wenye walikufa, waliuungaka mukono Sauli mu njia fulani ili kuua Wagibeoni. Ile njo ilifanya wale watoto saba wavune kile walipanda.

Hii habari inaonyesha kama mutu hawezi kufanya jambo fulani ya mubaya kwa kuwaza kama ao kusema kuwa alifanya vile kwa kufuata tu maagizo fulani. Mezali moya yenye hekima inasema hivi: “Sawazisha mahali miguu yako itapita, na njia zako zote zitakuwa hakika.”​—Mez. 4:24-27; Efe. 5:15.