Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaweza Kufanya Nini Kama Uko na Mahangaiko?

Unaweza Kufanya Nini Kama Uko na Mahangaiko?

MAHANGAIKO inaweza kuwa sawa vile muzigo muzito mu moyo wetu. (Mez. 12:25) Ulishakapata mahangaiko fulani mu maisha yako? Ulishakajisikia sawa vile hautaweza kuendelea na ile hali? Kama ni vile hauko weye peke. Wengi kati yetu wamejisikia kuwa wenye kuchoka sana, kuhangaika, na wamevunjika moyo juu ya sababu mingi. Kwa mufano, watu fulani wamekuwa wakihangaikia mutu fulani wa familia mwenye kuwa mugonjwa, wengine wamepoteza mupendwa wao katika kifo, na wengine wameteseka juu ya musiba fulani wa asili. Tunaweza kufanya nini wakati tuko na mahangaiko? *

Tunaweza kujifunza mambo mingi juu ya namna ya kupambana na mahangaiko yetu kwa kuchunguza mufano wa Mufalme Daudi. Alikuwa na magumu mingi mu maisha yake, na hata wakati fulani uzima wake ulikuwa mu hatari. (1 Sa. 17:34, 35; 18:10, 11) Wakati Daudi alikuwa na mahangaiko, nini njo ilimusaidia kupambana nayo? Namna gani tunaweza kuiga mufano wake?

MAMBO DAUDI ALIFANYA WAKATI ALIKUWA NA MAHANGAIKO

Daudi alikuwa na magumu mingi kwa wakati moya. Wazia mambo yenye ilimupata wakati alikuwa anamukimbia Mufalme Sauli mwenye alikuwa anapenda kumuua. Wakati Daudi na watu wake walirudia Siklagi walihuzunika kuona kama maadui wao waliiba vitu vyao, walilunguza nyumba zao, na walikamata mateka familia zao. Daudi alitenda namna gani? “Daudi na watu wenye walikuwa pamoja naye wakaanza kulia kwa sauti kubwa mupaka wakakosa nguvu za kuendelea kulia.” Kisha Daudi alihangaika tena sana, wakati watu wake walikuwa “wanasema apigwe majiwe.” (1 Sa. 30:1-6) Sasa Daudi anajikuta mbele ya magumu tatu, yote kwa wakati moya: Familia yake ilikuwa mu hatari, aliogopa watu wake wenye walikuwa wanapenda kumuua, na Mufalme Sauli alikuwa angali anamutafuta. Inawezekana Daudi alikuwa mwenye kuhangaika sana!

Kisha pale Daudi alifanya nini? Mara moya “akajitia nguvu kwa musaada wa Yehova Mungu wake.” Pengine Daudi alifanya vile namna gani? Tunajua kama, kwa kawaida Daudi alisali kwa Yehova ili amusaidie, na alifikiri kuhusu namna Yehova alimusaidia wakati wa zamani. (1 Sa. 17:37; Zb. 18:2, 6) Daudi aliona ulazima wa kutafuta muongozo wa Yehova, njo maana alimuuliza Yehova mambo yenye alipaswa kufanya. Kisha Daudi kupata muongozo wa Yehova, alitenda mara moya. Ile ilifanya yeye na watu wake wabarikiwe na Yehova, na walipata tena familia zao na vitu vyao. (1 Sa. 30:7-9, 18, 19) Uliona mambo tatu yenye Daudi alifanya? Alisali kwa Yehova ili amusaidie, alifikiri juu ya mambo yenye Yehova alimufanyia wakati wa zamani, na alitenda kulingana na muongozo wa Yehova. Namna gani tunaweza kumuiga Daudi? Fikiria hii mambo tatu.

UMUIGE DAUDI WAKATI UKO NA MAHANGAIKO

1. Usali. Wakati wowote wenye tuko na mahangaiko, tunaweza kumuomba Yehova musaada na hekima. Kuzungumuza na Yehova kwa muda murefu na kumuambia mambo yote yenye iko mu moyo wetu kunaweza kutusaidia kupunguza mahangaiko yetu. Ao tunaweza kutoa sala ya mufupi, ya kimya-kimya kama ile njo hali yetu inaturuhusu kufanya mu ile wakati. Kila wakati tunatafuta musaada wa Yehova, tunaonyesha kama tunamutumainia sawa vile Daudi alifanya, mwenye alisema: “Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu na Ule mwenye ananiokoa. Mungu wangu ni mwamba wangu, mwenye ninakimbilia.” (Zb. 18:2) Sala inasaidiaka kabisa? Dada Kahlia mwenye ni painia, anasema hivi: “Kisha kusali najisikiaka kuwa na amani. Sala inanisaidiaka kuwaza zaidi sawa vile Yehova anawazaka na kumutumainia zaidi.” Kusema kweli, sala ni zawadi yenye nguvu sana kutoka kwa Yehova yenye inatusaidia kupambana na mahangaiko yetu.

2. Ufikiri. Wakati unafikiria mambo yenye ilikupata, unakumbuka magumu yenye uliweza kuvumilia juu tu Yehova alikusaidia? Wakati tunafikiri juu ya namna Yehova alitusaidia na vile alisaidia watumishi wake zamani, ile itatusaidia tukuwe na amani zaidi na tumutumainie zaidi. (Zb. 18:17-19) Joshua, mwenye ni muzee anasema hivi: “Niko na liste ya sala zenye Yehova alijibia, na ile imenisaidia kukumbuka wakati nilimuomba jambo fulani na wakati alinipatia kabisa mambo yenye nilikuwa nayo lazima.” Wakati tunafikiri juu ya mambo yenye Yehova alishatufanyia, tunapata nguvu yenye tuko nayo lazima ili kuendelea kupiganisha mahangaiko yetu.

3. Utende. Mbele ya kuamua mambo yenye tutafanya mu hali fulani, tunaweza kutegemea Neno ya Mungu juu tupate muongozo wa muzuri zaidi. (Zb. 19:7, 11) Wengi wanaona kama wakati wanatafuta habari juu ya andiko fulani wanaelewa muzuri zaidi namna inawahusu mu maisha yao. Muzee moya mwenye jina yake ni Jarrod, anasema hivi: “Kutafuta habari kunanisaidiaka kujifunza mengi zaidi juu ya andiko fulani na kuelewa mambo yenye Yehova iko ananiambia. Ile inanisaidia kuamini kabisa mambo yenye niko nasoma juu niweze kutenda kulingana na muongozo wenye napata.” Wakati tunatafuta muongozo wa Yehova mu Maandiko na tunaifuata itakuwa mwepesi sana kwetu kuwa na amani na furaha wakati tuko na mahangaiko.

YEHOVA ATAKUSAIDIA KUPIGANISHA MAHANGAIKO YAKO

Daudi alielewa kama juu aweze kupiganisha mahangaiko yake alikuwa na lazima ya musaada wa Yehova. Alisamini sana musaada wa Yehova, njo maana alichochewa kusema hivi: “Kwa nguvu za Mungu ninaweza kupanda ukuta. Mungu wa kweli ndiye ananivalisha nguvu.” (Zb. 18:29, 32) Pengine tunaweza kujisikia sawa vile magumu yetu iko nguvu sana na kama hatuwezi kabisa kuivumilia. Lakini kwa musaada wa Yehova tunaweza kuvumilia magumu yoyote! Wakati tunasali kwa Yehova ili atusaidie, na kufikiri juu ya mambo yote yenye alishatufanyia, na pia kutenda kulingana na muongozo wake, tunaweza kuwa hakika kama atatupatia nguvu na hekima yenye tuko nayo lazima ili kupambana na mahangaiko yetu!

^ fu. 2 Mutu mwenye iko na mahangaiko sana anaweza kuwa na lazima ya kuonana na munganga.