Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 18

Namna ya Kujiwekea na Kufikia Miradi ya Kiroho

Namna ya Kujiwekea na Kufikia Miradi ya Kiroho

“Fikiri sana juu ya mambo hayo; zama katika mambo hayo, ili maendeleo yako yaonekane wazi kwa watu wote.”​—1 TI. 4:15.

WIMBO 84 Niko Tayari Kusaidia!

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni miradi gani ya kiroho yenye tunaweza kujiwekea?

 JUU tuko Wakristo wa kweli, tunamupenda sana Yehova. Tunapenda kufanya yetu yote mu utumishi wetu kwake. Lakini juu tufanye vile, tunapaswa kujiwekea miradi ya kiroho, sawa vile kuonyesha sifa za Kikristo, kujifunza ufundi mbalimbali, na kutafuta njia mbalimbali za kutumikia wengine. *

2. Juu ya nini tunapaswa kujiwekea miradi ya kiroho na kujikaza kuifikia?

2 Juu ya nini tunapaswa kujiwekea miradi ya kiroho? Kwanza kabisa, ni juu tunapenda kumufurahisha Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo. Yehova anafurahi wakati tunatumia kwa ukamili vipawa vyetu na uwezo wenye tuko nao mu kazi yake. Zaidi ya ile, tunapenda kufanya maendeleo ya kiroho juu tusaidie sana ndugu na dada zetu. (1 Te. 4:9, 10) Hata kama tulishafanya miaka ngapi katika kweli, siye wote tunaweza kufanya maendeleo ya kiroho. Tuone namna tunaweza kufanya vile.

3. Vile 1 Timoteo 4:12-16 inaonyesha, mutume Paulo alimutia moyo Timoteo afanye nini?

3 Wakati mutume Paulo alimuandikia kijana Timoteo barua ya kwanza, tayari Timoteo alikuwa muzee mwenye uzoefu. Hata vile, Paulo alimutia moyo aendelee kufanya maendeleo ya kiroho. (Soma 1 Timoteo 4:12-16.) Kama unafikiria muzuri maneno ya Paulo, utaona kama alipenda Timoteo afanye maendeleo mu njia mbili: (1) Kuonyesha sifa za Kikristo sawa vile upendo, imani, na kuwa na mwenendo safi. (2) Kuongeza ufundi wake katika kusoma mbele ya watu, kutia moyo, na kufundisha. Kupitia mufano wa Timoteo, tuone namna kujiwekea miradi yenye tunaweza kufikia kunaweza kutusaidia kufanya maendeleo ya kiroho. Tutazungumuzia pia njia fulani za kutusaidia kupanua utumishi wetu.

UONYESHE SIFA ZA KIKRISTO

4. Kulingana na Wafilipi 2:19-22, ni nini ilifanya Yehova amutumikishe Timoteo?

4 Ni nini ilifanya Yehova amutumikishe Timoteo? Ni sifa zake za Kikristo. (Soma Wafilipi 2:19-22.) Kupitia namna Paulo anamuzungumuzia Timoteo, tunaona kama Timoteo alikuwa munyenyekevu, mushikamanifu, mwenye bidii, na mwenye kutumainika. Alipenda ndugu zake na aliwahangaikia sana. Na ile ilifanya Paulo amupende Timoteo na amupatie migao yenye ilikuwa nguvu. (1 Ko. 4:17) Vilevile, Yehova atatupenda na kututumikisha mu kutaniko kama tunaonyesha sifa zenye anapenda.​—Zb. 25:9; 138:6.

Chagua sifa ya Kikristo yenye unapenda kuonyesha zaidi (Ona fungu ya 5-6)

5. (a) Ni nini inaweza kukusaidia ujue sifa ya Kikristo yenye unapaswa kufanyia maendeleo? (b) Vile picha inaonyesha, dada kijana anafanya nini juu ya kufikia muradi wake wa kuonyesha wengine huruma zaidi?

5 Chagua sifa yenye unapenda kufanyia maendeleo. Fikiria mu sala sehemu za utu wako zenye unapaswa kufanyia maendeleo. Chagua sifa yenye unapenda kufanyia maendeleo. Kwa mufano, unaweza kuonyesha huruma zaidi ao kukomalisha tamaa ya kupenda sana kutegemeza waabudu wenzako? Inaomba kabisa ujikaze kuwa mwenye kufanya amani zaidi na mwenye kusamehe? Unaweza kuomba rafiki yako wa karibu akuambie sifa zenye unaweza kufanyia maendeleo.​—Mez. 27:6.

6. Unaweza kufanya nini ili kufikia muradi wako wa kuonyesha sifa fulani?

6 Jikaze kufikia muradi wako. Unaweza kufanya vile namna gani? Njia moya ni kujifunza kwa uangalifu sifa yenye unapenda kuonyesha zaidi. Wazia unapenda kuwa mwenye kusamehe wengine zaidi. Unaweza kuanza kusoma na kufikiri sana juu ya mifano yenye kuwa mu Biblia ya watu wenye walisamehe wengine kwa kupenda na ya wenye hawakusamehe. Fikiria mufano wa Yesu. Alisamehe wengine kwa kupenda. (Lu. 7:47, 48) Hakukaza akili juu ya makosa yao, lakini alikaza akili juu ya mambo yenye wangeweza kufanya. Lakini mu wakati wa Yesu, wafarisayo ‘walizarau wengine.’ (Lu. 18:9) Kisha kufikiri sana juu ya ile mifano, ujiulize hivi: ‘Ni nini naona kwa wengine? Wako na sifa gani zenye niko nakazia akili?’ Kama uko unashindwa kusamehe mutu fulani, pima kuandika sifa mingi za muzuri zenye ule mutu iko nazo. Kisha ujiulize hivi: ‘Yesu iko namuona namna gani? Anaweza kumusamehe?’ Kujifunza vile kunaweza kutusaidia kubadilisha mawazo yetu. Ku mwanzo, inaweza kuwa nguvu kusamehe mutu mwenye alitukosea. Lakini kama tunajikaza, ku mwisho, tutapenda zaidi kumusamehe.

UJIFUNZE UFUNDI MBALIMBALI

Ujifunze namna ya kufanya kazi ya kutunza Jumba yenu ya Ufalme (Ona fungu ya 7) *

7. Ni mu njia gani Yehova iko anatumia wafanyakazi wenye ufundi leo? (Mezali 22:29)

7 Muradi ingine yenye unaweza kujiwekea ni ya kujifunza ufundi fulani. Fikiria wafanyakazi wengi wenye wanahitajiwa juu ya kujenga majengo ya Beteli, Majumba ya Mikusanyiko, na Majumba ya Ufalme. Wengi kati ya wale wafanyakazi walijifunza ufundi mbalimbali kwa kutumika pamoya na ndugu na dada wenye kuwa na uzoefu. Vile picha inaonyesha, ndugu na dada wako wanajifunza ufundi mbalimbali wenye unahitajiwa ili kusaidia kutunza Majumba ya Mikusanyiko na Majumba ya Ufalme. Kupitia zile njia na njia zingine, Yehova Mungu, “Mufalme wa umilele,” na Kristo Yesu, “Mufalme wa . . . wafalme,” wako wanatumia ndugu na dada wenye kuwa na ufundi ili kufanya mambo makubwa. (1 Ti. 1:17; 6:15; soma Mezali 22:29.) Tunapenda kabisa kutumia ufundi wenye tuko nao ili kumutukuza Yehova, hapana juu ya kujitukuza.​—Yoh. 8:54.

8. Unaweza kufanya nini ili kujua ni muradi gani wenye unaweza kufikia?

8 Chagua muradi wenye unaweza kufikia. Unapenda kufikia muradi gani? Uliza wazee wa mu kutaniko yenu na pengine mwangalizi wa muzunguko wenu ni ufundi gani wanaona unaweza kujifunza. Kama, kwa mufano, wanapendekeza uongeze ufundi wako wa kusema na kufundisha, uwaulize wakuambie ni sifa gani ya usemi yenye unapaswa kufanyia kazi. Kisha ujikaze kufanya vile wanakuambia. Unaweza kufanya vile namna gani?

9. Ni nini inaweza kukusaidia kufikia muradi wako wa kujifunza ufundi fulani?

9 Jikaze kufikia muradi wako. Tuseme unapenda kuongeza ufundi wako wa kufundisha. Unaweza kujifunza kwa uangalifu broshua Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha. Wakati uko na sehemu ku mukutano wa katikati ya juma, unaweza kuambia ndugu mwenye kuwa na uzoefu asikilize vile ulitayarisha na umuombe mapendekezo fulani ya kukusaidia kufanya muzuri zaidi. Usitayarishe migao yako juu tu ya kuwa mwenye ufundi, lakini pia juu watu waone kama uko mwenye bidii na mwenye kutumainika.​—Mez. 21:5; 2 Ko. 8:22.

10. Zungumuzia mufano wenye unaonyesha jambo ya kufanya ili kufikia muradi wa kujifunza ufundi fulani.

10 Utafanya nini kama ufundi wenye unapenda kujifunza hauko mwepesi kwako? Usivunjike moyo! Ndugu mwenye kuitwa Garry alikuwa na magumu ya kusoma muzuri. Anakumbuka vile alisikiaka haya wakati alijikazaka kusoma kwa sauti ku mikutano ya kutaniko. Lakini aliendelea kujikaza. Sasa anasema kama mazoezi yenye alipataka iko inamusaidia kutoa hotuba ku Majumba ya Ufalme, na ku mikusanyiko!

11. Sawa vile Timoteo, ni nini itatusaidia tukuwe na mambo mingi zaidi ya kufanya mu kazi ya Yehova?

11 Timoteo alifikiaka kuwa musemaji na mwalimu muzuri? Biblia haionyeshe. Lakini bila shaka, Timoteo alifikia kushugulikia muzuri zaidi madaraka yake juu alifuataka shauri ya Paulo. (2 Ti. 3:10) Vilevile, kama tunakomalisha ufundi wetu, tutakuwa na mambo mingi zaidi ya kufanya mu utumishi wetu kwa Yehova.

TAFUTA NJIA MBALIMBALI ZA KUTUMIKIA WENGINE

12. Kazi yenye wengine wako wanafanya, ilikuletea faida gani?

12 Kazi yenye wengine wako wanafanya inatuleteaka siye wote faida. Wakati tuko ku hopitale, tunashukuru wakati tunatembelewa na wazee wenye kutumika mu Halmashauri za Uhusiano na Hopitale ao mu Vikundi vya Kutembelea Wagonjwa. Wakati tunapambana na hali ya nguvu mu maisha yetu, tunashukuru wakati muzee mwenye kuwa na upendo anachukua wakati wa kutusikiliza na kutufariji. Wakati tuko na lazima ya mutu fulani wa kutusaidia kuongoza funzo, tunafurahi saa yenye painia mwenye kuwa na uzoefu anatusindikiza ku funzo na kututolea mapendekezo. Wale ndugu na dada wote wanafurahi kutusaidia. Na siye tunaweza kuwa na ile furaha kama tuko tayari kusaidia ndugu zetu. Yesu alisema hivi: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Kama unapenda kupanua utumishi wako mu hizi njia ao njia zingine, ni nini itakusaidia kufanya vile?

13. Wakati tuko najiwekea muradi fulani, tunapaswa kukumbuka nini?

13 Usijiwekee muradi wenye hauko wazi. Kwa mufano, unaweza kusema, ‘Napenda kufanya mingi zaidi mu kutaniko.’ Lakini inaweza kuwa nguvu kujua namna ya kufikia muradi wa vile, na inaweza hata kuwa nguvu kujua kama ulishakaufikia ao hapana. Kwa hiyo, ujiwekee muradi wenye kuwa wazi, wenye unapenda kufikia. Unaweza hata kuandika ule muradi na namna unapanga kuufikia.

14. Juu ya nini tunapaswa kuwa na usawaziko wakati tunajiwekea miradi?

14 Tunapaswa kuwa na usawaziko wakati tuko najiwekea miradi. Juu ya nini? Juu hali zetu zinaweza kubadilika. Kwa mufano: Mutume Paulo alisaidia kuanzisha kutaniko ya mupya mu muji wa Tesalonike. Na bila shaka, alikuwa na muradi wa kubakia mule juu asaidie Wakristo wapya. Lakini wapinzani walimulazimisha atoke mu ile muji. (Mdo. 17:1-5, 10) Paulo angebakia mule, angetia ndugu zake mu hatari. Lakini Paulo hakukata tamaa. Alijipatanisha na hali. Kisha, alituma Timoteo ili asaidie Wakristo wapya wenye walikuwa mu Tesalonike ili wakuwe na imani ya nguvu. (1 Te. 3:1-3) Wakristo wa Tesalonike walifurahi juu Timoteo alikuwa tayari kutumikia kila fasi kwenye watu walikuwa na lazima yake!

15. Mabadiliko inaweza kuwa na matokeo gani juu ya miradi yetu? Toa mufano.

15 Mambo yenye ilifikia Paulo mu Tesalonike inaweza kutufundisha mambo fulani. Tunaweza kuwa na muradi fulani, lakini hali zetu zinaweza kubadilika na kutuzuia tusiufikie. (Muh. 9:11) Kama ile inakufikia, ukuwe tayari kuchagua muradi ingine yenye unaweza kufikia. Ni vile Ted na Hiedi bibi yake walifanya. Juu walikuwa na magumu fulani ya afya, walitoka ku Beteli. Lakini juu walimupenda Yehova, walitafuta njia zingine za kupanua utumishi wao. Kwanza, walianza kazi ya upainia wa kawaida. Kisha, waliwekwa kuwa mapainia wa pekee, na Ted akazoezwa ili kuwa mwangalizi wa muzunguko wa badala. Kisha mabadiliko ikafanywa kuhusu miaka yenye waangalizi wa mizunguko wanapaswa kuachia wengine ile daraka. Ted na Hiedi walielewa kama hawangeendelea tena kutumikia ile daraka. Hata kama walivunjika moyo, walijua kama wanaweza kumutumikia Yehova mu njia zingine. Ted anasema: “Tulijifunza kama hatupaswe kukaza akili yetu juu ya aina moya tu ya utumishi.”

16. Ni somo gani tunapata mu Wagalatia 6:4?

16 Hakuna mwenye anaweza kujua kama maisha yake itakuwa namna gani kesho. Kwa hiyo, haiko muzuri kuwaza kama Yehova anatuona kuwa wa maana juu tu ya mapendeleo fulani ya utumishi yenye tuko nayo na haiko muzuri kulinganisha mapendeleo yenye tuko nayo na ya wengine. Hiedi anasema hivi: “Amani yako inapotea wakati unalinganisha maisha yako na ya watu wengine.” (Soma Wagalatia 6:4.) Ni jambo ya maana tutafute njia za kusaidia wengine na kumutumikia Yehova. *

17. Unaweza kufanya nini juu ufikie mapendeleo fulani ya utumishi?

17 Ukuwe na maisha ya mwepesi na uepuke madeni yenye haiko ya lazima juu ukuwe na mambo mingi zaidi ya kufanya mu kazi ya Yehova. Ujiwekee miradi ya kidogo-kidogo yenye itakusaidia kufikia miradi mikubwa. Kwa mufano, kama muradi wako ni kuwa painia wa kawaida, kuanzia sasa unawaza namna gani kama unakuwa painia musaidizi wa kila mwezi? Kama muradi wako ni kuwa mutumishi wa huduma, unawaza namna gani kama unaanza kupitisha wakati mingi zaidi mu mahubiri na kujikaza kutembelea wagonjwa na ndugu na dada wenye kuzeeka mu kutaniko yenu? Uzoefu wenye unapata sasa unaweza kukufungulia mulango wa kupata mapendeleo ingine ya utumishi mu wakati wenye kuya. Uazimie kufanya yako yote mu mugao wote wenye unapewa.​—Ro. 12:11.

Chagua muradi wenye kuwa wazi wenye unaweza kufikia (Ona fungu ya 18) *

18. Sawa vile picha inaonyesha, mufano wa Beverley unakufundisha nini?

18 Hata kama tulishazeeka tunaweza kujiwekea na kufikia miradi fulani ya kiroho. Fikiria mufano wa dada mwenye kuitwa Beverley, mwenye kuwa na miaka 75. Alikuwa na tatizo kubwa sana ya afya yenye ilifanya ikuwe nguvu kwake kutembea. Lakini alipenda kufanya mambo mingi ili kutegemeza kampanye ya Ukumbusho. Kwa hiyo, alijiwekea miradi yenye kuwa wazi. Wakati alifikia miradi yake kuhusu ile kampanye, alifurahi sana. Bidii yake ilichochea na wengine watumike sana mu kazi ya mahubiri. Yehova anasamini kazi ya ndugu na dada wenye kuzeeka, hata kama hali zao zinawazuia kufanya mambo yenye wanapenda kufanya.​—Zb. 71:17, 18.

19. Ni miradi gani ya kiroho yenye tunaweza kujiwekea?

19 Ujiwekee miradi yenye unaweza kufikia. Onyesha sifa zenye zitamufurahisha Yehova. Ujifunze ufundi mbalimbali wenye utafanya Mungu akutumikishe zaidi na pia tengenezo yake. Tafuta njia za kutumikia ndugu na dada zako kwa ukamili. * Sawa vile Timoteo, Yehova akubariki “ili maendeleo yako yaonekane wazi kwa watu wote.”​—1 Ti. 4:15.

WIMBO 38 Atakupatia Nguvu

^ fu. 5 Timoteo alikuwa muhubiri wa habari njema mwenye uzoefu. Lakini mutume Paulo alimutia moyo aendelee kufanya maendeleo ya kiroho. Juu Timoteo alifuata shauri ya Paulo, Yehova alimutumia zaidi na alisaidia sana ndugu na dada zake. Sawa vile Timoteo, na weye unapenda kumutumikia sana Yehova na pia waamini wenzako? Bila shaka unapenda. Ni miradi gani yenye inaweza kukusaidia kufanya vile? Na unapaswa kufanya nini juu ya kujiwekea na kufikia ile miradi?

^ fu. 1 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Miradi ya kiroho inatia ndani kila kitu yenye tunaweza kufanya ili tumutumikie Yehova kwa ukamili na kumufurahisha.

^ fu. 16 Ona habari “Kutumikia Fasi Kwenye Kuko Lazima Kubwa” mu kitabu Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova, sura ya 10, fu. 6-9.

^ fu. 19 Ona somo ya 60, “Usiache Kufanya Maendeleo,” yenye kuwa mu kitabu Furahia Maisha Milele!

^ fu. 63 MAFASIRIO YA PICHA Ndugu iko nazoeza dada wawili namna ya kufanya kazi ya kutunza majengo, kisha wanatumia muzuri ule ufundi wenye walipata.

^ fu. 65 MAFASIRIO YA PICHA Dada mwenye hatokake ku nyumba yake iko nahubiri kupitia telefone, na iko naalika watu ku Ukumbusho.