Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Biblia inasema nini juu ya kufanya kiapo?

Kiapo ni “tangazo nzito sana ao ahadi ya kufanya jambo fulani, mara mingi Mungu njo anakuwaka . . . shahidi wa ile kiapo.” Kiapo inaweza kusemwa kwa maneno ao kuandikwa.

Watu fulani wanaweza kusema kama ni mubaya kufanya kiapo juu Yesu alisemaka hivi: “Haupaswe kuapa . . . Muache tu neno lenu ‘Ndiyo’ limaanishe ndiyo, na ‘Hapana’ yenu imaanishe hapana, kwa maana lenye kupita hayo linatoka kwa ule muovu.” (Mt. 5:33-37) Yesu alijua kama, Sheria ya Musa iliomba Waisraeli wafanye kiapo mu hali fulani na kama watumishi fulani wa Mungu walifanyaka pia viapo. (Mwa. 14:22, 23; Kut. 22:10, 11) Alijua pia kama Yehova mwenyewe alifanyaka viapo. (Ebr. 6:13-17) Kwa hiyo, Yesu hakupenda kusema kama hatupaswe kufanya kiapo. Lakini, alikuwa njo anaonya watu kama hawapaswe kufanya viapo juu ya mambo yenye haiko ya maana ao mu njia yenye haifae. Sikuzote tunapaswa kutimiza mambo yenye tunaahidi, juu njo vile Yehova anapenda tufanye.

Sasa unapaswa kufanya nini kama wanakuomba ufanye kiapo? Kwanza, ukuwe hakika kama unaweza kufanya mambo yenye unataka kulapia. Kama hauko hakika, inaweza kuwa muzuri zaidi usifanye kiapo. Neno ya Mungu inatuonya hivi: “Ni muzuri zaidi usiweke naziri kuliko kuweka naziri na kukosa kuitimiza.” (Muh. 5:5) Pili, fikiria kanuni za Biblia zenye zinapatana na ile kiapo yako, kisha utende kulingana na zamiri yako. Tunaweza kufikiria kanuni gani fulani za Biblia?

Viapo fulani vinapatana na mapenzi ya Mungu. Kwa mufano, Mashahidi wa Yehova wanafanyaka naziri wakati wa kufunga ndoa. Zile naziri ni aina fulani ya kiapo. Mbele ya Mungu na mashahidi, bwana na bibi arusi wanaahidi kama watapendana sana na kuheshimiana “muda wote wenye wataishi pamoya.” (Pengine bibi na bwana hawatasema ile maneno vile iko, lakini watafanya naziri mbele ya Mungu.) Kisha wanatangazwa kuwa bibi na bwana na wanapaswa kuendelea kuishi pamoya maisha yao yote. (Mwa. 2:24; 1 Ko. 7:39) Ile naziri ya ndoa inafaa kabisa na inapatana na mapenzi ya Mungu.

Viapo fulani havipatane na mapenzi ya Mungu. Mukristo wa kweli hatafanya kiapo juu ya kupigania inchi ao juu ya kukana imani yake kwa Mungu. Kufanya vile itakuwa kuvunja sheria ya Mungu. Wakristo ‘hawapaswe kuwa sehemu ya ulimwengu,’ njo maana hatuwezi kujiingiza mu mabishano ya mambo ya hii ulimwengu na mu mambo ya vita.​—Yoh. 15:19; Isa. 2:4; Yak. 1:27.

Viapo fulani vinaomba kutumia zamiri. Wakati fulani, tunapaswa kuchunguza kwa uangalifu sana shauri ya Yesu yenye kusema hivi: “Mulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu,” mbele ya kuamua ikiwa tutafanya kiapo fulani ao hapana.​—Lu. 20:25.

Kwa mufano, waza Mukristo anapenda kupata uraia ao passeport na kisha wanamuambia kama anapaswa kufanya kiapo fulani. Kama mu ile inchi kufanya kiapo ya vile inamaanisha kutenda mu njia yenye inapingana na sheria ya Mungu, zamiri yake yenye kuzoezwa na Biblia haitamuruhusu kufanya vile. Lakini, serikali inaweza kumuruhusu abadilishe maneno fulani ya kiapo juu ya zamiri yake.

Kufanya kiapo yenye inabadilishwa kidogo inaweza kupatana na kanuni yenye kupatikana mu Waroma 13:1, yenye inasema: “Kila mutu ajitiishe kwa mamlaka zenye kuwa kubwa.” Mukristo fulani anaweza kuamua kama hakuna ubaya wa kufanya kiapo juu ya jambo fulani yenye tayari Mungu amemuomba afanye.

Zamiri inaweza pia kusaidia kama wanakuomba kutumia kitu fulani ao kufanya alama fulani wakati uko unaapa. Waroma na Wasikite wa zamani waliapa kwa kutumia mipanga yao na ile ilikuwa inaonyesha kama wanatumainia nguvu ya mungu wa vita. Wagiriki walikuwa wananyangula mukono yulu kuelekea mbinguni wakati wa kufanya kiapo. Kwa kufanya vile, walitambua kama kuko nguvu fulani ya kimungu yenye ilikuwa inaona mambo yote yenye walikuwa wanasema na kufanya na iliwakumbusha kama ni kwa nani njo wanapaswa kutoa hesabu.

Kwa kweli, mutumishi wa Yehova hawezi kuapa kwa kutumia kitu ao alama fulani ya taifa yenye iko na uhusiano na ibada ya uongo. Lakini, tuseme nini kama tribinali inakuomba utie mukono wako juu ya Biblia na kufanya kiapo yenye itatoa ushahidi wenye kuonyesha kama mambo yenye utasema ni ya kweli? Mu ile hali unaweza kuamua kufanya vile, juu Biblia inazungumuzia waaminifu wa zamani wenye walikuwa wanafanya alama fulani wakati wa kuapa. (Mwa. 24:2, 3, 9; 47:29-31) Ni jambo ya maana kukumbuka kama, wakati uko nafanya ile kiapo uko unaapa mbele ya Mungu kama utasema kweli. Inaomba ujitayarishe ili kusema kweli ku kila ulizo yenye unaweza kuulizwa.

Juu tanasamini uhusiano wetu na Yehova, tunapaswa kusali na kufikiri kwa uangalifu juu ya kila kiapo yenye tunaombwa kufanya, na kuhakikisha kama haipingane na zamiri yetu ao na kanuni za Biblia. Kama unaamua kufanya kiapo, ukuwe hakika kama utaitimiza.​—1 Pe. 2:12.