Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 15

Uko “Mufano ... Katika Kusema”?

Uko “Mufano ... Katika Kusema”?

“Ukuwe mufano kwa waaminifu katika kusema.”​—1 TI. 4:12.

WIMBO 90 Tutiane Moyo

KIFUPI YA HABARI *

1. Uwezo wetu wa kusema, ulitoka wapi?

 UWEZO wetu wa kusema ulitoka kwa Mungu wetu mwenye upendo. Adamu, mwanadamu wa kwanza kuumbwa, alianza kuzungumuza na Baba yake wa mbinguni kisha tu kuumbwa. Alikuwa pia anatunga maneno ingine ya mupya. Ni vile alifanya wakati alikuwa anapatia wanyama majina. (Mwa. 2:19) Na alifurahi sana wakati alisema kwa mara ya kwanza na mwanadamu mwingine, ni kusema, bibi yake mwenye alikuwa na sura na umbo ya muzuri, Eva!​—Mwa. 2:22, 23.

2. Ni nini inaonyesha kama zawadi ya kusema imetumiwa mubaya zamani na leo?

2 Bila kuchelewa, ile zawadi ya kusema ilianza kutumiwa mubaya. Shetani Ibilisi alimudanganya Eva, na ule uongo ukafanya mwanadamu akuwe na zambi na asikuwe mukamilifu. (Mwa. 3:1-4) Adamu alitumia mubaya uwezo wake wa kusema wakati alimulaumu Eva, na hata Yehova, kwa sababu ya makosa yake mwenyewe. (Mwa. 3:12) Kisha kuua ndugu yake Abeli, Kaini alimudanganya Yehova. (Mwa. 4:9) Kisha, muzao wa Kaini mwenye kuitwa Lameki alitunga wimbo wenye ulionyesha jeuri yenye ilikuwa mu wakati wake. (Mwa. 4:23, 24) Watu wako namna gani leo? Tunajionea namna viongozi wa politike wanatumia maneno machafu mbele ya watu. Na leo, iko nguvu kupata filme yenye haina maneno machafu. Wanafunzi wanasikiaka maneno machafu ku masomo, na watu wazima wanaisikiaka kwenye wanatumikiaka. Jambo ya kuhuzunisha ni kama namna maneno machafu iko inatumiwa sana leo, inaonyesha kama dunia ilishaharibika sana.

3. Tunapaswa kuwa waangalifu juu ya hatari gani, na tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Kama hatuko waangalifu, tunaweza kuzoea kusikiliza maneno machafu na ku mwisho tunaweza kuanza kuitumia. Kwa kweli, juu tuko Wakristo tunapenda kumufurahisha Yehova. Kwa hiyo, tunapaswa kuepuka kabisa kutumia maneno machafu. Tunapaswa kutumia pia zawadi yetu ya kusema mu njia ya muzuri ili kumusifu Mungu. Mu hii habari, tutazungumuzia namna ya kufanya vile (1) mu mahubiri, (2) ku mikutano ya kutaniko, na (3) mu mazungumuzo yetu ya kila siku. Kwanza, tuzungumuzie juu ya nini Yehova anakuwaka muangalifu juu ya namna tunatumia maneno yetu.

YEHOVA ANAKUWAKA MUANGALIFU JUU YA NAMNA TUNATUMIA MANENO YETU

Maneno yako inafunua nini juu ya mambo yenye kuwa mu moyo wako? (Ona fungu ya 4-5) *

4. Kulingana na Malaki 3:16, juu ya nini Yehova anakuwaka muangalifu juu ya namna tunatumia maneno yetu?

4 Soma Malaki 3:16. Unawaza ni juu ya nini Yehova anaandika mu ‘kitabu yake ya kumbukumbu’ majina ya wale wenye maneno yao inaonyesha kama wanamuogopa na kufikiri sana juu ya jina yake? Juu maneno yetu inafunua mambo yenye kuwa mu moyo wetu. Yesu alisema: “Kinywa kinasema mambo yenye kujaa katika moyo.” (Mt. 12:34) Mambo yenye tunazungumuziaka inaonyesha ni kwa kiasi gani tunamupenda Yehova. Na Yehova anapenda kupatia wale wenye wanamupenda, uzima wa milele mu dunia mupya.

5. (a) Kuko uhusiano gani kati ya maneno yetu na ibada yetu? (b) Sawa vile picha inaonyesha, tunapaswa kuepuka kufanya nini kama tunapenda kumufurahisha Yehova kupitia maneno yetu?

5 Maneno yetu inaweza kufanya Yehova akubali ao akatale ibada yetu. (Yak. 1:26) Watu fulani wenye hawamupende Mungu wanatumiaka maneno ya makali, yenye kukosa upendo, na ya kiburi. (2 Ti. 3:1-5) Hatupende kabisa kuwaiga. Tunapenda kumufurahisha Yehova kwa maneno yetu. Sasa, unawaza Yehova atafurahi kama tuko tunatumia maneno yenye upendo ku mikutano yetu ya Kikristo ao mu mahubiri, lakini wakati tuko na watu wa familia yetu tunatumia maneno ya makali na yenye kukosa upendo?​—1 Pe. 3:7.

6. Maneno ya muzuri ya Kimberly, ilikuwa na matokeo gani ya muzuri?

6 Wakati tunatumia muzuri zawadi yetu ya kusema, tunajitambulisha kama tuko waabudu wa Yehova. Tunasaidia wale wenye tunaishi nao waone waziwazi tofauti “kati ya mutu mwenye kumutumikia Mungu na mwenye hamutumikie.” (Mal. 3:18) Ni vile ilikuwa kwa dada moya mwenye kuitwa Kimberly. * Alikuwa na kazi fulani ya masomo ya kufanya yeye na mwanafunzi mwenzake. Kisha kutumika pamoya, mwanafunzi mwenzake aliona kama Kimberly alikuwa tofauti na wanafunzi wengine. Hakukuwa nasema watu mubaya, lakini alikuwa natumia maneno ya muzuri, na aliepuka kutumia maneno machafu. Ule mwanafunzi aliguswa moyo, na ku mwisho akaamua kuanza kujifunza Biblia. Wazia vile Yehova anakuwaka na furaha wakati tunasema mu njia yenye inafanya watu wapendezwe na kweli!

7. Utatumia namna gani zawadi ya kusema yenye Mungu alikupatia?

7 Siye wote tunapenda kusema mu njia yenye inamuletea Yehova heshima na yenye inafanya ndugu zetu watukaribie zaidi. Kwa hiyo, tuzungumuzie njia fulani zenye zinatupatia nafasi ya kuendelea kuwa “mufano . . . katika kusema.”

UKUWE MUFANO MU MAHUBIRI

Kutumia maneno yenye fazili wakati tuko nazungumuza na watu mu mahubiri kunamufurahishaka Yehova (Ona fungu ya 8-9)

8. Namna Yesu alitumia zawadi yake ya kusema mu mahubiri, inatufundisha nini?

8 Useme kwa fazili na kwa heshima wakati wengine wanakukasirisha. Wakati wa utumishi wake, Yesu alishitakiwa kimakosa kama alikuwa mulevi, mulafi, mutumishi wa Ibilisi, muvunjaji wa Sabato, na hata wengine walisema kama alikufuru Mungu. (Mt. 11:19; 26:65; Lu. 11:15; Yoh. 9:16) Hata vile, Yesu hakujibia kwa kutumia maneno makali. Kama vile Yesu, wakati wengine wanatukasirisha hatupaswe kuwajibia kwa ukali. (1 Pe. 2:21-23) Lakini, kufanya vile haiko mwepesi. (Yak. 3:2) Ni nini itatusaidia?

9. Ni nini inaweza kutusaidia kuzuia maneno yetu wakati tuko mu mahubiri?

9 Wakati mutu fulani mu mahubiri anakujibia kwa ukali, usikasirike. Ndugu Sam anasema hivi: “Miye najikazaka kukaza akili yangu juu ya uhitaji wenye musikilizaji iko nao wa kupenda kujua kweli na kujiambia kama siku moya anaweza kubadilika.” Wakati fulani musikilizaji anaweza kukasirika juu tu tunamufikia mu wakati wenye haufae. Wakati tunakutana na mutu mwenye kukasirika, tunaweza kufanya sawa vile dada Lucia. Tunaweza kutoa sala ya mufupi, ili kumuomba Yehova atusaidie tukuwe wenye kutulia na atusaidie kuepuka kusema maneno yenye haina upendo ao yenye haina heshima.

10. Kulingana na 1 Timoteo 4:13, tunapaswa kujiwekea muradi gani?

10 Ukuwe mwalimu muzuri zaidi. Timoteo alikuwa mutumishi Mukristo mwenye uzoefu, lakini iliomba aendelee kufanya maendeleo ya kiroho. (Soma 1 Timoteo 4:13.) Tunaweza kufanya nini juu tukuwe walimu wazuri zaidi mu mahubiri? Tunapaswa kujitayarisha muzuri. Inafurahisha kujua kama, tuko na vyombo mbalimbali vya kutusaidia ili tukuwe walimu wazuri zaidi. Unaweza kupata habari ya kukusaidia mu broshua Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha na mu sehemu “Tujitoe Kabisa mu Kazi ya Kuhubiri,” yenye kuwa mu Buku ya Mukutano​—Utumishi na Maisha ya Mukristo. Unatumiaka vile vyombo? Kama tunajitayarisha muzuri, hatutahangaika na tutasema na uhakika zaidi.

11. Ni nini imesaidia Wakristo fulani kuwa walimu wazuri zaidi?

11 Tunaweza pia kuwa walimu wazuri kwa kujikaza kuiga wengine mu kutaniko. Sam, mwenye tulishataya, anajiulizaka nini njo Wakristo fulani wanafanyaka juu wakuwe walimu wazuri. Anasikiliza kwa uangalifu wakati wako wanafundisha na anawaiga. Dada mwenye kuitwa Talia, anasikilizaka kwa uangalifu wasemaji wenye uzoefu wakati wako natoa hotuba za watu wote. Kwa kufanya vile, amejifunza namna ya kufasiria habari fulani zenye watu wanazoea kuuliza mu mahubiri.

UKUWE MUFANO KU MIKUTANO

Kuimba kwa moyo wote ku mikutano kunamuleteaka Yehova sifa (Ona fungu ya 12-13)

12. Watu fulani wanaogopaka kufanya nini?

12 Siye wote tunaweza kufanya mikutano ya kutaniko ikuwe muzuri kwa kuimba pamoya, na kwa kutoa maelezo yenye kutayarishwa muzuri. (Zb. 22:22) Watu fulani wanaogopaka kuimba ao kutoa maelezo mbele ya watu. Na weye ni vile? Kama ni vile, utafurahi kujua mambo yenye ilisaidia wengine washinde ile woga.

13. Ni nini inaweza kukusaidia kuimba kwa moyo wote ku mikutano?

13 Imba kwa moyo wote. Sababu kubwa zaidi yenye inafanya tukuwe tunaimba nyimbo za Ufalme, ni kumusifu Yehova. Dada mwenye kuitwa Sara, hajionake kuwa mwimbaji muzuri sana, lakini anapendaka kumusifu Yehova kupitia nyimbo. Njo maana anatayarishaka nyimbo sawa vile tu anatayarishaka sehemu zingine za mikutano. Anafanyaka mazoezi ya kuimba nyimbo na kujikaza kuona namna maneno ya nyimbo inapatana na mambo yenye itazungumuziwa ku mikutano. Anasema hivi: “Ile inanisaidiaka kukaza akili juu ya maneno ya wimbo kuliko kufikiria uwezo wangu wa kuimba.”

14. Kama uko mutu wa haya, unaweza kufanya nini juu ukuwe unatoa maelezo ku mikutano?

14 Toa maelezo kwa ukawaida. Kusema kweli, watu fulani wanaonaka kama haiko mwepesi kufanya vile. Talia, mwenye tulishataya, anasema hivi: “Naogopaka sana kusema mbele ya watu wengine, hata kama wengine hawatambuake ile juu kwa kawaida sauti yangu inakuwaka ya kutulia. Kwa hiyo, inakuwaka nguvu sana kwangu kujibia.” Hata vile, Talia hajizuiake kutoa maelezo. Wakati iko natayarisha mikutano, anakumbukaka kama jibu ya kwanza inapaswa kuwa ya mufupi na ya moja kwa moja ku ulizo. Anasema hivi: “Kwa hiyo, naonaka kama haiko mubaya kama jibu yangu iko ya mufupi, ya mwepesi, na yenye inajibia moja kwa moja ulizo, juu njo aina ya jibu yenye kiongozi iko natafuta.”

15. Tunapaswa kukumbuka nini kuhusu maelezo yetu?

15 Hata Wakristo wenye hawakuwake na haya ao wenye hawakuwake kimya-kimya, wakati fulani wanaweza kujizuia kutoa maelezo. Juu ya nini? Dada mwenye kuitwa Juliet anasema: “Wakati fulani naogopaka kujibia juu naonaka kama jibu yenye nitatoa ni ya mwepesi sana ao haitakuwa muzuri sana.” Lakini, kumbuka kama Yehova anapenda tutoe majibu ya muzuri sana kulingana na uwezo wetu. * Anafurahiaka sana kuona azimio yetu ya kumusifu ku mikutano ya kutaniko hata kama wakati fulani tunaogopaka.

UKUWE MUFANO MU MAZUNGUMUZO YA KILA SIKU

16. Tunapaswa kuepuka maneno ya namna gani?

16 Epuka kila aina ya “matukano.” (Efe. 4:31) Sawa vile tuliona, Mukristo hapaswe hata kidogo kusema maneno machafu. Lakini kuko aina ingine ya matukano yenye haiko wazi kabisa yenye pia tunapaswa kuepuka. Kwa mufano, haiko muzuri kusema mubaya watu wa desturi fulani, wa kabila fulani, ao wa inchi fulani. Zaidi ya ile, tunapaswa kuepuka kuumiza wengine kupitia maneno yenye kuchoma. Ndugu moya anasema hivi: “Wakati fulani, nilikuwa natumia maneno yenye kuchoma, ya mizaha-mizaha, na nilikuwa nawaza kama ni ya kuchekesha tu na haiko ya mubaya, kumbe nilikuwa naumiza hisia za wengine. Kwa miaka mingi, bibi yangu alinisaidia sana. Wakati maneno yangu ilimukosea heshima na kumuumiza yeye na watu wengine, alikuwa ananiambia wakati tulikuwa siye wawili.”

17. Kulingana na Waefeso 4:29, tunaweza kufanya nini juu ya kujenga wengine?

17 Sema mu njia yenye kujenga wengine. Ukuwe mwepesi kupongeza wengine kuliko kuwachambua ao kunungunika. (Soma Waefeso 4:29.) Waisraeli walikuwa na sababu mingi za kuwa wenye shukrani, lakini mara mingi walikuwa wananungunika. Roho ya kunungunika inaweza kuambukia wengine. Kumbuka kama habari ya mubaya yenye wale wapelelezi kumi walitoaka njo ilifanyaka “Waisraeli wote . . . wanungunikie Musa.” (Hes. 13:31–14:4) Tofauti na ile, kupongeza wengine kunafanyaka wakuwe na furaha. Tunaweza kuwa hakika kama, pongezi yenye mutoto mwanamuke wa Yefta alipata kutoka kwa marafiki wake wanamuke ilimutia moyo sana aendelee kushikamana na mugao wake. (Amu. 11:40) Sara, mwenye tulishataya, anasema hivi: “Wakati tunapongeza wengine, tunafanya waone kama Yehova anawapenda na kama ni wa maana mu tengenezo yake.” Kwa hiyo, utafute nafasi za kupongeza wengine kutoka mu moyo.

18. Kulingana na Zaburi 15:1, 2, juu ya nini tunapaswa kusema kweli, na ile inatia ndani nini?

18 Sema kweli. Hatuwezi kumufurahisha Yehova kama tunasemaka uongo. Anachukia kila aina ya uongo. (Mez. 6:16, 17) Hata kama watu wengi leo wanaona kama haiko mubaya kusema uongo, siye tunafuata mawazo ya Yehova. (Soma Zaburi 15:1, 2.) Ni kweli tunaepuka kusema uongo kimakusudi, lakini tunaepuka pia kusema kweli nusu-nusu juu ya kufanya watu waelewe mambo mubaya.

Kuacha mazungumuzo ya mubaya na kuanza kuzungumuzia mambo ya muzuri kutafanya Yehova atukubali (Ona fungu ya 19)

19. Ni jambo gani ingine yenye tunapaswa kuepuka?

19 Epuka kupiga porojo. (Mez. 25:23; 2 Te. 3:11) Juliet, mwenye tulishataya, anafasiria mawazo yake kuhusu kupiga porojo. Anasema hivi: “Kusikia mutu iko napiga porojo, kunanivunjaka moyo na kunafanyaka nisimutumainie. Na nawazaka kama ule mutu anaweza hata kupiga porojo juu yangu kwa mutu mwingine.” Ikiwa unaona kama mazungumuzo inaanza kugeuka na kuwa porojo, muzungumuzie mambo ingine yenye kujenga bila kuchelewa.​—Kol. 4:6.

20. Unaazimia kutumia namna gani zawadi yako ya kusema?

20 Juu tunaishi mu dunia yenye watu wengi wanazoea kutumia maneno machafu, tunapaswa kujikaza sana ili maneno yetu imufurahishe Yehova. Tukumbuke kama Yehova njo alitupatia zawadi ya kusema, na anakuwaka muangalifu juu ya namna tunaitumia. Atabariki bidii yetu ya kutumia maneno yetu mu njia ya muzuri mu mahubiri, ku mikutano, na mu mazungumuzo yetu ya kila siku. Wakati watu wenye hawamuogope Mungu wataharibiwa, itakuwa mwepesi zaidi kwetu kumuheshimia Yehova Mungu kupitia maneno yetu. (Yud. 15) Kwa sasa, azimia kumufurahisha Yehova kupitia “maneno ya kinywa” chako.​—Zb. 19:14.

WIMBO 121 Tukomalishe Sifa ya Kujizuia

^ fu. 5 Yehova alitupatia zawadi ya muzuri sana​—zawadi ya kusema. Jambo ya kuhuzunisha ni kama watu wengi wanatumia mubaya ile zawadi. Ni nini inaweza kutusaidia tuendelee kusema maneno ya muzuri na yenye kujenga hata kama tunaishi mu hii dunia ya mubaya? Tunaweza kufanya nini ili maneno yetu imufurahishe Yehova wakati tuko mu mahubiri, ku mikutano ya kutaniko, na wakati tuko nazungumuza na watu wengine? Hii habari itajibia ile maulizo.

^ fu. 6 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 15 Ili upate habari zaidi kuhusu kutoa maelezo, ona habari “Umusifu Yehova Katika Kutaniko” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 1, 2019.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA Ndugu moya anafokea mwenye nyumba mwenye kukasirika; ndugu moya anajizuia kuimba wakati wa mukutano wa kutaniko; na dada moya iko mu mazungumuzo ya kupiga porojo.