Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Chakula ya Imbwa Zangu

Chakula ya Imbwa Zangu

NICK mwenye anaishi Oregon, mu Amerika anasema hivi: “Ku mwanzo wa mwaka wa 2014, nilianza kutembeza imbwa zangu wadogo wawili mu katikati ya muji kwenye nilikuwa naishi. Kila mara Mashahidi wanakuwaka katikati ya muji na wanakuwaka wenye kusimama pembeni ya prezantware zao. Walikuwa walishavalia muzuri na walikuwa naonyesha sura ya kicheko kila mutu mwenye alikuwa anapita.

“Wale Mashahidi hawakutendea tu watu muzuri, walitendea pia muzuri imbwa zangu. Siku moya, Elaine mwenye alikuwa anasimama pembeni ya prezantware alipatia imbwa zangu wawili chakula. Kisha pale, saa yenye tulikuwa karibu kufika ku ile prezantware imbwa zangu zilikuwa napenda kuenda kwenye Mashahidi walikuwa juu zipate ‘chakula.’

“Kisha miezi fulani, imbwa zilifurahia chakula yao na miye nilifurahia mambo yenye tulizungumuza pamoya nao. Lakini sikukuwa napenda kuzungumuza sana pamoya nao. Nilikuwa na zaidi ya miaka 70, na sikukuwa hakika na mambo yenye Mashahidi waliamini. Juu dini za mingi za Kikristo zilinivunja moyo, niliwaza ni muzuri zaidi nijifunze miye peke Biblia.

“Mu ile kipindi, niliona Mashahidi wengine katika sehemu ingine ya muji walikuwa wenye kusimama pembeni ya prezantware zao. Nao pia walikuwa wanatendea wengine mu njia ya kirafiki. Kila mara, walikuwa wanajibia maulizo yangu kupitia Biblia na ile ilifanya niwaaminie zaidi.

“Siku moya Elaine aliniuliza hivi: ‘Unaamini kama wanyama ni zawadi kutoka kwa Mungu?’ Nikamuambia, ‘Ndiyo, naamini kabisa vile!’ Kisha Elaine akanisomea Isaya 11:6-9. Tangu pale na kuendelea nilipenda kujifunza Biblia, lakini nilikuwa na mashaka ya kuitika jambo fulani ya kusoma ya Mashahidi.

“Mu masiku yenye ilifuata, nilifurahia mazungumuzo ya mufupi lakini ya maana sana yenye tulikuwa nayo pamoya na Elaine na bwana yake Brent. Waliniomba nisome Matayo mupaka Matendo juu nielewe kama, kuwa Mukristo wa kweli inatia ndani nini. Nilifanya vile. Muda kidogo kisha pale, nilikubali kujifunza Biblia pamoya na Brent na Elaine. Ilikuwa mu katikati ya mwaka wa 2016.

“Nilichunga kwa hamu funzo yangu ya Biblia ya kila juma na kuenda ku mikutano ku Jumba ya Ufalme. Nilijisikia kuwa mwenye kubarikiwa na mwenye furaha juu nilijifunza mambo yenye Biblia inasema kabisa. Zaidi ya mwaka moya hivi kisha pale, nilifikia kubatizwa na kuwa Shahidi. Kwa sasa niko na miaka 79, na niko mwenye shukrani sana kuona vile nimepata dini ya kweli. Yehova amenibariki kwa kunisaidia nikuwe mu familia ya watumishi wake wa mu dunia yote.”