Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 25

Yehova Anabariki Wale Wenye Wanasamehe

Yehova Anabariki Wale Wenye Wanasamehe

“Kama vile Yehova aliwasamehe ninyi kwa kupenda, ninyi pia munapaswa kufanya vilevile.”​—KOL. 3:13.

WIMBO 130 Tusameheane

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni ahadi gani yenye Yehova anatolea watenda-zambi wenye kutubu?

 YEHOVA ni Muumbaji wetu, Mupaji-Sheria wetu, Muamuzi wetu, lakini pia ni Baba yetu mwenye upendo. (Zb. 100:3; Isa. 33:22) Wakati tunamukosea Yehova na kutubu kikweli, iko tayari kutusamehe na pia iko na mamlaka ya kufanya vile. (Zb. 86:5) Kupitia nabii Isaya, Yehova alitoa hii ahadi yenye kutia moyo: “Hata kama zambi zenu ziko na rangi nyekundu yenye kungaa, zitafanywa kuwa nyeupe kama teluji.”​—Isa. 1:18.

2. Kama tunapenda kuwa na uhusiano muzuri na wengine, tunapaswa kufanya nini?

2 Juu siye wote hatukamilike, tunasemaka na kufanya mambo yenye inakwaza wengine. (Yak. 3:2) Lakini ile haimaanishe kama hatuwezi kuwa na uhusiano muzuri nao. Siri tu ni kujifunza kusamehe. (Mez. 17:9; 19:11; Mt. 18:21, 22) Wakati wengine wanatukosea mu mambo ya kidogo-kidogo, Yehova anapenda tuwasamehe. (Kol. 3:13) Yehova anatusameheaka “kwa njia kubwa,” njo maana na siye tunapaswa kufanya vile.​—Isa. 55:7.

3. Tutaona nini mu hii habari?

3 Mu hii habari, tutaona namna wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kuiga Yehova kwa kusamehe wengine. Ni zambi gani njo tunapaswa kujulisha wazee? Juu ya nini Yehova anapenda tusamehe wengine? Na mufano wa ndugu na dada wenye walishakateseka juu ya zambi ya wengine unaweza kutufundisha nini?

WAKATI MUKRISTO ANAFANYA ZAMBI NZITO

4. (a) Wakati mutumishi wa Yehova anafanya zambi nzito, anapaswa kufanya nini? (b) Na wazee wako na daraka gani?

4 Zambi nzito inapaswa kujulishwa kwa wazee. Tunapata mifano fulani ya zambi nzito mu 1 Wakorinto 6:9, 10. Zambi nzito ni kosa kubwa ya kuvunja sheria ya Mungu. Kama Mukristo anafanya zambi nzito, anapaswa kusali kwa Yehova, na kuenda kuona wazee wa kutaniko. (Zb. 32:5; Yak. 5:14) Juu ya nini aende kuona wazee? Ni Yehova tu njo iko na mamlaka ya kusamehe kabisa zambi, na ile inawezekana juu Yesu alishakatoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi. * Lakini Yehova alipatia wazee daraka ya kuamua kulingana na Maandiko ikiwa mutenda-zambi anastahili kubakia mu kutaniko ao hapana. (1 Ko. 5:12) Juu ya kuamua vile, wazee wanafikiriaka hii maulizo: Alifanya zambi kimakusudi? Alipanga kufanya zambi? Alizoea kufanya zambi kwa muda murefu? Na zaidi sana, kuko mambo yenye inaonyesha kama ametubu kikweli? Kuko mambo yenye inaonyesha kama Yehova amemusamehe?​—Mdo. 3:19.

5. Kazi yenye wazee wanafanyaka iko na faida gani?

5 Wakati wazee wanazungumuza na mutenda-zambi, kusudi yao ni kufikia uamuzi wenye tayari umechukuliwa mbinguni. (Mt. 18:18) Kufanya vile kunaletea kutaniko faida gani? Kunasaidia watenda-zambi wenye hawatubu na wenye wanaweza kutendea mubaya kondoo wa Yehova waondolewe mu kutaniko. (1 Ko. 5:6, 7, 11-13; Tit. 3:10, 11) Kunaweza pia kusaidia mutenda-zambi atubu na apate musamaha wa Yehova. (Lu. 5:32) Wazee wanasali kwa ajili ya mutenda-zambi mwenye kutubu na wanamuomba Yehova amusaidie akuwe tena na hali ya muzuri ya kiroho.​—Yak. 5:15.

6. Kama mutu anatengwa na kutaniko, Yehova anaweza kumusamehe?

6 Tuseme nini kama mutenda-zambi haonyeshe kama anatubu wakati wazee wako nazungumuza naye? Kama ni vile, atatengwa na kutaniko. Kama amevunja sheria ya serikali, wazee hawatamuzuia asipate matokeo ya mubaya ya matendo yake. Yehova anaruhusu serikali zihukumu na zipatie malipizi kila mutu mwenye anavunja sheria, ikuwe anatubu ao hapana. (Ro. 13:4) Lakini, kama mutu anafikia kutambua makosa yake na anatubu kikweli na kubadilisha mwenendo wake, Yehova atakuwa tayari kumusamehe. (Lu. 15:17-24) Yehova atamusamehe hata kama alifanya zambi nzito sana.​—2 Ny. 33:9, 12, 13; 1 Ti. 1:15.

7. Kusamehe mutu mwenye alitukosea maana yake nini?

7 Inatia moyo kujua kama haiko daraka yetu kuamua ikiwa mutenda-zambi anastahili kusamehewa na Yehova ao hapana! Lakini, kuko jambo fulani yenye siye tunapaswa kuamua. Jambo gani? Wakati fulani, mutu anaweza kutukosea ao hata kutukosea sana. Lakini kisha, anaweza kuhuzunikia makosa yake na kutuomba musamaha. Wakati ingine, mutu anaweza kushindwa kutuomba musamaha. Hata vile, tunaweza kuamua kumusamehe, ni kusema, kuacha kumukasirikia na kumuwekea kinyongo. Kusema kweli, inaomba wakati na kujikaza sana ili kufikia kumusamehe, zaidi sana kama matendo yake ilituumiza sana. Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 9, 1994, unasema hivi: “Kusamehe mutu mwenye alitukosea, haimaanishe kama hatuone uzito wa kosa yenye alifanya. Kwa Mukristo, kusamehe ni kuacha mambo yote mu mikono ya Yehova. Yeye njo Muamuzi wa ulimwengu wote, na atahakikisha kama tunatendewa kwa haki kwa wakati yenye kufaa.” Juu ya nini Yehova anatutia moyo kusamehe na kuacha mambo mu mikono yake?

JUU YA NINI YEHOVA ANAPENDA TUSAMEHE WENGINE?

8. Nini njo itatusaidia tukuwe tayari kusamehe wengine?

8 Kusamehe kunaonyesha kama tuko wenye shukrani. Mu mufano moya, Yesu alilinganisha Yehova na bwana mwenye alifuta deni kubwa yenye mutumwa wake hangeweza kulipa. Lakini, mutumwa mwenye alisamehewa alishindwa kuonyesha rehema mutumwa mwingine mwenye alikuwa na deni yake ya makuta kidogo. (Mt. 18:23-35) Yesu alipenda kutufundisha nini? Kama tuko wenye shukrani juu ya rehema yenye Yehova anatuonyesha, tutakuwa tayari kusamehe wengine. (Zb. 103:9) Munara wa Mulinzi ulifasiriaka ile wazo mu hii njia: “Hata tusamehe wanadamu wenzetu mara ngapi, hatuwezi kufikia kiasi ya musamaha na rehema yenye Mungu anatuonyeshaka kwa musingi wa bei ya ukombozi ya Kristo.”

9. Nani njo Yehova anaonyeshaka rehema? (Matayo 6:14, 15)

9 Wenye kusamehe watasamehewa. Yehova anaonyeshaka rehema wale wenye wanaonyeshaka rehema. (Mt. 5:7; Yak. 2:13) Yesu alionyesha vile waziwazi wakati alifundisha wanafunzi wake kusali. (Soma Matayo 6:14, 15.) Mambo yenye Yehova alimuambia mutumishi wake Yobu inaonyesha pia ile jambo. Ule mwanaume muaminifu aliumizwa sana na maneno makali ya Elifazi, Bildadi, na Zofari. Yehova alimuambia Yobu asali kwa ajili yao. Na kisha Yobu kufanya vile, Yehova alimubariki.​—Yob. 42:8-10.

10. Juu ya nini kuweka kinyongo ni kujiumiza siye peke? (Waefeso 4:31, 32)

10 Kuweka kinyongo ni kujiumiza siye peke. Yehova anapenda tupate kitulizo yenye mutu anapataka wakati anaacha kuwekea wengine kinyongo. (Soma Waefeso 4:31, 32.) Anatutia moyo ‘kucha hasira na kuacha kasirani kali.’ (Zb. 37:8) Kuko faida kama tunafuata ile shauri. Wakati tunawekea mutu kinyongo, tunajiumiza kimwili na kiakili. (Mez. 14:30) Kwa kweli, wakati tunawekea mutu kinyongo, ile haimuumize yeye. Ni sawa vile tu mutu mwenye anakunywa sumu. Ni yeye njo ile sumu italetea matokeo ya mubaya, hapana mutu mwingine. Kwa hiyo, wakati tunasamehe wengine, tunajiletea faida. (Mez. 11:17) Tunapata amani ya akili na ya moyo, na tunakuwa na nguvu ya kuendelea kumutumikia Yehova.

11. Biblia inasema nini juu ya kulipiza kisasi? (Waroma 12:19-21)

11 Kisasi ni ya Yehova. Yehova hatupatie mamlaka ya kulipiza kisasi wakati mutu fulani anatukosea. (Soma Waroma 12:19-21.) Juu hatukamilike, hatuna uwezo wa kuamua mambo bila kukosea, sawa vile Mungu. (Ebr. 4:13) Na wakati fulani, hisia zetu zinaweza kutudanganya na kutufanya tusiamue mambo kwa njia yenye kufaa. Roho ya Yehova ilimuongoza Yakobo aandike hivi: “Kasirani ya mwanadamu haitokeze haki ya Mungu.” (Yak. 1:20) Tunapaswa kuwa hakika kama Yehova atatenda kwa haki na atahakikisha kama haki inatimizwa.

Acha kuweka kasirani na kinyongo. Acha mambo mu mikono ya Yehova. Atatosha mambo yote ya mubaya yenye inatokana na zambi (Ona fungu ya 12)

12. Namna gani tunaweza kuonyesha kuwa tunatumainia haki ya Yehova?

12 Kusamehe kunaonyesha kama tunatumainia haki ya Yehova. Wakati tunaacha mambo mu mikono ya Yehova, tunaonyesha kama tuko hakika kuwa Yehova atatosha mambo yote ya mubaya yenye inatokana na zambi. Mu dunia mupya yenye anatuahidi, mambo yote yenye kuhuzunisha “hayatakumbukwa, wala hayataingia katika moyo” hata siku moya. (Isa. 65:17) Lakini kama mutu anatukosea sana, inawezekana kabisa kuacha kumukasirikia na kuacha kumuwekea kinyongo? Ona namna watu fulani wameweza kufanya vile.

KUSAMEHE KUNALETA BARAKA

13-14. Habari ya Tony na José inakufundisha nini kuhusu kusamehe?

13 Ndugu na dada wengi waliamua kusamehe hata kama waliumizwa sana na matendo ya wengine. Kufanya vile kumewaletea baraka gani?

14 Miaka mingi mbele akuwe Shahidi wa Yehova, Tony, * mwenye anaishi Ufilipino, alivumbula kama mwanaume mwenye kuitwa José aliuaka ndugu yake mukubwa. Ile wakati, Tony alikuwa mukali sana na mwenye jeuri, na alipenda kulipiza kisasi. José alikamatwa na kufungwa juu ya makosa yake. Kisha, wakati José alifunguliwa, Tony alilapa kama atamuwinda mupaka amuue. Aliuza bunduki juu afanye vile. Tony alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Anasema hivi: “Funzo yangu ya Biblia ilinisaidia kujua kama nilipaswa kubadilika, na kama nilipaswa pia kuacha kuweka kasirani.” Kisha, Tony alibatizwa na akafikia kuwa muzee wa kutaniko. Wazia namna alishangala wakati alisikia kama José amefikia kubatizwa na kuwa mutumishi wa Yehova! Wakati walionana, walikumbatiana kwa furaha, na Tony alimuambia José kama alishamusamehe. Tony anasema kama kumusamehe José kulimuletea furaha kubwa sana, yenye hawezi hata kueleza. Yehova alibariki utayari wa Tony wa kusamehe.

Mufano wa Peter na Sue unaonyesha kama tunaweza kuacha kuweka kasirani na kinyongo (Ona fungu ya 15-16)

15-16. Habari ya Peter na Sue inakufundisha nini kuhusu kusamehe?

15 Mu 1985, Peter na Sue walikuwa ku mukutano mu Jumba ya Ufalme, na kwa kushitukia bombe ikalipuka. Mwanaume moya alitega bombe ndani ya Jumba ya Ufalme! Sue aliumia sana na hakukuwa tena anaona wala kusikia. Hakukuwa pia anasikia harufu ya kitu. * Mara mingi Peter na Sue walikuwa najiuliza, ‘Ni mutu wa namna gani njo anaweza kufanya jambo ya mubaya vile?’ Kisha miaka mingi, ule mwanaume mwenye alitegaka bombe, mwenye hakukuwa Shahidi wa Yehova, alikamatwa na kufungwa maisha yote. Wakati Peter na Sue waliulizwa kama walishakamusamehe, walisema hivi: “Yehova anatufundisha kama kuweka kinyongo na kasirani kunaweza kutuumiza kimwili, kihisia, na kiakili. Wakati tu ile mambo ilitokea, tulimuomba Yehova atusaidie tusiweke kinyongo na kasirani juu tuendelee na maisha yetu.”

16 Ilikuwa mwepesi kwao kusamehe kila mara? Hapana. Wanaendelea kusema hivi: “Kila mara wakati maumivu ya Sue inalamukaka, kasirani nayo inalamukaka. Lakini tunajikaza tusiendelee kufikiri juu ya hali yenye ilitupataka, na ile maumivu inakimbia haraka. Kusema kweli, kama siku moya ule mwanaume mwenye alitegaka ile bombe anakuwa Shahidi wa Yehova, tutamukaribisha kwa furaha. Tumejifunza kama kanuni za Biblia zinawekaka mutu huru, zinatuweka huru mu njia yenye hatuwezi hata kuwazia! Pia inatia moyo kujua kama karibuni Yehova atatosha mambo yote ya mubaya.”

17. Habari ya Myra inakufundisha nini kuhusu kusamehe?

17 Wakati Myra alijifunza kweli, alikuwa alishaolewa na alikuwa na watoto wawili. Bwana yake hakukubali kweli. Kisha, bwana yake alifanya uzinifu na akaacha familia yake. Myra anasema hivi: “Wakati bwana yangu aliniacha pamoya na watoto wetu wawili, nilijisikia sawa vile wengi wanajisikiaka kisha kusalitiwa na mutu mwenye wanapenda. Nilihuzunika sana, sikuamini, nililia, nilisikitika, nilijilaumu, na nilikasirika. Hata kama ndoa iliisha, niliendelea kuumia juu bwana yangu alinisaliti.” Myra anaongezea hivi: “Niliendelea kujisikia mubaya kwa miezi mingi, na nilitambua kama uhusiano wangu na Yehova na pia na wengine uliharibika.” Myra anasema kama, kwa sasa hawekee bwana yake wa zamani kasirani na hamutakie mambo ya mubaya. Anatumainia kama siku moya bwana yake wa zamani atakuwa mutumishi wa Yehova. Myra anajikaza kusahau mambo ya zamani. Amesaidia watoto wake wawili wamutumikie Yehova. Leo, Myra iko na furaha ya kutumikia Yehova na watoto wake na familia zao.

YEHOVA NI MUAMUZI MUKAMILIFU

18. Juu Yehova ni Muamuzi Mukubwa Zaidi, tuko hakika na jambo gani?

18 Inatia moyo kujua kama haiko daraka yetu kuamua hukumu yenye watu fulani wanastahili kupewa! Yehova njo atafanya ile kazi, juu yeye njo Muamuzi Mukubwa Zaidi. (Ro. 14:10-12) Tuko hakika kabisa kama sikuzote atahukumu kulingana na kanuni zake kamilifu za mema na mabaya. (Mwa. 18:25; 1 Fa. 8:32) Hawezi hata kidogo kutenda bila haki!

19. Juu Yehova ni Muamuzi mukamilifu, atafanya nini?

19 Tunachunga kwa hamu sana wakati yenye Yehova atatosha mambo yote ya mubaya yenye inatokana na zambi na kutokamilika. Wakati atafanya vile, ataponyesha kabisa maumivu yote ya mwili na vidonda vya moyo. (Zb. 72:12-14; Ufu. 21:3, 4) Hatutakumbuka tena ile mambo yote. Wakati tunaendelea kuchunga ile wakati ya muzuri sana ifike, tuko wenye shukrani sana juu Yehova ametupatia uwezo wa kumuiga kwa kusamehe wengine.

WIMBO 18 Tuko na Shukrani juu ya Bei ya Ukombozi

^ Yehova iko tayari kusamehe watenda-zambi wenye wanatubu. Juu tuko Wakristo, tunapenda kuiga mufano wake kwa kusamehe wakati mutu fulani anatukosea. Mu hii habari, tutazungumuzia zambi ao makosa yenye tunaweza kusamehe kipekee na zambi zenye inaomba kujulisha wazee. Tutazungumuzia pia juu ya nini Yehova anapenda tusameheane na baraka zenye tutapata kama tunafanya vile.

^ Ona “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 4, 1996.

^ Majina fulani imebadilishwa.

^ Ona Amuka! ya tarehe 8 Mwezi wa 1, 1992, uku. 9-13 (katika Kifaransa). Ona pia ku JW Télédiffusion video yenye kichwa Peter et Sue Schulz : Un traumatisme peut être surmonté.