Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 27

“Umutumainie Yehova”

“Umutumainie Yehova”

“Umutumainie Yehova; ukuwe hodari na moyo wako ukuwe na nguvu.”​—ZB. 27:14.

WIMBO 128 Vumilia Mupaka Mwisho

KIFUPI YA HABARI *

1. (a) Yehova ametupatia wale wenye wanamupenda tumaini gani? (b) ‘Kumutumainia Yehova,’ maana yake nini? (Ona “Mafasirio ya Maneno Fulani.”)

 YEHOVA amepatia wale wenye wanamupenda tumaini ya muzuri. Karibuni atamaliza magonjwa, huzuni, na kifo. (Ufu. 21:3, 4) Atasaidia “wapole” wenye kumutumainia kugeuza dunia kuwa paradiso. (Zb. 37:9-11) Tena, atasaidia kila mumoja wetu akuwe na uhusiano wa karibu sana naye, wenye utapita uhusiano wenye tuko nao pamoya naye leo. Ni tumaini ya muzuri sana! Lakini, juu ya nini tunaamini kama ahadi za Mungu zitatimia? Juu Yehova hakosake kufanya mambo yenye anaahidi. Njo maana tunapaswa ‘kumutumainia Yehova.’ * (Zb. 27:14) Tunafanya vile kwa kungoya kwa uvumilivu na kwa furaha atimize ahadi zake.​—Isa. 55:10, 11.

2. Yehova alishafanya nini?

2 Yehova alishaonyesha kama anatimizaka ahadi zake. Kwa mufano, mu kitabu ya Ufunuo, Yehova aliahidi kama, mu siku zetu, atakusanya watu wa kila taifa, kabila, na luga, juu wamuabudu kwa umoja. Leo, wale watu wanafanyiza kikundi fulani ya pekee yenye Biblia inaita “kundi kubwa la watu.” (Ufu. 7:9, 10) Hata kama ile kikundi inafanyizwa na wanaume, wanamuke, na watoto wa rangi zote za ngozi, luga, na desturi mbalimbali, wote wanafanyiza familia moya yenye amani na umoja. (Zb. 133:1; Yoh. 10:16) Wale watu wa kundi kubwa wanahubiri pia kwa bidii. Kila mara wako tayari kuambia mutu yeyote mwenye anawasikiliza tumaini ya muzuri yenye wako nayo. (Mt. 28:19, 20; Ufu. 14:6, 7; 22:17) Kama uko kati ya wale wenye kufanyiza kundi kubwa, bila shaka unafurahia sana tumaini ya muzuri yenye uko nayo.

3. Nia ya Shetani ni nini?

3 Nia ya Shetani ni kutunyanganya tumaini yetu. Anapenda kutufanya tuamini kama Yehova hatuhangaikie na kama hatatimizaka ahadi zake. Kama Shetani anaweza kutunyanganya tumaini yetu, tutapoteza uhodari wetu, na tunaweza hata kuacha kumutumikia Yehova. Vile tutaona mu hii habari, Shetani alijaribu kumunyanganya Yobu tumaini yake na kumufanya aache kumutumikia Yehova.

4. Tutazungumuzia mambo gani mu hii habari? (Yobu 1:9-12)

4 Mu hii habari, tutazungumuzia mambo yenye Shetani alitumia juu ya kujaribu kumukaza Yobu aache kuwa mushikamanifu kwa Yehova. (Soma Yobu 1:9-12.) Tutazungumuzia pia mambo yenye mufano wa Yobu unatufundisha na juu ya nini hatupaswe kusahau kama Yehova anatupenda na kama atatimiza ahadi zake.

SHETANI ANAJARIBU KUMUFANYA YOBU APOTEZE TUMAINI

5-6. Ni mambo gani njo ilimufikia Yobu mu siku moya tu?

5 Yobu alikuwa na maisha ya muzuri. Alikuwa na urafiki muzuri na Yehova. Alikuwa na familia kubwa yenye furaha, na alikuwa tajiri sana. (Yob. 1:1-5) Lakini mu siku moya tu, Yobu alipoteza karibu kila kitu. Kwanza, alipoteza wanyama wake wote. (Yob. 1:13-17) Kisha, watoto wake wote walikufa. Waza kidogo: Wazazi wanahuzunikaka sana wakati mutoto wao mumoja tu anakufa. Wazia namna Yobu na bibi yake walishituka, walihuzunika, na kuishiwa wakati walisikia kama watoto wao kumi wote wamekufa. Inaeleweka kuona kama Yobu alipasua nguo zake, akalia sana, na kujitupa chini!​—Yob 1:18-20.

6 Kisha pale, Shetani alimupiga Yobu kwa ugonjwa wenye kuleta maumivu sana na haya. (Yob. 2:6-8; 7:5) Mbele ya pale, Yobu alikuwa anaheshimiwa sana fasi kwenye alikuwa naishi. Watu walikuwa nakuya muomba mashauri. (Yob. 31:18) Sasa walianza kumuepuka. Ndugu zake, marafiki wake wa karibu, na hata watumishi wa nyumba yake, wote walimukatala!​—Yob. 19:13, 14, 16.

Ndugu na dada wengi wanaweza kuelewa namna Yobu alijisikia wakati alipata magumu (Ona fungu ya 7) *

7. (a) Yobu aliwaza kama mateso yake ilitoka wapi, lakini aliendelea kufanya nini? (b) Mukristo anaweza kupata magumu gani yenye inafanana na ile yenye tunaona ku picha ku ukurasa wa 22?

7 Shetani alipenda Yobu aamini kama alikuwa anateseka juu Yehova hamukubali tena. Kwa mufano, Shetani alitumia upepo mukali juu ya kuangusha nyumba kwenye watoto wote kumi wa Yobu walikuwa wanafurahia chakula pamoya. (Yob. 1:18, 19) Alifanya pia moto utoke mbinguni na kuharibu mifugo ya Yobu na watumishi wenye walikuwa naichunga. (Yob. 1:16) Juu upepo na moto vilitoka mbinguni, Yobu aliwaza kama vilitoka kwa Yehova. Na ile ilifanya Yobu awaze kama alikuwa amemuhuzunisha Yehova kwa kiasi fulani. Hata vile, Yobu alikatala kumulaani Baba yake wa mbinguni. Yobu alijua kama Yehova alikuwa amemufanyia mambo mingi ya muzuri mu miaka mingi yenye ilikuwa imepita. Kwa hiyo, aliwaza kama, sawa vile alikubali mambo ya muzuri, alipaswa pia kuwa tayari kukubali mambo ya mubaya. Njo maana alisema hivi: “Jina la Yehova liendelee kusifiwa.” (Yob. 1:20, 21; 2:10) Hata kama Yobu alipoteza mali yake, watoto wake, na aligonjwa sana, aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Yehova. Lakini, Shetani alikuwa hayaachia pale.

8. Shetani alimutendea tena Yobu nini?

8 Tena, Shetani alichochea marafiki wa uongo wa Yobu wamufanye ajione kuwa wa bure. Walisema kama Yobu iko nateseka juu alifanya mambo mingi ya mubaya. (Yob. 22:5-9) Walijaribu pia kumufanya awaze kama, hata ikiwa alifanya mambo mingi ya muzuri, Mungu haione hata kidogo. (Yob. 4:18; 22:2, 3; 25:4) Walijaribu kumufanya Yobu awaze kama Mungu hamupendi, hamuhangaikie, na kama hakuna faida ya kumutumikia Mungu. Maneno yao ingemufanya Yobu awaze kama hali yake haingebadilikaka.

9. Nini njo ilisaidia Yobu aendelee kuwa na nguvu na uhodari?

9 Wazia hali yenye Yobu iko ndani: Anaikala mu majifu, na iko na maumivu mingi sana. (Yob. 2:8) Marafiki wake wanaendelea kumuambia kama haiko mutu muzuri na kama mambo yote yenye alishakafanya ni ya bure. Magumu yake inamulemea kabisa sawa vile mutu mwenye kubeba majiwe makubwa-makubwa, na huzuni ya kupoteza watoto wake inamumaliza nguvu. Ku mwanzo, Yobu anabakia kimya. (Yob. 2:13–3:1) Marafiki wa Yobu wanawaza kama atamuacha Yehova, lakini wanajidanganya. Wakati fulani, inawezekana Yobu anainua kichwa yake na kuangalia wale marafiki wake wa uongo, macho kwa macho, na kusema: “Mupaka wakati nitakufa, sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!” (Yob. 27:5) Nini njo ilisaidia Yobu aendelee kuwa na nguvu na uhodari ijapokuwa magumu yote yenye ilimupataka? Hata wakati alikuwa amevunjika moyo sana, hakuacha hata kidogo kutumainia kama kuko siku Mungu wake mwenye upendo angemaliza magumu yake. Alijua kuwa, hata kama angekufa, Yehova angemufufua.​—Yob. 14:13-15.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUMUIGA YOBU?

10. Habari ya Yobu inatufundisha nini?

10 Habari ya Yobu inatufundisha kama Shetani hawezi kutukaza tumuache Yehova na kama Yehova anaonaka hali yote yenye inatupata. Mambo yenye ilimupata Yobu inaweza pia kutusaidia kuelewa muzuri zaidi juu ya nini aliteseka. Tuone mambo fulani yenye habari ya Yobu inatufundisha.

11. Biblia inatuhakikishia nini ikiwa tunaendelea kumutumainia Yehova? (Yakobo 4:7)

11 Yobu alionyesha kama, ikiwa tunaendelea kumutumainia Yehova, tutaweza kuvumilia magumu yoyote na tutaweza kumupinga Shetani. Matokeo itakuwa nini? Biblia inatuhakikishia kama Shetani atatukimbia.​—Soma Yakobo 4:7.

12. Kuamini ufufuo kulimusaidia Yobu namna gani?

12 Tunapaswa kuamini kabisa kama kutakuwa ufufuo. Sawa vile tuliona mu habari yenye kutangulia, mara mingi Shetani anatumiaka woga wa kifo juu ya kutufanya tukane imani yetu. Shetani alisema kama Yobu angefanya jambo yoyote, hata kama ingeomba aache ushikamanifu wake, juu aokoe uzima wake. Shetani alisema uongo. Hata wakati Yobu aliona kama maisha yake inakaribia mwisho, hakumuacha Yehova. Alikuwa hakika kama Yehova ni mwema na alitumainia kama kuko siku yenye Yehova atatengeneza mambo, na ile njo ilimusaidia aendelee kuvumilia. Yobu alikuwa na imani kama ikiwa Yehova hatengeneze mambo wakati alikuwa muzima, angemufufua mu siku zenye ziko nakuya. Yobu aliamini kabisa ufufuo. Kama na siye tunaamini kabisa ufufuo, hatutakana imani yetu hata wakati wanatuogopesha kama watatuua.

13. Juu ya nini tunapaswa kujua muzuri njia zenye Shetani alitumia ili kumujaribu Yobu?

13 Tunapaswa kujua muzuri njia zenye Shetani alitumia ili kumujaribu Yobu juu ni zile njia njo anatumiaka leo ili kutujaribu. Fikiria hii mashitaka ya Shetani: “Mutu [hapana tu Yobu] atatoa kila kitu chenye iko nacho ili aokoe uzima wake.” (Yob. 2:4, 5) Kwa kusema vile, Shetani alionyesha kama hatumupendi kabisa Yehova, na kama tutamuacha Mungu ikiwa kufanya vile kutatusaidia kuokoa uzima wetu. Tena, Shetani alionyesha kama Mungu hatupendi na haonake mambo yenye tunajikazaka kufanya juu ya kumufurahisha. Hatuamini uongo wa Shetani juu tunajua nia yake ni nini.

14. Majaribu inatusaidiaka kujua nini? Leta mufano.

14 Majaribu inatusaidiaka kujijua muzuri. Majaribu yenye Yobu alipata ilimusaidia kujua na kurekebisha uzaifu fulani wenye alikuwa nao. Kwa mufano, alijifunza kama alikuwa na lazima ya kuwa muvumilivu zaidi. (Yob. 42:3) Na siye tunaweza kujijua muzuri wakati tuko mu majaribu. Tufikirie mufano wa ndugu mwenye kuitwa Nikolay. * Alifungwa hata kama alikuwa na matatizo makubwa ya afya. Anasema hivi: “Kufungwa mu gereza ni sawa vile kupitishwa mu radio, juu kunatusaidia kuvumbula mambo yenye tunapaswa kufanyia mabadiliko.” Wakati tunajua uzaifu wetu, tunaweza sasa kuurekebisha.

15. Nani njo tunapaswa kusikiliza, na juu ya nini?

15 Tunapaswa kumusikiliza Yehova, hapana maadui wetu. Yobu alisikiliza kwa uangalifu wakati Yehova alikuwa nazungumuza naye. Wakati Mungu alikuwa nazungumuza na Yobu, ni sawa vile alimuambia hivi: ‘Unaona nguvu yenye nilitumia juu ya kuumba vitu? Ninajua kila kitu yenye ilikufikia. Unawaza kama siwezi kukusaidia?’ Yobu alionyesha unyenyekevu na shukrani juu ya wema wa Yehova. Alisema hivi: “Masikio yangu yalisikia habari juu yako, lakini sasa ninakuona na macho yangu.” (Yob. 42:5) Wakati Yobu alisema ile maneno, inawezekana alikuwa angali mu majifu, mwili wake ulikuwa unayala vidonda, na watoto wake walikuwa mu kaburi. Hata vile, Yehova alimuhakikishia Yobu kama anamupenda na anamukubali.​—Yob. 42:7, 8.

16. Kulingana na Isaya 49:15, 16, tunapaswa kukumbuka nini wakati tuko mu magumu?

16 Leo pia, watu wanaweza kututukana na kutuzarau. Wanaweza kujaribu kuharibisha sifa yetu ao ya tengenezo yetu na ‘kutusingizia kila namna ya uovu.’ (Mt. 5:11) Habari ya Yobu inatufundisha kwamba Yehova anaamini kama tutaendelea kuwa waaminifu kwake hata wakati tuko mu magumu. Yehova anatupenda na hataacha hata kidogo wale wenye wanamutumainia. (Soma Isaya 49:15, 16.) Usifuatane na maneno ya uongo ya maadui wa Mungu! James, ndugu wa Turquie mwenye familia yake ilipata magumu ya nguvu, anasema hivi: “Tulielewa kama kusikiliza mambo ya ungo yenye watu wanasema juu ya Mashahidi wa Yehova kungetuvunja moyo. Kwa hiyo, tulikaza akili yetu juu ya tumaini ya Ufalme na tuliendelea kumutumikia Yehova kwa bidii. Ile ilitusaidia tuendelee kuwa na furaha.” Kama tunamusikiliza Yehova sawa vile Yobu, mambo ya uongo yenye maadui wetu wanasema haitaharibu tumaini yetu.

TUMAINI YAKO ITAKUSAIDIA

Yehova alimubariki Yobu juu ya ushikamanifu wake. Yeye na bibi yake waliishi miaka mingi na walikuwa na furaha (Ona fungu ya 17) *

17. Mufano wa wanaume na wanamuke waaminifu wenye kuzungumuziwa mu Waebrania sura ya 11 unakufundisha nini?

17 Yobu iko kati ya watumishi wa Yehova wenye waliendelea kuwa hodari na wenye nguvu wakati walipambana na magumu ya nguvu sana. Mu barua yenye mutume Paulo aliandikia Waebrania, alizungumuzia wengine wengi, na aliwaita kuwa “wingu kubwa . . . la mashahidi.” (Ebr. 12:1) Wote walipata magumu ya nguvu, lakini waliendelea kuwa waaminifu kwa Yehova mu maisha yao yote. (Ebr. 11:36-40) Uvumilivu na kazi yenye walifanya ilikuwa ya bure? Hapana! Hata kama hawakujionea hata kidogo mu maisha yao namna ahadi za Mungu zinatimia, waliendelea kumutumainia Yehova. Na juu walikuwa hakika kama Yehova anawakubali, walikuwa hakika kama kuko siku yenye wataona namna ahadi za Mungu zitatimia. (Ebr. 11:4, 5) Kufikiria mufano wao kunaweza kutusaidia tuazimie kuendelea kumutumainia Yehova.

18. Unaazimia kufanya nini? (Waebrania 11:6)

18 Leo, tunaishi mu dunia yenye inaendelea kuharibika sana. (2 Ti. 3:13) Shetani hayamaliza kujaribu watu wa Mungu. Hata kama hatujue ni magumu gani njo itatufikia kule mbele, tuazimie basi kumutumikia Yehova kwa bidii, na tukuwe hakika kama “tumeweka tumaini letu katika Mungu mwenye kuishi.” (1 Ti. 4:10) Na tusisahau kama, baraka yenye Mungu alipatia Yobu inaonyesha “kwamba Yehova ni mwenye upendo mwingi sana na mwenye rehema.” (Yak. 5:11) Tuendelee pia kuwa waaminifu kwa Yehova, na tukuwe hakika kama atabariki “wale wenye wanamutafuta kwa bidii.”​—Soma Waebrania 11:6.

WIMBO 150 Umutafute Mungu ili Akukomboe

^ Wakati tunafikiria mutu mwenye alivumiliaka magumu ya nguvu sana, mara mingi tunamukumbukaka Yobu. Mambo yenye ilimufikia inaweza kutufundisha nini? Inatufundisha kama Shetani hawezi kutukaza tumuache Yehova. Inatufundisha pia kama sikuzote Yehova anajua mambo yote yenye iko natufikia. Na sawa vile Yehova alimaliza magumu ya Yobu, siku moya atamaliza pia magumu yetu. Ikiwa tunaonyesha kupitia matendo yetu kama tunaamini vile, ile inaonyesha kama ‘tunamutumainia [kabisa] Yehova.’

^ MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Maana ya kwanza ya neno ya Kiebrania yenye kutafsiriwa ‘kutumainia’ ni “kungoya” ao kuchunga jambo fulani kwa hamu. Inaweza pia kumaanisha kutumainia ao kutegemea mutu fulani.​—Zb. 25:2, 3; 62:5.

^ Majina fulani imebadilishwa.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Yobu na bibi yake wanapoteza watoto wao.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Yobu alivumilia majaribu yake mupaka mwisho. Yeye na bibi yake wanafikiria namna Yehova alibariki familia yao.