Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Acha “Sheria ya Fazili” Ikuongoze

Acha “Sheria ya Fazili” Ikuongoze

LISA * alisema hivi: “Fazili yenye ndugu na dada walinionyesha njo ilinigusa sana.” Alikuwa anazungumuzia jambo ya kwanza yenye ilimufanya avutiwe na kweli. Ilikuwa pia vile kuhusu Anne. Alisema hivi: “Ku mwanzo, nilivutiwa na kweli juu Mashahidi walinitendea kwa fazili, hapana tu juu ya mambo yenye walifundisha.” Kwa sasa wale dada wawili wanapenda kusoma Biblia na kufikiri sana juu ya mambo yenye wanasoma, lakini matendo ya fazili yenye walionyeshwa iliwagusa sana.

Namna gani tunaweza kuonyesha fazili yenye itagusa moyo wa wale wenye kutuzunguka? Tuzungumuzie njia mbili: Kupitia maneno yetu na matendo yetu. Kisha tutazungumuzia nani njo tunapaswa kuonyesha fazili.

ACHA “SHERIA YA FAZILI” IONGOZE MANENO YAKO

Mwanamuke mwenye uwezo, mwenye kuzungumuziwa mu Mezali sura ya 31, iko na “sheria ya fazili” kwenye ulimi wake. (Mez. 31:26) Anaacha ile “sheria” iongoze mambo yenye anasema na namna anaisema. Baba wanapaswa pia kuwa na ile “sheria” kwenye ulimi wao. Wazazi wengi wanajua muzuri kama maneno makali inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya watoto wao. Kama wazazi wanazungumuza kwa ukali, inawezekana watoto wao wasisikilize mambo yenye wanasema. Kama wazazi wanazungumuza kwa fazili ao kwa upole, inaweza kuwa mwepesi kwa watoto wao kuwasikiliza na kuwatii.

Ikuwe uko muzazi ao hapana, namna gani unaweza kuacha fazili iongoze maneno yako? Tunapata jambo yenye inaweza kusaidia mu sehemu ya kwanza ya Mezali 31:26: “Anafungua kinywa chake kwa hekima.” Maana yake, tunapaswa kuchagua kwa hekima maneno yetu na ni mu sauti gani njo tutaisema. Inakuwaka muzuri kujiuliza hivi: ‘Mambo yenye ninataka kusema, itawasha moto, ao itafanya mambo itulie?’ (Mez. 15:1) Kwa kweli, ni jambo ya hekima kuwaza mbele ya kusema.

Mezali ingine inasema hivi: “Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga.” (Mez. 12:18) Kujiuliza ikiwa maneno na sauti yenye tutatumia itafanya wengine wajisikie namna gani, kutatusaidia tujue tutasema nini. Kuacha “sheria ya fazili” ituongoze kutatusaidia tuepuke maneno yenye kuumiza na sauti ya ukali. (Efe. 4:31, 32) Kuliko kuwa na mawazo ya mubaya na kusema maneno ya mubaya, tutatumia maneno ya muzuri, na sauti ya upole. Yehova alituachia mufano muzuri wakati alitia nguvu mutumishi wake Eliya, mwenye alikuwa ameogopa sana. Malaika mwenye alimuwakilisha Yehova alizungumuza na “sauti tulivu, ya chini.” (1 Fa. 19:12) Lakini, zaidi ya kuzungumuza kwa fazili, kuko jambo ingine yenye tunapaswa kufanya. Tunapaswa pia kutenda kwa fazili. Namna gani?

MATENDO YA FAZILI INAGUSAKA WENGINE

Tunamuiga Yehova kwa kuzungumuza kwa fazili na kutenda kwa fazili. (Efe. 4:32; 5:1, 2) Lisa, mwenye tulishazungumuzia, alifasiria fazili yenye Mashahidi walimuonyesha. Alisema hivi: “Wakati familia yetu ililazimika kuhama haraka sana, bwana wawili na bibi zao, wenye walikuwa Mashahidi, walitumia wakati yao yenye hawakukuwa nafanya kazi juu ya kutusaidia kufunga mizigo. Ile wakati, nilikuwa siyaanza hata kujifunza Biblia!” Ile matendo ya fazili ilinichochea nipende kujua mambo mingi kuhusu Mashahidi wa Yehova.

Anne, mwenye tulizungumuzia ku mwanzo wa hii habari, alifurahia pia matendo ya fazili yenye Mashahidi walimutendea. Alisema hivi: “Kuona namna watu walikuwa nanitendea kulifanya nikuwe na mashaka sana. Ilikuwa nguvu sana kwangu kutumainia watu.” Aliongezea hivi: “Wakati nilionana na Mashahidi, nao pia sikuwatumainia. Nilijiuliza, ‘Juu ya nini wananihangaikia?’ Lakini fazili ya kweli ya mwalimu wangu wa Biblia ilinifanya nimutumainie.” Matokeo ilikuwa nini? Anne alisema hivi: “Nilianza kufikiri sana juu ya mambo yenye nilikuwa najifunza.”

Tunaona kama Lisa na Anne waliguswa sana na matendo ya fazili yenye ndugu na dada mu kutaniko waliwatendea, na ile iliwasaidia wapende kujifunza kweli. Matendo ya fazili yenye ndugu na dada waliwatendea iliwasaidia waanze kumutumainia Yehova na watu wake.

JIFUNZE KUTENDEA WENGINE KWA FAZILI

Wengine wanazoea kutumia maneno ya fazili na kuonyesha sura ya kicheko juu ile njo ilikuwa desturi ya fasi kwenye walikomalia. Ni muzuri vile desturi ya kwao ao utu wao unawachochea kuwa wenye fazili. Lakini, kama ni ile tu njo inatufanya tukuwe wenye fazili, ile haionyeshe kama tuko naiga fazili ya Mungu.​—Linganisha na Matendo 28:2.

Fazili ya kweli ni sehemu ya tunda ya roho ya Mungu. (Gal. 5:22, 23) Ni kusema, tuko na lazima ya roho takatifu ya Mungu juu tuweze kuonyesha fazili. Wakati tunaonyesha fazili, tunamuiga Yehova na Yesu. Tena, sawa vile Yesu, tunahangaikia wengine. Kumupenda Yehova na jirani njo kunatuchochea kuonyesha fazili. Wakati tunafanya vile, fazili yenye tunaonyesha wengine inafikia kuwa sifa yenye nguvu yenye inatoka ku moyo na yenye Mungu anakubali.

NANI NJO TUNAPASWA KUONYESHA FAZILI?

Inaweza kuwa mwepesi kuonyesha fazili wale wenye wanatutendeaka kwa fazili ao wale wenye tunajua. (2 Sa. 2:6) Tunaweza kufanya vile kwa kuwashukuru. (Kol. 3:15) Lakini, tuseme nini kama tunaona kuwa mutu fulani hastahili kuonyeshwa fazili?

Fikiria hii jambo: Yehova njo mufano muzuri zaidi wa kuonyesha fazili zenye hazistahiliwe, na Neno yake inatufundisha namna ya kuonyesha ile sifa. Maneno “fazili zenye hazistahiliwe” inatumiwa mara mingi mu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Namna gani Mungu anatuonyesha fazili?

Fikiria mamilioni na mamilioni ya watu wenye Yehova anaonyesha fazili zake kwa kuwapatia mambo yenye wako nayo lazima ili kuishi. (Mt. 5:45) Kwa kweli, hata mbele wanadamu wamujue Yehova, tayari alikuwa nawaonyesha fazili. (Efe. 2:4, 5, 8) Kwa mufano, alitoa Mwana wake, muzaliwa-pekee, kwa ajili ya watu wote. Mutume Paulo aliandika kama Yehova alitoa bei ya ukombozi “kulingana na utajiri wa fazili zake zenye hazistahiliwe.” (Efe. 1:7) Lakini, hata kama tunafanyaka zambi na kumuhuzunisha Yehova, anaendelea kutuongoza na kutufundisha. Muongozo na maneno yake iko sawa vile “mvua ya kidogo-kidogo.” (Kum. 32:2) Hatuna kabisa jambo yenye tunaweza kumulipa juu ya fazili yote yenye anatuonyeshaka. Na kusema kweli, hatungekuwa na tumaini kama Yehova hangetuonyesha fazili zenye hazistahiliwe.​—Linganisha na 1 Petro 1:13.

Kwa kweli, fazili ya Yehova inapendeza na inatia moyo. Kwa hiyo, kuliko kuonyesha fazili watu fulani tu, tunapaswa kujikaza kumuiga Yehova kwa kuonyesha watu wote fazili kila siku. (1 Te. 5:15) Wakati tunazoea kuonyesha wengine fazili, tunakuwa sawa vile moto wenye kuleta kifukutu wakati ya baridi. Tunakuwa faraja kwa watu wa familia yetu, ndugu na dada zetu, wafanyakazi wenzetu, wanafunzi wenzetu, na majirani wetu.

Fikiria watu wa mu familia ao kutaniko yako wenye watapata faida kama unazungumuza nao kwa fazili na kuwatendea kwa fazili. Pengine mu kutaniko yako muko ndugu ao dada mwenye iko na lazima mutu amusaidie kutunza nyumba ao bustani yake ao kufanya jambo ingine sawa vile kuenda kuuza vitu. Zaidi ya ile, wakati unakutana na mutu mu mahubiri mwenye iko na lazima ya musaada, ujikaze kufanya jambo fulani juu ya kumusaidia.

Tuendelee basi kumuiga Yehova kwa kuacha “sheria ya fazili” iongoze maneno na matendo yetu.

^ Majina imebadilishwa.