Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Yesu alimaanisha nini wakati alisema: “Musiwaze nilikuja kuleta amani”?

Yesu alifundisha watu kuishi kwa amani na wengine. Lakini, wakati fulani aliambia mitume wake hivi: “Musiwaze nilikuja kuleta amani katika dunia; sikukuja kuleta amani, lakini upanga. Kwa maana, nilikuja kuleta mugawanyiko kati ya mwana na baba yake, kati ya binti na mama yake, na kati ya binti-mukwe na mama-mukwe wake.” (Mt. 10:34, 35) Yesu alimaanisha nini?

Yesu hakupenda kuleta migawanyiko kati ya watu wa familia. Lakini, alijua kama mambo yenye alikuwa nafundisha ingeleta migawanyiko mu familia fulani. Kwa hiyo, wale wote wenye wanapenda kuwa wanafunzi wa Yesu na kubatizwa wanapaswa kujua kama watu wa familia yao hawatafurahia uamuzi wao. Wakati fulani, bibi ao bwana yao ao mutu mwingine wa familia yao anaweza kuwapinga na ile inaweza kufanya ikuwe nguvu kwao kufuata kwa uaminifu mafundisho ya Yesu.

Biblia inatia moyo Wakristo ‘wakuwe wenye kufanya amani na watu wote.’ (Ro. 12:18) Lakini, mafundisho ya Yesu inaweza kuwa sawa vile “upanga” mu familia fulani. Inakuwaka vile wakati mutu fulani mu familia anakubali mafundisho ya Yesu lakini wengine wanaipinga ao wanaikatala. Mu hali ya vile, wale watu wa familia wanajifanya “maadui” wa ule mwenye iko najifunza kweli.​—Mt. 10:36.

Wakati fulani, wanafunzi wa Yesu wenye wanaishi mu familia yenye kila mutu iko na dini yake wanajikuta mu hali zenye zinafanya ikuwe nguvu kwao kumufurahisha Yehova na Yesu. Kwa mufano, watu wa familia wenye hawako Mashahidi wanaweza kuwakaza wafanye sikukuu fulani ya kidini. Wakati wanajikuta mu ile jaribu, nani njo wanapaswa kufurahisha? Yesu alisema hivi: “Kila mutu mwenye anamupenda baba ao mama kuliko mimi hanistahili; na kila mutu mwenye anamupenda mwana ao binti kuliko mimi hanistahili.” (Mt. 10:37) Kusema kweli, Yesu hakumaanisha kama juu mutu akuwe mwanafunzi wake, hakupaswa kupenda sana wazazi wake. Lakini, alikuwa nafundisha wanafunzi wake namna ya kuamua mambo ya maana zaidi mu maisha yao. Kama watu wa familia wenye hawako Mashahidi wanatupinga juu tunamuabudu Yehova, tunapaswa kuendelea kuwapenda. Lakini, tusisahau kama Yehova njo tunapaswa kupenda kwanza.

Bila shaka, kupingwa na familia ni jaribu ya nguvu sana. Lakini, wanafunzi wa Yesu wanapaswa kukumbuka hii maneno yake: “Kila mutu mwenye hakubali muti wake wa mateso na kunifuata hanistahili.” (Mt. 10:38) Mu maneno ingine, Wakristo wanapaswa kuona upinzani wa familia kuwa mateso yenye wanafunzi wa Yesu wanapaswa kuwa tayari kukubali. Lakini, wanatumaini kama mwenendo wao muzuri utachochea watu wa familia yao wabadilishe mawazo na wapende kujifunza Biblia.​—1 Pe. 3:1, 2.