Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JI LIFUNZU 37

Guwesa kwa Atumaini aka Ndugu na Dada Bako

Guwesa kwa Atumaini aka Ndugu na Dada Bako

“Upalani . . . guamina mambu gowa, gutumaini mambu gowa.”​—1 KOR. 13:4, 7.

NHAMBU 124 Washikamanifu Sikuzote

MUHTASARI a

1. Kwa ndaba jaki ngase tusanga kubona hali jukusindwa kuaminiana pani pundema?

 WATU katika ulimwengu wa Shetani hawajui wamtumaini nani. Kila mara wanavunjwa moyo na wafanyabiashara, wanasiasa, na viongozi wa kidini. Huenda pia ikawa vigumu kwao kuwatumaini marafiki, majirani, na hata watu wa familia zao. Hilo halitushangazi. Biblia ilitabiri hivi: “Katika siku za mwisho . . . , watu watakuwa . . . wasio washikamanifu, . . . wachongezi, . . . wasaliti.” Kwa maneno mengine, watu wangeonyesha tabia za mungu wa mfumo huu wa mambo, ambaye hawezi kutumainika.—2 Tim. 3:1-4; 2 Kor. 4:4.

2. (a) Nya jotuwesa kuntumaini kabisa ku uhakika? (b) Pangi tuwesa kulilaluki liswali bole?

2 Hata hivyo, tukiwa Wakristo, tunajua kwamba tunaweza kumtumaini kabisa Yehova. (Yer. 17:7, 8) Tunasadiki kwamba anatupenda na kwamba ‘hatawaacha kamwe’ rafiki zake. (Zab. 9:10) Pia, tunaweza kumtumaini Kristo Yesu kwa sababu alitoa uhai wake kwa ajili yetu. (1 Pet. 3:18) Na tumejifunza kutokana na mambo ambayo tumejionea kibinafsi kwamba Biblia inatoa mwongozo unaotegemeka. (2 Tim. 3:16, 17) Tuna uhakika kwamba tunaweza kumtumaini Yehova, Yesu, na Biblia. Lakini huenda tukajiuliza, je, sikuzote tunaweza kuwatumaini ndugu na dada zetu kutanikoni? Ikiwa jibu ni ndiyo, kwa nini tunaweza kuwatumaini?

TWAHITAJI AKA NDUGU NA DADA BITU

Ulimwenguni pote tuna ndugu na dada wanaotumainika, ambao kama sisi, wanampenda Yehova (Tazama fungu la 3)

3. Tubi ni lipendeleu bo li pikanzika? (Marko 10:29, 30)

3 Yehova ametuchagua tuwe katika familia ya waabudu wake wa ulimwenguni pote. Hilo ni pendeleo kubwa ambalo linatunufaisha sana! (Soma Marko 10:29, 30.) Ulimwenguni pote tuna ndugu na dada, ambao kama sisi, wanampenda Yehova na wanajitahidi kabisa kuishi kulingana na viwango vyake. Huenda lugha, utamaduni, na mavazi yetu yakawa tofauti na yao, lakini tunawapenda, hata tunapokutana nao kwa mara ya kwanza. Tunapenda hasa kuwa pamoja nao ili kumsifu na kumwabudu Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo.​—Zab. 133:1.

4. Kwa ndaba jaki twahitaji aka ndugu na dada bito?

4 Kuliko wakati mwingine wowote, tunahitaji kudumisha umoja pamoja na ndugu na dada zetu. Wakati mwingine, wanatusaidia kubeba mizigo yetu. (Rom. 15:1; Gal. 6:2) Pia, wanatutia moyo tuendelee kuwa na bidii katika utumishi wa Yehova na kubaki imara kiroho. (1 The. 5:11; Ebr. 10:23-25) Fikiria jinsi ambavyo tungehisi ikiwa hatungekuwa na ulinzi wa kutaniko unaotusaidia kusimama imara dhidi ya maadui wetu, yaani, Shetani Ibilisi na ulimwengu wake mwovu. Hivi karibuni, Shetani na wale anaowaongoza watawashambulia watumishi wa Mungu. Wazia jinsi tutakavyothamini kuwa na utegemezo wa ndugu na dada zetu!

5. Kwa ndaba jaki pangi kuwesa kuba vigumu kwa bangi kwa atumaini aka ndugu na dada babo?

5 Hata hivyo, ni vigumu kwa wengine kuwatumaini ndugu na dada zao, labda kwa sababu mwamini mwenzao alifunua siri au alikosa kutimiza ahadi aliyotoa. Au labda mtu fulani kutanikoni alisema au kufanya jambo ambalo liliwaumiza sana. Hali hizo zinapotokea, huenda ikawa vigumu kuwatumaini wengine. Basi, ni nini kinachoweza kutusaidia kuwatumaini waabudu wenzetu?

UPALANI GUTUJANGATI KUTUMAINIANA

6. Upalani guwesa bo kutujangati kwa atumaini bange? (1 Wakorintho 13:4-8)

6 Upendo ndio msingi wa kutumainiana. Wakorintho ya Kwanza sura ya 13 inafafanua mambo mengi kuhusu upendo ambayo yanaweza kutusaidia kuwatumaini au kuanza kuwatumaini tena wengine. (Soma 1 Wakorintho 13:4-8.) Kwa mfano, mstari wa 4 unasema kwamba “upendo ni wenye subira na fadhili.” Yehova anatuonyesha subira hata tunapomtendea dhambi. Bila shaka, sisi pia tunaweza kuwaonyesha subira ndugu zetu ikiwa watasema au kufanya mambo ambayo yanatuudhi au kutuumiza. Mstari wa 5 unaongezea hivi: “[Upendo] hauchokozeki. Hauweki hesabu ya ubaya.” Hatungependa ‘kuweka hesabu ya ubaya,’ kwa kutunza akilini kumbukumbu ya makosa ya ndugu zetu ili tuwakumbushe wakati ujao. Mhubiri 7:9 inasema kwamba hatupaswi ‘kukasirika haraka.’ Badala yake, ni bora kufuata maneno ya Waefeso 4:26: “Jua lisitue mkiwa bado mmekasirika”!

7. Kanuni yeibi mu Mathayo 7:1-5 iwesa kutujangati bo kwa atumaini bange?

7 Jambo lingine litakalotusaidia kuwapenda ndugu na dada zetu ni kuwaona kama Yehova anavyowaona. Mungu anawapenda na haweki hesabu ya dhambi zao. Sisi pia tunapaswa kumwiga Yehova. (Zab. 130:3) Badala ya kukazia fikira udhaifu wao, tunapaswa kujitahidi kuona sifa zao nzuri na kutambua uwezo wao wa kufanya mambo mema. (Soma Mathayo 7:1-5.) Tunaamini kwamba wana nia nzuri kwa sababu upendo “huamini mambo yote.” (1 Kor. 13:7) Maneno hayo hayamaanishi kwamba Yehova anatarajia tuwatumaini wengine bila msingi wowote, badala yake, anatarajia tuwatumaini kwa sababu wamethibitika kuwa wenye kutumainika. b

8. Guwesa kuhenga ki ili gwa atumainia aka ndugu bako?

8 Kama vile inavyochukua muda ili mtu astahili kuheshimiwa, ndivyo ilivyo inapohusu kutumainiana. Unawezaje kuwatumaini ndugu zako? Jitahidi kuwafahamu vizuri. Zungumza nao kwenye mikutano ya kutaniko. Fanya mpango wa kushiriki katika huduma pamoja nao. Waonyeshe subira na uwapatie nafasi ya kuonyesha kwamba wanaweza kutumainika. Mwanzoni, huenda ukawa mwangalifu kuhusu kumwambia mambo ya kibinafsi mtu ambaye mmefahamiana hivi karibuni. Uhusiano wenu unapozidi kuimarika huenda ukajihisi huru zaidi kumweleza hisia zako. (Luka 16:10) Lakini unaweza kufanya nini ndugu akikosa kuwa mwenye kutumainika? Usifanye haraka kuvunja urafiki wenu. Badala yake, ruhusu muda upite. Na usiruhusu matendo ya watu wachache yakuzuie kuwatumaini ndugu zako. Kuhusiana na jambo hilo, tutachunguza mifano michache iliyowekwa na watumishi waaminifu wa Yehova, ambao licha ya kuvunjwa moyo na watu fulani, waliendelea kuwatumaini wengine.

LIBOLA KUBOKANA NA BA AKAENDALI KWA ATUMAINI BANGI

Licha ya itikio la awali la Eli, Hana aliendelea kutumaini mpango wa Yehova (Tazama fungu la 9)

9. (a) Hana jwalangiabo kwamba jwatumainia mpangu guka Yehova licha ja makosa ga baadhi ja awakilishi bake? (b) Kisa saka Hana sutupundisa ki kuhusu kutumaini mpangu guka Yehova? (Linga picha.)

9 Je, umewahi kuvunjwa moyo na jambo ambalo ndugu mwenye mapendeleo kutanikoni alifanya? Ikiwa ndivyo, utanufaika kwa kuchunguza mfano wa Hana. Wakati huo, Kuhani Mkuu Eli ndiye aliyeongoza ibada ya Yehova huko Israeli. Lakini familia yake haikuweka mfano mzuri. Wanawe, ambao walikuwa makuhani, walizoea kujihusisha katika mwenendo mpotovu kiadili na wenye kuaibisha; ingawa hivyo, baba yao hakuwarekebisha kwa uthabiti. Yehova hakumwondoa papo hapo Eli kuwa kuhani mkuu. Ingawa hivyo, Hana hakuacha kutumaini mpango wa Mungu kwa kukataa kuabudu kwenye hema la ibada kipindi ambacho Eli alikuwa kuhani mkuu. Eli alipomwona Hana akisali akiwa na mkazo mkubwa, alifikiri kimakosa kwamba alikuwa amelewa. Bila kupata habari kamili, alimkosoa mwanamke huyo mwenye mkazo. (1 Sam. 1:12-16) Ingawa hivyo, Hana alitoa nadhiri kwamba ikiwa angepata mwana, angemleta atumikie kwenye hema la ibada ambapo angekuwa chini ya utunzaji wa Eli. (1 Sam. 1:11) Je, wana wa Eli walihitaji kurekebishwa? Ndiyo, na hatimaye Yehova alichukua hatua. (1 Sam. 4:17) Na katika kipindi hicho, Mungu alimthawabisha Hana kwa kumpa mwana, yaani, Samweli.​—1 Sam. 1:17-20.

10. Mfalme Daudi jwaendalya bo kwa atumaini bangi licha juku salitiwa?

10 Je, umewahi kuhisi kwamba umesalitiwa na rafiki wa karibu? Ikiwa ndivyo, fikiria jambo lililompata Mfalme Daudi. Mmoja wa rafiki zake alikuwa mwanamume aliyeitwa Ahithofeli. Lakini Absalomu, mwana wa Daudi, alipojaribu kunyakua ufalme kutoka kwa baba yake, Ahithofeli alijiunga na Absalomu katika uasi huo. Bila shaka, Daudi aliumia sana mwanaye alipoasi na rafiki yake wa karibu akamuunga mkono! Ingawa hivyo, Daudi hakuruhusu usaliti huo umzuie kuwatumaini wengine. Aliendelea kumtumaini rafiki mwingine mshikamanifu, Hushai, ambaye alikataa kujiunga na uasi huo. Daudi alikuwa na sababu nzuri za kumtumaini. Hushai alithibitika kuwa rafiki mzuri, hata alihatarisha uhai wake ili kumsaidia Daudi.​—2 Sam. 17:1-16.

11. Jumu kati ja atumishi bika Nabali jwalangia bo kwamba antumainia Abigaile?

11 Fikiria pia mfano uliowekwa na mmoja kati ya watumishi wa Nabali. Daudi na wanaume wake walikuwa wamewalinda kwa fadhili watumishi wa Mwisraeli aliyeitwa Nabali. Muda fulani baadaye, Daudi alimwomba Nabali aliyekuwa tajiri awape wanaume wa Daudi chakula, kiasi chochote ambacho Nabali angeweza kutoa. Nabali alipokataa ombi hilo, Daudi alikasirika sana hivi kwamba akaamua kumuua kila mwanamume katika nyumba ya Nabali. Mtumishi mmoja aliripoti hali hiyo kwa Abigaili, mke wa Nabali. Akiwa mshiriki wa nyumba ya Nabali, alijua kwamba Abigaili angeweza kuokoa uhai wake. Badala ya kutoroka, alitumaini kwamba Abigaili angeweza kurekebisha hali hiyo. Alikuwa na uhakika huo kwa sababu kila mtu alijua kwamba Abigaili alikuwa mwanamke mwenye hekima. Mambo yaliyofuata yalithibitisha kwamba alikuwa na sababu nzuri ya kumtumaini Abigaili. Abigaili alitenda kwa ujasiri kwa kumshawishi Daudi asitende kulingana na mpango wake. (1 Sam. 25:2-35) Abigaili alitumaini kwamba Daudi angetenda kwa busara.

12. Yesu jwalangia bo kwamba jwa atumainia wanafunzi baki ata ingawa bahengiki makosa?

12 Yesu aliwatumaini wanafunzi wake licha ya makosa yao. (Yoh. 15:15, 16) Yakobo na Yohana walipomwomba Yesu awape nafasi ya pekee katika Ufalme, Yesu hakutilia shaka nia yao ya kumtumikia Yehova, wala hakuwaondoa kuwa mitume wake. (Marko 10:35-40) Baadaye, wanafunzi wote wa Yesu walimwacha usiku aliokamatwa. (Mt. 26:56) Hata hivyo, Yesu hakuacha kamwe kuwatumaini. Alielewa vizuri hali yao ya kutokamilika; na “aliwapenda mpaka mwisho.” (Yoh. 13:1) Baada ya kufufuliwa, Yesu aliwapa mitume wake waaminifu 11 jukumu muhimu la kuongoza kazi ya kufanya wanafunzi na kuwatunza kondoo wake wenye thamani. (Mt. 28:19, 20; Yoh. 21:15-17) Alikuwa na sababu nzuri za kuwatumaini wanaume hao wasio wakamilifu. Wote walitumikia kwa uaminifu hadi mwisho wa maisha yao duniani. Bila shaka, Hana, Daudi, mtumishi wa Nabali, Abigaili, na Yesu waliweka mfano mzuri wa kuwatumaini wanadamu wasio wakamilifu.

KWA ATUMAINI KABE AKA NDUGU BITO

13. Libi lijambu bo leliwesa kufanya kubya vigumu kwa atumaini bange?

13 Je, umewahi kumwomba ndugu unayemwamini atunze jambo fulani likiwa siri, kisha baadaye ukagundua amewaambia wengine? Hilo linaweza kukuvunja moyo sana. Dada mmoja, alimwambia mzee wa kutaniko jambo fulani la kibinafsi. Siku iliyofuata, dada huyo alipigiwa simu na mke wa yule mzee ili amtie moyo, na ilikuwa wazi kwamba alijua jambo ambalo mzee aliambiwa faraghani. Inaeleweka kwamba sasa ilikuwa vigumu kwa yule dada kumtumaini mzee huyo. Lakini inafurahisha kwamba dada huyo alitafuta msaada, alizungumza na mzee mwingine ambaye alimsaidia kuanza tena kuwatumaini wazee.

14. Ki sesunzangatya ndugu fulani juanza kabe kwa atumaini azee?

14 Kwa muda mrefu, ndugu mmoja alikuwa amewakasirikia wazee wawili ambao alihisi hawezi kuwatumaini. Hata hivyo, alianza kufikiria kuhusu jambo ambalo lilisemwa na ndugu fulani ambaye alimheshimu sana. Alisema maneno haya yenye nguvu: “Shetani ndiye adui yetu, si ndugu zetu.” Ndugu huyo alifikiria kwa makini na kusali kuhusu jambo hilo, na mwishowe akafaulu kufanya amani pamoja na wazee wote wawili.

15. Kwasabu jaki pangi kuwesa kujuku muda kuanza kabe kwa atumaini bange? Pia mfanu.

15 Je, umewahi kupoteza pendeleo fulani kutanikoni? Jambo hilo linaweza kuumiza. Dada anayeitwa Grete na mama yake walikuwa Mashahidi washikamanifu miaka ya 1930 kazi yetu ilipokuwa imepigwa marufuku katika Ujerumani ya Wanazi. Grete alifurahia pendeleo la kuchapa nakala za Mnara wa Mlinzi kwa ajili ya waabudu wenzake. Lakini akina ndugu walipogundua kwamba baba yake alipinga kweli, alinyang’anywa pendeleo hilo kwa sababu waliogopa kwamba baba yake angelisaliti kutaniko kwa wapinzani wao. Grete hakuvumilia tu jaribu hilo. Katika kipindi chote cha Vita vya Pili vya Ulimwengu, akina ndugu hawakumpa Grete na mama yake nakala za magazeti na hawakuzungumza naye walipokutana barabarani. Hilo lilimuumiza sana! Grete aliumia sana kihisia na alisema kwamba ilimchukua muda mrefu kuwasamehe na kuanza tena kuwatumaini ndugu hao. Hata hivyo, baada ya muda, alitambua kwamba ni lazima Yehova amewasamehe, naye pia anapaswa kuwasamehe. c

“Shetani ndiye adui yetu, si ndugu zetu”

16. Kwa ndaba jaki tupaswa kujitahidi ngani kwa atumaini kabe aka ndugu na dada bito?

16 Ikiwa umekabiliana na hali kama hiyo yenye kuumiza, jitahidi kuwatumaini tena akina ndugu. Huenda ikachukua muda, lakini jitihada zako si za bure. Kwa mfano, ikiwa umewahi kula chakula ambacho kilikusababishia madhara tumboni, huenda ukawa mwangalifu kuhusu chakula unachokula. Hata hivyo, tukio hilo moja haliwezi kukuzuia usile tena chakula. Vivyo hivyo, hatupaswi kuruhusu tukio moja baya lifanye tuache kuwatumaini ndugu na dada zetu, ambao tunajua kwamba si wakamilifu. Tunapojitahidi kuwatumaini tena, tutakuwa na furaha zaidi na itakuwa rahisi zaidi kwetu kukazia fikira mambo ambayo sisi tunaweza kufanya ili kuchangia hali ya kutumainiana kutanikoni.

17. Kwa ndaba jaki kubi muhimu kutumainiana, na twiilongalya ki mu makala jejipwata?

17 Ni vigumu kwa watu katika ulimwengu wa Shetani kutumainiana, lakini sisi tunawatumaini ndugu na dada zetu kwa sababu tunawapenda. Hali hiyo ya kutumainiana inachangia shangwe yetu na umoja sasa, na itatulinda tutakapokabili hali ngumu wakati ujao. Namna gani ikiwa mtu fulani amefanya jambo linalofanya iwe vigumu kumtumaini tena? Jitahidi kuona mambo kama Yehova anavyoyaona, tumia kanuni za Biblia, sitawisha upendo mwingi kuelekea ndugu zako, na ujifunze kutokana na mifano ya watu katika Biblia. Tunaweza kushinda hisia zetu za kuvunjika moyo na kuanza kuwatumaini tena wengine. Tukifanya hivyo, tutafurahia baraka ya kuwa na marafiki wengi ‘wanaoshikamana nasi kwa ukaribu kuliko ndugu.’ (Met. 18:24) Hata hivyo, ili wengine watutumaini, sisi pia tunapaswa kuwa wenye kutumainika. Katika makala inayofuata, tutazungumzia jinsi tunavyoweza kuwaonyesha ndugu zetu kwamba wanaweza kututumaini.

NHAMBU 99 Ndugu Makumi ya Elfu

a Tunahitaji kuwatumaini ndugu zetu. Si rahisi kufanya hivyo sikuzote kwa sababu wakati mwingine wanafanya mambo yanayotuvunja moyo. Katika makala hii, tutachunguza jinsi ambavyo kutumia kanuni za Biblia na kutafakari mifano ya watu wa kale, kunaweza kutusaidia kuwatumaini waamini wenzetu na kurudisha tena hali ya kuaminiana wanapotuvunja moyo.

b Biblia inatuonya kwamba baadhi ya watu katika kutaniko hawangestahili kutumainiwa. (Yuda 4) Katika visa vichache, huenda ndugu wa uwongo wakajaribu kuwapotosha wengine kwa kusema “mambo yaliyopotoka.” (Mdo. 20:30) Tunaepuka kuwatumaini au kuwasikiliza watu hao.