Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 37

Tutumainie Ndugu na Dada Zetu

Tutumainie Ndugu na Dada Zetu

“Upendo . . . unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote.”​—1 KO. 13:4, 7.

WIMBO 124 Tukuwe Washikamanifu

KIFUPI YA HABARI *

1. Leo watu wengi hawajue watumainie nani. Juu ya nini ile haipaswe kutushangaza?

 MU HII dunia ya Shetani, watu hawajue watumainie nani. Wengi wamevunjika moyo juu ya matendo ya viongozi wa biashara, wa politike na wa dini. Ile inawafanya pia wasitumainie marafiki wao, majirani, na hata watu wa familia yao. Ile haipaswe kutushangaza, juu Biblia ilisemaka hivi: “Katika siku za mwisho . . . , watu watakuwa . . . wenye hawana ushikamanifu, . . . wachongezi, . . . wasaliti.” Ile inamaanisha kama watu watakuwa kama Shetani, Mungu wa hii dunia mwenye hawezi kutumainiwa.​—2 Ti. 3:1-4; 2 Ko. 4:4.

2. (a) Nani njo tunapaswa kabisa kutumainia? (b) Wamoja wanaweza kujiuliza nini?

2 Lakini siye Wakristo, tunajua kama tunapaswa kabisa kumutumainia Yehova. (Yer. 17:7, 8) Tuko hakika kama Yehova anatupenda na kama ‘hataacha hata kidogo’ marafiki wake. (Zb. 9:10) Tunamutumainia pia Yesu Kristo juu alitoa uzima wake kwa ajili yetu. (1 Pe. 3:18) Na tumejionea mu maisha yetu kama mashauri ya Biblia ni yenye kutumainika. (2 Ti. 3:16, 17) Tunapaswa kabisa kutumainia Yehova, Yesu, na Biblia. Lakini wamoja wanaweza kujiuliza hivi: Sikuzote tunaweza kabisa kutumainia ndugu na dada zetu? Kama ni vile, juu ya nini tunaweza kuwatumainia?

TUKO NA LAZIMA YA NDUGU NA DADA ZETU

Mu dunia yote, tuko na ndugu na dada wenye kutumainika, wenye wanamupenda Yehova sawa siye (Ona fungu ya 3)

3. Ni pendeleo gani kubwa sana yenye tuko nayo? (Marko 10:29, 30)

3 Yehova ametuchagua juu tukuwe mu familia ya mu dunia yote ya waabudu wake. Ile ni pendeleo kubwa sana na inatuletea faida mingi sana! (Soma Marko 10:29, 30.) Mu dunia yote, tuko na ndugu na dada wenye wanamupenda Yehova sawa siye, na wenye wanajikaza kuishi kulingana na kanuni zake. Luga yetu, desturi, na namna yetu ya kuvala, inaweza kuwa tofauti na yao. Lakini tunajisikia tu tunawapenda, hata wakati tunakutana nao kwa mara ya kwanza. Tunapenda zaidi sana kukutana nao juu ya kumusifu na kumuabudu Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo.​—Zb. 133:1.

4. Juu ya nini tuko na lazima ya ndugu na dada zetu?

4 Hii njo wakati yenye tunapaswa kuendelea kuishi kwa umoja na ndugu na dada zetu. Juu wakati fulani, wanatusaidia kubeba mizigo yetu. (Ro. 15:1; Gal. 6:2) Wanatutia pia moyo tuendelee kumutumikia Yehova kwa bidii na kuendelea kuwa nguvu kiroho. (1 Te. 5:11; Ebr. 10:23-25) Unafikiri mambo ingekuwa namna gani kama hatungekuwa na ndugu na dada zetu juu ya kutusaidia kupambana na maadui wetu, ni kusema, Shetani na wale wenye kumuunga mukono? Karibuni Shetani na wale wenye kumuunga mukono watashambulia watumishi wa Mungu. Ile wakati, tutakuwa wenye shukrani sana kuona vile ndugu na dada zetu watakuwa pale juu ya kutusaidia!

5. Juu ya nini wamoja wanaweza kuona kama ni nguvu kutumainia ndugu na dada zao?

5 Lakini, wamoja wanaona kuwa ni nguvu kutumainia ndugu na dada zao, juu pengine ndugu ao dada fulani alifunuaka jambo yao ya siri kwa wengine, ao juu alishindwaka kutimiza ahadi fulani. Ao pengine, ndugu ao dada fulani mu kutaniko alisema ao kufanya jambo fulani yenye iliwaumiza sana. Mambo sawa ile inaweza kufanya ikuwe nguvu kutumainia wengine. Sasa, nini njo inaweza kutusaidia kutumainia ndugu na dada zetu?

UPENDO UNATUSAIDIA KUTUMAINIA WENGINE

6. Fasiria namna upendo unatusaidia kutumainia wengine. (1 Wakorinto 13:4-8)

6 Upendo njo unatusaidia kutumainia wengine. Wakorinto wa kwanza sura ya 13 inaonyesha njia mbalimbali za kuonyesha upendo zenye zinaweza kutusaidia kutumainia ao kuanza tena kutumainia wengine. (Soma 1 Wakorinto 13:4-8.) Kwa mufano, mustari wa 4 unasema kama “upendo ni wenye uvumilivu na wenye fazili.” Yehova anatuvumiliaka hata wakati tunamutendea zambi. Na siye pia tunapaswa kuvumilia ndugu na dada zetu kama wanasema ao kufanya jambo fulani yenye kutukasirisha ao kutuumiza. Mustari wa 5 unaongezea: “[Upendo] haukasirike haraka. Hauweke hesabu ya ubaya.” Hatupaswe ‘kuweka hesabu ya ubaya,’ ni kusema, kuchunga mu akili ni mara ngapi ndugu na dada zetu walitukosea. Muhubiri 7:9 inatuambia kama hatupaswe ‘kuwa haraka kukasirika.’ Ni muzuri sana kutumikisha hii maneno yenye kupatikana mu Waefeso 4:26: “Jua lisishuke wakati mungali katika kasirani”!

7. Kanuni zenye kuwa mu Matayo 7:1-5 zinaweza kutusaidia namna gani kutumainia wengine?

7 Jambo ingine yenye inaweza kutusaidia kutumainia ndugu na dada zetu ni kuwaona sawa vile Yehova anawaona. Mungu anawapenda na hakuwake iko nahesabia zambi zao. Na siye pia hatupaswe kufanya vile. (Zb. 130:3) Kuliko kukazia akili makosa yao, tunapaswa kujikaza kuona sifa zao za muzuri, na kufikiria mambo ya muzuri yenye wanaweza kufanya. (Soma Matayo 7:1-5.) Juu upendo “unaamini mambo yote,” tunaamini kama ndugu na dada zetu wanapenda kufanya mambo ya muzuri na hawawezi kupenda kutuumiza kimakusudi. (1 Ko. 13:7) Ile haimaanishe kama Yehova anapenda tutumainie wengine ovyo-ovyo, lakini anapenda tuwatumainie juu walionyesha kama ni wenye kutumainika. *

8. Unaweza kufanya nini juu ufikie kutumainia ndugu na dada zako?

8 Inakamataka wakati juu tufikie kutumainia ndugu na dada zetu. Unaweza kufanya nini juu ufikie kutumainia ndugu na dada zako? Ujikaze kuwajua muzuri. Uzungumuze nao ku mikutano. Upange kuhubiri nao, uwavumilie, uwapatie nafasi ya wao kuonyesha kama ni wenye kutumainika. Ku mwanzo, pengine hautapenda kuambia mambo yako ya kipekee mutu mwenye hayakuwa rafiki yako sana. Lakini kadiri urafiki wenu unakomaa, unaweza kujisikia huru kumuambia mambo yako. (Lu. 16:10) Sasa, unaweza kufanya nini kama ndugu ao dada anafanya jambo fulani yenye inafanya usimutumainie tena? Usikuwe haraka kuvunja urafiki naye. Lakini, uache wakati fulani ipite. Usiache matendo ya watu fulani tu ikuvunje moyo na ikufanye uache kutumainia ndugu na dada zako. Juu ya kuelewa muzuri ile jambo, tuchunguze mifano ya watumishi fulani waaminifu wa Yehova wenye hata kama watu fulani waliwavunja moyo, hawakuacha kutumainia wengine.

HAWAKUACHA KUTUMAINIA WENGINE

Hata kama Eli alimujibu mubaya, Hana aliendelea kutumainia mipango yenye Yehova ameweka kwa ajili ya ibada (Ona fungu ya 9)

9. (a) Hata kama Eli na watoto wake wanaume hawakujiendesha muzuri, nini njo inaonyesha kama Hana aliendelea kutumainia mipango yenye Yehova aliweka kwa ajili ya ibada? (b) Habari ya Hana inakufundisha nini kuhusu kutumainia mipango yenye Yehova ameweka kwa ajili ya ibada? (Ona picha.)

9 Ulishakavunjika moyo juu ya matendo fulani ya ndugu mwenye kuwa na madaraka? Kama ni vile, mufano wa Hana unaweza kukusaidia. Ile wakati, kuhani mukubwa Eli njo alikuwa anaongoza mambo ya ibada ya Yehova mu Israeli. Lakini watu wa familia yake hawakukuwa mufano muzuri. Watoto wake wanaume wenye walikuwa makuhani walizoea kufanya mambo ya haya, mambo ya uasherati. Lakini, baba yao hakujikaza kabisa kuwarekebisha. Yehova hakumuambia mara moya Eli aache kuwa kuhani mukubwa. Ijapokuwa vile, Hana aliendelea kutumainia mipango yenye Yehova aliweka kwa ajili ya ibada, hakukatala kuabudu ku tabenakulo wakati Eli alikuwa angali kuhani mukubwa. Hana alikuwa nasali juu alikuwa na mahangaiko sana. Wakati Eli alimuona, alisema mara moya kama Hana alikuwa mulevi, lakini Hana hakukuwa mulevi. Kuliko kutafuta kujua ukweli wa mambo, Eli alichambua-chambua tu ule mwanamuke mwenye alikuwa na mahangaiko sana. (1 Sa. 1:12-16) Hata vile, Hana alimuahidi Yehova kama, ikiwa anapata mutoto, atamutuma ku tabenakulo juu amutumikie. Na kule ule mutoto angekuwa chini ya usimamizi wa Eli. (1 Sa. 1:11) Mambo ilikuwa imeishia pale kuhusu matendo ya mubaya ya watoto wanaume wa Eli? Hapana. Yehova aliwapatia malipizi wakati yenye kufaa. (1 Sa. 4:17) Na ni mu ileile kipindi njo Mungu alimubariki Hana kwa kumupatia mutoto mwanaume, Samweli.​—1 Sa. 1:17-20.

10. Nini njo inaonyesha kama Daudi aliendelea kutumainia wengine hata kama watu fulani walimuvunja moyo?

10 Rafiki yako wa karibu alishakakuvunja moyo? Kama ni vile, habari ya Mufalme Daudi inaweza kukusaidia. Alikuwa na rafiki moya mwenye kuitwa Ahitofeli. Lakini wakati Absalomu mwana wa Daudi alijaribu kunyanganya ufalme wa baba yake, Ahitofeli alijiunga naye mu uasi wake. Inawezekana Daudi aliumia sana kuona vile mwana wake na mwanaume mwenye aliwaza ni rafiki yake wanamugeuzia mugongo! Lakini Daudi hakuruhusu ile imufanye aache kutumainia wengine. Aliendelea kutumainia rafiki yake mwingine mushikamanifu, Hushai, mwenye hakujiunga mu uasi wa Absalomu. Daudi alikuwa na sababu za kumutumainia Hushai. Hushai alionyesha kama alikuwa rafiki muzuri, na hata alitia uzima wake mu hatari juu ya kumusaidia Daudi.​—2 Sa. 17:1-16.

11. Mutumishi fulani wa Nabali alifanya nini yenye inaonyesha kama alitumainia Abigaili?

11 Fikiria pia mufano wa mutumishi fulani wa Nabali. Daudi na watu wake walilinda watumishi wa Mwisraeli mumoja mwenye kuitwa Nabali. Kisha wakati fulani, Daudi aliomba Nabali, mwanaume tajiri, apatie wanaume wake chakula. Nabali angeweza kuleta chakula yoyote yenye angepata. Wakati Nabali alikatala ile ombi yenye usawaziko, Daudi alikasirika sana na aliamua kuua kila mwanaume wa nyumba ya Nabali. Mutumishi fulani alienda kuelezea Abigaili, bibi wa Nabali, ile jambo. Juu aliishi mu ile nyumba, alijua kama maisha yake ilikuwa mu mikono ya Abigaili. Kuliko kukimbia, alitumainia kama Abigaili angeweza kutengeneza mambo. Alikuwa na sababu ya kutumainia Abigaili juu kila mutu alijua kama ni mwanamuke mwenye hekima. Mambo yenye ilitokea kisha inaonyesha kama ule mutumishi hakudanganyika. Abigaili alitenda kwa uhodari kwa kumuzuia Daudi asimwange damu. (1 Sa. 25:2-35) Abigaili alitumainia kama Daudi atatenda kwa hekima.

12. Nini njo inaonyesha kama Yesu alitumainia wanafunzi wake hata kama walikuwa nafanya makosa?

12 Yesu alitumainia wanafunzi wake hata kama walikuwa nafanya makosa. (Yoh. 15:15, 16) Wakati Yakobo na Yohana walimuomba Yesu nafasi ya pekee mu Ufalme, Yesu hakusema kama walikuwa namutumikia Yehova na nia ya mubaya, ao hakuwatosha ku liste ya mitume. (Mk. 10:35-40) Kisha, usiku wenye Yesu alikamatwa, wanafunzi wake wote walimuacha. (Mt. 26:56) Lakini, Yesu hakuacha hata kidogo kuwatumainia. Hata kama alijua muzuri uzaifu wao, “aliwapenda mupaka mwisho.” (Yoh. 13:1) Na hata kisha ufufuo wake, Yesu alipatia mitume wake waaminifu 11 daraka ya maana ya kuongoza kazi ya kufanya wanafunzi na kuhangaikia kondoo wake wenye samani. (Mt. 28:19, 20; Yoh. 21:15-17) Kutumainia wale wanadamu wenye hawakamilike haikukuwa kudanganyika. Wote waliendelea kutumika kwa uaminifu mupaka mwisho wa maisha yao hapa ku dunia. Bila shaka, Hana, Daudi, mutumishi wa Nabali, Abigaili, na Yesu, waliweka mufano muzuri kuhusu kutumainia wanadamu wenye hawakamilike.

NAMNA YA KUANZA TENA KUTUMAINIA WENGINE

13. Ni jambo gani inaweza kufanya ikuwe nguvu kutumainia wengine?

13 Ulishakaambia ndugu ao dada fulani habari yako ya siri na kisha ukafikia kutambua kama alishaambia wengine? Ile inaweza kuvunja moyo sana. Siku moya, dada fulani aliambiaka muzee mambo yake ya kipekee. Siku yenye kufuata, bibi ya ule muzee akaita ule dada juu ya kumutia moyo, ni wazi kama alijua mambo ya kipekee yenye ule dada aliambiaka bwana yake. Kwa hiyo, ule dada aliona kama ni nguvu sana kutumainia ule muzee. Lakini ule dada alikamata uamuzi muzuri wa kuenda kuomba musaada. Alizungumuza na muzee mwingine na ule muzee alimusaidia kuanza tena kutumainia wazee.

14. Nini njo ilisaidia ndugu moya aanze tena kutumainia wengine?

14 Kwa muda murefu, ndugu moya alikasirishwa na wazee wawili, na alijisikia kama hawezi tena kuwatumainia. Lakini, alianza kufikiria jambo fulani yenye ndugu moya mwenye anaheshimiaka sana alisemaka. Ule ndugu alisemaka hii maneno ya mwepesi lakini yenye nguvu: “Shetani njo adui yetu, hapana ndugu zetu.” Ndugu yetu alifikiri sana juu ya ile maneno na juu ya mambo yenye alipaswa kufanya. Kisha kumuomba Yehova amusaidie, aliweza kufanya amani na wale wazee wawili.

15. Juu ya nini inaweza kuomba wakati mingi ipite juu tuanze tena kutumainia wengine? Leta mufano.

15 Ulishakapoteza pendeleo fulani? Inaumizaka sana. Grete na mama yake walikuwa Mashahidi waaminifu mu Alemanye yenye ilikuwa natawaliwa na Wanazi mu miaka ya 1930. Ile wakati, kazi yetu ilikuwa imekatazwa mu Alemanye. Grete alikuwa na pendeleo ya kuandika na mashini kopi za Munara wa Mulinzi kwa ajili ya ndugu na dada zake. Wakati ndugu walifikia kujua kama baba yake alikuwa napinga kweli, walimuondoa pendeleo yenye alikuwa nayo juu waliogopa kama baba yake anaweza kupatia wapinzani habari kuhusu kutaniko. Majaribu ya Grete haikuishia pale. Wakati ya Vita ya Pili ya Ulimwengu, ndugu hawakukuwa napatia Grete na mama yake magazeti na walikatala kuzungumuza nao wakati walikutana nao mu barabara. Iliumiza kabisa! Grete alihuzunika sana, na alisema kama ilikamata wakati mingi juu afikie kusamehe wale ndugu na aanze tena kuwatumainia. Lakini kisha wakati fulani, alitambua kama Yehova alipaswa kuwa alishawasamehe, njo maana naye alipaswa kuwasamehe. *

“Shetani njo adui yetu, hapana ndugu zetu”

16. Kama tunajikaza juu tuanze tena kutumainia ndugu na dada zetu, tutapata faida gani?

16 Kama ulishakakutana na jambo ya vile, ujikaze juu uanze tena kutumainia wengine. Pengine itakamata wakati, lakini ujikaze. Kwa mufano, kama ulishakakula sumu mu chakula, ile inaweza fanya ukuwe muangalifu sana kuhusu chakula yenye unakula. Lakini, chakula moya ya mubaya haitafanya ukatale kula chakula yote. Vilevile, hatupaswe kuacha kutumainia ndugu na dada zetu wote juu tu ndugu ao dada fulani, mwenye tunajua hakamilike, alituvunja moyo. Kama tunaanza tena kutumainia wengine, tutakuwa na furaha zaidi na tutaweza kukaza akili juu ya mambo yenye tunaweza kufanya ili kuendeleza hali ya kutumainiana mu kutaniko.

17. Juu ya nini ni jambo ya maana sana kutumainiana, na tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

17 Ni nguvu sana kutumainia wengine mu hii dunia ya Shetani. Lakini, tunaweza kutumainia ndugu na dada zetu juu tunawapenda nao wanatupenda. Kutumainiana kunafanya tukuwe na furaha na umoja sasa, na kutatulinda wakati tutapambana na magumu ya nguvu sana yenye iko nakuya. Unapaswa kufanya nini kama mutu fulani anakuvunja moyo na ile inafanya usimutumainie tena? Ujikaze kuona mambo namna Yehova anaiona, utumikishe kanuni za Biblia, ujifunze kupenda sana ndugu na dada zako, na ujifunze mifano ya watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia. Tunaweza kupiganisha mawazo yenye kuumiza na kuanza tena kutumainia wengine. Kama tunafanya vile, tutakuwa na marafiki wengi ‘wenye watashikamana sana na [siye] kuliko ndugu.’ (Mez. 18:24) Ni muzuri kutumainia wengine, lakini, nao pia wanapaswa kuwa wenye kutumainika. Mu habari yenye kufuata, tutazungumuzia mambo yenye tunaweza kufanya juu ndugu na dada zetu watutumainie.

WIMBO 99 Ndugu na Dada Wote

^ Tunapaswa kutumainia ndugu na dada zetu. Haikuwake mwepesi kufanya vile, juu wakati fulani wanaweza kutukosea. Mu hii habari, tutazungumuzia kanuni fulani za Biblia na mifano fulani ya watu wa zamani yenye itatusaidia kutumainia ndugu na dada zetu, na kuanza tena kuwatumainia ikiwa walitukosea.

^ Biblia inasema kama kunaweza kuwa watu fulani mu kutaniko wenye hatupaswe kutumainia. (Yud. 4) Haiko sana, lakini mu hali fulani, ndugu wa uongo wanaweza kujaribu kudanganya wengine kwa “kusema mambo yenye kupotoka.” (Mdo. 20:30) Hatupaswe kutumainia ao kusikiliza wale ndugu.

^ Juu ya kujua mambo mingi zaidi kuhusu habari ya Grete, ona Annuaire des témoins de Jéhovah 1974, uku. 129-131.