Amila mo ibi abali

Amila mu gagabi

MAKALA JI LIFUNZU 38

Gujithibitisha Kuba gwa Mundu Jojuaminika

Gujithibitisha Kuba gwa Mundu Jojuaminika

“Mundu jojuaminika jutunza sili.​—MET. 11:13.

NHAMBU 101 Kufanya Kazi Pamoja kwa Umoja

MUHTASARI a

1. Tuwesa bo kummanya mundu jojutumainika?

 MTU anayeaminika au kutumainika hujitahidi kutimiza ahadi anazotoa na kusema ukweli. (Zab. 15:4) Watu wanajua kwamba wanaweza kumtegemea. Tungependa ndugu na dada zetu wahisi hivyo kutuhusu. Tunaweza kufanya nini ili tustahili kutumainika?

2. Tuwesa kuthibitisha bo kwamba tutenda kutumainika?

2 Hatuwezi kuwalazimisha wengine watutumaini. Ni lazima tuthibitishe kwamba tunatumainika. Sifa ya kutumainika inaweza kulinganishwa na pesa. Ingawa ni vigumu kuipata sifa hiyo, ni rahisi kuipoteza. Yehova amethibitisha kabisa kwamba tunaweza kumtumaini. Hawezi kamwe kufanya jambo litakalofanya tuache kumtumaini kwa sababu “kila jambo analofanya linategemeka.” (Zab. 33:4) Na anatarajia kwamba tutamwiga. (Efe. 5:1) Acheni tuchunguze baadhi ya mifano ya watumishi wa Yehova waliomwiga Baba yao wa mbinguni na kuthibitisha kwamba wanaweza kutumainika. Pia, tutachunguza sifa tano zinazoweza kutusaidia kuwa wenye kutumainika.

LIBOLA KUHUMA KWA ATUMISHI BIKA YEHOVA BA AMINIKA

3-4. Nabii Danieli jwathibitika bo kuba jojuaminika, na tupaswa kulilaluki maswali bole?

3 Nabii Danieli aliweka mfano mzuri sana wa kuaminika. Ingawa alipelekwa utekwani na Wababiloni, baada ya muda alijulikana kuwa mtu anayeweza kutumainika. Na aliaminika hata zaidi wakati alipofafanua kwa msaada wa Yehova ndoto ya Mfalme Nebukadneza wa Babiloni. Pindi moja, Danieli alilazimika kumwambia mfalme kwamba Yehova hakufurahishwa naye​—bila shaka ujumbe huo haukumfurahisha mfalme. Danieli alihitaji ujasiri kwa sababu Nebukadneza alikuwa mwenye hasira kali! (Dan. 2:12; 4:20-22, 25) Miaka mingi baadaye, Danieli alithibitika tena kuwa mwenye kuaminika alipofafanua kwa usahihi ujumbe wa kustaajabisha ulioandikwa kwenye ukuta wa makao ya mfalme huko Babiloni. (Dan. 5:5, 25-29) Isitoshe, baadaye Dario Mmedi na maofisa wake waliochaguliwa, walitambua pia kwamba Danieli alikuwa na ‘roho isiyo ya kawaida ndani yake.’ Walisema Danieli “alikuwa mwenye kutegemeka, naye hakupatikana kamwe akiwa mzembe wala mfisadi.” (Dan. 6:3, 4) Naam, hata watawala wapagani walitambua kwamba mwabudu huyo wa Yehova angeweza kutumainika!

4 Baada ya kuchunguza mfano wa Danieli, ni vizuri tujiulize hivi: ‘Nina sifa gani kwa watu walio nje ya kutaniko? Je, ninajulikana kuwa mtu anayetimiza majukumu na anayeweza kutumainika?’ Kwa nini tunapaswa kujiuliza maswali hayo? Kwa sababu tunamletea Yehova sifa tunapokuwa watu wanaoaminika.

Nehemia alichagua wanaume wanaotegemeka ili kushughulikia kazi muhimu (Tazama fungu la 5)

5. Kwa sabu jaki Hanania jwamanyakini kuba mundu jojutumainika?

5 Mwaka wa 455 K.W.K., baada ya Gavana Nehemia kujenga upya kuta za Yerusalemu, alitafuta wanaume wanaotegemeka ambao wangetunza jiji hilo. Kati ya watu wengine, Nehemia alimchagua Hanani, awe mkuu wa Ngome. Biblia inamfafanua Hanani kuwa “mwanamume mwaminifu zaidi [ambaye] alimwogopa Mungu wa kweli kuliko watu wengine wengi.” (Neh. 7:2) Kumpenda Yehova na kuogopa kufanya jambo ambalo litamkasirisha, kulimchochea Hanani achukue kwa uzito mgawo wowote aliopewa. Sifa hizo zitatusaidia sisi pia tuwe wenye kutegemeka katika utumishi wa Mungu.

6. Tikiko jwathibitikabo kuba nkonsi jojuaminika kuka mtumi Paulo?

6 Fikiria mfano wa Tikiko, mwandamani aliyetumainika wa mtume Paulo. Paulo alipokuwa katika kifungo cha nyumbani, alimtegemea Tikiko na alimfafanua kuwa “mhudumu mwaminifu.” (Efe. 6:21, 22) Paulo alikuwa na uhakika kwamba Tikiko angepeleka barua kwa akina ndugu huko Efeso na Kolosai na pia angewatia moyo na kuwafariji. Tikiko anatukumbusha kuhusu wanaume waaminifu wanaotegemeka ambao leo wanatutunza kiroho.​—Kol. 4:7-9.

7. Guwesa kulibola ki kuhusu kuaminika kuhuma kwa azee na atumishi ba huduma mu likutaniku lino?

7 Leo, tunawathamini sana wazee na watumishi wa huduma wanaoaminika. Kama Danieli, Hanani, na Tikiko wanachukua majukumu yao kwa uzito. Kwa mfano, tunapohudhuria mkutano wa katikati ya juma tuna uhakika kwamba sehemu zote kwenye programu zitashughulikiwa. Na wazee wanathamini sana wale walio na migawo wanapojitayarisha na kutimiza migawo yao kwenye mkutano! Kwa mfano, hatusiti kumwalika mwanafunzi wetu wa Biblia kuhudhuria mkutano wa mwisho juma kwa sababu tuna wasiwasi kwamba mtu fulani amesahau kupanga hotuba ya watu wote itolewe. Na tuna uhakika kwamba tutapata machapisho tunayohitaji kwa ajili ya huduma. Tunatunzwa vizuri na ndugu hao waaminifu, na tunamshukuru Yehova kwa ajili yao! Hata hivyo, tunaweza kuthibitisha kwa njia gani kwamba tunaaminika?

GUBYA MUNDU JOJUAMINIKA KU KUTUNZA SILI

8. Tuwesa kulangi bo usawaziku patushugulika na bange? (Methali 11:13)

8 Tunawapenda ndugu na dada zetu na tunahangaikia hali yao njema. Hata hivyo, tunapaswa kuwa wenye usawaziko na kuheshimu faragha yao. Baadhi ya watu katika kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza walikuwa “wanapiga porojo na kujiingiza katika mambo ya watu wengine, wakiongea kuhusu mambo ambayo hawapaswi.” (1 Tim. 5:13) Bila shaka, hatungependa kuwa kama wao. Lakini namna gani ikiwa mtu atatuambia habari zake za kibinafsi, akitumaini kwamba hatutawaambia wengine. Kwa mfano, dada fulani anaweza kutuambia kuhusu tatizo lake la kiafya au jaribu lingine analokabiliana nalo na kutuomba tusiwaambie wengine. Tunapaswa kuheshimu ombi lake. b (Soma Methali 11:13.) Acheni sasa tuzungumzie hali nyingine ambazo ni muhimu kwetu kutunza siri.

9. Ashiliki ba familia awesa kulangi bo kwamba atenda kuaminika?

9 Katika familia. Kila mshiriki wa familia ana jukumu la kutunza siri kuhusu mambo ya faragha ya familia. Kwa mfano, huenda mwanamke Mkristo ana tabia fulani ambayo inamchekesha mume wake. Je, mume huyo atawaambia watu wengine kuhusu jambo hilo na kumwaibisha mke wake? Bila shaka hatafanya hivyo! Anampenda mke wake, na hawezi kamwe kufanya jambo litakalomuumiza. (Efe. 5:33) Matineja wanapenda kutendewa kwa heshima. Wazazi wanapaswa kutambua jambo hilo. Wazazi hawapaswi kuwaaibisha watoto wao kwa kuwaambia watu wengine kuhusu makosa yao. (Kol. 3:21) Watoto wanapaswa kujifunza kuwa wenye busara, hawapaswi kuwaambia watu wengine mambo ambayo yatamwaibisha mshiriki wa familia yao. (Kum. 5:16) Kila mshiriki wa familia anapojitahidi kutunza mambo ya faragha ya familia yakiwa siri, uhusiano wao katika familia unaimarika.

10. Kuba gunkosi jwa sakaka kuhusisha kike? (Methali 17:17)

10 Kati ya marafiki. Wakati fulani, wengi wetu huhisi kwamba tunahitaji kumweleza rafiki yetu wa karibu jambo linalotuhangaisha. Wakati mwingine huenda ikawa vigumu kufanya hivyo. Labda hatujazoea kuwafunulia watu hisia zetu za ndani, na tutavunjika moyo sana tunapotambua kwamba baadaye rafiki yetu amewaambia watu wengine jambo tulilomwambia. Kinyume chake, tunathamini tunapopata mtu anayeweza kutunza siri! Huyo ni “rafiki wa kweli.”​—Soma Methali 17:17.

Wazee hawawaambii mambo ya siri watu wa familia yao (Tazama fungu la 11) c

11. (a) Azee na aka ahanamundu alangi bo kwamba atenda kutegameka? (b) Tulibola lijambu bo kuhuma kuka mzee jojwashughulakya lijambu la falagha mu likutaniku na baadai jaki jwabi pamu na familia jake? (Linga picha.)

11 Katika kutaniko. Wazee ambao wanatunza siri ni “mahali pa kujificha kutokana na upepo, na mahali pa kujisitiri” kwa ajili ya ndugu zao. (Isa. 32:2) Tunajua kwamba tunaweza kuzungumza kwa uhuru na wanaume hao, tukiwa na uhakika kuwa mambo tunayowaambia yatatunzwa yakiwa siri. Hatuwashinikizi watuambie kuhusu mambo yanayopaswa kuwa siri. Isitoshe, tunawathamini wake wa wazee kwa sababu hawajaribu kupata habari za siri kuhusu wengine kutoka kwa waume zao. Kwa kweli, ni tendo la fadhili kwamba mke wa mzee haambiwi mambo ya kibinafsi kuhusu akina ndugu na dada. Mke mmoja wa mzee alisema hivi: “Ninashukuru kwamba mume wangu anatunza habari za siri kuhusu wale anaowafanyia ziara za uchungaji, au wale wanaohitaji msaada wa kiroho, na hata haniambii majina yao. Ninashukuru kwamba sibebi mzigo wa mambo ambayo siwezi kuyashughulikia. Kwa hiyo, ninaweza kushirikiana na wote kwa uhuru kutanikoni. Na ninaweza kuwa na uhakika kwamba ikiwa nitamwambia mume wangu hisia zangu au matatizo yangu ya kibinafsi, atatunza habari hizo zikiwa siri.” Bila shaka, sisi sote tungependa kuwa na sifa ya kuaminika. Ni sifa gani zitakazotusaidia kufikia lengo hilo? Acheni tuchunguze sifa tano.

SITAWISHA SIFA YEYAGUJANGATYA GUBYA JOJUAMINIKA

12. Kwa ndaba jaki tuwesa kupwaga kwamba upalani ndo msingi gu kutumainiana? Pia mfanu.

12 Upendo ndio msingi wa kutumainiana. Yesu alisema kwamba amri mbili kuu zaidi ni kumpenda Yehova na kumpenda jirani yetu. (Mt. 22:37-39) Upendo wetu kwa Yehova unatuchochea kuiga mfano wake mkamilifu wa kuaminika. Kwa mfano, upendo wetu kuelekea ndugu na dada zetu unatuchochea kutunza siri kuhusu mambo yao ya faragha. Hatungependa kamwe kufunua jambo ambalo litawasababishia madhara, aibu, au maumivu.​—Yoh. 15:12.

13. Unyenyekevu guwesa kutujangati bo tubya twetutumainika?

13 Unyenyekevu utatusaidia tuwe wenye kutumainika. Mkristo ambaye ni mnyenyekevu hajaribu kujitafutia sifa kwa kuwa wa kwanza kufunua habari fulani. (Flp. 2:3) Hajaribu kujionyesha kuwa mtu wa maana kwa kusema kwamba ana habari ambazo ni siri. Unyenyekevu utatuzuia pia tusisambaze habari za kukisia kuhusu mambo ambayo hayajazungumziwa katika Biblia au katika machapisho yetu yanayotegemea Biblia.

14. Sifa ju utambuzi jutujangati bo tubya twetutumainika?

14 Utambuzi utamsaidia Mkristo atofautishe kati ya “wakati wa kunyamaza na wakati wa kuongea.” (Mhu. 3:7) Katika tamaduni fulani kuna msemo huu, “Kuzungumza ni kama fedha, lakini kukaa kimya ni kama dhahabu.” Inamaanisha kwamba kuna nyakati ambazo ni bora kukaa kimya badala ya kuzungumza. Hiyo ndiyo sababu andiko la Methali 11:12 linatushauri hivi: “Mtu mwenye utambuzi wa kweli hukaa kimya.” Fikiria mfano ufuatao. Mara kwa mara, mzee fulani mwenye uzoefu huombwa akasaidie makutaniko mengine ambayo yanakabili matatizo makubwa. Akizungumzia jambo hilo, mzee mwenzake alisema: “Sikuzote yuko makini ili asifunue kamwe habari za siri kuhusu makutaniko mengine.” Sifa ya utambuzi ya mzee huyo imefanya ndugu anaotumikia pamoja nao kwenye baraza la wazee wamheshimu. Wana hakika kwamba hatawafunulia wengine habari zao za siri.

15. Pia mfanu gogulangi jinsi kuba twa anyoofu ekuwesa kwaafanya bangi bututumainia.

15 Unyoofu ni sifa nyingine inayohusiana na kutumainika. Mtu mnyoofu anatumainika kwa sababu tunajua kwamba sikuzote atasema ukweli. (Efe. 4:25; Ebr. 13:18) Kwa mfano, tuseme kwamba ungependa kuboresha uwezo wako wa kufundisha. Basi, unamwomba mtu fulani asikilize unapotoa hotuba kisha atoe mapendekezo yatakayokusaidia kufanya maendeleo. Ni nani ambaye unaweza kumtumaini akupe mapendekezo ya unyoofu? Je, utachagua mtu anayekuambia mambo unayotaka kusikia au anayekuambia ukweli kwa fadhili? Jibu ni wazi. Biblia inasema: “Karipio la wazi ni afadhali kuliko upendo uliofichwa. Majeraha yanayosababishwa na rafiki ni ya uaminifu.” (Met. 27:5, 6) Ingawa huenda mwanzoni tusifurahie jambo ambalo rafiki yetu atatuambia, mwishowe maelezo yake ya unyoofu yatatusaidia.

16. Liandiku la Methali 10:19 likazi bo umuhimu gukujizuia?

16 Kujizuia ni sifa muhimu sana inayotusaidia tuwe watu wanaotumainika. Sifa hiyo itatusaidia kukaa kimya tunaposhawishiwa kufunua jambo la siri tuliloambiwa. (Soma Methali 10:19.) Huenda ikawa vigumu kujizuia tunapotumia mitandao ya kijamii. Tusipokuwa waangalifu, tunaweza wapinzani wanapojaribu kutunasa kwa ujanja ili tufunue habari ambazo zitawahatarisha ndugu na dada zetu. Hilo linaweza kutokea tunapohojiwa na polisi katika nchi ambayo kazi yetu imepigwa marufuku au kuwekewa vizuizi. Tunaweza kutumia kanuni ya ‘kulinda kinywa chetu kwa lijamu’ katika hali kama hizo na nyinginezo. (Zab. 39:1) Iwe tunashughulika na watu wa familia yetu, marafiki, ndugu na dada zetu, au mtu mwingine yeyote, tungependa kuwa wenye kutumainika. Na ili tuwe wenye kutumainika tunahitaji sifa ya kujizuia.

17. Tuwesabo kusangi loho ju kuaminiana mu likutaniko?

17 Tunashukuru sana kwamba Yehova ametuvuta katika undugu uliofanyizwa na watu ambao ni wenye upendo na wenye kuaminika! Tuna jukumu la kujitahidi kuwafanya ndugu na dada zetu watuamini. Sisi binafsi tunapojitahidi kuonyesha kufunua habari za siri bila kukusudia kwa idadi kubwa ya watu. Na baada ya kueneza habari hizo mtandaoni, hatuwezi kudhibiti jinsi zitakavyotumiwa au madhara ambayo zitasababisha. Sifa ya kujizuia itatusaidia pia kukaa kimya upendo, unyenyekevu, utambuzi, unyoofu, na kujizuia, tunachangia roho ya kuaminiana kutanikoni. Tunapaswa kuendelea kusitawisha sifa ya kuaminika. Acheni tuendelee kumwiga Mungu wetu, Yehova, na tuendelee kuthibitisha kwamba sisi ni wenye kuaminika.

NHAMBU 123 Kutii Utaratibu wa Kitheokrasi kwa Ushikamanifu

a Ikiwa tunataka watu wengine watutumaini, ni lazima kwanza tuthibitishe kwamba tunaweza kuaminika. Katika makala hii, tutachunguza kwa nini sifa ya kutumainika ni muhimu sana na ni sifa gani zitakazotusaidia tuwe watu ambao wanaweza kutumainika.

b Tukitambua kwamba mtu fulani kutanikoni ana hatia ya kufanya dhambi nzito, tunapaswa kumhimiza azungumze na wazee. Asipofanya hivyo, ushikamanifu wetu kwa Yehova na kutaniko la Kikristo unapaswa kutuchochea kuripoti jambo hilo kwa wachungaji Wakristo.

c MAELEZO YA PICHA: Mzee hawaambii watu wa familia yake habari za siri kuhusu jambo ambalo ametoka kushughulikia.