Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 38

Ukuwe Mwenye Kutumainika

Ukuwe Mwenye Kutumainika

“Mutu mwenye kutumainika anachunga siri.”​—MEZ. 11:13.

WIMBO 101 Tutumike kwa Umoja

KIFUPI YA HABARI *

1. Mutu mwenye kutumainika ni mutu wa namna gani?

 MUTU mwenye kutumainika ni mutu mwenye anajikazaka kutimiza ahadi yake na mwenye anajikazaka kusema kweli. (Zb. 15:4) Watu wanajua kama wanaweza kumutumainia. Tunapenda ndugu na dada zetu watutumainie. Tunapaswa kufanya nini juu watutumainie?

2. Nini njo itafanya wengine watutumainie?

2 Hatuwezi kukaza wengine watutumainie. Matendo yetu njo itafanya wengine watutumainie. Watu wanasemaka kama kutumainiwa iko sawa vile makuta. Ni nguvu kuipata, lakini ni mwepesi kuipoteza. Yehova anaonyesha kama anastahili kutumainiwa. Sikuzote tunaweza kumutumainia juu “kila jambo lenye anafanya linategemeka.” (Zb. 33:4) Na anapenda tumuige. (Efe. 5:1) Tuchunguze mifano fulani ya watumishi wa Yehova wenye walimuiga Baba yao wa mbinguni na walionyesha kama ni wenye kutumainika. Tutazungumuzia pia sifa tano zenye zinaweza kutusaidia tukuwe wenye kutumainika.

IGA WATUMISHI WA YEHOVA WENYE WALIKUWA WENYE KUTUMAINIKA

3-4. Namna gani nabii Danieli alionyesha kama alikuwa mwenye kutumainika, na mufano wake unapaswa kutuchochea kujiuliza maulizo gani?

3 Nabii Danieli alituachia mufano muzuri sana: Alikuwa mutu mwenye kutumainika. Alikuwa amepelekwa mu uhamisho katika Babiloni. Lakini wakati kidogo tu kisha kufika Babiloni, alionyesha kama alikuwa mutu mwenye kutumainika. Watu walimutumainia hata zaidi, wakati kwa musaada wa Yehova, alifasiria ndoto za Mufalme Nebukadneza wa Babiloni. Wakati fulani, Danieli alipaswa kuambia Mufalme kama Yehova hakupendezwa naye. Ile ni habari yenye Mufalme hakupenda kusikia. Danieli alikuwa na lazima ya uhodari ili kuambia Mufalme ile habari juu Nebukadneza alikuwa mukali sana! (Da. 2:12; 4:20-22, 25) Kisha miaka mingi, Danieli alionyesha tena kama alikuwa mutu mwenye kutumainika wakati alifasiria bila makosa maneno yenye ilikuwa nguvu kuelewa, yenye ilionekana ku ukuta mu nyumba ya mufalme kule Babiloni. (Da. 5:5, 25-29) Kisha, Dario Mumedi na maofisa wake walitambua pia kama Danieli alikuwa na “roho ya pekee ndani yake.” Walikubali kama Danieli “alikuwa mwenye kutumainika na hakuna uzembe wala udanganyifu wenye ungepatikana ndani yake.” (Da. 6:3, 4) Hata watawala wapagani walitambua kama ule muabudu wa Yehova alikuwa mwenye kutumainika!

4 Wakati tunafikiria mufano wa Danieli, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Najulikana namna gani inje ya kutaniko? Najulikana kuwa mutu mwenye anatimizaka kazi yenye anapewa na mwenye watu wanaweza kutumainia?’ Juu ya nini ni jambo ya maana kujiuliza ile maulizo? Juu tunamuletea Yehova sifa wakati tuko wenye kutumainika.

Nehemia alichagua wanaume wenye kutumainika juu ya kutumika kazi ya maana sana (Ona fungu ya 5)

5. Juu ya nini Hanania alijulikana kuwa mutu mwenye kutumainika?

5 Mu mwaka wa 455 M.K.Y., kisha Gavana Nehemia kujenga upya kuta za Yerusalemu, alitafuta wanaume wenye kutumainika, wenye wangesimamia muji. Kati yao, Nehemia alichagua Hanania, mukubwa wa ngome. Biblia inasema kama Hanania alikuwa “mwanaume mwenye kutumainika sana na [mwenye] alimuogopa Mungu wa kweli kuliko wengine wengi.” (Ne. 7:2) Juu alimupenda Yehova na juu alipenda kumufurahisha, ile ilimuchochea Hanania atumike kwa bidii kazi yoyote yenye alipewa. Zile sifa zinaweza pia kutusaidia kuwa wenye kutumainika mu kazi yoyote yenye Yehova anatuomba tufanye.

6. Nini njo inaonyesha kama mutume Paulo alimutumainia rafiki yake Tikiko?

6 Fikiria mufano wa Tikiko, ndugu mwenye mutume Paulo alitumainia. Wakati Paulo alifungwa mu nyumba fulani kule Roma, alimutumainia Tikiko. Alisema kama Tikiko alikuwa “mutumishi muaminifu.” (Efe. 6:21, 22) Juu Paulo alimutumainia, alimutuma apelekee barua zake ndugu wenye kuwa katika Efeso na katika Kolosai na awatie moyo na kuwafariji. Tikiko anatukumbusha wanaume waaminifu na wenye kutumainika wenye wanahangaikia mahitaji yetu ya kiroho leo.​—Kol. 4:7-9.

7. Kuona vile wazee na watumishi wa huduma wa kutaniko yako ni wenye kutumainika kumekufundisha nini?

7 Leo, tunasamini sana kazi ya wazee wetu na watumishi wa huduma wenye kutumainika. Sawa vile Danieli, Hanania, na Tikiko, wanachukua madaraka yao kwa uzito. Kwa mufano, wakati tunaenda ku mukutano wa katikati ya juma, tuko hakika kama kila mutu mwenye iko ku programu alipewa mugao wake. Na wazee wanafurahiaka sana wakati ndugu na dada wenye walipewa migao ku mukutano wanaitayarisha na kuipitisha! Tena, hatusite kualika wanafunzi wetu wa Biblia ku mukutano juu ya kuogopea kama hakutakuwa mutu wa kutoa hotuba ya watu wote. Na tunatumainia kama vichapo vyenye tuko navyo lazima kwa ajili ya mahubiri vitakuwa tayari. Wale ndugu waaminifu wanatuhangaikia muzuri na tunamushukuru sana Yehova! Sasa, namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye kutumainika?

UKUWE MWENYE KUTUMAINIKA KWA KUWEKA SIRI

8. Hata kama tunapendaka kujua hali za wengine, namna gani tunaweza kuonyesha usawaziko? (Mezali 11:13)

8 Tunapendaka ndugu na dada zetu, na tunapendaka kujua hali yao. Lakini, tunapaswa kuonyesha usawaziko kwa kuheshimia mambo yao ya kipekee. Wakristo fulani wa karne ya kwanza walikuwa ‘wanapiga porojo na kujiingiza katika mambo ya watu wengine, wakizungumuza juu ya mambo yenye hawapaswe kuzungumuzia.’ (1 Ti. 5:13) Hatupendi kabisa kuwa vile. Waza mutu fulani anatuambia mambo yake ya kipekee na anatuomba tusiambie wengine. Kwa mufano, dada fulani anaweza kutuambia kama iko na ugonjwa fulani ao iko napambana na jaribu fulani, na anatuomba tusiambie wengine. Tunapaswa kuheshimia mambo yenye anatuomba. * (Soma Mezali 11:13.) Tuzungumuzie sasa ni mu hali gani zingine inaomba kuweka siri.

9. Watu wa familia wanaweza kuonyesha namna gani kama ni wenye kutumainika?

9 Ukuwe mutu mwenye wengine mu familia wanaweza kutumainia. Kila mutu mu familia iko na daraka ya kuchunga mambo ya siri ya familia. Kwa mufano, pengine dada Mukristo anaweza kuwa na tabia fulani yenye inachekeshaka sana bwana yake. Ni muzuri aiambie wengine na kumupatisha haya bibi yake? Bila shaka hapana! Juu anapenda bibi yake, hawezi kupenda kumufanyia jambo fulani yenye itamuumiza. (Efe. 5:33) Vijana wanapendaka wengine wawaheshimie. Wazazi hawapaswe kusahau ile. Hawapaswe kupatisha haya watoto wao kwa kuelezea wengine makosa yao. (Kol. 3:21) Na watoto hawapaswe kuambia wengine mambo yenye inaweza kupatisha haya watu wa familia yao. (Kum. 5:16) Familia itakuwa na umoja kama kila mutu anaepuka kuambia wengine mambo ya kipekee ya familia.

10. Rafiki wa kweli anafanyaka nini wakati anaambiwa habari fulani? (Mezali 17:17)

10 Ukuwe mutu mwenye marafiki wako wanaweza kutumainia. Mu maisha, kuko wakati tunapendaka kuambia rafiki yetu wa karibu namna tuko najisikia kabisa. Wakati fulani, inaweza kuwa nguvu kufanya vile. Pengine hatuzoee kuambia kila mutu mawazo yetu ya ndani, na tunaweza kujisikia mubaya kama tunafikia kujua kuwa rafiki yetu aliambia watu wengine mambo yenye tulimuambia. Lakini tunafurahiaka sana kuwa na rafiki mwenye anachungaka siri! Ni “rafiki wa kweli.”​—Soma Mezali 17:17.

Wazee hawafunuliake watu wa familia yao mambo ya siri ya wengine (Ona fungu ya 11) *

11. (a) Wazee na bibi zao wanaonyesha namna gani kama ni wenye kutumainika? (b) Namna muzee fulani alitenda wakati alikuwa na familia yake kisha kuhangaikia mambo ya siri ya kutaniko inaweza kutufundisha nini? (Ona picha.)

11 Ukuwe mutu mwenye ndugu na dada zako wanaweza kutumainia. Ndugu na dada wanaonaka wazee wenye wanawekaka siri kuwa “mahali pa kujificha kwa sababu ya upepo.” (Isa. 32:2) Tunajua kama tunaweza kuwaambia kila kitu, juu tuko hakika kama hawataambia wengine mambo yetu. Hatuwakaze watuambie mambo yenye wanapaswa kuweka siri. Tena, tunafurahiaka sana bibi za wazee wetu juu hawatafutake bwana zao wawaambie mambo ya siri ya wengine. Ni muzuri kabisa bibi ya muzee asijue mambo ya siri ya ndugu na dada zake. Bibi ya muzee fulani alisema hivi: “Nafurahiaka sana kuona vile bwana yangu haniambiake mambo ya siri ya wale wenye anakutanaka nao mu kazi ya uchungaji ao wale wenye kuwa na lazima ya musaada wa kiroho. Haniambiake hata majina yao. Niko mwenye shukrani sana kuona namna bwana yangu haniambiake mambo ya siri ya wengine. Ile inanisaidiaka nisihangaikie mambo yenye hainihusu. Tena, inafanyaka nijisikie huru kuongea na kila mutu. Na natumaini kama wakati naambia bwana yangu mambo yangu ya kipekee ao magumu yangu, najua pia kama ile nayo hataiambia mutu.” Siye wote tunapendaka kujulikana kuwa watu wenye kutumainika. Ni sifa gani zitatusaidia tukuwe wenye kutumainika? Tuchunguze sifa tano.

SIFA ZENYE ZITAKUSAIDIA UKUWE MWENYE KUTUMAINIKA

12. Fasiria juu ya nini upendo njo sifa ya maana zaidi yenye inaweza kutusaidia tukuwe wenye kutumainika.

12 Upendo njo sifa ya maana zaidi yenye inatusaidia tukuwe wenye kutumainika. Yesu alisema kama amri mbili kubwa zaidi ni kumupenda Yehova na kupenda jirani. (Mt. 22:37-39) Kupenda Yehova kunatuchochea kuwa wenye kutumainika kama yeye. Kwa mufano, kupenda ndugu na dada zetu kunatuchochea tusiambie wengine mambo yao ya siri. Hatupaswe kufunua jambo fulani yenye inaweza kuumiza ao kupatisha haya ndugu ao dada fulani.​—Yoh. 15:12.

13. Namna gani unyenyekevu unatusaidia kuwa wenye kutumainika?

13 Unyenyekevu utatusaidia tukuwe wenye kutumainika. Mukristo munyenyekevu hatafutake kushangaza wengine kwa kuwa wa kwanza kuwaambia jambo fulani. (Flp. 2:3) Hafanyake wengine wawaze kama anajua mambo ya siri yenye haruhusiwe kuambia wengine. Unyenyekevu utatuzuia pia tusiambie watu wengine mawazo yetu kuhusu mambo yenye Biblia ao vichapo vyetu havizungumuzie.

14. Namna gani utambuzi unaweza kutusaidia tukuwe wenye kutumainika?

14 Utambuzi utatusaidia kujua “wakati wa kunyamaza na wakati wa kusema.” (Muh. 3:7) Mu maeneo fulani, watu wanazoea kutumia hii mezali: “Kusema ni feza, lakini kunyamaza ni zahabu.” Ni kusema, kuko wakati ni muzuri zaidi kuikala kimya kuliko kusema. Njo maana Mezali 11:12 inatushauria hivi: “Mutu mwenye utambuzi wa kweli anabakia kimya.” Kwa mufano, wazee wa makutaniko ingine wanazoea kuomba muzee fulani mwenye kuwa na uzoefu mashauri juu ya kujua namna ya kuhangaikia matatizo fulani ya nguvu sana. Muzee mwingine alisema hivi kuhusu ule muzee mwenye uzoefu: “Hafunuake hata kidogo mambo ya siri ya makutaniko ingine.” Juu ule muzee iko na utambuzi, wazee wengine wenye anatumika nao mu kutaniko yake wanamuheshimia. Wako hakika kama hawezi kufunua mambo ya siri ya wengine.

15. Leta mufano wenye kuonyesha namna unyoofu unafanya wengine watutumainie.

15 Unyoofu ni sifa ingine yenye inatusaidia tukuwe wenye kutumainika. Tunatumainiaka mutu munyoofu juu tunajua kama anasemaka kweli. (Efe. 4:25; Ebr. 13:18) Kwa mufano, waza unapenda ufundi wako wa kufundisha ukuwe muzuri zaidi. Kwa hiyo, unaomba mutu fulani asikilize kipindi, ao hotuba yako na akupatie mashauri fulani yenye inaweza kukusaidia. Nani njo utatumainia kama atakupatia shauri ya kweli? Utatumainia mutu mwenye anakuambia mambo yenye unapenda kusikia, ao mutu mwenye kwa busara anakuambia kweli? Jibu iko wazi. Biblia inasema: “Karipio lenye kuwa wazi ni muzuri zaidi kuliko upendo wenye kufichwa. Vidonda vyenye kutokezwa na rafiki ni vya uaminifu.” (Mez. 27:5, 6) Hata kama ku mwanzo haufurahie mashauri yenye kuwa wazi yenye rafiki yako anakupatia, lakini itakuleteaka faida.

16. Kulingana na Mezali 10:19 juu ya nini tunapaswa kujizuia?

16 Kujizuia inafanya wengine watutumainie. Ile sifa inatusaidia tuikale kimya wakati tunataka kufunua mambo ya siri ya wengine. (Soma Mezali 10:19.) Inaweza kuwa nguvu kujizuia wakati tuko tunatumia site za Enternete za kupashana habari. Kama hatuko waangalifu, tunaweza bila kupenda kufunua mambo ya siri kwa watu wengi. Na kisha tu kutia habari fulani ku site za Enternete za kupashana habari, hatuna tena uwezo wa kufanya jambo fulani kuhusu namna wengine wataitumia, ao matatizo yenye ile italeta. Kujizuia kutatusaidia pia tuendelee kubakia kimya wakati wale wenye kutupinga wanajaribu kutufanya tufunue mambo yenye inaweza kutia mu hatari ndugu na dada zetu. Ile inaweza kutokea wakati polisi inatuuliza maulizo mu inchi kwenye kazi yetu imekatazwa ao kutiliwa vizuizi. Mu zile hali na mu hali zingine, tunapaswa ‘kulinda kinywa chetu kwa kitu cha kufunga kinywa.’ (Zb. 39:1) Tunapaswa kujikaza juu watu wa familia yetu, marafiki, ndugu na dada zetu, ao watu wengine, watutumainie. Na juu watutumainie, tuko na lazima ya kujizuia.

17. Tunaweza kufanya nini juu roho ya kutumainiana ikuwe ndani ya kutaniko?

17 Tuko wenye shukrani sana kuona vile Yehova ametuvuta mu familia ya ndugu na dada wenye kuwa na upendo na wenye kutumainika! Siye wote, tuko na daraka ya kufanya ndugu na dada zetu watutumainie. Juu tunajikaza kuonyesha upendo, unyenyekevu, utambuzi, unyoofu, na kujizuia, tunafanya roho ya kutumainiana ikuwe mu kutaniko. Tunapaswa kuendelea kujikaza sana kuonyesha kama tuko watu wenye wengine wanaweza kutumainia. Tumuige basi, Mungu wetu Yehova, na tuendelee kuonyesha kama tuko wenye kutumainika.

WIMBO 123 Tutii Mupango wa Kiteokrasi

^ Kama tunapenda wengine watutumainie, tunapaswa kwanza kuonyesha kama tuko wenye kutumainika. Mu hii habari, tutazungumuzia tena juu ya nini ni jambo ya maana kutumainiana na tutazungumuzia sifa zenye zinaweza kutusaidia tukuwe watu wenye wengine wanaweza kutumainia.

^ Ikiwa tunajua kama mutu fulani mu kutaniko amefanya zambi nzito, tunapaswa kumuomba aende kuona wazee juu wamusaidie. Kama hafanye vile, ushikamanifu wetu kwa Yehova na kwa kutaniko ya Kikristo utatuchochea kuenda kuambia wazee ile jambo.

^ MAFASIRIO YA PICHA: Muzee moya haambie familia yake mambo ya siri yenye alikuwa amehangaikia mu kazi yake ya uchungaji.