Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 40

‘Kuleta Watu Wengi Kwenye Haki’

‘Kuleta Watu Wengi Kwenye Haki’

“Wenye wanaleta watu wengi kwenye haki watangaa kama nyota, milele na milele.”​—DA. 12:3.

WIMBO 151 Yehova Ataita

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni mambo gani ya muzuri yenye tutajionea mu kipindi ya Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo?

 SIKU yenye ufufuo utaanza ku dunia mu kipindi ya Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo itakuwa siku ya furaha sana! Wale wote wenye wamepoteza wapendwa wao wako na hamu sana ya kuwaona tena. Yehova naye iko na hamu sana ya kuwaona tena. (Yob. 14:15) Wazia furaha yenye itakuwa ku dunia wakati kila mutu ataona tena mupendwa wake. Vile tulijifunza mu habari yenye kutangulia, majina ya “wenye haki” imeandikwa mu kitabu ya uzima. Kwa hiyo, watapata “ufufuo wa uzima.” (Mdo. 24:15; Yoh. 5:29) Pengine wengi kati ya wapendwa wetu watafufuliwa kisha tu Armagedoni. * Zaidi ya ile, wale “wenye hawako wenye haki,” sawa vile wale wenye hawakupata kabisa nafasi ya kumujua Yehova ao kumutumikia kwa uaminifu mbele wakufe, watapata “ufufuo wa hukumu.”

2-3. (a) Sawa vile Isaya 11:9, 10 inaonyesha, kutakuwa kazi gani kubwa ya kufundisha watu yenye haiyafanyikaka? (b) Tutazungumuzia maulizo gani mu hii habari?

2 Wale wote wenye watafufuliwa watakuwa na lazima ya kufundishwa. (Isa. 26:9; 61:11) Njo maana, Ufalme wa Mungu utaanzisha kazi kubwa ya kufundisha watu yenye haiyafanyikaka. (Soma Isaya 11:9, 10.) Juu ya nini? Juu wenye hawako wenye haki wenye watafufuliwa watakuwa na lazima ya kujifunza juu ya Yesu Kristo, Ufalme, bei ya ukombozi, jina ya Yehova, na juu ya nini yeye tu njo iko na haki ya kutawala. Hata wenye haki watakuwa na lazima ya kujifunza juu ya mambo yenye Yehova amefundisha pole kwa pole watu wake kuhusu mipango yenye iko nayo juu ya dunia. Wamoja kati ya wale waaminifu walikufaka zamani sana mbele kazi ya kuandika Biblia imalizike. Wenye hawako wenye haki na wenye haki, wote watakuwa na mambo mingi ya kujifunza.

3 Mu hii habari, tutazungumuzia maulizo yenye kufuata: Ile kazi kubwa ya kufundisha watu itafanywa namna gani? Itakuwa namna gani kama mutu anatumikisha mambo yenye atafundishwa? Itakuwa namna gani kama mutu hatumikishe mambo yenye atafundishwa? Majibu ya ile maulizo ni ya maana sana kwetu leo. Sawa vile tutaona, maunabii fulani yenye kufurahisha yenye kupatikana mu kitabu ya Danieli na Ufunuo itatusaidia kuelewa muzuri zaidi namna mambo itakuwa wakati watu watafufuliwa. Tuzungumuzie kwanza mambo fulani yenye kufurahisha yenye kuwa mu Danieli 12:1, 2.

“WALE WENYE WAMELALA KATIKA MAVUMBI . . . WATAAMUKA”

4-5. Danieli 12:1 inasema nini kuhusu siku za mwisho?

4 Soma Danieli 12:1. Kitabu ya Danieli inaonyesha mambo ya kufurahisha yenye itatokea mu siku za mwisho na namna itafuatana. Kwa mufano, Danieli 12:1 inaonyesha kama Mikaeli, mwenye ni Yesu Kristo, iko “anasimama kwa ajili ya watu [wa Mungu].” Ile maneno ya unabii ilianza kutimia mu 1914 wakati Yesu aliwekwa kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu mbinguni.

5 Lakini, Danieli aliambiwa pia kama Yesu ‘angesimama’ mu “wakati wa taabu yenye haijatokea tangu kuwapo kwa taifa lolote mupaka wakati huo.” “Wakati wa taabu” njo wakati ya “taabu kubwa” yenye kuzungumuziwa mu Matayo 24:21. Yesu anasimama, maana yake, anapigania watu wa Mungu, ku mwisho wa wakati ya taabu, ni kusema, ku Armagedoni. Watu wa Mungu wenye Yesu atapigania njo wenye kitabu ya Ufunuo inaita “kundi kubwa [la] wale wenye wanatoka katika ile taabu kubwa.”​—Ufu. 7:9, 14.

6. Nini njo itatokea kisha kundi kubwa kuokoka taabu kubwa? Fasiria. (Ona pia mu hii gazeti habari “Maulizo ya Wasomaji Wetu” kuhusu ufufuo wenye utafanyika ku dunia.)

6 Soma Danieli 12:2. Ni mambo gani itatokea kisha kundi kubwa kuokoka taabu kubwa? Mbele, tulielewa kama Danieli 12:2 inazungumuzia ufufuo wa mbinguni ao namna kazi yetu ya kuhubiri ilifanywa tena kwa bidii kisha wapinzani kujaribu kuizuia mu 1918. * Lakini sasa, tunaelewa kama ile maneno inazungumuzia njo ufufuo wa wafu wenye utafanyika mu dunia mupya yenye iko nakuya. Maneno “mavumbi” mu Danieli 12:2 inatumiwa pia mu Yobu 17:16, na yote mbili inamaanisha “kaburi.” Juu mavumbi inamaanisha kaburi, tunaweza kusema kama Danieli 12:2 inapaswa kuwa inazungumuzia ufufuo wenye utatokea ku mwisho wa siku za mwisho na kisha vita ya Armagedoni.

7. (a) Danieli 12:2 inamaanisha nini wakati inasema kama watu fulani watafufuliwa juu wapate “uzima wa milele”? (b) Juu ya nini ufufuo wao utakuwa “ufufuo wa muzuri zaidi”?

7 Sasa, Danieli 12:2 inamaanisha nini wakati inasema kama watu fulani watafufuliwa juu wapate “uzima wa milele”? Inamaanisha kama wale wenye watafufuliwa na kufikia kumujua Mungu, ao kuendelea kujikaza ili kumujua muzuri zaidi, na kutii Yehova na Yesu mu kipindi ya miaka 1 000 watapata ku mwisho uzima wa milele. (Yoh. 17:3) Utakuwa “ufufuo wa muzuri zaidi” kuliko ufufuo wenye ulifanyikaka zamani. (Ebr. 11:35) Juu ya nini? Juu wale wenye walifufuliwaka zamani walikufaka tena.

8. Danieli 12:2 inamaanisha nini wakati inasema kama watu fulani watafufuliwa juu wapate “haya na zarau ya milele”?

8 Lakini, haiko wote wenye watafufuliwa njo watakubali kufundishwa na Yehova. Unabii wa Danieli unasema kama watu fulani watafufuliwa juu wapate “haya na zarau ya milele.” Juu watamuasi Yehova, majina yao haitaandikwa mu kitabu ya uzima na hawatapata uzima wa milele. Lakini, watapata “zarau ya milele,” ni kusema, wataharibiwa. Kwa hiyo, Danieli 12:2 inazungumuzia mambo yenye itafikia ku mwisho wale wote wenye watafufuliwa ikitegemea mambo yenye watafanya kisha kufufuliwa. * (Ufu. 20:12) Wamoja watapata uzima wa milele; wengine hapana.

‘KULETA WATU WENGI KWENYE HAKI’

9-10. Ni jambo gani ingine itatokea kisha taabu kubwa, na nani njo “watangaa kama mwangaza wa mbinguni”?

9 Soma Danieli 12:3. Ni jambo gani ingine itatokea kisha “wakati wa taabu”? Zaidi ya mambo yenye inazungumuziwa mu Danieli 12:2, mustari wa 3 unazungumuzia jambo fulani yenye itatokea kisha taabu kubwa. Unaonyesha kama “wenye kuwa na ufahamu watangaa kama mwangaza wa mbinguni.”

10 Wale “wenye kuwa na ufahamu [wenye] watangaa kama mwangaza wa mbinguni” njo wanani? Tunapata jibu mu maneno ya Yesu yenye kupatikana mu Matayo 13:43: “Wakati huo wale wenye haki watangaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao.” Mu mistari yenye kutangulia ile andiko, Yesu alikuwa nazungumuzia “wana wa Ufalme,” ni kusema, ndugu zake watiwa-mafuta wenye watatumika pamoya naye katika Ufalme wa mbinguni. (Mt. 13:38) Kwa hiyo, ni wazi kama Danieli 12:3 inazungumuzia watiwa-mafuta na kazi yenye watafanya mu kipindi ya Utawala wa Miaka Elfu.

Wale 144 000 watatumika pamoya na Yesu Kristo ili kuongoza kazi ya kufundisha watu yenye itafanywa mu kipindi ya miaka 1 000 (Ona fungu ya 11)

11-12. Ni kazi gani yenye wale 144 000 watafanya mu kipindi ya miaka 1 000?

11 Namna gani watiwa-mafuta wataleta “watu wengi kwenye haki”? Watafanya vile kwa kutumika pamoya na Yesu Kristo ili kuongoza kazi ya kufundisha watu yenye itafanywa hapa ku dunia mu kipindi ya miaka 1 000. Wale 144 000 watakuwa wafalme na pia makuhani. (Ufu. 1:6; 5:10; 20:6) Kwa hiyo, watasaidia “kuponyesha mataifa,” ni kusema, pole kwa pole watasaidia wanadamu wafikie kuwa wakamilifu. (Ufu. 22:1, 2; Eze. 47:12) Itakuwa furaha sana kwa watiwa-mafuta kufanya vile!

12 Wale “watu wengi” wenye wataletwa kwenye haki ni wanani? Ni wale wenye watafufuliwa, wale wenye wataokoka Armagedoni, na pia watoto wenye wanaweza kuzaliwa mu dunia mupya. Ku mwisho wa miaka 1 000, watu wote ku dunia watakuwa wakamilifu. Kwa hiyo, ni wakati gani majina yao itaandikwa kwa lote na bike mu kitabu ya uzima, hapana na kreyo?

JARIBU YA MWISHO

13-14. Watu wote wakamilifu wenye watakuwa ku dunia watakuwa na lazima ya kufanya nini mbele wapate uzima wa milele?

13 Tusisahau kama kuwa tu mukamilifu haimaanishe kama mutu atapata mara moya uzima wa milele. Fikiria mufano wa Adamu na Eva. Walikuwa wakamilifu, lakini walipaswa kuonyesha kama wataendelea kumutii Yehova mbele awapatie uzima wa milele. Jambo ya kuhuzunisha, hawakumutii Mungu.​—Ro. 5:12.

14 Halafu wale wenye watakuwa ku dunia ku mwisho wa miaka 1 000? Wote watakuwa wakamilifu. Lakini, wale watu wote wakamilifu wataunga kabisa mukono utawala wa Yehova milele? Ao wamoja watakuwa sawa vile Adamu na Eva, wenye hata kama walikuwa wakamilifu, hawakumutii Mungu? Itaomba ile maulizo ijibiwe. Lakini, namna gani?

15-16. (a) Ni wakati gani wanadamu wote watapewa nafasi ya kuonyesha kama wanaunga mukono utawala wa Yehova? (b) Mambo itakuwa namna gani kwa wale wenye wataasi wakati ya jaribu ya mwisho, na kwa wale wenye wataishinda?

15 Shetani atafungwa kwa miaka 1 000. Mu ile kipindi, hatapotosha mutu yeyote. Lakini, ku mwisho wa miaka 1 000, Shetani atafunguliwa. Kisha, atajaribu kudanganya wanadamu wakamilifu. Mu ile kipindi, wanadamu wote wakamilifu ku dunia watakuwa na nafasi ya kuonyesha kama wanaheshimia jina ya Mungu na kama wanaunga mukono utawala wake. (Ufu. 20:7-10) Mambo yenye mutu atafanya ile wakati njo itaonyesha kabisa kama jina yake inastahili kuandikwa kwa lote mu kitabu ya uzima.

16 Biblia inatuambia kama watu fulani watakatala utawala wa Yehova, sawa vile Adamu na Eva. Nini njo itawapata? Ufunuo 20:15 inatuambia hivi: “Kila mutu mwenye hakupatikana ameandikwa katika kile kitabu cha uzima alitupwa ndani ya lile ziwa la moto.” Ni kusema, wale waasi wataharibiwa kabisa milele. Lakini, wanadamu wengi wakamilifu watashinda ile jaribu ya mwisho. Kisha, majina yao itaandikwa kwa lote mu kitabu ya uzima.

MU “WAKATI WA MWISHO”

17. Ni mambo gani yenye Danieli aliambiwa yenye ingetokea wakati yetu? (Danieli 12:4, 8-10)

17 Inafurahisha sana kufikiria mambo yenye itatokea kule mbele! Lakini pia, malaika alimuambia Danieli habari fulani ya maana kuhusu wakati yetu, ni kusema, “wakati wa mwisho.” (Soma Danieli 12:4, 8-10; 2 Ti. 3:1-5) Ule malaika alimuambia Danieli hivi: “Ujuzi wa kweli utakuwa mwingi.” Ni kusema, watu wa Mungu wangeelewa muzuri zaidi maneno ya unabii wa Danieli. Malaika aliongezea kama mu hii wakati “waovu watatenda kwa uovu, na hakuna muovu yeyote mwenye ataelewa.”

18. Hivi karibuni waovu watapatwa na nini?

18 Leo, inaweza kuonekana sawa vile waovu hawako napata malipizi ya matendo yao ya uovu. (Mal. 3:14, 15) Lakini hivi karibuni Yesu atahukumu wanadamu. Ataamua nani njo mbuzi, na nani njo kondoo. (Mt. 25:31-33) Waovu hawataokoka taabu kubwa, na hawatafufuliwa ili kuishi mu dunia mupya. Majina yao haitakuwa mu “kitabu cha kumbukumbu,” chenye Malaki 3:16 inazungumuzia.

19. Sasa njo wakati ya kufanya nini, na juu ya nini? (Malaki 3:16-18)

19 Sasa njo wakati ya kuonyesha kama hatuko waovu. (Soma Malaki 3:16-18.) Yehova iko nakusanya wale wenye anaona kuwa “mali ya pekee,” ao wale wenye anaona kuwa wa maana sana kwake. Tunapenda kabisa kuwa kati yao.

Itakuwa jambo ya kufurahisha sana kuona Danieli, wapendwa wetu, na watu wengine wengi wenye ‘watasimama’ juu wapewe fungu yao mu dunia mupya! (Ona fungu ya 20)

20. Mungu alimuahidi Danieli nini, na juu ya nini unachunga kwa hamu utimizo wa ile ahadi?

20 Kusema kweli, tunaishi mu kipindi ya maana sana. Lakini, mambo ingine ya kushangaza inakaribia kutokea. Karibuni tutajionea uharibifu wa waovu wote. Kisha pale, tutajionea utimizo wa hii ahadi yenye Yehova alimuahidi Danieli: “Utasimama kwa ajili ya fungu lako kwenye mwisho wa zile siku.” (Da. 12:13) Unachunga kwa hamu wakati yenye Danieli pamoya na wapendwa wako ‘watasimama’ tena? Kama ni vile, ufanye yako yote juu ya kuwa muaminifu sasa. Ukifanya vile, jina yako itabakia mu kitabu ya uzima ya Yehova.

WIMBO 80 Uonje na Uone Vile Yehova Ni Mwema

^ Hii habari iko na mafasirio ya mupya kuhusu kazi kubwa ya kufundisha watu yenye kuzungumuziwa mu Danieli 12:2, 3. Tutaona ni wakati gani ile kazi itafanywa, na wanani njo wataifanya. Tutaona pia namna ile kazi kubwa ya kufundisha itatayarisha watu kwa ajili ya jaribu ya mwisho yenye itatokea ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo.

^ Inawezekana wale wenye walikufa na wako waaminifu mu siku za mwisho njo wenye wataanza kufufuliwa. Kisha, wale wenye walikufaka zamani watafufuliwa, kizazi kisha kizazi. Kama vile njo mambo itakuwa, ni kusema, kila kizazi itakaribisha wale wenye walikuwa najuana nao. Ikuwe mambo itakuwa namna gani, Maandiko inasema kama wale wenye watafufuliwa juu ya kuenda mbinguni, kila mumoja atafufuliwa “kwa wakati wake mwenyewe.” Njo maana, tunaweza kusema kama wale wenye watafufuliwa ku dunia watafufuliwa pia kila mumoja kwa wakati wake mwenyewe.​—1 Ko. 14:33; 15:23.

^ Hii ni mafasirio ya mupya. Inarekebisha mambo yenye ilitolewa mu kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! sura ya 17, na mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 7, 1987, uku. 21-23.

^ Lakini, maneno “wenye haki” na “wenye hawako wenye haki” yenye kupatikana mu Matendo 24:15 na maneno “wale wenye walitenda mambo ya muzuri” na “wale wenye walizoea kutenda mambo maovu” yenye kupatikana mu Yohana 5:29 inazungumuzia mambo yenye wale wenye watafufuliwa walifanyaka mbele wakufe.