Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

2 | ‘Faraja Kutoka Kwenye Maandiko’

2 | ‘Faraja Kutoka Kwenye Maandiko’

BIBLIA INASEMA HIVI: “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha, ili kupitia uvumilivu wetu na kupitia faraja kutoka kwa Maandiko tuwe na tumaini.”​—WAROMA 15:4.

Inamaanisha Nini?

Biblia ina mawazo yenye kufariji yanayotusaidia kupata nguvu na uvumilivu, tunapokabiliana na mawazo yasiyofaa. Pia, Biblia inatuahidi kwamba hivi karibuni maumivu ya kihisia yataisha.

Hilo Linaweza Kutusaidiaje?

Sisi sote huhisi huzuni nyakati fulani; lakini wale wenye mshuko moyo au mahangaiko huenda wakahisi maumivu ya kihisia wakati wote. Biblia inaweza kuwasaidiaje?

  • Biblia ina mawazo mengi mazuri yanayoweza kuchukua nafasi ya mawazo mabaya. (Wafilipi 4:8) Inaweza kujaza akili zetu mawazo yenye kufariji na yanayotuliza, ambayo yatatusaidia kudhibiti hisia zetu.​—Zaburi 94:18, 19.

  • Biblia inaweza kutusaidia tuache kufikiri kwamba hatufai.​—Luka 12:6, 7.

  • Mistari mingi ya Biblia inatuhakikishia hatuko peke yetu na kwamba Mungu, Muumba wetu, anaelewa kikamili hisia zetu.​—Zaburi 34:18; 1 Yohana 3:19, 20.

  • Biblia inaahidi kwamba Mungu atatuondolea kumbukumbu mbaya. (Isaya 65:17; Ufunuo 21:4) Tunaposumbuliwa na mawazo na hisia zenye kuumiza, ahadi hiyo inaweza kutupatia nguvu za kuvumilia.