Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 1

Ukuwe Hakika Kama ‘Neno la Mungu Ni Kweli’

Ukuwe Hakika Kama ‘Neno la Mungu Ni Kweli’

ANDIKO YETU YA MWAKA WA 2023: “Chanzo kabisa cha neno lako ni kweli.”​—ZB. 119:160.

WIMBO 96 Biblia Ni Kitabu ya Maana Sana

KIFUPI YA HABARI a

1. Juu ya nini watu wengi leo hawatumainie Biblia?

 WATU wengi leo hawajue watumainie nani. Hawako hakika kama watu wenye wanaheshimia, sawa vile watu wa politike, wanasayansi na wafanyabiashara wanawahangaikia kabisa. Zaidi ya ile, hawaheshimie viongizi wa dini wenye wanasema kama wao ni Wakristo. Njo maana hawatumainie Biblia, kitabu yenye wale viongizi wa dini wanasema kama wanafuata.

2. Kulingana na Zaburi 119:160, tunapaswa kuwa hakika na nini?

2 Siye watumishi wa Yehova tuko hakika kama Mungu ni “Mungu wa ukweli” na kama anatutakiaka mambo ya muzuri. (Zb. 31:5; Isa. 48:17) Tunajua kama tunaweza kutumainia mambo yenye tunasoma mu Biblia juu “chanzo kabisa cha neno [la Mungu] ni kweli.” b (Soma Zaburi 119:160.) Tunakubaliana na hii mambo yenye mutu moya mwenye elimu ya Biblia aliandika: “Hakuna jambo yenye Mungu amesema yenye ni ya uongo ao yenye haitakosa kutimia. Watu wa Mungu wanaweza kutumainia mambo yenye anasema juu wanatumainia Mungu mwenye aliisema.”

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Namna gani tunaweza kusaidia wengine watumainie Neno ya Mungu sawa vile siye? Tutazungumuzia sababu tatu zenye zinafanya tutumainie Biblia. Tutaona kama mambo yenye Biblia inasema haikubadilishwa, tutaona vile maunabii ya Biblia ilitimia, na namna Biblia iko na nguvu ya kubadilisha maisha ya watu.

HAKUNA MUTU MWENYE ALIWEZA KUBADILISHA UJUMBE WA BIBLIA

4. Juu ya nini watu fulani wanawaza kama Biblia imebadilishwa?

4 Yehova Mungu alitumia wanaume waaminifu 40 ili kuandika Biblia. Lakini, hakuna hata moya kati ya maandishi ya kwanza kwanza yenye iko leo. c Hata vile, tuko njo na kopi. Ile inafanya watu fulani wajiulize ikiwa mambo yenye tunasoma mu Biblia leo inapatana kabisa na ile maandishi ya kwanza kwanza. Ulishakajiuliza namna gani tunaweza kuwa hakika kama ile maandishi ya kwanza kwanza inapatana na ile yenye tuko nayo leo?

Watu wenye walizoezwa ili kufanya kopi ya Maandiko ya Kiebrania walikuwa waangalifu sana juu kopi zao za Neno ya Mungu zisikuwe na makosa (Ona habari ya kujifunza ya 1, fungu ya 5)

5. Namna gani kopi za Maandiko ya Kiebrania zilifanywa? (Ona picha ku jalada.)

5 Juu ya kulinda ujumbe wa Biblia, Yehova aliambia watu wafanye kopi ya ule ujumbe. Aliambia Waisraeli wajifanyie kopi za Sheria yenye kuandikwa na alichagua Walawi ili wafundishe watu ile Sheria. (Kum. 17:18; 31:24-26; Ne. 8:7) Kisha Wayahudi kutoka mu uhamisho mu Babiloni, watu wenye walizoezwa ili kufanya kopi walianza kufanya kopi mingi za Maandiko ya Kiebrania. (Ezr. 7:6, maelezo ya chini.) Wale wanaume walikuwa waangalifu. Ku mwisho, walianza kuhesabia maneno na herufi juu ya kuhakikisha kama hawakukosea wakati walikuwa wanafanya kopi. Lakini, juu hawakuwa wakamilifu, makosa kidogo iliingia mu kopi za Biblia zenye walifanya. Hata vile, kopi za mingi za ileile maandishi zilifanywa. Ile njo ilisaidia ile makosa ipatikane kisha. Namna Gani?

6. Ni nini yenye inaweza kusaidia kutambua makosa yenye wale wenye walifanya kopi za Biblia walifanya?

6 Leo watu wenye elimu wanajua njia ya muzuri ya kutambua makosa yenye ilifanywa na wale wenye walifanya kopi za Maandishi ya Biblia. Tukamate mufano: Wazia wanaume 100 wanaambiwa wafanye kopi ya Maandishi yenye kuwa ku ukurasa moya. Mumoya kati ya wale wanaume anafanya kosa kidogo mu kopi yake. Njia moya ya kusaidia kutambua ile kosa ni kulingalisha kopi yake na kopi za wale wengine. Vilevile, wakati watu wenye elimu wanalinganisha maandishi mbalimbali ya Biblia, wanafikia kutambua makosa yenye pengine mutu mwenye alifanya kopi ya maandishi ya Biblia alifanya ao mambo fulani yenye pengine alitosha.

7. Nini inaonyesha kama wale wenye walifanya kopi za Maandishi ya Biblia walikuwa waangalifu sana?

7 Wale wenye walifanya kopi za maandishi ya Biblia walijikaza sana ili kopi zao zisikuwe na makosa. Tuzungumuzie mufano moya wenye unaonyesha ile. Maandishi ya zamani kabisa yenye kuwa na Maandiko yote ya Kiebrania ilifanywa mu 1008 ao 1009 K.K.Y. Inaitwa Kodeksi ya Leningrad. Lakini, hakuyapita siku mingi wachunguzi walivumbula maandishi mingi ya Biblia na sehemu za maandishi ya Biblia zenye zilifanywa miaka 1 000 hivi mbele Kodeksi ya Leningrad ifanywe. Mutu anaweza kuwaza kama kisha kufanya kopi ya ile maandishi tena na tena kwa zaidi ya miaka 1,000, mambo yenye kuandikwa mu Kodeksi ya Leningrad itakuwa tofauti sana na ile maandishi ya zamani. Lakini mambo haiko vile. Kisha wachunguzi kulinganisha maandidishi ya zamani na ya sasa walivumbula kama kulikuwa tofauti kidogo mu maneno yenye ilitumiwa. Hata vile, ujumbe wa Biblia haukubadilishwa.

8. Kuko tofauti gani kati ya kopi za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo na kopi za vitabu vingine vya zamani?

8 Wakristo wa kwanza kwanza walifanya pia kopi za Maandiko ya Kiebrania. Walifanya kwa uangalifu kopi za vitabu 27 vya Maandiko ya Kigiriki zenye walikuwa natumia ku mikutano yao na mu kazi ya kuhubiri. Kisha kulingalisha maandishi ya Maandiko ya Kigiriki na vitabu vingine vya ileile wakati, muchunguzi moya alisema hivi : “Kwa ujumla, leo kopi za Maandiko ya Kigiriki ni za mingi kuliko kopi za vile vitabu vingine.” Kitabu Anatomy of the New Testament inasema hivi: “Tuko hakika kama hakuna tofauti kati ya mambo yenye tunasoma leo mu tafsiri ya muzuri [ya Maandiko ya Kigiriki] na ile yenye waandikaji wa zamani waliandika.”

9. Isaya 40:8 inasema jambo gani ya kweli kuhusu Neno ya Mungu?

9 Kwa miaka mingi wale wenye walifanya kopi ya maandishi ya Biblia walijikaza kuifanya kwa uangalifu. Njo maana leo tuko nasoma na kujifunza Biblia yenye haina makosa. d Bila shaka, Yehova njo aliongoza mambo ili ujumbe wenye kuwa mu Neno yake usibadilishwe. (Soma Isaya 40:8.) Lakini, wengine wanaweza kusema kama hata kama ujumbe wa Biblia haukubadilishwa, ile haionyeshe kabisa kama iliongozwa na roho ya Mungu. Kwa hiyo, tuzungumuzie sasa mambo yenye inahakikisha kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu.

MAUNABII YA BIBLIA NI YA KWELI

Left: C. Sappa/DeAgostini/Getty Images; right: Image © Homo Cosmicos/Shutterstock

Maunabi yenye kuwa mu Biblia ilitimiaka zamani na iko natimia leo (Ona fungu ya 10-11) f

10. Ni unabii gani wenye ulitimia wenye unahakikisha kama maneno yenye kuwa mu 2 Petro 1:21 ni ya kweli? (Ona picha.)

10 Mu Biblia muko maunabii mingi yenye ilitimia. Maunabii fulani iliandikwa na ikatimia kisha miaka mingi kupita. Historia inahakikisha kama ile maunabii ilitimia kabisa. Ile haitushangaze juu tunajua kama ile maunabii yote yenye kuwa mu Biblia inatoka kwa Yehova. (Soma 2 Petro 1:21.) Fikiria unabii kuhusu kuanguka kwa muji wa zamani wa Babiloni. Mu karne ya munane M.K.Y., Yehova aliongoza nabii Isaya atabiri kama muji wenye nguvu wa Babiloni utakamatwa. Alitaya na mutu wa kukamata ule muji, ni kusema, Koreshi, na alionyesha waziwazi namna ule muji ungekamatwa. (Isa. 44:27–45:2) Alitabiri pia kama Babiloni itaharibiwa na haitaikaliwa tena. (Isa. 13:19, 20) Ni vile mambo ilikuwa kabisa. Wamedi na Waajemi walikamata muji wa Babibloni mu mwaka wa 539 M.K.Y. Leo, fasi kwenye kulikuwa ule muji kuko tu mabomoko.​—Ona video Biblia Ilisemaka Kama Babiloni Itaharibiwa mu kitabu Furahia Maisha Milele! ya kielektroniki, somo ya 03, nukta ya 5.

11. Fasiria namna Danieli 2:41-43 iko natimia leo.

11 Maunabii yenye kuwa mu Biblia haikutimiaka tu zamani; iko pia natimia leo. Kwa mufano, fikiria unabii wa Danieli kuhusu serikali kubwa ya Uingereza na Amerika. (Soma Danieli 2:41-43.) Ule unabii ulionyesha bila kukosea kama serikali ya Uingereza na Amerika itakuwa ‘yenye nguvu sehemu moja’ sawa vile chuma na “zaifu sehemu ile ingine” sawa vile udongo. Ni vile mambo iko leo. Uingereza na Amerika walionyesha kama wako nguvu sawa vile chuma kwa kuongoza mambo ili kupata ushindi juu ya Vita Mbili vya Ulimwengu na kwa kuendelea kujifanyia majeshi yenye nguvu. Lakini, wakaaji wa zile inchi wamefanya pia ile serikali ikuwe zaifu. Wanafanya vile kwa kuunda vikundi vya kutetea haki za wafanyakazi, wanafanya kampanye za kutetea haki za wanainchi, na wanaunda vikundi vya kupigania uhuru. Hakuyapita masiku mingi tangu muchunguzi moya wa mambo ya politike alisema hivi: “Leo, hakuna inchi ya kidemokrasia mu dunia yenye kugawanyika sana mu mambo ya politike sawa vile Amerika.” Na sehemu ya pili ya ile serikali kubwa, ni kusema Uingereza, imegawanyika zaidi sana mu miaka ya hivi karibuni juu mu Uingereza watu hawapatane kuhusu uhusiano wenye wanapaswa kuwa nao na inchi za umoja wa Ulaya. Ile migawanyiko imefanya ikuwe nguvu kwa serikali kubwa ya Uingereza na Amerika kutimiza muzuri maamuzi yao.

12. Maunabii ya Biblia inatusaidia tukuwe hakika na nini?

12 Maunabii mingi yenye kuwa mu Biblia yenye tayari imetimia inatusaidia tukuwe hakika kabisa kama ahadi za Mungu zitatimia. Tunajisikia sawa vile muandikaji wa zaburi mwenye alimuambia Yehova hivi: “Ninatamani sana wokovu wako, kwa maana neno lako ni tumaini langu.” (Zb. 119:81) Kupitia Biblia, Yehova ametupatia “wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini.” (Yer. 29:11) Ni ahadi za Yehova njo zinatupatia tumaini, hapana mambo yenye watu wako najikaza kufanya juu maisha ikuwe muzuri. Tuendelee basi kutumainia Neno ya Mungu kwa kujifunza kwa uangalifu maunabii yenye kuwa ndani.

MASHAURI YA BIBLIA IKO NASAIDIA WATU WENGI SANA

13. Kulingana na Zaburi 119:66, 138, ni jambo gani ingine yenye inafanya tutumainie Biblia?

13 Jambo ingine yenye inafanya tutumainie Biblia ni juu iko nasaidia watu wakati wanafuata mashauri yake. (Soma Zaburi 119:66, 138.) Kwa mufano, bibi na bwana wenye walikuwa karibu kuvunja ndoa, sasa wako na ndoa yenye furaha juu walijaribu kufuata mashauri ya Biblia. Watoto wao wako na furaha ya kuwa mu familia ya Kikristo pamoya na wazazi wenye wanawapenda na kuwahangaikia.​—Efe. 5:22-29.

14. Zungumuzia mufano wenye unaonyesha kama kutumikisha mashauri ya Biblia kunaweza kubadilisha maisha ya watu.

14 Hata watu wenye walikuwa nafanya mambo ya mubaya sana walishabadilisha maisha yao kwa kufuata mashauri yenye hekima ya Biblia. Fikiria namna mashauri ya Biblia ilisaidia mufungwa fulani mwenye kuitwa Jack. e Yeye njo alikuwa mwenye jeuri sana kupita wafungwa wote wenye walihukumiwa hukumu ya kifo. Lakini siku moya alisikiliza wakati mutu fulani alikuwa anafundishwa Biblia. Ndugu wenye walikuwa wanaongoza ile funzo walikuwa wenye fazili. Ile ilimugusa sana Jack, na akaamua kuanza pia kujifunza Biblia. Wakati Jack alianza kutumikisha mambo yenye alikuwa najifunza, alibadilisha tabia yake na kuanza kutendea wengine kwa fazili. Ku mwisho akakuwa muhubiri na akabatizwa. Alikuwa nazungumuza kwa bidii na wafungwa wenzake kuhusu Ufalme wa Mungu, na alisaidia watu ine hivi kati yao wajifunze Biblia. Wakati siku yenye alipaswa kuuwawa ilifika, Jack alikuwa alishabadilika. Mumoya kati ya wanasheria wake alisema hivi: “Jack haiko tena uleule mwenye nilijuaka miaka 20 yenye ilipita. Mafundisho ya Mashahidi wa Yehova ilibadilisha maisha yake.” Hata kama Jack aliuwawa, mufano wake unaonyesha kabisa kama tunaweza kutumainia Neno ya Mungu na kama iko na nguvu ya kubadilisha maisha ya watu.​—Isa. 11:6-9.

Mashauri yenye kuwa mu Biblia ilishabadilisha maisha ya watu wengi wa desturi mbalimbali (Ona fungu ya 15) g

15. Namna gani kutumikisha mashauri ya Biblia kunafanya watu wa Yehova wakuwe tofauti? (Ona picha.)

15 Watu wa Yehova wako na umoja juu wanatumikishaka mashauri ya Biblia. (Yoh. 13:35; 1 Ko. 1:10) Amani na umoja wenye tuko nao iko wazi kabisa juu leo mu dunia watu wengi ni wenye kugawanyika kwa sababu ya politike, rangi ya ngozi, na hali ya maisha. Kijana mwenye kuitwa Jean aliguswa sana wakati aliona umoja kati ya watu wa Yehova. Alikomalia mu inchi fulani ya Afrika. Wakati kulitokea vita aliingia mu kazi ya jeshi, lakini kisha alikimbilia mu inchi fulani ya karibu. Kule alikutana na Mashahidi wa Yehova. Jean anasema hivi: “Nilijifunza kama watu wenye kuwa mu dini ya kweli hawajiingizake mu mambo ya politike na hawagawanyike, wanapendana.” Anasema tena hivi: “Nilitoa maisha yangu ili kupigania inchi. Lakini kweli yenye nilijifunza mu Biblia ilinichochea nitoe maisha yangu ili kumutumikia Yehova.” Jean alibadilika kabisa. Kuliko kupigana na watu wa desturi ingine, kwa sasa Jean iko nafundisha watu wote mambo yenye kuwa mu Biblia yenye kusaidia watu wakuwe na amani na umoja. Mashauri ya Biblia iko nasaidia watu wa kila kabila, luga na desturi mbalimbali. Ile ni jambo ingine yenye kutufanya tutumainie Biblia.

ENDELEA KUTUMAINIA NENO YA MUNGU

16. Ju ya nini ni jambo ya maana sana tutumainie kabisa Neno ya Mungu?

16 Kadiri dunia inaendelea kuharibika, ni vile itakuwa nguvu zaidi kutumainia Neno ya Mungu. Watu wanaweza kufanya tuone kama Biblia haisemake kweli na kama Yehova hakuweka mutumwa mwaminifu na mwenye busara ili atuongoze leo. Lakini kama tunaamini kuwa Neno ya Yehova ni ya kweli sikuzote, tutaweza kupinga ile mambo yenye inaweza kuregeza imani yetu. ‘Tutaazimia kutii masharti [ya Yehova] nyakati zote, mupaka mwisho.’ (Zb. 119:112) ‘Hatutasikia haya’ ya kuambia wengine kweli yenye kuwa mu Biblia na kuwatia moyo watumikishe mashauri yenye kuwa ndani. (Zb. 119:46) Na tutavumilia “kwa subira na furaha” magumu ya nguvu sana, sawa vile mateso.​—Kol. 1:11; Zb. 119:143, 157.

17. Andiko ya mwaka itatusaidia namna gani?

17 Tuko wenye shukrani sana kwa Yehova juu ametusaidia kujua kweli! Ile kweli inatufanya tutulie, na inatuonyesha waziwazi namna tunaweza kuishi mu hii dunia yenye inaendelea kuharibika. Inatupatia tumaini ya kama mambo itakuwa muzuri zaidi wakati Ufalme wa Mungu utatawala. Andiko ya mwaka wa 2023 iendelee basi kutusaidia tuamini kabisa kama Neno yote ya Mungu, ni kusema, chanzo kabisa cha ile neno, ni kweli!​—Zb. 119:160.

WIMBO 94 Aksanti Yehova kwa Kutupatia Neno Yako

a Andiko ya mwaka wa 2023 ni andiko yenye kutia nguvu imani, inasema hivi: “Chanzo kabisa cha neno lako ni kweli.” (Zb. 119:160) Bila shaka unaamini pia ile jambo. Lakini watu wengi hawaamini kama Biblia ni ya kweli na kama inaweza kutupatia muongozo wenye kufaa. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo tatu yenye tunaweza kufanya ili kusaidia wenye kupendezwa wakuwe hakika kama wanaweza kutumainia Biblia na mashauri yake.

b MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mu Kiebrania, maneno yenye inatafsiriwa “chanzo kabisa cha neno lako ni kweli” maana yake Neno yote ya Mungu ni ya kweli.

c Neno “maandishi” maana yake dokima ya maandishi ya zamani.

d Juu ujue mambo mingi zaidi kuhusu namna Biblia imelindwa, fungula site jw.org na andika “Historia na Biblia” mu sehemu ya kutafutia.

e Majina fulani imebadilishwa.

f MAFASIRIO YA PICHA: Mungu alisema kama muji wa Babiloni utaharibiwa.

g MAFASIRIO YA PICHA: Kuliko kupigana na watu, kijana mwanaume anajifunza mu Biblia namna ya kuishi kwa amani na wengine na anawasaidia wafanye pia vile.