Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 3

Yehova Iko Anakusaidia

Yehova Iko Anakusaidia

“Yehova alikuwa pamoja na Yosefu . . . , alikuwa anafanya kila jambo lenye Yosefu alifanya liendeke muzuri.”—MWA. 39:2, 3.

WIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, na Rafiki Yangu

KIFUPI YA HABARI a

1-2. (a) Juu ya nini hatushangae wakati magumu inatufikia? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?

 TUKO watu wa Yehova, njo maana hatushangae wakati magumu inatufikia. Vile tunajua, Biblia inasema kama “lazima tuingie katika Ufalme wa Mungu kupitia taabu nyingi.” (Mdo. 14:22) Tunajua pia kama magumu fulani yenye tuko nayo haiwezi kuisha kabisa. Lakini, itaishaka tu wakati tutakuwa mu dunia Mupya ya Mungu, mwenye “kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”—Ufu. 21:4.

2 Yehova hatulinde ili tusipatwe na magumu. Lakini, wakati tunapata magumu anatusaidiaka ili tuivumilie. Tuone mambo yenye mutume Paulo aliambiaka Wakristo wenye walikuwa wanaishi kule Roma. Kwanza, alizungumuzia magumu yenye yeye na ndugu zake walipataka. Kisha aliandika hivi: “Tunatoka tukiwa tumeshinda kabisa kupitia yeye mwenye alitupenda.” (Ro. 8:35-37) Ile inamaanisha kama Yehova anaweza kukusaidia hata kama magumu yako haiishe. Tuone namna Yehova alimusaidia Yosefu na namna anaweza pia kukusaidia.

WAKATI HALI INABADILIKA BILA KUTAZAMIA

3. Ni hali gani yenye haitazamiwe yenye ilimufikia Yosefu?

3 Mambo yenye Yakobo alifanya ilionyesha wazi kama alimupenda sana mutoto wake Yosefu. (Mwa. 37:3, 4) Ile ilifanya watoto wakubwa wa Yakobo waanze kumuchukia ndugu yao mudogo Yosefu. Wakati nafasi ilijitokeza, walimuuzisha ku kikundi fulani ya wafanyabiashara Wamidiani. Wale wafanyabiashara walimupeleka Yosefu mbali sana mu inchi ya Misri, kwenye walimuuzisha tena kwa Potifa, mukubwa wa walinzi wa Farao. Maisha ya Yosefu ilibadilika haraka, alikuwa mwana mupendwa wa baba yake kisha akakuwa mutumwa wa hali ya chini ya mwanaume Mumisri!—Mwa. 39:1.

4. Tunaweza kupata magumu gani?

4 Biblia inasema kama “mambo ya mubaya inafikiaka kila mutu.” (Muh. 9:11Holy Bible—Easy-to-Read Version) Wakati fulani tunapataka magumu yenye iko “kawaida kwa watu,” ni kusema, magumu yenye watu wote wanapataka. (1 Ko. 10:13) Ao tunaweza kupata magumu juu tu tuko wanafunzi wa Yesu. Kwa mufano, watu wanaweza kutucheka, kutupinga, ao hata kututesa juu ya imani yetu. (2 Ti. 3:12) Hata upate magumu ya namna gani, Yehova anaweza kukusaidia. Alimusaidia Yosefu namna gani?

Hata kama Potifa alimuuza Yosefu na kumufanya kuwa mutumwa, Yehova alikuwa anafanya kila jambo yenye Yosefu alifanya iendeke muzuri (Ona fungu ya 5)

5. Juu kila jambo yenye Yosefu alikuwa nafanya ilikuwa naendeka muzuri, ile ilifanya Potifa avumbule nini? (Mwanzo 39:2-6)

5 Soma Mwanzo 39:2-6. Potifa alivumbula kama Yosefu alikuwa kijana mwenye akili na mwenye ufundi mu kazi. Na alijua ni juu ya nini alikuwa vile. Potifa aliona kama “Yehova alikuwa anafanya kila jambo lenye [Yosefu] alifanya liendeke muzuri.” b Ku mwisho, ule Mumisri alimufanya Yosefu kuwa mutumishi wake mwenyewe kwa kumuweka kuwa musimamizi wa nyumba yake yote. Ile ilikuwa na matokeo gani? Mambo ilimuendea Potifa muzuri.

6. Inawezekana Yosefu alikuwa anapenda nini wakati alikuwa mu hali ya nguvu?

6 Pima kuwazia namna Yosefu alijisikia. Ni jambo gani yenye alipenda zaidi kupitia mambo yote? Ilikuwa kuonwa na kupewa mapendeleo na Potifa? Inawezekana, Yosefu alikuwa anapenda kutoka mu gereza juu arudie kwa baba yake. Kusema kweli, hata kama alikuwa na mapendeleo mingi mu nyumba ya Potifa, Yosefu alikuwa angali mutumwa mwenye alikuwa anaongozwa na bwana mwenye hakukuwa anamuabudu Yehova. Yehova hakumufanya Potifa amuachilie Yosefu. Na hali ya Yosefu ilikuwa karibu kuharibika hata zaidi.

WAKATI HALI INAHARIBIKA ZAIDI

7. Ni nini inaonyesha kama hali ya Yosefu ilikuwa inaendelea kuwa mubaya zaidi? (Mwanzo 39:14, 15)

7 Sawa vile Mwanzo sura ya 39 inaonyesha, bibi ya Potifa alianza kuvutiwa na Yosefu na alianza kumuomba tena na tena alale naye. Kila mara Yosefu alikuwa anakatala. Ku mwisho bibi ya Potifa akamukasirikia Yosefu na kumushitaki kama alikuwa anatafuta kumulala kinguvu. (Soma Mwanzo 39:14, 15.) Wakati Potifa alisikia vile, akamutupa Yosefu mu gereza, na akabakia mule kwa miaka fulani. (Mwa. 39:19, 20) Hali ilikuwa namna gani mu gereza? Neno ya Kiebrania “gereza” yenye Yosefu alitumikisha inaweza kumaanisha “tangi” ao “shimo.” Alisema vile juu ya kuonyesha kama alikuwa fasi kwenye kulikuwa giza na aliona sawa vile hatatokaka mule. (Mwa. 40:15, maelezo ya chini.) Tena, Biblia inasema kama migulu ya Yosefu ilikuwa inafungwa kwa pingu na shingo yake ilitiwa katika vyuma. (Zb. 105:17, 18) Hali ya Yosefu ilikuwa inaendelea kuharibika hata zaidi. Wazia mutumwa mwenye alikuwa mwenye kutumainiwa, sasa anakuwa mufungwa wa hali ya chini.

8. Hata kama magumu yetu inaendelea kuwa mubaya zaidi, tuko hakika na jambo gani?

8 Ulishakajikuta mu hali ya nguvu yenye ilikuwa inaendelea kuwa mubaya hata zaidi hata kama ulikuwa unasali sana? Ile inawezekana. Yehova hatulinde ili tusipatwe na magumu mu hii dunia yenye kutatawaliwa na Shetani. (1 Yo. 5:19) Lakini, ukuwe hakika na jambo moya: Yehova anajua kabisa magumu yenye iko nakufikia na anakuhangaikia. (Mat. 10:29-31; 1 Pe. 5:6, 7) Tena, anasema hivi: “Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.” (Ebr. 13:5) Yehova anaweza kukusaidia uvumilie hata kama inaonekana sawa vile hakuna tumaini. Ni vile hali ya Yosefu ilikuwa. Acha tuone.

Hata wakati wenye Yosefu alikuwa mu gereza, Yehova aliendelea kumusaidia na aliwekwa kuwa musimamizi wa wafungwa wote (Ona fungu ya 9)

9. Nini njo inaonyesha kama Yehova alikuwa pamoya na Yosefu wakati alikuwa mu gereza? (Mwanzo 39:21-23)

9 Soma Mwanzo 39:21-23. Hata wakati wenye Yosefu alikuwa mu gereza, Yehova aliendelea kuwa pamoya naye. Namna gani? Kisha wakati fulani, ofisa mukubwa wa gereza alianza kumutumainia na kumuheshimia Yosefu sawa vile tu Potifa alifanyaka. Ku mwisho, ule ofisa alimuweka Yosefu kuwa musimamizi wa wafungwa wote. Kwa kweli, Biblia inasema kama “ule ofisa mukubwa wa gereza hakukuwa anaangalia kitu chochote chenye kilikuwa katika mikono ya Yosefu.” Yosefu alikuwa na kazi ya muziri ya kufanya. Ile ilikuwa mabadiliko yenye haikutazamiwa! Iliwezekana namna gani mufungwa mwenye alishitakiwa kama alikuwa natafuta kulala kwa nguvu bibi ya ofisa wa makao ya Farao apewe ile cheo ya maana? Kuko tu jibu moya yenye kuwa wazi. Mwanzo 39:23 inasema, “Yehova alikuwa pamoja na Yosefu na Yehova alifanya kila jambo lenye Yosefu alifanya liendeke muzuri.”

10. Yosefu aliona kama Yehova alikuwa anamusaidia ili kila jambo yenye alikuwa anafanya iendeke muzuri? Fasiria.

10 Pima tena kuwazia namna Yosefu alijisikia. Kisha kushitakiwa mambo ya uongo na kutupwa mu gereza, unawaza Yosefu aliona kama Yehova alikuwa anamusaidia ili kila jambo yenye alikuwa anafanya iendeke muzuri? Ni jambo gani yenye Yosefu alipenda zaidi kupita mambo yote? Ilikuwa kukubaliwa mbele ya macho ya ofisa mukubwa wa gereza? Inawezekana, Yosefu alikuwa anapenda kutoka mu gereza. Na hata wakati alikuwa mu gereza aliambiaka mufungwa mwingine mwenye alikuwaka karibu kutoshwa aende amutaye mbele ya Farao ili naye pia afikie kutoka mu ile mateso ya mu gereza. (Mwa. 40:14) Lakini, ule mwanaume hakumuambiaka Farao palepale. Ile ilifanyaka Yosefu abakie mu gereza kwa miaka ingine mbili. (Mwa. 40:23; 41:1, 14) Hata vile, Yehova aliendelea tu kumusaidia. Namna gani?

11. Ni uwezo gani wa pekee wenye Yehova alipatia Yosefu, na namna gani ile ilisaidia kutimizwa kwa kusudi ya Yehova?

11 Wakati Yosefu alikuwa mu gereza, Yehova alifanya Mufalme wa Misri alote ndoto mbili zenye zilimuhangaisha. Farao alipenda kujua kabisa maana ya zile ndoto mbili. Wakati alijua kama Yosefu alikuwa na uwezo wa kutafsiri ndoto, aliomba aletwe kwake. Yehova alimusaidia Yosefu atafsiri zile ndoto na tena Yosefu alimupatia Farao mashauri ya muzuri yenye ilimushangaza. Kisha kutambua kama Yehova alikuwa pamoya na Yosefu, Farao alimuweka ili asimamie chakula mu inchi yote ya Misri. (Mwa. 41:38, 41-44) Kisha wakati fulani, njala kubwa iliingia mu Misri yote na pia Kanaani, inchi kwenye familia ya Yosefu ilikuwa inaishi. Sasa Yosefu alikuwa na uwezo wa kulinda familia yake. Na kwa kufanya vile alilinda ile kizazi yenye ingetokeza Masiya.

12. Ni mu njia gani Yehova alifanya kila jambo yenye Yosefu alikuwa anafanya iendeke muzuri?

12 Waza mambo yenye haiko ya kawaida yenye ilimufikia Yosefu. Ni nani alifanya Potifa akaze akili yake juu ya Yosefu, mutumwa bure? Ni nani alifanya ofisa mukubwa wa gereza amukubali Yosefu, mufungwa wa hali ya chini? Ni nani alifanya Farao alote ndoto zenye zilimuhangaisha na kupatia Yosefu uwezo wa kuzitafsiri? Ni nani alifanya Yosefu awekwe kuwa musimamizi wa chakula mu Misri yote? (Mwa. 45:5) Jibu iko wazi, ni Yehova njo alifanya kila jambo yenye Yosefu alifanya iendeke muzuri. Ndugu za Yosefu walikuwa wanatafuta kumuua. Lakini, Yehova alibadilisha mambo ili atimize kusudi yake.

NAMNA YEHOVA IKO ANAKUSAIDIA

13. Yehova njo anaongozaka kila jambo yenye inatufikiaka mu maisha? Fasiria.

13 Habari ya Yosefu inaweza kutufundisha nini? Yehova njo anaongazaka kila jambo yenye inatufikiaka mu maisha? Anapangaka kila jambo mu maisha yetu ili mambo yote ya mubaya yenye inatokea ikuwe na sababu fulani ya muzuri? Hapana, Biblia haifundishe vile. (Muh. 8:9; 9:11) Lakini, tunajua kama wakati tunapata magumu fulani, Yehova anajua na anasikiliza kilio yetu ya kuomba musaada. (Zb. 34:15; 55:22; Isa. 59:1) Zaidi ya ile, Yehova anaweza kutusaidia tuvumilie magumu. Namna gani?

14. Namna gani Yehova anatusaidiaka wakati wa magumu?

14 Njia moya yenye Yehova anatumia ili kutusaidia ni kutufariji na kututia moyo, anafanyaka vile mara mingi na kwa wakati wenye kufaa. (2 Ko. 1:3, 4) Ile ni jambo yenye ndugu Eziz, wa mu Turkmenistan alijionea. Alihukumiwa kifungo ya miaka mbili mu gereza juu ya imani yake. Anasema hivi: “Asubui, siku ya magumu yangu, ndugu fulani alinionyesha Isaya 30:15, yenye inasema: ‘Mutakuwa na nguvu kama munaendelea kuwa watulivu na kuwa na tumaini.’ Ile andiko inanisaidiaka kuendelea kuwa mutulivu na kumutumainia Yehova mu mambo yote. Kutafakari sana ile andiko kulinisaidia wakati wote wenye nilikuwa mu gereza.” Unakumbuka wakati yenye Yehova alikusaidia kwa kukufariji na kukutia moyo saa yenye ulikuwa na lazima kabisa ya musaada?

15-16. Habari ya Tori inatufundisha nini?

15 Mara mingi, ni kisha jaribu kupita njo tunatambuaka kama Yehova njo alitusaidia tuivumilie. Dada mwenye kuitwa Tori alijionea kama ile ni kweli. Mutoto wake mwanaume, Mason, aligonjwa kansere kwa muda wa miaka sita mupaka akafikia kufa. Kusema kweli, Tori alivunjika moyo sana. Alisema hivi: “Miye niko mama, siwazie kama kunaweza kuwa magumu ya nguvu zaidi kupita ile.” Anaongeza hivi: “Niko hakika kama wazazi wengine watakubaliana na miye kama mama anaumiaka sana wakati mutoto wake iko anateseka. Anapendaka hata ateseke panafasi yake.”

16 Hata kama Tori aliumia sana wakati aliona mutoto wake iko anateseka, alianza kufikiri juu ya namna Yehova alikuwa namusaidia ili avumilie ile magumu. Anasema hivi: “Saa nafikiria ile wakati, naona namna Yehova alikuwa nanisaidia wakati wote wenye mutoto wangu alikuwa mugonjwa. Kwa mufano, Mason alikuwa mugonjwa sana, kwa hiyo haingewezekana aonane na watu wenye walikuwa wanakuya kumuangalia. Hata vile, ndugu na dada walikuwa wanafanya safari ya murefu sana mu barabara juu wafike ku hopitale kwenye alikuwa. Kila mara hakukuwa kunakosa mutu wa kuya kutuangalia ili kututegemeza. Zaidi ya ile, wale ndugu na dada walikuwa wanatupatia vitu vya kimwili vyenye tulikuwa navyo lazima. Hata wakati hali ilikuwa nguvu sana, hatukukuwa nakosa kitu.” Yehova alisaidia Tori na Mason wavumilie magumu yao.—Ona kisanduku “ Yehova Alitupatia Mambo Yenye Tulikuwa Nayo Lazima Kabisa.”

USISAHAU MAMBO YOTE YA MUZURI YENYE YEHOVA ALISHA KUFANYIA

17-18. Wakati wa magumu, tunaweza kufanya nini juu tuone kama Yehova iko natusaidia, na nini njo itafanya tukuwe wenye shukrani? (Zaburi 40:5)

17 Soma Zaburi 40:5. Mutu mwenye anapandaka mulima, anakuwaka na muradi wa kufika yulu kabisa ya ule mulima. Lakini, wakati iko anapanda ule mulima, anaweza kusimama kidogo na kuanza kufurahia mambo ya muzuri yenye iko anaona. Vilevile, hata wakati wa magumu, simama kidogo na ufikirie namna Yehova iko anakusaidia. Kila siku ujiulize hivi: ‘Ni mambo gani ya muzuri yenye Yehova alinifanyia leo? Hata kama magumu yangu haiyaisha, namna gani Yehova iko nanisaidia kuivumilia?’ Ujikaze kupata hata jambo moya ya muzuri yenye Yehova alifanya ili kukusaidia.

18 Kwa kweli, unaweza kumuomba Yehova amalize magumu yako. Haiko mubaya kufanya vile. (Flp. 4:6) Lakini, hatupaswe pia kusahau mambo ya muzuri yenye Yehova iko natufanyia sasa. Yehova anaahidi kututia nguvu na kutusaidia ili tuvumilie magumu. Kwa hiyo, juu Yehova iko nakusaidia, endelea kuwa mwenye shukrani kila siku. Kama unafanya vile, utajionea namna Yehova ataendelea kukusaidia sawa vile alisaidiaka Yosefu, hata wakati wa magumu ya nguvu.—Mwa. 41:51, 52.

WIMBO 32 Ukuwe Upande wa Yehova!

a Wakati tuko napitia magumu ya nguvu, tunaweza kuanza kuwaza kama Yehova haiko “anatusaidia.” Tunaweza kuwaza kama ikiwa Yehova iko anatusaidia inaomba magumu yenye tuko nayo iishe. Lakini, mambo yenye ilimufikia Yosefu inatufundisha somo ya maana sana, ya kama Yehova anaweza kutusaidia hata kama magumu yetu haiishe. Hii habari itafasiria namna gani ile inawezekana.

b Mu Biblia, ni mistari fulani tu njo inazungumuzia ile mabadiliko mu maisha ya Yosefu wakati alikuwa mutumwa, lakini pengine ile mabadiliko ilitokea kwa kipindi ya miaka mingi.