Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 5

“Upendo Wenye Kristo Iko nao Unatulazimisha”

“Upendo Wenye Kristo Iko nao Unatulazimisha”

“Upendo wenye Kristo iko nao unatulazimisha . . . Na alikufa kwa ajili ya watu wote ili wale wenye wanaishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe.”—2 KO. 5:14, 15.

WIMBO 13 Kristo Ni Mufano Muzuri

KIFUPI YA HABARI a

1-2. (a) Tunaweza kujisikia namna gani wakati tunawaza sana juu ya maisha na utumishi wa Yesu? (b) Tutaona nini mu hii habari?

 WAKATI mutu fulani mwenye tunapendaka anakufa, tunahuzunikaka sana! Ku mwanzo tunaweza kuumia sana wakati tunakumbuka mambo yenye alifanya mu masiku yenye tulikuwa naye mbele akufe, zaidi sana kama aliteseka mbele akufe. Lakini, wakati fulani kama tunakumbuka jambo fulani yenye alitufundisha ao yenye alifanya ao jambo fulani yenye alisema juu ya kututia moyo ao kutuchekesha, ile inafanya tukuwe na furaha.

2 Vilevile, tunahuzunikaka sana wakati tunasoma habari juu ya mateso na kifo ya Yesu. Mu kipindi ya Ukumbusho, tunakamataka wakati wa kuwaza sana juu ya ulazima wa zabihi ya bei ya ukombozi. (1 Ko. 11:24, 25) Hata vile, tunakuwaka na furaha sana wakati tunawaza sana juu ya mambo yenye Yesu alisema na kufanya wakati alikuwa hapa ku dunia. Tena tunatiwaka moyo wakati tunawaza juu ya mambo yenye iko nafanya sasa na yenye atatufanyia wakati wenye kuya. Mu hii habari, tutaona namna kuwaza sana juu ya ile mambo na juu ya upendo wake kunaweza kutuchochea tuonyeshe shukrani mu njia mbalimbali.

SHUKRANI INATUCHOCHEA TUENDELEE KUMUFUATA YESU

3. Sababu gani tunapaswa kuonyesha shukrani juu ya bei ya ukombozi?

3 Kuwaza sana juu ya maisha na kifo ya Yesu kunafanya tukuwe wenye shukrani. Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, alifundisha watu kuhusu baraka zenye Ufalme wa Mungu utaleta. Kujua ile kunafanya tukuwe wenye shukrani sana. Tuko wenye shukrani juu ya bei ya ukombozi kwa sababu inatufungulia njia ya kuwa na urafiki wa karibu pamoya na Yehova na Yesu. Wale wenye kumuamini Yesu wako pia na tumaini ya kuishi milele na ya kuona tena wapendwa wao wenye walikufaka. (Yoh. 5:28, 29; Ro. 6:23) Hakuna kitu yenye tulifanya juu tustahili kupata zile baraka, na hatuwezi hata kidogo kumulipa Mungu na Kristo juu ya mambo yenye walitufanyia. (Ro. 5:8, 20, 21) Lakini tunaweza kuwaonyesha shukrani kubwa sana. Mu njia gani?

Ni mu njia gani kuwaza sana juu ya mufano wa Maria Magdalene kunakuchochea kuonyesha shukrani? (Ona fungu ya 4-5)

4. Ni mu njia gani Maria Magdalene alionyesha shukrani yake kwa Yesu juu ya mambo yenye alimufanyia? (Ona picha.)

4 Fikiria mufano wa mwanamuke moya Muyahudi mwenye kuitwa Maria Magdalene. Alikuwa anateseka sana juu alikuwa na pepo wachafu saba wenye walikuwa wanamuhangaisha. Pengine aliona kama hakuna mutu mwenye angeweza kumusaidia. Kwa hiyo, pima kuwazia namna alikuwa mwenye shukrani wakati Yesu alimutosha wale pepo wachafu! Shukrani yake ilimuchochea amufuate Yesu na atumie wakati, nguvu, na mali yake ili kumutegemeza mu kazi ya kuhubiri. (Lu. 8:1-3) Hata kama Maria alimushukuru sana Yesu juu ya mambo yenye alimufanyia, pengine hakujua kama kulikuwa mambo ingine ya muzuri zaidi yenye Yesu angemufanyia wakati wenye kuya, ni kusema, kutoa uzima wake kwa ajili ya wanadamu “ili kila mutu mwenye anamuamini” apate uzima wa milele. (Yoh. 3:16) Tena, Maria alionyesha shukrani yake kwa Yesu kwa kuendelea kushikamana naye. Wakati Yesu alikuwa anateseka ku muti wa mateso, Maria alikuwa karibu yake juu alimuhangaikia na juu alikuwa napenda kufariji wengine wenye walikuwa pale. (Yoh. 19:25) Kisha Yesu kufa, Maria na wanamuke wengine wawili walileta ku makaburi manukato ya kupakala mwili wa Yesu mbele ya kumuzika. (Mk. 16:1, 2) Yehova alimubariki sana Maria juu alikuwa mushikamanifu kwa Yesu. Kisha Yesu kufufuliwa, alifurahi kumuona tena na kuongea naye. Ile ni pendeleo yenye wanafunzi wengi wa Yesu hawakupata.—Yoh. 20:11-18.

5. Ni mu njia gani tunaweza kuonyesha shukrani yetu juu ya mambo yote yenye Yehova na Yesu walitufanyia?

5 Siye pia tunaweza kuonyesha shukrani yetu juu ya mambo yote yenye Yehova na Yesu walitufanyia kwa kutumia wakati, nguvu, na makuta juu ya kutegemeza kazi ya Ufalme. Kwa mufano, tunaweza kusaidia mu kazi ya kujenga na kuchunga muzuri majengo yenye tunatumiaka ili kumuabudu Yehova.

KUPENDA YEHOVA NA YESU KUNATUCHOCHEA TUPENDE WENGINE

6. Juu ya nini tunasema kama Yesu alikufa kwa ajili ya kila mutu kipekee?

6 Kujua kama Yehova na Yesu wanatupenda sana, kunatuchochea tuwapende pia. (1 Yo. 4:10, 19) Tunawapenda tena zaidi wakati tunakumbuka kama Yesu alikufa kwa ajili ya kila mutu kipekee. Mutume Paulo alikubaliana na ile, na alionyesha shukrani yake wakati aliandikia Wagalatia hii maneno: “Mwana wa Mungu . . . alinipenda na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.” (Gal. 2:20) Kwa musingi wa bei ya ukombozi, Yehova alikuvuta ili ukuwe rafiki yake. (Yoh. 6:44) Bila shaka unaguswa moyo sana juu unajua kama Yehova aliona kitu fulani ya muzuri sana ndani yako na kama alilipa bei kubwa sana ili ukuwe rafiki yake. Tena ile inafanya upende sana Yehova na Yesu. Ni muzuri basi kila mutu ajiulize hivi: ‘Ule upendo unapaswa kunilazimisha kufanya nini?’

Kupenda Mungu na Kristo kunatuchochea kuhubiria watu wote (Ona fungu ya 7)

7. Sawa vile picha inaonyesha, ni mu njia gani tunaweza kuonyesha kama tunapenda Yehova na Yesu? (2 Wakorinto 5:14, 15; 6:1, 2)

7 Kupenda Mungu na Kristo kunatuchochea tupende wengine. (Soma 2 Wakorinto 5:14, 15; 6:1, 2.) Njia moya ya kuonyesha upendo ni kuwa na bidii mu kazi ya kuhubiri. Tunaongea na kila mutu mwenye tunakutana naye. Hatuepuke kuongea na mutu juu ni wa rangi ao kabila ingine. Tena, hatuepuke kuongea na mutu juu ni tajiri ao maskini, juu alisoma sana ao juu hakusoma sana. Kwa kufanya vile, tuko natumika kulingana na mapenzi ya Yehova ya kwamba “watu wa namna zote waokolewe na wapate ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli.”—1 Ti. 2:4.

8. Ni mu njia gani tunaweza kuonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu?

8 Tunaonyesha pia kama tunapenda Yehova na Kristo kwa kupenda ndugu na dada zetu. (1 Yo. 4:21) Tunawahangaikia na kuwasaidia wakati wako na magumu. Tunawafariji wakati wanafiwa na mupendwa, tunawatembelea wakati wanagonjwa, na tunafanya yetu yote ili kuwatia moyo. (2 Ko. 1:3-7; 1 Te. 5:11, 14) Tunaendelea kusali kwa ajili yao juu tunajua kama “sala ya kumulilia Mungu ya mwenye haki iko na nguvu nyingi.”—Yak. 5:16.

9. Ni mu njia gani ingine tunaweza kuonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu?

9 Tunaonyesha tena kama tunapenda ndugu na dada zetu kwa kuendelea kuishi nao kwa amani. Tunajikaza kumuiga Yehova kwa kusamehe wengine. Yehova aliruhusu Mwana wake akufe juu ya zambi zetu. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa tayari kusamehe ndugu na dada zetu wakati wanatukosea. Hatupendi kuwa sawa ule mutumwa muovu mwenye Yesu alizungumuzia mu mufano moya wenye alitoa. Hata kama bwana wake alifuta deni kubwa yenye alikuwa nayo, ule mutumwa muovu hakumuhurumia mutumwa mwenzake mwenye alikuwa na deni yake kidogo. (Mt. 18:23-35) Kama hauelewane na ndugu ao na dada fulani mu kutaniko, unaweza kuwa wa kwanza kuenda kumuona na kufanya amani naye mbele siku ya Ukumbusho ifike? (Mt. 5:23, 24) Kama unafanya vile, utaonyesha kama unapenda sana Yehova na Yesu.

10-11. Ni mu njia gani wazee wanaweza kuonyesha kama wanapenda Yehova na Yesu? (1 Petro 5:1, 2)

10 Ni mu njia gani wazee wanaweza kuonyesha kama wanapenda Yehova na Yesu? Njia moya ya kufanya vile ni kuhangaikia kondoo wa Yesu. (Soma 1 Petro 5:1, 2.) Yesu alionyesha wazi ile jambo kwa mutume Petro. Hata kisha kumukatala Yesu mara tatu, inawezekana Petro alikuwa na hamu sana ya kuonyesha kama alimupenda. Kisha Yesu kufufuliwa, alimuuliza Petro hivi: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?” Tuko hakika kama hakuna kitu yenye Petro angefanya juu ya kuonyesha kama anamupenda Bwana wake. Yesu alimuambia Petro hivi: “Lisha kondoo wangu wadogo.” (Yoh. 21:15-17) Mu maisha yake yote, Petro aliendelea kuhangaikia kondoo wa Bwana wake Yesu. Ile ilionyesha kama alimupenda.

11 Wazee, mu kipindi ya Ukumbusho, ni mu njia gani munaweza kuonyesha kama maneno yenye Yesu alimuambia Petro ni ya lazima pia kwenu? Munaweza kuonyesha kama munapenda sana Yehova na Yesu kwa kufanya kwa ukawaida kazi ya uchungaji na kwa kujikaza sana kusaidia wale wenye hawatende tena ili wamurudilie Yehova. (Eze. 34:11, 12) Zaidi ya ile, tunaweza kutia moyo wanafunzi wa Biblia na wapya wenye wanahuzuria Ukumbusho. Ni muzuri mufanye yenu yote ili kuwasaidia wakuwe na furaha juu siku moya watafikia pia kuwa wanafunzi wa Yesu.

KUMUPENDA KRISTO KUNATUCHOCHEA TUKUWE NA UHODARI

12. Juu ya nini kuwaza sana juu ya maneno yenye Yesu alisema usiku mbele akufe kunatupatia uhodari? (Yoh. 16:32, 33)

12 Usiku mbele Yesu akufe, aliambia wanafunzi wake hivi: “Katika ulimwengu mutapata taabu, lakini musiogope! Mimi nimeshinda ulimwengu.” (Soma Yohana 16:32, 33.) Ni nini ilimusaidia Yesu aonyeshe uhodari wakati maadui wake walimuogopesha? na ni nini ilimusaidia aendelee kuwa muaminifu mupaka kifo? Alimutegemea Yehova. Juu Yesu alijua kama wanafunzi wake watapata majaribu ya vile, alimuomba Yehova awalinde. (Yoh. 17:11) Juu ya nini ile inatupatia uhodari? Juu Yehova iko na nguvu zaidi kupita maadui wetu. (1 Yo. 4:4) Anaonaka kila kitu. Tuko hakika kama ikiwa tunamutegemea, atatusaidia tuonyeshe uhodari.

13. Ni mu njia gani Yosefu wa Arimatea alionyesha uhodari?

13 Fikiria mufano wa Yosefu wa Arimatea. Wayahudi walikuwaka namuheshimia sana. Alikuwa mushiriki wa Sanedrini, mahakama kubwa ya Wayahudi. Lakini, wakati wa utumishi wa Yesu hapa ku dunia, Yosefu hakukuwa na uhodari. Yohana anasema kama Yosefu alikuwa “mwanafunzi wa Yesu lakini kwa uficho kwa sababu aliogopa Wayahudi.” (Yoh. 19:38) Hata kama Yosefu alipenda mambo ya Ufalme, hakupenda watu wengine wajue kama alimuamini Yesu. Bila shaka aliwaza kuwa ikiwa watu wanajua kama alikuwa mwanafunzi wa Yesu, hawatamuheshimia tena. Hata vile, kisha Yesu kufa, Biblia inasema hivi kuhusu Yosefu: “akajipatia uhodari, akaingia na kuja mbele ya Pilato na akaomba apewe mwili wa Yesu.” (Mk. 15:42, 43) Kwa kufanya vile, Yosefu alionyesha waziwazi kama alikuwa mwanafunzi wa Yesu.

14. Unapaswa kufanya nini kama unaogopaka watu?

14 Na weye unaogopaka watu sawa vile Yosefu? Saa uko ku masomo ao ku kazi, wakati fulani unasikiaka haya ya kuambia wengine kama uko Shahidi wa Yehova? Uko naogopa kuwa muhubiri ao kubatizwa juu uko nahangaikia mambo yenye wengine wanaweza kuwaza juu yako? Usiache mawazo ya vile ikuzuie kufanya mambo yenye unajua kama ni ya muzuri. Sali kwa Yehova kwa moyo wote. Umuombe akupatie uhodari wa kufanya mapenzi yake. Wakati unaona vile Yehova iko najibia sala zako, utakuwa na nguvu na uhodari zaidi.—Isa. 41:10, 13.

FURAHA INATUCHOCHEA TUMUTUMIKIE YEHOVA BILA KUACHA

15. Kisha Yesu kutokea wanafunzi wake, furaha yao iliwachochea wafanye nini? (Luke 24:52, 53)

15 Wanafunzi walihuzunika sana wakati Yesu alikufa. Pima kwanza kujitia pa nafasi yao. Zaidi tu ya kupoteza mupendwa wao, waliona sawa vile tumaini yenye walikuwaka nayo ilipotea pia. (Lu. 24:17-21) Lakini, wakati Yesu aliwatokea, aliwasaidia waelewe kama alitimiza unabii wenye kuwa mu Biblia. Aliwapatia pia kazi ya maana ya kufanya. (Lu. 24:26, 27, 45-48) Wakati Yesu alipanda mbinguni kisha siku 40, wanafunzi hawakukuwa tena na huzuni, lakini walifurahi sana juu walijua kama Bwana wao alikuwa muzima na kama alikuwa tayari ili kuwasaidia watimize kazi ya maana yenye aliwapatia. Furaha yao iliwachochea wamusifu Yehova bila kuacha.—Soma Luka 24:52, 53; Mdo. 5:42.

16. Ni mu njia gani tunaweza kuiga wanafunzi wa Yesu?

16 Ni mu njia gani tunaweza kuiga wanafunzi wa Yesu? Tunaweza kuwa na furaha ya kumuabudu Yehova mu mwaka wote, hapana tu mu kipindi ya Ukumbusho. Juu ya kufanya vile, inaomba tutie Ufalme wa Mungu pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu. Kwa mufano, ndugu na dada fulani wamebadilisha programu yao ya kazi ili wahubiri sana, wakusanyike, na kufanya ibada ya familia kwa ukawaida. Wengine waliamua kuepuka kuwa na vitu vya kimwili vyenye wengine wanaona kama ni vya maana sana mu maisha ili watumike sana mu kutaniko ao watumikie fasi kwenye kuwa lazima sana ya wahubiri wa Ufalme. Hata kama tunapaswa kuvumilia ili tuendelee kumutumikia Yehova, anaahidi kama atatubariki sana ikiwa tunatia mambo ya Ufalme pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu.—Mez. 10:22; Mt. 6:32, 33.

Mu kipindi ya Ukumbusho, panga wakati wa kuwaza sana juu ya mambo yenye Yehova na Yesu walishakufanyia kipekee (Ona fungu ya 17)

17. Unaazimia kufanya nini mu hii kipindi ya Ukumbusho? (Ona picha.)

17 Tuko nachunga kwa hamu kufanya Ukumbusho siku ya Pili, tarehe 4 Mwezi wa 4. Lakini, tusichunge mupaka ile tarehe ifike njo tuanze kuwaza sana juu ya maisha na kifo ya Yesu na juu ya upendo wenye yeye na Yehova walituonyesha. Waza sana juu ya ile mambo yote kadiri inawezekana majuma fulani mbele na kisha ukumbusho. Kwa mufano, panga wakati wa kusoma na kutafakari juu ya matukio yenye inapatikana ku sehemu “Juma la Mwisho la Maisha ya Yesu Katika Dunia” yenye kuwa ku Nyongeza B12 ya Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Wakati uko nasoma habari juu ya maisha ya Yesu, tafuta maandiko yenye itakusaidia ukuwe mwenye shukrani, upendo, uhodari na furaha zaidi. Kisha fikiria ni mu njia gani mbalimbali unaweza kuonyesha shukrani kwa moyo wako wote. Ukuwe hakika kama Yesu atafurahia sana mambo yote yenye uko nafanya ili kumukumbuka mu hii kipindi ya Ukumbusho.—Ufu. 2:19.

WIMBO 17 “Ninataka”

a Mu kipindi ya Ukumbusho, tunatiwa moyo kuwaza sana juu ya maisha na kifo ya Yesu na juu ya upendo wenye yeye na Baba yake walituonyesha. Ile itatuchochea tufanye mambo fulani ili kuwashukuru. Mu hii habari tutaona ni mu njia gani mbalimbali tunaweza kuonyesha shukrani yetu juu ya bei ya ukombozi na namna tunaweza kuonyesha kama tunapenda Yehova na Yesu. Tutaona pia namna tunaweza kuonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu, namna ya kuonyesha uhodari na namna ya kupata furaha mu kazi yetu.