Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 6

Jarĩa Bibiria Ĩguũraga Jegie Mũtungi Waayo

Jarĩa Bibiria Ĩguũraga Jegie Mũtungi Waayo

“Andika mantu jonthe jaria mbaritie nagwe iukune.”—JER. 30:2.

RWĨMBO 96 Kitabu cha Mungu Ni Hazina

MUHTASARI a

1. Nĩkĩ twonaga Bibiria ĩrĩ ya gĩtũmi?

 TUNAMSHUKURU sana Yehova Mungu kwa kutupatia Biblia! Kupitia kurasa zake, anatupatia ushauri wenye hekima unaoweza kutusaidia kushughulikia kwa mafanikio matatizo tunayokabili leo. Pia, anatupatia tumaini zuri ajabu la wakati ujao. Jambo muhimu hata zaidi, Yehova ametumia Biblia kutufunulia sifa nyingi za utu wake. Tunapotafakari sifa zake maridadi, mioyo yetu inaguswa na tunachochewa kumkaribia zaidi Mungu wetu kwa kusitawisha urafiki wa karibu pamoja naye.​—Zab. 25:14.

2. Nĩ njĩra irĩkũ mwanya mwanya Jehova atumĩrĩte kwimenyithania kĩrĩ antũ?

2 Yehova anataka watu wamjue. Zamani, alijifunua kupitia ndoto, maono, na hata malaika. (Hes. 12:6; Mdo. 10:3, 4) Lakini watu wangejifunzaje kuhusu ndoto, maono, au jumbe kutoka kwa malaika ikiwa hazingeandikwa? Hiyo ndiyo sababu Yehova aliwaagiza wanaume ‘waandike katika kitabu’ yale ambayo alitaka sisi tujue. (Yer. 30:2) Kwa sababu “njia ya Mungu wa kweli ni kamilifu,” tunaweza kuwa na uhakika kwamba njia hii ya kuwasiliana nasi ni bora na inatunufaisha.​—Zab. 18:30.

3. Nĩatĩa Jehova aathithĩrie nĩkenda akaria Bibiria? (Isaya 40:8)

3 Soma Isaya 40:8. Neno la Mungu limewapa mwongozo wenye hekima wanaume na wanawake waaminifu kwa maelfu ya miaka. Hilo limewezekanaje? Kwa kuwa Maandiko yaliandikwa zamani sana kwenye vitu vinavyoweza kuharibika, basi hakuna hati za awali kabisa ambazo zinapatikana leo. Lakini Yehova alihakikisha kwamba hati hizo za maandishi matakatifu zilinakiliwa. Ingawa waandishi walionakili hawakuwa wakamilifu, walikuwa makini sana. Kwa mfano, kuhusu Maandiko ya Kiebrania, msomi mmoja aliandika hivi: “Tunaweza kusema kwa uhakika kwamba hakuna kitabu kingine cha kale ambacho kimenakiliwa kwa umakini kama hicho.” Basi, ingawa muda mrefu umepita, na licha ya vitu vinavyoweza kuharibika ambavyo vilitumiwa, na hali ya kutokamilika ya waandishi, tunaweza kuwa na uhakika kwamba maneno tunayosoma katika Biblia leo yanawasilisha mawazo ya Mtungaji wake, Yehova.

4. Nĩmbi tũkarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

4 Yehova ndiye Chanzo cha “kila zawadi njema na kila tuzo kamilifu.” (Yak. 1:17) Biblia ni mojawapo kati ya zawadi bora ambazo Yehova ametupatia. Zawadi hutufunulia jambo fulani kuhusu yule anayeitoa—kwamba anatujua vizuri sisi na mahitaji yetu. Ndivyo ilivyo kuhusu Mpaji wa Biblia. Tunapochunguza zawadi hiyo, tunajifunza mengi kumhusu Yehova. Tunajifunza kuhusu jinsi anavyotujua vizuri sisi na mambo tunayohitaji. Katika makala hii, tutachunguza jinsi Biblia inavyofunua sifa tatu za Yehova: hekima yake, haki yake, na upendo wake. Kwanza, acheni tuchunguze njia ambazo Biblia inafunua hekima ya Mungu.

BIBIRIA NĨGUŨRAGA ŨŨME BWA MŨRUNGU

5. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ ĩmwe Bibiria ĩguũraga ũũme bwa Mũrungu?

5 Yehova anajua kwamba tunahitaji mwongozo wake wenye hekima. Na Biblia, zawadi ambayo ametupatia, imejaa hekima yake. Mwongozo wa Biblia huleta matokeo mazuri kwa watu. Biblia inabadili maisha. Vitabu vya kwanza vya Biblia vilipoandikwa, Musa aliwaambia hivi watu wa Mungu, Waisraeli: “Haya si maneno matupu kwenu, bali yanamaanisha uhai wenu.” (Kum. 32:47) Wale waliotii Maandiko wangefurahia maisha yenye furaha na yenye mafanikio. (Zab. 1:2, 3) Ingawa muda umepita tangu Neno la Mungu liandikwe, bado lina nguvu za kuboresha maisha ya watu. Kwa mfano, kwenye jw.org, kwenye mfululizo “Biblia Inabadili Maisha,” utapata zaidi ya masimulizi halisi 50 ya maisha yanayoonyesha jinsi ambavyo leo, nguvu za Biblia ‘zinafanya kazi ndani ya wanaoiamini.’​—1 The. 2:13.

6. Nĩkĩ tũũmba kuuga Bibiria ĩrĩ mwanya na mauku jangĩ jonthe?

6 Hakuna kitabu kinachoweza kulinganishwa na Neno la Mungu. Kwa nini? Kwa sababu Mtungaji wa kitabu hicho, Yehova Mungu, ni Mweza-Yote, anaishi milele, na ana hekima isiyo na kifani. Vitabu vingine vingi huendelea kuwapo baada ya watungaji wake kufa, na mara nyingi ushauri ulio katika vitabu hivyo hupitwa na wakati. Kwa upande mwingine, kanuni zenye hekima zinazopatikana katika Biblia hudumu milele; zimewanufaisha watu ambao wameishi katika vipindi mbalimbali. Tunaposoma kitabu hicho kitakatifu na kutafakari mambo tunayojifunza, Mtungaji wake hutumia roho yake takatifu yenye nguvu kutusaidia kuona jinsi tunavyoweza kutumia mwongozo wa Biblia katika maisha yetu. (Zab. 119:27;Mal. 3:16;Ebr. 4:12) Naam, Mtungaji wa Biblia aliye hai, anatamani sana kukusaidia. Hilo linatuchochea kusoma Biblia kwa ukawaida!

Biblia imewasaidiaje watu wa Mungu wawe na umoja wakati uliopita na leo? (Tazama fungu la 7 na 8)

7. Nĩatĩa Bibiria yaatetherie antũ ba Mũrungu kwĩthĩrwa na ũrumwe ĩgiita rĩa karaaja?

7 Njia nyingine kuu ambayo Biblia inafunua hekima ya Mungu ni jinsi inavyowasaidia watu wa Mungu wawe na umoja. Waisraeli walipoingia kwenye Nchi ya Ahadi, waliishi katika eneo kubwa sana. Baadhi yao walikuwa wavuvi, wengine walifuga wanyama, na wengine walikuwa wakulima. Ingekuwa rahisi kwa Waisraeli walioishi katika eneo moja kutojishughulisha na hali ya Waisraeli wenzao walioishi katika maeneo mengine ya nchi hiyo. Lakini Yehova alifanya mpango ili Waisraeli wakusanyike pamoja kwenye pindi mbalimbali kusikiliza Neno lake lililoandikwa likisomwa na kufafanuliwa. (Kum. 31:10-13;Neh. 8:2,8,18) Wazia jinsi Mwisraeli mwaminifu alivyohisi alipowasili Yerusalemu na labda kuwaona mamilioni ya waabudu wenzake kutoka kila sehemu ya nchi hiyo! Hivyo, Yehova aliwasaidia watu wake waendelee kuwa na umoja. Baadaye, kutaniko la Kikristo lilipoanzishwa, lilikuwa na wanaume na wanawake ambao walizungumza lugha nyingi na waliotoka katika malezi na tamaduni mbalimbali. Lakini kwa kuwa waliyapenda Maandiko, walikuwa na umoja katika ibada ya Mungu wa kweli. Wale waliokubali kuwa waamini wangeweza tu kuelewa Neno la Mungu kwa msaada wa waabudu wenzao na kwa kukusanyika pamoja nao.​—Mdo. 2:42; 8:30, 31.

8. Nĩatĩa Bibiria ĩgwatithanĩtie antũ ba Mũrungu naarua?

8 Mungu wetu mwenye hekima anaendelea kuwafundisha na kuwaunganisha watu wake kupitia Biblia. Biblia ndiyo chanzo cha chakula cha kiroho ambacho tunafurahia sana. Sisi hukusanyika pamoja kwa ukawaida kwenye mikutano yetu ya kutaniko, makusanyiko ya mzunguko, na ya eneo ili kusikiliza Maandiko yakisomwa, kufafanuliwa, na kuzungumziwa. Basi, Biblia inatimiza jukumu muhimu katika kutimiza kusudi la Yehova la kuwafanya waabudu wake “wamtumikie bega kwa bega.”​—Sef. 3:9.

9. Nĩ nkuma ĩrĩkũ muntũ abuĩrĩte kwĩthĩrwa nayo nĩkenda aciũkĩrwa nĩ jarĩa jarĩ Bibiriene? (Luka 10:21)

9 Fikiria uthibitisho mwingine wa hekima ya Yehova. Alihakikisha kwamba sehemu nyingi za Maandiko ziliandikwa kwa njia ambayo ingeeleweka kwa wasomaji wanyenyekevu tu. (Soma Luka 10:21.) Watu kila mahali husoma Biblia. Msomi mmoja alisema, Biblia “ni kitabu ambacho kimesambazwa kwa wingi zaidi, na pia kusomwa kwa makini zaidi kuliko vitabu vyote.” Lakini ni watu wanyenyekevu tu ambao kwa kweli wanaelewa na kutumia mambo ambayo Biblia inasema.​—2 Kor. 3:15, 16.

10. Nĩ njĩra ĩrĩkũ ĩngĩ Bibiria yonanĩtie ũũme bwa Jehova?

10 Tunatambua hekima ya Yehova katika Biblia kwa njia nyingine pia. Yehova anatumia Maandiko kutufundisha tukiwa kikundi na pia kutufundisha na kutufariji tukiwa mtu mmojammoja. Sisi sote tunaweza kutambua jinsi Yehova anavyopendezwa nasi kibinafsi tunaposoma Neno lake. (Isa. 30:21) Ulipokabili tatizo, ni mara ngapi ambazo ulichunguza Maandiko na kusoma mstari ambao ulihisi kwamba umeandikwa hasa kwa ajili yako? Ingawa hivyo, Biblia inaeleweka kwa mamilioni ya watu. Basi, inawezaje kuwa na habari ambazo hazijapitwa na wakati zinazokufaa leo na ambazo hasa zinahusu mahitaji yako ya kibinafsi? Hilo linawezekana tu kwa sababu Mtungaji wa Biblia ndiye mwenye hekima zaidi ulimwenguni pote.​—2 Tim. 3:16, 17.

BIBIRIA NĨGUŨRAGA ATĨ MŨRUNGU NĨ WA ĨOTA

11. Mũrungu oonanĩrie atĩa aatarĩ na mpathũ rĩrĩa Bibiria yaandĩkagwa?

11 Haki ni sifa nyingine ya Yehova. (Kum. 32:4) Haki inahusiana kwa ukaribu na kutokuwa na ubaguzi, na Yehova hana ubaguzi. (Mdo. 10:34, 35;Rom. 2:11) Tunaona kwamba hana ubaguzi kupitia lugha ambazo zilitumiwa kuandika Biblia. Vitabu vya kwanza 39 vya Biblia viliandikwa hasa katika Kiebrania, lugha ambayo wakati huo watu wa Mungu walielewa kwa urahisi. Hata hivyo, kufikia karne ya kwanza W.K., watu wengi walizungumza Kigiriki, basi vitabu vya mwisho 27 vya Biblia viliandikwa hasa katika lugha hiyo. Yehova hakuamua kwamba Neno lake liandikwe katika lugha moja tu. Leo, watu bilioni nane hivi walio duniani huzungumza lugha nyingi. Watu wengi hivyo wanaweza kujifunzaje kumhusu Yehova?

12. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ ĩmwe Danieli 12:4 yũjũrĩtue ntukũne iji cia mũthia?

12 Kupitia nabii Danieli, Yehova aliahidi kwamba katika wakati wa mwisho “ujuzi wa kweli” unaopatikana katika Biblia ‘ungekuwa mwingi.’ Na watu wengi wangeuelewa. (Soma Danieli 12:4.) Njia moja ambayo ujuzi huo umekuwa mwingi ni kupitia kutafsiriwa, kuchapishwa, na kusambazwa kwa Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia. Biblia ndicho kitabu ambacho kimetafsiriwa na kusambazwa kwa wingi zaidi duniani. Tafsiri za Biblia zinazotokezwa na makampuni ya kibiashara wakati mwingine ni za bei ghali sana. Kufikia sasa, watu wa Yehova wametafsiri Biblia, ikiwa nzima au kwa sehemu, katika lugha zaidi ya 240, na mtu yeyote anaweza kupata nakala bila malipo. Matokeo ni kwamba watu wa mataifa yote wanajifunza “habari njema ya Ufalme” kabla ya mwisho kuja. (Mt. 24:14) Mungu wetu mwenye haki anataka kuwapa watu wengi iwezekanavyo nafasi ya kumjua kwa kusoma Neno lake. Hii ni kwa sababu anatupenda sana sisi sote.

BIBIRIA NĨGUŨRAGA WENDO BWA MŨRUNGU

13. Nĩkĩ tũũmba kuuga Bibiria nĩguũraga wendo bwa Mũrungu? (Johana 21:25)

13 Biblia inatupatia uthibitisho kuhusu sifa kuu zaidi ya Mtungaji wake, yaani, upendo. (1 Yoh. 4:8) Fikiria mambo ambayo Yehova alitia ndani ya Biblia na yale ambayo hayakutiwa ndani. Alituandalia kile tunachohitaji hasa ili kuwa na uhusiano pamoja naye, kuishi maisha yenye furaha sasa, na kupata uzima wa milele. Hata hivyo, kwa sababu Yehova anatupenda, hakutulemea na habari ambazo hatuhitaji kwa sasa.​—Soma Yohana 21:25.

14. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ ĩngĩ jarĩa jarĩ Bibiriene jarikithagia atĩ Mũrungu natwendete?

14 Pia, Yehova alionyesha upendo kwa kuwasiliana nasi kupitia njia inayoonyesha kwamba anatuheshimu. Katika Biblia, hajatupatia orodha ndefu ya mambo madogo-madogo ambayo tunapaswa kufanya na ambayo hatupaswi kufanya. Badala yake, anachochea uwezo wetu wa kufikiri kupitia masimulizi halisi ya maisha, unabii wenye kusisimua, na ushauri unaofaa. Kupitia njia hizo, Neno la Mungu linatuchochea kumpenda na kumtii Yehova kutoka moyoni.

Kwa nini tunapaswa kutafakari kuhusu jinsi Yehova alivyoshughulika na watumishi wake wakati uliopita? (Tazama fungu la 15)

15. (a) Nĩatĩa Jehova onanĩtie arĩ bata na barĩa bathoomaga Rũteto rwawe? (b) Kĩrĩ mbica ĩjĩ, kamwarĩ gaka kaniini, mũtaana ũmwĩthĩ, na mwarĩ-wa-baaba ũmũkũrũ barĩthũgaanĩria antũ barĩkũ barĩa bagweti Bibiriene? (Kĩa. 39:1, 10-12; 2 An. 5:1-3; Luka 2:25-38)

15 Biblia inafunua kwamba Yehova anapendezwa sana nasi. Jinsi gani? Neno lake limejaa masimulizi yanayoeleza kuhusu hisia za wanadamu. Tunaweza kuelewa hisia za wale wanaotajwa katika Biblia kwa sababu walikuwa watu wenye “hisia kama zetu.” (Yak. 5:17) Jambo muhimu zaidi, kwa kuchunguza jinsi alivyoshughulika na watu walio kama sisi, tunaweza kuelewa waziwazi zaidi kwamba “Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema.”​—Yak. 5:11.

16. Nĩmbi twiritanaga biegie Jehova rĩrĩa twathooma Bĩbiriene bwegie antũ barĩa baamwatĩrĩtie? (Isaya 55:7)

16 Biblia inafunua upendo wa Yehova kwetu kwa njia nyingine pia. Maandiko yanatuhakikishia kwamba Mungu wetu hatatuacha tunapofanya makosa. Waisraeli walimtendea Yehova dhambi tena na tena; hata hivyo, walipotubu kikweli Mungu aliwasamehe. (Soma Isaya 55:7.) Wakristo wa karne ya kwanza pia walijua kwamba Mungu aliwapenda. Mtume Paulo aliongozwa na roho takatifu kuwahimiza waabudu wenzake ‘wamsamehe na kumfariji’ mwanamume ambaye alikuwa amefanya dhambi nzito lakini akatubu. (2 Kor. 2:6, 7;1 Kor. 5:1-5) Inapendeza sana kwamba Yehova hakuwakataa waabudu wake kwa sababu tu walifanya makosa! Badala yake, kwa upendo aliwasaidia, akawarekebisha, na kuwakaribisha tena wawe rafiki zake. Anaahidi kufanya vivyo hivyo kwa watenda dhambi wote wanaotubu leo.​—Yak. 4:8-10.

ONANIA NKAATHO TONTŨ BWA ‘KĨEWA GĨKĨEGA’ KĨA RŨTETO RWA MŨRUNGU

17. Nĩkĩ Bibiria ĩrĩ kĩewa kĩa gĩtũmi mono?

17 Yehova ametupatia zawadi maridadi. Kwa nini Neno lake ni la pekee sana? Kama ambavyo tumejifunza, Biblia inafunua hekima ya Mungu, haki yake, na upendo wake. Kitabu hicho kinathibitisha kwamba Yehova anataka tumjue. Anataka tuwe rafiki zake.

18. Nĩatĩa tũũmba kwonia Jehova tũrĩ na nkaatho tontũ bwa gũtwa ‘kĩewe gĩkĩega’ takĩo Bĩbiria?

18 Hatungependa kupuuza thamani ya “zawadi njema” ya Neno la Mungu. (Yak. 1:17) Basi, acheni tuendelee kuonyesha kwamba tunalithamini. Tunaweza kufanya hivyo kwa kusali, kusoma, na kutafakari maneno yake matakatifu. Tunapofanya hivyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mtungaji wake mkuu atabariki jitihada zetu, nasi “[tutapata] ujuzi kumhusu Mungu.”​—Met. 2:5.

RWĨMBO 98 Maandiko—Yaliongozwa na Roho ya Mungu

a Biblia inatusaidia kumkaribia Yehova. Tunaweza kujifunza nini kuhusu hekima, haki, na upendo wa Mungu katika kitabu hicho kitakatifu? Mambo tunayojifunza yanaweza kutusaidia kuthamini zaidi Neno la Mungu na kuelewa kwamba kwa kweli—Biblia ni zawadi kutoka kwa Baba yetu wa mbinguni.