Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 6

Mambo Yenye Biblia Inatufundisha Kuhusu Mutungaji Wake

Mambo Yenye Biblia Inatufundisha Kuhusu Mutungaji Wake

“Andika katika kitabu maneno yote yenye ninakuambia.”​—YER. 30:2.

WIMBO 96 Biblia Ni Kitabu ya Maana Sana

KIFUPI YA HABARI a

1. Juu ya nini tunamushukuru sana Yehova kwa kutupatia Biblia?

 TUNAMUSHUKURU sana Yehova Mungu kwa kutupatia Biblia! Mu Biblia muko mashauri ya hekima yenye inaweza kutusaidia tujue mambo ya kufanya wakati tunapambana na magumu leo. Yehova anatupatia pia tumaini ya muzuri sana juu ya wakati yenye kuya. Na jambo ya maana sana, anatumiaka Biblia juu ya kutuonyesha mambo mingi kuhusu utu wake. Tunaguswa sana wakati tunatafakari juu ya sifa zake za muzuri, na ile inatuchochea tumukaribie na tupende kabisa kuwa marafiki wake.​—Zb. 25:14.

2. Yehova alisaidia watu wamujue kupitia nini?

2 Yehova anapenda watu wamujue. Zamani alisaidia watu wamujue kupitia ndoto, maono, na hata malaika. (Hes. 12:6; Mdo. 10:3, 4) Lakini hatungeweza kujifunza juu ya zile ndoto, maono, na ujumbe wenye malaika walikuwa wanatoa kama ile mambo haikuandikwa. Njo maana Yehova alitumia watu ili ‘waandike katika kitabu’ mambo yenye alipenda tujue. (Yer. 30:2) Juu “njia ya Mungu wa kweli ni kamilifu,” tuko hakika kama namna yake ya kuzungumuza na siye ni ya muzuri sana na yenye kutuletea faida.​—Zb. 18:30.

3. Yehova alifanya nini ili tukuwe na Biblia mupaka leo? (Isaya 40:8)

3 Soma Isaya 40:8. Kwa maelfu ya miaka, Neno ya Mungu, Biblia, imeongoza muzuri wanaume na wanamuke waaminifu. Ile iliwezekana namna gani? Ile ni ulizo ya muzuri. Juu Maandiko iliandikwa kwanza ku vitabu vya kukunjwa vyenye viliharibika, njo maana, hatuna hata dokima ya ile maandishi ya kwanza-kwanza. Lakini, Yehova aliongoza watu fulani ili wafanye kopi za ile maandishi matakatifu. Hata kama wale wenye walifanya kopi hawakukuwa wakamilifu, walijikaza kukuwa waangalifu kabisa. Kwa mufano, mwanaume fulani mwenye elimu aliandika hivi kuhusu Maandiko ya Kiebrania: “Tofauti na vitabu vingine vya zamani, watu wenye walifanya kopi ya Biblia hawakubadilisha ujumbe wenye ulikuwa ndani.” Kwa hiyo, hata kama Biblia iliandikwa zamani ku vitabu vya kukunjwa vyenye viliharibika, na hata kama watu wenye walifanya kopi hawakukuwa wakamilifu, tuko hakika kama mambo yote yenye kuwa mu Biblia ni mawazo ya Yehova mwenye aliitunga.

4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Yehova njo anatupatia “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu.” (Yak. 1:17) Biblia ni moya kati ya zawadi za muzuri zenye Yehova ametupatia. Kwa kawaida, wakati mutu anatupatia zawadi fulani, ile inaonyesha kama anatujua muzuri na kama anajua mambo yenye tuko nayo lazima. Ni vile pia kuhusu Yehova, mwenye alitupatia Biblia. Tunajifunza mambo mingi juu yake wakati tunachunguza ile zawadi. Tunajifunza pia kama anatujua na kama anajua muzuri sana mambo yenye tuko nayo lazima. Mu hii habari, tutazungumuzia namna Biblia inahakikisha kama Yehova iko na hizi sifa tatu: Hekima, haki, na upendo. Kwanza tuzungumuzie namna Biblia inahakikisha kama Mungu iko na hekima.

BIBLIA INAHAKIKISHA KAMA MUNGU IKO NA HEKIMA

5. Ni mu njia gani moya Biblia inahakikisha kama Mungu iko na hekima?

5 Yehova anajua kama tuko na lazima ya mashauri yake yenye hekima. Biblia, zawadi yenye ametupatia, iko na hekima mingi sana. Mashauri yenye kuwa ndani inakuwaka na matokeo ya muzuri kwa watu. Biblia inabadilishaka maisha ya watu. Wakati Musa aliandika vitabu vya kwanza vya Biblia, aliambia hivi watu wa Mungu, ni kusema, Waisraeli: “Hili haliko neno lenye halina maana kwenu, lakini linamaanisha uzima wenu.” (Kum. 32:47) Wale wenye walitii mambo yenye ilikuwa mu ile Maandiko walikuwa na maisha ya muzuri na yenye furaha. (Zb. 1:2, 3) Hata kama Neno ya Mungu iliandikwaka zamani, ingali na nguvu ya kubadilisha maisha ya watu. Kwa mufano, ku jw.org, ku sehemu “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu,” kuko mifano mingi ya watu wenye walifanya mabadiliko makubwa mu maisha yao, na leo wako na maisha ya muzuri juu walianza kutii mashauri ya Biblia.​—1 Te. 2:13.

6. Juu ya nini tunasema kama hakuna kitabu yenye iko sawa Biblia?

6 Hakuna kitabu ingine yenye iko sawa Biblia. Juu ya nini tunasema vile? Juu Yehova Mungu, Mutungaji wa ile kitabu ni mweza-yote, ni wa milele, na iko na hekima kupita watu wote. Watu wanaendelea kusoma vitabu vingine hata kama mwenye aliviandikaka alishakakufa. Lakini, mashauri ya vile vitabu haiendeleake kuwa na faida. Tofauti na ile, kanuni za hekima zenye kuwa mu Biblia ni za milele, zinasaidiaka watu wa vizazi vyote na wa mu kila kipindi ya wakati. Wakati tuko nasoma Biblia na kutafakari juu ya mambo yenye tuko najifunza, Mutungaji anatumia roho yake takatifu ili kutusaidia tuone namna gani tunaweza kutumikisha mashauri yenye kuwa ndani mu maisha yetu. (Zb. 119:27; Mal. 3:16; Ebr. 4:12) Bila shaka, Mutungaji wa Biblia iko tayari kukusaidia. Ile njo inatuchochea tupende kusoma Biblia kwa ukawaida!

Ni mu njia gani Biblia imesaidia watu wa Yehova wakuwe na umoja zamani na leo? (Ona fungu ya 7-8)

7. Ni mu njia gani Biblia ilisaidia watu wa Mungu wakuwe na umoja zamani?

7 Biblia inasaidiaka watu wa Mungu wakuwe na umoja. Ile njo jambo ingine yenye kuwa mu Biblia, yenye inahakikisha kama Mungu iko na hekima. Wakati Waisraeli waliingia mu inchi ya ahadi, walikuwa naishi mu maeneo mbalimbali. Wamoja walikuwa wavuvi wa samaki, wengine walikuwa wachungaji wa ngombe, na wengine walikuwa walimaji. Ilikuwa mwepesi kwa Waisraeli wenye walikuwa naishi mu eneo moya kuacha kuhangaikia Waisraeli wenzao wenye walikuwa naishi mu maeneo ingine ya inchi. Lakini Yehova alifanya mipango ili Waisraeli wakuwe nakusanyika kwa ajili ya matukio mbalimbali ili kusikiliza Neno yake yenye kuandikwa wakati ilikuwa nasomwa na kufasiriwa. (Kum. 31:10-13; Ne. 8:2, 8, 18) Pima kuwazia namna Mwisraeli mwaminifu angejisikia wakati anafika Yerusalemu na pengine anaona mamilioni ya waabudu wenzake wa kutoka mu kila sehemu ya inchi! Ni mu ile njia njo Yehova alisaidia watu wake waendelee kuwa na umoja. Kisha, wakati kutaniko ya Kikristo ilianzishwa, mulikuwa wanaume na wanamuke wenye walikuwa nasema luga mingi na wenye walitoka fasi tofauti na wenye walikuwa na hali ya maisha tofauti. Lakini juu walipenda Maandiko, walimuabudu Mungu wa kweli kwa umoja. Wale wenye walifikia kuwa waamini walielewa Neno ya Mungu kupitia tu musaada wa waabudu wenzao na juu walikusanyika pamoya nao.​—Mdo. 2:42; 8:30, 31.

8. Ni mu njia gani Biblia iko nasaidia watu wa Yehova wakuwe na Umoja leo?

8 Mungu wetu mwenye hekima anaendelea kufundisha na kufanya watu wake wakuwe na umoja kupitia Biblia. Mu Biblia muko chakula ya kiroho yenye tuko nayo lazima sana. Tunakusanyika kwa ukawaida ku mikutano yetu ya kutaniko na ku mikusanyiko mikubwa ili kusikiliza wakati Maandiko inasomwa, inafasiriwa, na kuzungumuziwa. Kwa hiyo, Biblia ni chombo ya maana sana yenye Yehova anatumia ili kusaidia watu wake “wamutumikie bega kwa bega.”​—Sef. 3:9.

9. Inaomba mutu akuwe na sifa gani juu aelewe mambo yenye kuwa mu Biblia? (Luka 10:21)

9 Tuzungumuzie jambo ingine yenye inahakikisha kama Yehova iko na hekima. Aliandikisha sehemu mingi za Maandiko mu namna yenye kuwa mwepesi kwa wasomaji wanyenyekevu tu kuelewa. (Soma Luka 10:21.) Fasi yote watu wanasomaka Biblia. Mwanaume fulani mwenye elimu alisema kama “watu wengi wanasomaka Biblia sana, tena kwa uangalifu sana kupita vitabu vingine vyote.” Lakini, ni wanyenyekevu tu njo wanaielewaka na kutumikisha mambo yenye kuwa ndani.​—2 Ko. 3:15, 16.

10. Ni jambo gani ingine, yenye kuwa mu Biblia, yenye inahakikisha kama Yehova iko na hekima?

10 Mu Biblia muko jambo ingine yenye inahakikisha kama Yehova iko na hekima. Yehova anatumia Maandiko, hapana tu juu ya kutufundisha kwa ujumla, lakini pia ili kufundisha na kufariji kila mumoja wetu kipekee. Wakati tunasoma Biblia, tunaweza kujionea kama Yehova anapendezwa na kila mutu kipekee. (Isa. 30:21) Wakati unapambana na magumu, ni mara ngapi ulisoma mu Maandiko jambo fulani yenye ilionekana sawa vile iliandikwa tu kwa ajili yako? Bila shaka, mamilioni ya watu wanapendezwaka na Biblia. Nini njo inafanya mutu apate mu Biblia habari yenye inapatana kabisa na mambo yenye iko nayo lazima? Ni juu tu Mutungaji wa Biblia iko na hekima sana kupita watu wote.​—2 Ti. 3:16, 17.

BIBLIA INAHAKIKISHA KAMA MUNGU IKO NA HAKI

11. Wakati Biblia ilikuwa inaandikwa, Yehova alifanya nini ili kuonyesha kama hana ubaguzi?

11 Haki ni sifa ingine ya Yehova. (Kum. 32:4) Mara mingi mutu mwenye haki hakuwake pia na ubaguzi; na njo vile Yehova iko. (Mdo. 10:34, 35; Ro. 2:11) Yehova aliandikisha Biblia mu luga mingi zenye watu walikuwa nasema zamani. Ile inaonyesha kama hana ubaguzi. Vitabu 39 vya kwanza vya Biblia viliandikwa zaidi sana mu Kiebrania. Zamani watu wa Mungu walikuwa naelewa muzuri ile luga. Lakini mu karne ya kwanza, watu wengi walikuwa nasema Kigiriki. Njo maana, vitabu 27 vya mwisho vya Biblia viliandikwa mu ile luga. Yehova hakupenda Neno yake iandikwe mu luga moya tu. Leo, karibu watu miliare munane wanasemaka luga mingi. Kwa hiyo, ni nini inaweza kusaidia wale watu wengi wajifunze juu ya Yehova?

12. Ni mu njia gani moya unabii wa Danieli 12:4 uko natimia mu hizi siku za mwisho?

12 Kupitia nabii Danieli, Yehova aliahidi kama wakati ya mwisho “ujuzi wa kweli” wenye kuwa mu Biblia “utakuwa mwingi.” Watu wengi wangeelewa ule ujuzi. (Soma Danieli 12:4.) Kazi ya kutafsiri, ya kutoa, na kugawanya Biblia na vichapo vyenye kutegemea Biblia njo njia moya inafanya ujuzi ukuwe mwingi. Biblia njo kitabu yenye imetafsiriwa na kugawanywa sana mu dunia. Wakati fulani tafsiri za Biblia zenye kutafsiriwa na kompanyi fulani zinakuwaka bei sana. Lakini, watu wa Yehova wametafsiri Neno ya Mungu, ikuwe kwa sehemu ao yote, mu luga zaidi ya 240. Na kila mutu anaweza kuipata bila kulipa. Ile inafanya watu wa mataifa yote wajifunze kuhusu “habari njema ya Ufalme” mbele ule mwisho ufike. (Mt. 24:14) Mungu wetu mwenye haki iko napatia watu wengi kadiri inawezekana nafasi ya kumujua. Anafanya vile juu anatupenda sana.

BIBLIA INAHAKIKISHA KAMA MUNGU IKO NA UPENDO

13. Juu ya nini tunaweza kusema kuwa Biblia inahakikisha kama Mungu iko na upendo? (Yohana 21:25)

13 Biblia inatuhakikishia kama sifa kubwa zaidi ya Yehova ni upendo. (1 Yo. 4:8) Fikiria mambo yenye Yehova aliandikisha na mambo yenye hakupenda iandikwe mu Biblia. Aliandikisha tu mambo yenye tuko nayo lazima ili tukuwe na urafiki pamoya naye, tukuwe na maisha yenye furaha leo, na ili tupate uzima wa milele. Lakini, juu Yehova anatupenda hakuandikisha habari zingine mingi zaidi zenye hatuna nazo lazima.​—Soma Yohana 21:25.

14. Ni mu njia gani ingine mambo yenye kuwa mu Biblia inahakikisha kama Yehova anatupenda?

14 Yehova anaonyesha pia kama anatupenda kwa kuzungumuza na siye mu njia yenye inatuheshimisha. Mu Biblia, hatupatie liste ya murefu sana ya sheria kuhusu mambo yenye tunapaswa kufanya na yenye hatupaswe kufanya mu kila sehemu ya maisha yetu. Kuliko kufanya vile, anatumia habari juu ya maisha ya watu, maunabii yenye kufurahisha, na mashauri ya hekima yenye itatusaidia tukamate maamuzi ya muzuri. Kupitia ile mambo yote, Neno ya Mungu inatuchochea tumupende na tumutii kwa kupenda.

Juu ya nini tunapaswa kufikiri sana kuhusu namna Yehova alitendea watumishi wake zamani? (Ona fungu ya 15)

15. (a) Yehova alionyesha namna gani kama alihangaikia wale wenye walikuwa wanasoma Neno yake? (b) Vile picha inaonyesha, ule mutoto mwanamuke, ule ndugu, na ule dada mwenye kuzeeka wako natafakari juu ya watu gani wenye kuzungumuziwa mu Biblia? (Mwa. 39:1, 10-12; 2 Fa. 5:1-3; Lu. 2:25-38)

15 Biblia inahakikisha kama Yehova anatuhangaikiaka sana. Namna gani? Mu Biblia muko habari mingi sana zenye zinaonyesha vile watu wanajisikiaka. Tunaweza kuelewa namna watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia walikuwa najisikia juu walikuwa watu wenye kuwa na “hisia kama zetu.” (Yak. 5:17) Jambo ya maana zaidi, wakati tunachunguza namna Yehova alitendea watu wenye walikuwa sawa vile siye, tunaelewa muzuri zaidi kama “ni mwenye upendo mwingi sana na mwenye rehema.”​—Yak. 5:11.

16. Wakati tunasoma mu Biblia habari juu ya watu fulani wenye walimukosea Yehova, ile inatufundisha nini juu yake? (Isaya 55:7)

16 Biblia inazungumuzia njia ingine yenye inahakikisha kama Yehova anatupenda. Maandiko inatuhakikishia kama Mungu wetu hatatuacha wakati tunafanya makosa. Waisraeli walimukosea Yehova Mungu tena na tena. Lakini, wakati walikuwa natubu kikweli alikuwa anawasamehe. (Soma Isaya 55:7.) Wakristo wa karne ya kwanza walijua pia kama Mungu aliwapenda sana. Wakati aliongozwa na roho ya Mungu, Mutume Paulo aliambia waamini wenzake ‘wasamehe na kufariji’ mutu fulani mwenye aliendelea kufanya zambi nzito lakini akatubu. (2 Ko. 2:6, 7; 1 Ko. 5:1-5) Inafurahisha kabisa kuona kama Yehova hakuacha waabudu wake juu tu walimukosea! Lakini, aliwasaidia kwa upendo, aliwarekebisha, na aliwaalika ili wakuwe marafiki wake tena. Anaahidi kufanyia pia vile watenda-zambi wote wenye wanatubu leo.​—Yak. 4:8-10.

SAMINI “ZAWADI YA MUZURI” YA NENO YA MUNGU

17. Juu ya nini Neno ya Mungu ni zawadi ya maana sana?

17 Yehova ametupatia zawadi ya muzuri. Juu ya nini Neno ya Mungu ni ya maana sana? Vile tumejifunza, Biblia inahakikisha kama Mungu iko na hekima, haki, na upendo. Hii kitabu inaonyesha kama Yehova anapenda tumujue na anapenda tukuwe marafiki wake.

18. Tunaweza kufanya nini ili kumushukuru Yehova kwa kutupatia Biblia yenye ni “zawadi ya muzuri?”

18 Tunapaswa kukamata kwa uzito Neno ya Mungu juu ni “zawadi ya muzuri.” (Yak. 1:17) Kwa hiyo basi, tuendelee kumushukuru Mungu kwa kutupatia ile zawadi. Tunaweza kufanya vile kwa kusoma maneno matakatifu yenye kuwa ndani na kufikiri sana juu ya ile maneno. Tuko hakika kama ikiwa tunafanya vile, Yehova Mungu, Mutungaji mukubwa wa Biblia, atabariki bidii yetu na atatusaidia ‘tupate ujuzi juu yake.’​—Mez. 2:5.

WIMBO 98 “Kila Andiko Limeongozwa na Roho ya Mungu”

a Biblia inatusaidia kumukaribia Yehova. Kile kitabu kitakatifu kinatufundisha nini kuhusu hekima, haki, na upendo wa Mungu? Mambo yenye tutajifunza, inaweza kutusaidia tumushukuru sana Yehova Mungu, Baba yetu wa mbinguni, kwa kutupatia Biblia. Tena, inaweza kutusaidia tuione kuwa zawadi.