Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 9

Usamini Zawadi ya Mungu ya Uzima

Usamini Zawadi ya Mungu ya Uzima

“Kupitia kwake tuko na uzima na tunatembea na tuko.”​—MDO. 17:28.

WIMBO 141 Uzima Ni Muujiza

KIFUPI YA HABARI a

1. Nini inaonyesha kama Yehova anaona uzima wetu kuwa wa maana sana?

 WAZIA rafiki yako anakupatia nyumba. Ile nyumba ilishaanza kutoka rangi na ilishatoboka manjanja. Lakini, hata kama iko vile, iko na samani ya mamilioni ya dolare. Kusema kweli, utaifurahia na utaichunga muzuri. Vilevile, Yehova ametupatia zawadi yenye samani sana, ni kusema, zawadi ya uzima. Bila shaka, juu Yehova alitoa Mwana wake kuwa bei ya ukombozi kwa ajili yetu, ile inaonyesha kama anaona uzima wetu kuwa wa maana sana.​—Yoh. 3:16.

2. Kulingana na 2 Wakorinto 7:1, Yehova anapenda tufanye nini?

2 Yehova njo Chanzo ya uzima. (Zb. 36:9) Mutume Paulo pia aliamini ile kweli wakati alisema hivi: “Kupitia kwake tuko na uzima na tunatembea na tuko.” (Mdo. 17:25, 28) Kwa hiyo, tunaweza kusema kama uzima wetu ni zawadi kutoka kwa Mungu. Kwa upendo anatupatia mambo yenye tuko nayo lazima juu tuendelee kuishi. (Mdo. 14:15-17) Lakini Yehova hatulindake kimuujiza. Njo maana, anapenda tufanye yote yenye tunaweza juu tukuwe na afya ya muzuri na tuendelee kumutumikia. (Soma 2 Wakorinto 7:1.) Juu ya nini tunapaswa kulinda afya na uzima wetu, na tunaweza kufanya vile namna gani?

USAMINI ZAWADI YA UZIMA

3. Ni sababu gani moya yenye inafanya tujikaze kuwa na afya ya muzuri?

3 Sababu moya yenye inafanya tujikaze kuwa na afya ya muzuri ni juu tuweze kumutumikia Yehova kwa uwezo wetu wote. (Mk. 12:30) Tunapenda kutoa ‘miili yetu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu.’ Njo maana tunaepuka kufanya mambo fulani yenye tunajua kama inaweza kuharibisha afya yetu. (Ro. 12:1) Kusema kweli, hata tufanye jambo gani hatuwezi kuzuia ugonjwa utupate. Lakini, tunafanya yenye tunaweza juu tunapenda kuonyesha Baba yetu wa mbinguni kama tunasamini zawadi ya uzima.

4. Mufalme Daudi alipenda kufanya nini?

4 Mufalme Daudi alifasiria juu ya nini alisamini zawadi ya uzima wakati aliandika hivi: “Kuko faida gani kama ninakufa, kama ninashuka katika shimo? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yataongea kuhusu uaminifu wako?” (Zb. 30:9) Inawezekana Daudi aliandika ile maneno mu kipindi yenye ilikaribia mwisho wa maisha yake. Hata vile, alipenda kuendelea kuishi na kuwa na afya ya muzuri, kadiri inawezekana, ili kumutumikia Yehova. Bila shaka, siye wote tunakuwaka na ile azimio.

5. Hata kama tulishazeeka na kugonjwa namna gani, tunaweza kufanya nini?

5 Magonjwa na uzee vinaweza kutuzuia kufanya mambo mingi yenye tulikuwa nafanya zamani. Ile inaweza kutufanya tuvunjike moyo ao kuhuzunika. Lakini tunapaswa kufanya yote yenye tunaweza juu ya kuhangaikia afya yetu. Juu ya nini? Juu hata kama tulishazeeka na kugonjwa namna gani, tunaweza kuendelea kumutumikia Yehova, sawa vile Mufalme Daudi. Ni jambo yenye kutia moyo sana kujua kama Mungu wetu anatusamini ijapokuwa uzaifu wetu! (Mt. 10:29-31) Hata kama tunakufa, anatamani sana kutufufua. (Yob. 14:14, 15) Njo maana, vile tungali wazima, tufanye yote yenye tunaweza juu ya kulinda afya yetu na uzima wetu.

UEPUKE KUFANYA MAMBO YENYE ITAKUUMIZA

6. Yehova anapenda tuonyeshe sifa gani kuhusu kula na kunywa?

6 Hata kama Biblia haiko kitabu yenye inazungumuzia namna ya kuhangaikia afya yako na nini njo unapaswa kula, lakini inazungumuzia mawazo mingi ya Yehova juu ya ile mambo. Kwa mufano, anatuambia tuepuke “mambo yenye kuleta mahangaiko,” yenye inaweza kuharibisha mwili wetu. (Muh. 11:10) Biblia inasema kama tunapaswa kuepuka ulafi na ulevi juu inaweza kuharibisha afya yetu. (Mez. 23:20) Yehova anapenda tuonyeshe sifa ya kujizuia kuhusu kula na kunywa.​—1 Ko. 6:12; 9:25.

7. Namna gani Mezali 2:11 inaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri kuhusu afya yetu?

7 Tunaweza kukamata maamuzi yenye kuonyesha kama tunamushukuru sana Yehova juu ya zawadi ya uzima kwa kutumia uwezo wetu wa kufikiri. (Zb. 119:99, 100; soma Mezali 2:11.) Kwa mufano, tutachagua kwa hekima chakula yenye tutakula. Kama tunapendaka chakula fulani lakini tunajua kama inatugonjweshaka, uwezo wetu wa kufikiri utatusaidia tusiikule. Tutaonyesha pia kama tunatumia muzuri uwezo wetu wa kufikiri kwa kulala vya kutosha, kufanya mazoezi kwa ukawaida, na kwa kuendelea kufanya usafi wa mwili na wa nyumba yetu.

UISHI KWA USALAMA

8. Ni mambo gani yenye Biblia inazungumuzia yenye kuonyesha kama Mungu anaona usalama kuwa jambo ya maana?

8 Mu Sheria yenye Yehova alipatia Waisraeli, mulikuwa maagizo kuhusu mambo ya kufanya juu ya kuepuka aksida ku kazi na ku nyumba. (Kut. 21:28, 29; Kum. 22:8) Kama mutu anaua mwenzake bila kutazamia, ile ilikuwa na matokeo ya mubaya sana. (Kum. 19:4, 5) Sheria ilisema kama, ikiwa mutu anaumiza mutoto mwenye hayazaliwa alipaswa kupewa malipizi. (Kut. 21:22, 23) Maandiko inaonyesha wazi kama Yehova anapenda tuishi kwa usalama.

Mu hizi hali, ni mu njia gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia uzima? (Ona fungu ya 9)

9. Ni mambo gani tunapaswa kufanya juu ya kuepuka aksida?(Ona pia picha.)

9 Tunaonyesha kama tunasamini zawadi ya Mungu ya uzima kwa kujikaza kuishi kwa usalama ku nyumba na ku kazi. Kwa mufano, kama tunapenda kutupa vitu vyenye vinaweza kutuumiza, vitu vyenye kuwa na sumu, ao kutupa dawa, tunapaswa kufanya vile mu njia yenye haitaumiza wengine, na tunapaswa kuvitia mbali na watoto. Wakati tunawasha moto, tunatokosha maji, na kutumia vyombo vyenye vinatumikaka na courant, tunapaswa kuwa waangalifu. Tena, hatupaswe kutoka pale kama hatuyamaliza kuvitumikisha. Haiko muzuri kutembeza gari kama tuko nakunywa dawa fulani, kama tulikunywa pombe, ao kama tulishachoka sana na tunaona kama ni hatari kufanya vile. Tunaepuka pia kutumia telefone juu tusikengeushwe wakati tuko natembeza.

WAKATI MUSIBA FULANI UNATOKEA

10. Tunapaswa kufanya nini mbele musiba utokee na wakati unatokea?

10 Wakati fulani, hatuwezi kuzuia hali fulani ya mubaya itokee. Sawa vile misiba ya asili, magonjwa ya kuambukiza, na vita. Lakini wakati misiba ya vile inatokea, tunaweza kufanya yetu yote ili kuwa salama kadiri inawezekana, na tunaweza kuokoa uzima wetu kwa kutii wakati wenye mamlaka wanatuomba tutoke mu eneo ao wakati wanatupatia maagizo ingine. (Ro. 13:1, 5-7) Ni muzuri kujitayarisha mbele ya wakati, njo maana tunapaswa kufuata maagizo yenye inatolewa na wenye mamlaka wa mu eneo yetu yenye itatusaidia tukuwe tayari wakati musiba unatokea. Kwa mufano, ni muzuri kuwa na maji na chakula yenye haitaoza, na pia vitu vya musaada wa kwanza

11. Tunapaswa kufanya nini kama ugonjwa fulani wa kuambukiza unaenea fasi kwenye tunaishi?

11 Tunapaswa kufanya nini kama ugonjwa fulani wa kuambukiza unaenea fasi kwenye tunaishi? Tunapaswa kutii maagizo ya wenye mamlaka, sawa vile kunawa mikono, kuheshimia umbali, kuvala maske, na kujitenga na wengine. Wakati tunajikaza kufanya ile mambo yote tutaonyesha kama tunasamini zawadi ya Mungu ya uzima.

12. Wakati musiba fulani unatokea, namna gani kanuni yenye kuwa mu Mezali 14:15 inaweza kutusaidia kuwa waangalifu wakati habari fulani inaenea mu eneo?

12 Wakati musiba fulani unatokea, tunaweza kusikia marafiki ao majirani wetu wako naongea kuhusu habari fulani ya uongo, tunaweza pia kusikia habari ya vile kupitia vyombo vya kupashana habari. Kuliko kuamini “kila neno” yenye tunasikia, tunapaswa kusikiliza habari ya kweli yenye inatolewa na watu wenye kuwa na mamlaka ao yenye inatolewa na wanganga. (Soma Mezali 14:15.) Ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza na wa biro za tawi wanajikazaka kupata habari za kweli mbele ya kutoa muongozo kuhusu mikutano ya kutaniko na kazi ya kuhubiri. (Ebr. 13:17) Tukifuata ile maagizo, tunajilinda na tunalinda wengine. Ile inasaidia pia watu wakuwe na mawazo ya muzuri juu ya Mashahidi wa Yehova.​—1 Pe. 2:12.

KUEPUKA DAMU

13. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunasamini zawadi ya Mungu ya uzima kuhusu mambo ya damu?

13 Watu wengi wanajua kama Mashahidi wa Yehova wanaamini kuwa damu ni kitu kitakatifu. Njo maana, tunatii Sheria ya Yehova kwa kukatala kutiwa damu hata wakati wa matunzo yenye inaomba kutenda haraka. (Mdo. 15:28, 29) Lakini, ile haimaanishe kama tunapenda kufa. Tofauti na ile, tunasamini zawadi ya Mungu ya uzima. Tunatafutaka musaada wa wanganga wenye kuwa na ufundi na wenye wanapendaka kutunza muzuri bila kutumia damu.

14. Tunaweza kufanya nini juu ya kupunguza hatari ya kupata magonjwa yenye itaomba kufanyiwa upasuaji wa haraka?

14 Kama tunajikaza kufuata mapendekezo yenye tumezungumuzia mu hii habari kuhusu afya, pengine tunaweza kuepuka kufanyiwa upasuaji ao kupata matunzo ya nguvu. Kama tuko na afya ya muzuri, tunaweza kupona haraka kisha kufanyiwa upasuaji. Juu ya kupunguza hatari ya kupata magonjwa yenye itaomba kufanyiwa upasuaji wa haraka tunapaswa kuendelea kufanya usafi wa nyumba, wa fasi kwenye tunatumikia, na kuendelea kabisa kutii sheria juu ya namna ya kutembeza gari.

Juu tunasamini sana uzima, tunajazaka karte DPA na kujikaza kuwa nayo kila wakati (Ona fungu ya 15) d

15. (a) Juu ya nini ni jambo ya lazima tukuwe na karte DPA yenye kuwa na habari za sasa? (Ona pia picha.) (b) Sawa vile video inaonyesha, namna gani tunaweza kukamata maamuzi ya muzuri kuhusu matumizi ya damu mu matunzo?

15 Juu tunasamini zawadi ya uzima, tunajazaka karte yenye inaitwa pas de sang na tunajikazaka kuwa nayo kila wakati.  b Kupitia hii karte, tunaonyesha musimamo wetu kuhusu damu na matunzo fulani yenye tunakubali na yenye hatukubali. Karte yako DPA iko na habari za sasa? Kama unapenda kuijaza ao kuifanya upya haupaswe kuchelewa. Kama tunafanya vile mbele ya wakati, ile itasaidia tusipoteze wakati kwa kuzungumuza na wanganga juu ya aina ya matunzo yenye tunapenda kupata. Na ile itatusaidia kuwa hakika kama tumepata matunzo ao dawa fulani yenye haitatutia mu hatari. c         

16. Unaweza kufanya nini kama haujue namna ya kujaza karte DPA?

16 Hata kama tuko vijana ao tuko na afya ya muzuri namna gani, siye wote tunaweza kupatwa na aksida ao kugonjwa. (Muh. 9:11) Njo maana ni jambo ya hekima kujaza karte DPA. Kama haujue namna ya kujaza ile karte, utafute musaada kwa wazee wa kutaniko yako, juu kwa kawaida wanajuaka namna ya kujaza ile karte. Lakini, hawatakukamatia maamuzi kuhusu aina ya matunzo yenye utapata. Ile ni daraka yako. (Gal. 6:4, 5) Wanaweza kukusaidia uelewe muzuri mawazo yako na kuandika musimamo wako.

UKUWE NA USAWAZIKO

17. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tuko na usawaziko kuhusu mambo ya afya?

17 Maamuzi ya mingi yenye tunakamataka kuhusu afya yetu na matunzo inategemea mambo yenye tunajifunzaka mu Biblia. (Mdo. 24:16; 1 Ti. 3:9) Wakati tunakamata maamuzi na kuiambia wengine, ni muzuri kutumikisha kanuni yenye kuwa mu Wafilipi 4:5 yenye inasema hivi: “Usawaziko wenu ujulikane kwa watu wote.” Kama tuko na usawaziko hatutakuwa na wasiwasi kuhusu afya yetu na hatutakaza wengine wakuwe na mawazo sawa yetu juu ya mambo ya afya. Tunapenda na kuheshimia ndugu na dada zetu hata kama maamuzi yenye wanakamata iko tofauti na yetu.​—Ro. 14:10-12.

18. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha shukrani yetu juu ya zawadi ya uzima?

18 Tunaonyesha shukrani kwa Yehova, Chanzo ya uzima, kwa kulinda uzima wetu na kwa kumutumikia kwa uwezo wetu wote. (Ufu. 4:11) Kwa sasa, tunaendelea kugonjwa na kufikiwa na misiba. Lakini, Muumbaji wetu hapendi tuishi maisha ya vile. Njo maana hivi karibuni atatupatia uzima wa milele na tutaishi bila maumivu wala kifo. (Ufu. 21:4) Mbele ile wakati ifike, tuko na furaha ya kuishi na ya kumutumikia Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, Yehova!

WIMBO 140 Utaishi Milele!

a Hii habari itatusaidia kuonyesha shukrani zaidi juu ya zawadi ya Mungu ya uzima. Tutaona mambo yenye tunaweza kufanya juu tukuwe na afya ya muzuri na kuwa salama wakati musiba fulani unatokea, na namna tunaweza kuepuka kuangukia mu aksida fulani. Tutaona pia mambo yenye tunapaswa kufanya juu ya kujitayarisha kwa ajili ya matunzo yenye inaomba kutenda haraka.

b Ile karte inaitwa pia DPA (Instruction médical/Désignation d’une personne de confiance)

d MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu fulani kijana iko najaza karte DPA na anajikaza kukuwa nayo fasi yote.