Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 12

Ujifunze Mambo Mingi Zaidi juu ya Yehova Kupitia Uumbaji

Ujifunze Mambo Mingi Zaidi juu ya Yehova Kupitia Uumbaji

“Sifa zake zenye hazionekane zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaonekana kupitia vitu vyenye vilifanywa.”​—RO. 1:20.

WIMBO 6 Mbingu Zinatangaza Utukufu wa Mungu

KIFUPI YA HABARI a

1. Nini njo ilimusaidia Yobu afikie kumujua Yehova muzuri zaidi?

 MU MAISHA yake, Yobu alizungumuza na watu wengi. Lakini mazungumuzo yenye ilikuwa ya pekee ni ile yenye alifanya na Yehova Mungu. Mu ile mazungumuzo, Yehova alimuambia Yobu aangalie vitu fulani vya ajabu vyenye aliumba. Alifanya vile juu ya kumusaidia aelewe kama iko na hekima na uwezo wa kuhangaikia watumishi wake. Kwa mufano, alimukumbusha Yobu kama anahangaikiaka wanyama, kwa hiyo, angemuhangaikia yeye pia. (Yob. 38:39-41; 39:1, 5, 13-16) Wakati alifikiria uumbaji, Yobu alijifunza mambo mingi ya muzuri kuhusu sifa za Mungu.

2. Juu ya nini wakati fulani haikuwake mwepesi kuchunguza kwa uangalifu uumbaji?

2 Na siye pia tunaweza kujifunza mambo mingi zaidi juu ya Mungu wetu wakati tunachunguza kwa uangalifu vitu vyenye aliumba. Lakini, pengine kila mara haikuwake mwepesi kwetu kufanya vile. Kama tunaishi mu muji, pengine hatutaona kila siku mambo mingi yenye Yehova aliumba. Hata kama tunaishi mu kijiji, tunaweza kukosa wakati ya kuchunguza kwa uangalifu vitu vyenye Yehova aliumba. Kwa hiyo, tuone basi juu ya nini tunapaswa kupanga wakati na kujikaza sana ili kuchunguza kwa uangalifu uumbaji. Tutaona pia namna Yehova na Yesu walifundisha mambo fulani kupitia uumbaji. Tena, tutaona mambo yenye tunaweza kufanya juu tujifunze mambo mingi zaidi kupitia uumbaji.

JUU YA NINI TUNAPASWA KUCHUNGUZA KWA UANGALIFU UUMBAJI?

Yehova alipenda Adamu afurahie uumbaji na apatie wanyama majina (Ona fungu ya 3)

3. Nini inaonyesha kama Yehova alipenda Adamu afurahie uumbaji?

3 Yehova alipenda mwanadamu wa kwanza afurahie uumbaji. Wakati aliumba Adamu, alimutia mu paradiso ya muzuri juu aishi ndani na alimupatia kazi ya kuilinda na kuitunza. (Mwa. 2:8, 9, 15) Wazia namna Adamu alifurahi wakati aliona mbegu na mimea viko naota. Adamu alikuwa na pendeleo kubwa sana ya kuhangaikia bustani ya Edeni! Yehova alimuambia pia Adamu apatie wanyama majina. (Mwa. 2:19, 20) Kama Yehova angependa, yeye mwenyewe angepatia kila munyama jina, lakini, alimupatia Adamu ile kazi. Bila shaka, mbele Adamu apatie wanyama majina, alijifunza juu yao kwa uangalifu na aliwachunguza ili kuona namna walikuwa wanaonekana na namna walikuwa natenda. Adamu alipaswa kufurahia kufanya vile. Bila shaka, ile ilimusaidia aelewe kama Yehova iko na hekima na kama vitu vyote vyenye aliumba ni vya muzuri sana.

4. (a) Juu ya nini tunapaswa kuchunguza kwa uangalifu uumbaji? (b) Kati ya vitu mbalimbali vyenye Yehova aliumba, weye unapendaka zaidi sana nini?

4 Tunapaswa kuchunguza kwa uangalifu uumbaji juu Yehova anapenda tufanye vile. Anatuambia hivi: “Muinue macho yenu mbinguni na muone.” Kisha anauliza hivi: “Ni nani ameumba vitu hivi?” Jibu ya ile ulizo iko wazi. (Isa. 40:26) Yehova aliumba vitu vyote vyenye kuwa mbinguni, ku dunia, na mu bahari. Vile vitu vyote vinatufundisha mambo mingi kumuhusu. (Zb. 104:24, 25) Fikiria pia namna Yehova alituumba. Alituumba na uwezo wa kufurahia vitu mbalimbali vyenye aliumba; njo maana, alitupatia uwezo wa kuona, kusikia, kugusa, kuonja, na kunusa.

5. Kulingana na Waroma 1:20, tutapata faida gani kama tunachunguza kwa uangalifu uumbaji?

5 Biblia inazungumuzia sababu ingine ya maana yenye inapaswa kutuchochea kuchunguza kwa uangalifu uumbaji. Unatufundisha sifa mbalimbali zenye Yehova iko nazo. (Soma Waroma 1:20.) Kwa mufano, kama unafikiria vitu vyenye Yehova aliumba, utaona kama ni vya ajabu. Vile vitu vinatufundisha kama Yehova iko na hekima sana. Fikiria pia chakula mbalimbali yenye unaweza kupenda kula. Ile yote inaonyesha kama Yehova anatupenda. Wakati tunajifunza sifa mbalimbali zenye Yehova iko nazo kupitia vitu vyenye aliumba, tunafikia kumujua muzuri zaidi, na ile inatusaidia tumukaribie zaidi. Sasa, tuzungumuzie namna Yehova alifundisha watu mambo fulani ya maana kupitia uumbaji.

MUNGU ANATUFUNDISHA JUU YAKE KUPITIA UUMBAJI

6. Tunaweza kujifunza nini wakati tunaangalia ndege wenye wako nahama?

6 Yehova amepanga wakati. Kila mwaka, kati ya mwisho wa Mwezi wa pili na mu katikati ya Mwezi wa tano, Waisraeli walikuwa naona korongo wenye walikuwa naruka na kuhamia upande wa kaskazini. Mungu aliambia Waisraeli kama “korongo katika anga anajua vipindi vyake.” (Yer. 8:7) Sawa vile tu Yehova amepanga wakati juu ya wale ndege, ameweka pia wakati yenye ataleta hukumu. Leo, kuangalia ndege wenye wako nahama kunafanya tutumainie kabisa kama Yehova “ameweka wakati” ya kuharibu huu ulimwengu muovu.​—Hab. 2:3.

7. Kuangalia ndege wenye wako naruka kunatuhakikishia nini? (Isaya 40:31)

7 Yehova anapatiaka nguvu watumishi wake. Kupitia Isaya, Yehova aliahidi kama atapatia watu wake nguvu ya ‘kuruka juu kwa mabawa kama tai’ wakati wako wazaifu ao wakati wanavunjika moyo. (Soma Isaya 40:31.) Waisraeli walizoea kuona tai wanaruka juu kwa mabawa bila kutumia nguvu mingi sana. Ni Yehova njo alipatia wale ndege ile nguvu. Ile inatuhakikishia kama anaweza pia kupatia nguvu watumishi wake! Wakati unaona ndege mwenye nguvu anaruka juu sana mu anga bila kutumia nguvu sana, ukuwe hakika kama Yehova anaweza kukupatia nguvu ya kupiganisha magumu yako.

8. Yobu alijifunza nini wakati alifikiria vitu vyenye Mungu aliumba, na tunaweza kujifunza nini?

8 Tunapaswa kumutumainia Yehova. Yehova alimusaidia Yobu amutumainie zaidi. (Yob. 32:2; 40:6-8) Alizungumuza naye juu ya vitu mbalimbali vyenye aliumba, kutia ndani nyota, mawingu, na miali ya umeme wa radi. Alizungumuzia pia wanyama, sawa vile ngombe-dume wa pori na farasi. (Yob. 38:32-35; 39:9, 19, 20) Ile yote inaonyesha kama zaidi ya nguvu ya ajabu yenye iko nayo, Yehova iko pia na upendo na hekima sana. Kupitia ile mazungumuzo, Yobu alifikia kumutumainia Yehova zaidi kupita zamani. (Yob. 42:1-6) Vilevile, wakati tunajifunza juu ya uumbaji, tunakumbuka kama Yehova iko na hekima na nguvu sana kutupita. Iko pia na uwezo na atamaliza magumu yetu yote. Kujua vile, kunaweza kufanya tumutumainie zaidi.

YESU ALIFUNDISHA JUU YA BABA YAKE KUPITIA UUMBAJI

9-10. Jua na mvua vinatufundisha nini juu ya Yehova?

9 Yesu alijua mambo mingi kuhusu uumbaji. Alikuwa na pendeleo ya kutumika pamoya na Baba yake wakati alikuwa naumba ulimwengu; na alikuwa “fundi wa kazi.” (Mez. 8:30) Kisha, wakati Yesu alikuwa ku dunia, alifundisha wanafunzi wake juu ya Baba yake kupitia uumbaji. Ona mambo fulani yenye alifundishaka.

10 Yehova anapendaka watu wote. Mu Mahubiri yake Kwenye Mulima, Yesu aliambia wanafunzi wake kuhusu jua na mvua; ile ni mambo yenye watu wengi hawakaziake sana uangalifu. Jua na mvua ni vitu vyenye vinatusaidia tuendelee kuishi. Kama Yehova hangependa, hangeangazia jua na hangeacha mvua inyeshee wale wenye hawamutumikie. Lakini, kwa upendo anaacha jua iangazie na mvua inyeshee watu wote. (Mt. 5:43-45) Yesu alitumia ule mufano ili kufundisha wanafunzi wake kama Yehova anapenda tupende watu wote. Wakati tunaona Yehova anaacha jua itue na mvua inyeshee watu wote, ile inaonyesha kama hana ubaguzi. Tunaweza kuiga upendo wake kwa kuhubiria watu wote.

11. Kuangalia kwa uangalifu ndege wa mbinguni, kunatutia moyo namna gani?

11 Yehova anatutimiziaka mahitaji yetu ya kimwili. Mu ileile mahubiri, Yesu alisema pia hivi: “Muangalie kwa uangalifu ndege wa mbinguni; hawapande mbegu ao kuvuna ao kukusanya katika madepo, lakini Baba yenu wa mbinguni anawalisha.” Inawezekana, watu wenye walikuwa namusikiliza Yesu waliona ndege wako naruka, wakati aliwauliza hivi: “Je, ninyi hamuko wa maana kuliko wao?” (Mt. 6:26) Ile ni njia ya upendo kabisa yenye Yesu alitumia juu ya kutuhakikishia kama Yehova atatutimizia mahitaji yetu ya kimwili! (Mt. 6:31, 32) Kujua vile, kutaendelea kutia moyo watumishi waaminifu wa Yehova. Dada fulani kijana, mwenye alikuwa painia mu Espagne, alivunjika moyo juu hakupata fasi ya muzuri ya kuishi. Lakini, alitiwa moyo wakati aliona ndege wako nakula mbegu na matunda fulani. Anasema hivi: “Kuangalia kwa uangalifu wale ndege kulinikumbusha kama Yehova anawahangaikia na kama atanihangaikia pia.” Wakati mufupi kisha pale, ule dada alipata fasi ya kuishi.

12. Kulingana na Matayo 10:29-31, tunaweza kujifunza nini juu ya Yehova kupitia ndege shomoro?

12 Yehova anasamini kila mumoja wetu. Mbele Yesu atume mitume wake kuhubiri, aliwatia moyo juu wasiogope watu wenye wangewatesa. (Soma Matayo 10:29-31.) Alifanya vile kwa kuzungumuzia ndege moya kati ya ndege wenye kujulikana sana mu Israeli: Ndege shomoro. Wale ndege walikuwa wa samani kidogo. Lakini, Yesu aliambia hivi wanafunzi wake: “Hakuna hata mumoja wao mwenye ataanguka chini bila Baba yenu kujua.” Alisema tena hivi: “Ninyi ni wa maana kuliko ndege shomoro wengi.” Kwa kusema vile, Yesu alihakikishia wanafunzi wake kama Yehova alisamini kila mumoja wao, kwa hiyo, hawakupaswa kuogopa wale wenye wangewatesa. Bila shaka, wakati wanafunzi wa Yesu walikuwa wanahubiri mu miji na mu vijiji walikumbuka maneno yake wakati waliona ndege shomoro. Kwa hiyo, wakati unaona ka ndege kadogo, ukumbuke kama Yehova anakusamini juu weye pia ‘uko wa maana kuliko ndege shomoro wengi.’ Juu Yehova iko nakusaidia, hauna lazima ya kuogopa wakati watu wanakutesa.​—Zb. 118:6.

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI JUU YA MUNGU KUPITIA UUMBAJI?

13. Tunaweza kufanya nini ili tujifunze mambo mingi zaidi kupitia uumbaji?

13 Tunaweza kujifunza mambo mingi zaidi juu ya Mungu kupitia uumbaji. Namna gani? Kwanza, tunapaswa kupanga wakati ya kuchunguza kwa uangalifu uumbaji. Pili, tunapaswa kufikiria mambo yenye uumbaji unatufundisha juu ya Yehova. Pengine kila mara haitakuwa mwepesi kufanya ile mambo mbili. Géraldine, dada wa Kameruni, anasema hivi: “Nilikomalia mu muji, kwa hiyo, iliomba nijikaze sana juu nichunguze kwa uangalifu uumbaji.” Muzee fulani mwenye kuitwa Alfonso, anasema hivi: “Nilijifunza kama nilikuwa na lazima ya kupanga wakati ya kuwa miye peke ili kuchunguza kwa uangalifu uumbaji na kufikiri sana juu ya mambo yenye ule uumbaji unanifundisha juu ya Yehova.”

Wakati Daudi aliangalia uumbaji, alifikiri sana juu ya mambo yenye ule uumbaji ulimufundisha juu ya Yehova (Ona fungu ya 14)

14. Daudi alijifunza nini wakati alifikiri sana juu ya uumbaji?

14 Daudi alifikiri sana juu ya uumbaji. Alimuambia Yehova hivi: “Wakati ninaona mbingu zako, kazi za vidole vyako, mwezi na nyota zenye umetayarisha, mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umuweke katika akili?” (Zb. 8:3, 4) Kusema kweli, wakati Daudi aliangalia mu anga usiku, aliona nyota na alizifurahia. Lakini pia, alifikiri sana juu ya mambo yenye zile nyota zilimufundisha juu ya Yehova Mungu. Alijifunza kama Yehova iko na hekima na nguvu sana. Wakati ingine, Daudi alifikiria namna mwili wake ulikuwa nakomala mu tumbo ya mama yake. Wakati alifikiri sana juu ya namna mwili wake uliumbwa mu njia ya ajabu, alifikia hata kuwa mwenye shukrani juu ya hekima ya Yehova.​—Zb. 139:14-17.

15. Leta mifano fulani ya vitu vyenye Yehova aliumba, vyenye vinaweza kutusaidia kujua muzuri sifa zake. (Zaburi 148:7-10)

15 Sawa vile Daudi, pengine ni mwepesi kwetu kupata kitu fulani yenye Yehova aliumba ili kukifikiria sana. Kuko vitu mingi vyenye vinaweza kutusaidia kujua muzuri sifa za Yehova. Kwa mufano, unaweza kuona kama Yehova iko na nguvu wakati unasikia kivukutu ya jua. (Yer. 31:35) Fikiria hekima ya Yehova wakati unaona ndege wanajenga chicha. Wakati unaangalia kitoto ya imbwa iko nazungusha-zungusha mukia, fikiria namna Yehova ni Mungu mwenye furaha na mwenye anapenda tukuwe pia na furaha. Na wakati unaona mama iko nacheza na mutoto wake, umushukuru sana Yehova juu iko na upendo. Tuko na nafasi mingi za kujifunza kuhusu Yehova juu vitu vyote vyenye aliumba, vikuwe vikubwa ao vya kidogo, vikuwe mbali ao karibu, vyote vinamusifu.​—Soma Zaburi 148:7-10.

16. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

16 Mungu wetu iko na hekima, upendo, na nguvu. Vitu vyote vyenye aliumba ni vya muzuri. Tunaweza kuona zile sifa na sifa zingine mingi kama tunachunguza kwa uangalifu uumbaji. Tuazimie basi kila mara kupanga wakati ya kuchunguza uumbaji na kufikiri juu ya mambo yenye ule uumbaji unaweza kutufudisha juu ya Yehova. Kama tunafanya vile, tutamukaribia zaidi Muumbaji wetu. (Yak. 4:8) Mu habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna wazazi wanaweza kufundisha watoto wao kupitia uumbaji juu wamukaribie Yehova.

WIMBO 5 Kazi za Mungu Ni za Ajabu

a Vitu vyote vyenye Yehova aliumba vinatushangaza. Kuanzia ku nguvu ya jua mupaka ku sehemu za kidogo-kidogo zenye zinafanyiza liua ya muzuri. Uumbaji unaweza pia kutufundisha mambo mingi juu ya sifa za Yehova. Mu hii habari, tutaona juu ya nini tunapaswa kuchunguza kwa uangalifu uumbaji na namna gani ile inaweza kutusaidia kumukaribia zaidia Mungu wetu.