Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 35

Muendelee Kuwa na Uvumilivu

Muendelee Kuwa na Uvumilivu

“Muvae. . . uvumilivu.”​—KOL. 3:12.

WIMBO 114 “Mukuwe na Uvumilivu”

KIFUPI YA HABARI a

1. Juu ya nini unafurahiaka watu wenye kuwa na uvumilivu?

 SIYE wote tunapendaka watu wenye kuwa na uvumilivu. Juu ya nini? Juu tunafurahiaka wale wenye wanaweza kungoya jambo fulani bila kukasirika. Na tunafurahiaka wakati wengine wanatuvumilia saa tunafanya makosa. Tena tulifurahi sana kuona vile mwalimu wetu wa Biblia alituvumilia wakati ilikuwa nguvu kwetu kujifunza, kukubali, ao kutumikisha mafundisho ya Biblia. Zaidi ya ile, tuko wenye shukrani kuona vile Yehova Mungu anatuvumiliaka!​—Ro. 2:4.

2. Ni mu hali gani inaweza kuwa nguvu kwetu kuwa na uvumilivu?

2 Wakati mutu anaonyesha uvumilivu, ile inatufurahishaka. Hata vile, pengine kila mara haikuwake mwepesi kwetu kuwa wavumilivu. Kwa mufano, inaweza kuwa nguvu kwetu kuendelea kutulia wakati tuko nangoya bisi, zaidi sana kama tulishachelewa. Pengine tunaweza kushindwa kuzuia kasirani yetu wakati wengine wanatukasirisha. Na wakati fulani, inaweza kuwa nguvu kwetu kuendelea kungoya ahadi ya Yehova ya dunia mupya. Unapenda kuwa na uvumilivu zaidi? Mu hii habari, tutaona namna ya kuwa na uvumilivu na juu ya nini ni jambo ya maana sana kuwa vile. Tutaona pia mambo yenye inaweza kutusaidia kuwa na uvumilivu zaidi.

KUWA NA UVUMILIVU MAANA YAKE NINI?

3. Mutu mwenye kuwa na uvumilivu anatendaka namna gani wakati wengine wanamuchokoza?

3 Tuone mambo ine yenye tunaweza kufanya ili kuonyesha kama tuko na uvumilivu. Kwanza, mutu mwenye kuwa na uvumilivu hakasirikake haraka. Anakuwaka mwenye kutulia na anaepukaka kulipiza kisasi wakati wengine wanamuchokoza ao wakati iko na mahangaiko. Mara ya kwanza yenye maneno “hakasirike haraka” inapatikana mu Biblia ni wakati Yehova anazungumuziwa kuwa “Mungu mwenye rehema na huruma, hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu na kweli.”​—Kut. 34:6.

4. Mutu mwenye kuwa na uvumilivu anatendaka namna gani wakati inamuomba kungoya?

4 Pili, mutu mwenye kuwa na uvumilivu anangoyaka kwa utulivu. Wakati jambo fulani inakawia kuliko vile ilitazamiwa, mutu mwenye kuwa na uvumilivu ataendelea kungoya bila kuchoka ao bila kukasirika. (Mt. 18:26, 27) Tunapaswa kungoya kwa uvumilivu mu hali mingi. Kwa mufano, tunapaswa kusikiliza kwa uvumilivu wakati mutu fulani iko naongea, bila kumukatiza. (Yob. 36:2) Tunapaswa pia kuwa wavumilivu wakati tuko nasaidia mwanafunzi wa Biblia aelewe fundisho fulani ya Biblia ao aachane na tabia fulani ya mubaya.

5. Ni mu hali gani ingine yenye tunapaswa kuonyesha uvumilivu?

5 Tatu, mutu mwenye kuwa na uvumilivu hatendake haraka bila kufikiri. Kusema kweli, mu hali fulani inaombaka kutenda haraka. Lakini, wakati mutu mwenye kuwa na uvumilivu iko na jambo ya maana ya kufanya, hakuwake haraka kuianza, ao hakuwake haraka kuimaliza. Kuliko kufanya vile, anahakikishaka kama iko na wakati wa kutosha ili kupanga mambo yenye atafanya. Kisha, anafanyaka ile kazi kwa wakati wenye alipanga.

6. Mutu mwenye kuwa na uvumilivu anatendaka namna gani wakati iko na magumu?

6 Ine, mutu mwenye kuwa na uvumilivu anavumiliaka magumu bila kulalamika. Kusema kweli, haiko mubaya kuambia waziwazi rafiki wa karibu namna tuko najisikia kuhusu magumu yetu. Lakini, mutu mwenye kuwa na uvumilivu atafanya yake yote ili kuendelea kuvumilia na wakati uleule anaendelea kuwa na mutazamo wenye kufaa. (Kol. 1:11) Juu tuko Wakristo, tunapaswa kuwa na uvumilivu mu zile hali zote. Juu ya nini? Tuzungumuzie sababu fulani.

JUU YA NINI UVUMILIVU NI SIFA YA MAANA SANA

Sawa vile mulimaji anangoyaka kwa uvumilivu kwa kutumainia kama atavuna mbegu kwa wakati wenye kufaa, tunangoyaka kwa uvumilivu na tuko hakika kama kwa wakati wenye kufaa Yehova atatimiza ahadi zake zote (Ona fungu ya 7)

7. Kulingana na Yakobo 5:7, 8, juu ya nini uvumilivu ni sifa ya maana sana? (Ona pia picha.)

7 Kama tuko na uvumilivu, tutaokolewa. Sawa vile watumishi waaminifu wa zamani, tunapaswa kungoya kwa uvumilivu Mungu atimize ahadi zake. (Ebr. 6:11, 12) Biblia inalinganisha hali yetu na hali ya mulimaji. (Soma Yakobo 5:7, 8.) Mulimaji anatumikaka sana juu ya kupanda mbegu na kuimwangia maji, lakini hajuake kabisa ni wakati gani itaota. Kwa hiyo, anangoyaka kwa uvumilivu na anakuwaka hakika kama ile mbegu itaota. Vilevile, na siye tunafanyaka kazi ya kiroho kwa bidii, hata kama ‘hatujue Bwana [wetu] atakuja siku gani.’ (Mt. 24:42) Tunangoyaka kwa uvumilivu na tunakuwaka hakika kama kwa wakati wenye kufaa Yehova atatimiza ahadi zake zote. Kama hatufanye vile, tunaweza kuchoka kungoya na kuacha kweli pole kwa pole. Tunaweza hata kuanza kutafuta vitu vyenye tunaweza kuwaza kama vitafanya tukuwe na furaha palepale. Lakini kama tuko na uvumilivu, tunaweza kuvumilia mupaka mwisho na kuokolewa.​—Mik. 7:7; Mt. 24:13.

8. Namna gani kuwa na uvumilivu kunaweza kutusaidia mu uhusiano wetu pamoya na wengine? (Wakolosai 3:12, 13)

8 Kama tuko na uvumilivu, tunaweza kuwa na uhusiano wa muzuri pamoya na wengine, tutasikiliza wengine kwa uangalifu wakati wako nasema. (Yak. 1:19) Na kama tuko na uvumilivu, tutaendeleza amani. Ile sifa itatuzuia tusitende haraka sana ao kusema jambo fulani yenye haifae wakati tuko na mahangaiko. Tena, kama tuko na uvumilivu, hatutakasirika haraka wakati mutu fulani anatukwaza. Kuliko kulipiza kisasi, ‘tutaendelea kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda.’​—Soma Wakolosai 3:12, 13.

9. Namna gani kuwa na uvumilivu kunaweza kutusaidia wakati inatuomba tukamate maamuzi? (Mezali 21:5)

9 Tena, kama tuko na uvumilivu, tutakamata maamuzi ya muzuri zaidi. Kuliko kukamata maamuzi haraka-haraka, tutafanya utafiti juu ya kuchunguza ni uamuzi gani njo wa muzuri sana. (Soma Mezali 21:5.) Kwa mufano, kama tuko natafuta kazi, pengine tunaweza kuitika kazi yoyote yenye tunapata hata kama inaweza kufanya tuanze kukosa mikutano fulani ao tusikuwe nahubiri tena sana. Lakini, kama tuko na uvumilivu, tutakamata wakati wa kuchunguza mambo, sawa vile fasi, saa, na matokeo yenye ile kazi inaweza kuwa nayo juu ya familia yetu na juu ya hali yetu ya kiroho. Tena, ile sifa itatusaidia tuepuke kukamata uamuzi wa mubaya.

MAMBO YA KUFANYA JUU TUKUWE NA UVUMILIVU ZAIDI

10. Mukristo anaweza kufanya nini juu akuwe na uvumilivu na aendelee kuwa nayo?

10 Umuombe Yehova akusaidie ukuwe na uvumilivu zaidi. Uvumilivu ni sehemu ya tunda ya roho. (Gal. 5:22, 23) Tunapaswa kumuomba Yehova atupatie roho yake takatifu na kumuomba atusaidie tukomalishe tunda ya ile roho. Kama tunajikuta mu hali yenye inatuomba tuonyeshe uvumilivu, tunapaswa ‘kuendelea kumuomba’ Yehova roho takatifu ili tuonyeshe uvumilivu. (Lu. 11:9, 13) Tunapaswa pia kumuomba atusaidie tuone mambo vile yeye anaiona. Na kisha kusali, tunapaswa kufanya yetu yote juu tuendelee kuwa wavumilivu kila siku. Kama tunaendelea kumuomba Yehova atusaidie tukuwe na uvumilivu na kama tunaendelea kufanya yetu yote juu ya kuonyesha ile sifa, atatusaidia tukuwe na uvumili zaidi hata kama hatukukuwaka na ile sifa zamani.

11-12. Ni mu hali gani Yehova alionyesha uvumilivu?

11 Utafakari juu ya mifano yenye kuwa mu Biblia. Mu Biblia muko mifano mingi ya watu wenye walikuwa na uvumilivu. Kama tunatafakari juu ya ile mifano, tunaweza kujifunza njia mbalimbali za kuonyesha uvumilivu. Mbele ya kuona mifano fulani kati ya ile, tuzungumuzie kwanza Yehova mufano mukubwa sana wa uvumilivu.

12 Mu bustani ya Edeni, Shetani alisema uongo juu ya jina ya Yehova na alimufanya Eva amuone Yehova kuwa mutawala mwenye hatawale kwa haki na upendo. Lakini, Yehova hakumuua ule muchongezi palepale; alionyesha sifa ya uvumilivu na kujizuia. Alijua kama itakamata wakati juu ya kuonyesha kama utawala wake njo wa muzuri sana. Na wakati iko nangoya, anaendelea kuvumilia uongo wote wenye uko nasemewa juu ya jina yake. Zaidi ya ile, Yehova anaendelea kungoya kwa uvumilivu juu watu wengi zaidi wakuwe na nafasi ya kupata uzima wa milele. (2 Pe. 3:9, 15) Ile inafanya mamilioni ya watu wafikie kumujua. Kama tunakaza uangalifu juu ya faida yenye uvumilivu wa Yehova unaleta, itakuwa mwepesi kwetu kungoya wakati wenye ataleta mwisho.

Uvumilivu utatusaidia tusikasirike haraka wakati wanatukasirisha (Ona fungu ya 13)

13. Namna gani Yesu aliiga kwa ukamili uvumilivu wa Baba yake? (Ona pia picha.)

13 Yesu aliiga kwa ukamili uvumilivu wa Baba yake na alionyesha ile sifa wakati alikuwa ku dunia. Kila mara haikukuwa mwepesi kwake kuonyesha uvumilivu, zaidi sana kuelekea waandishi na Mafarisayo wenye walikuwa wanafiki. (Yoh. 8:25-27) Hata vile, sawa Baba yake, Yesu hakukuwa nakasirika haraka. Hakulipiza kisasi wakati walimutukana ao kumuchokoza. (1 Pe. 2:23) Yesu alivumilia magumu bila kulalamika. Njo maana Biblia inatuambia ‘tufikirie sana ule mwenye amevumilia maneno makali kama hayo’! (Ebr. 12:2, 3) Kwa musaada wa Yehova, siye pia tunaweza kuvumilia magumu yoyote yenye tunaweza kupata.

Kama tunaiga uvumilivu wa Abrahamu, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatubariki sasa na hata zaidi mu dunia mupya yenye anatuahidi (Ona fungu ya 14)

14. Uvumilivu wa Abrahamu unaweza kutufundisha nini? (Waebrania 6:15) (Ona pia picha.)

14 Tuseme nini kama mambo yenye tulitazamia kuhusu mwisho haiyatokea? Pengine tangu zamani tulikuwa nangoya mwisho ufike. Pengine tunaweza kuogopa kama tutakufa mbele ule mwisho ufike. Nini njo inaweza kutusaidia tuendelee kungoya kwa uvumilivu? Fikiria mufano wa Abrahamu. Wakati alikuwa na miaka 75 hakukuwa na mutoto, Yehova alimuahidi hivi: “Nitakufanya kuwa taifa kubwa.” (Mwa. 12:1-4) Abrahamu alijionea utimizo wa ile ahadi? Hapana yote. Kisha kutambuka Muto Efrati na kisha kungoya miaka 25, Abrahamu alijionea muujiza wa kuzaliwa kwa mutoto yake Isaka, na kisha miaka ingine 60, wajukuu wake, Esau na Yakobo walizaliwa. (Soma Waebrania 6:15.) Lakini, Abrahamu hakujioneaka namna wazao wake walifikia kuwa taifa kubwa na kuriti Inchi ya Ahadi. Hata vile, ule mwanaume muaminifu alikuwa na urafiki wa karibu pamoya na Muumbaji wake. (Yak. 2:23) Wazia furaha yenye Abrahamu atakuwa nayo wakati atafufuliwa na kujua kama imani yake na uvumilivu wake njo ilifanya Yehova abariki mataifa yote! (Mwa. 22:18) Ile inatufundisha nini? Pengine leo hatutajionea kutimizwa kwa ahadi zote za Yehova. Lakini, kama tuko na uvumilivu sawa vile wa Abrahamu, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatubariki sasa na atatubariki hata zaidi mu dunia mupya yenye anaahidi.​—Mk. 10:29, 30.

15. Tunaweza kujifunza mambo gani wakati wa funzo yetu ya pekee?

15 Biblia iko na mifano mingi ya watu wenye walikuwaka na uvumilivu. (Yak. 5:10) Hauone kama ni jambo ya muzuri kama unajiwekea muradi wa kujifunza ile mifano? b Kwa mufano, hata kama Daudi alitiwa mafuta wakati alikuwa angali kijana sana ili akuwe mufalme wa Israeli, alipaswa kungoya miaka mingi mbele akuwe mufalme. Simeoni na Ana walimuabudu Yehova kwa uaminifu wakati walikuwa nangoya Masiya mwenye aliahidiwa. (Lu. 2:25, 36-38) Wakati utakuwa najifunza ile mifano, tafuta majibu ya hii maulizo: Pengine ni nini ilisaidia huyu mutu aonyeshe uvumilivu? Alipata faida gani juu alikuwa na uvumilivu? Namna gani naweza kumuiga? Unaweza pia kupata faida kwa kujifunza kuhusu wale wenye hawakuonyesha uvumilivu. (1 Sa. 13:8-14) Unaweza kujiuliza hivi: ‘Nini njo ilifanya wale watu washindwe kuonyesha uvumilivu? Ni matokeo gani ya mubaya yenye walipata juu hawakukuwa na uvumilivu?’

16. Kama tuko na uvumilivu tunaweza kupata faida gani zingine?

16 Fikiria faida za kuwa na uvumilivu. Kama tuko na uvumilivu, tutakuwa na furaha zaidi na tutatulia zaidi. Kama tuko na uvumilivu, tunaweza kuwa na afya ya muzuri kimwili na kiakili. Kama tunavumilia wengine, tutakuwa na uhusiano wa muzuri zaidi pamoya nao. Kutaniko yetu itakuwa na umoja zaidi. Kama hatukasirike haraka wakati mutu fulani anatuchokoza, ile itafanya hali isiharibike zaidi. (Zb. 37:8, maelezo ya chini; Mez. 14:29) Lakini, zaidi ya yote, kama tuko na uvumilivu, tutamuiga Baba yetu wa mbinguni na tutamukaribia hata zaidi.

17. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

17 Uvumilivu ni sifa ya muzuri kabisa yenye inatuleteaka siye wote faida! Kusema kweli, haiko mwepesi kila mara kuwa na uvumilivu, lakini kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuendelea kuonyesha ile sifa. Na vile tuko naendelea kungoya kwa uvumilivu dunia mupya, tuko hakika kama “jicho la Yehova linalinda wale wenye kumuogopa, wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu.” (Zb. 33:18) Tuazimie basi kuendelea kuvaa uvumilivu.

WIMBO 41 Tafazali, Sikia Sala Yangu

a Watu wengi leo, hawakuwake na uvumilivu. Lakini, Biblia inatuambia tuvae uvumilivu. Hii habari itatuonyesha juu ya nini ile sifa ni ya maana sana na itatuonyesha namna tunaweza kuwa na uvumilivu zaidi.

b Juu ya kupata habari zenye kuzungumuzia uvumilivu, unaweza kuangalia neno “Uvumilivu” mu kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova.