Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

1923​—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa

1923​—Kumepita Miaka Mia Moya Sasa

KATIKA Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 1, 1923 mulikuwa hii maneno: “Tunatazamia kama mu mwaka wa 1923 kutakuwa mambo ya kutia moyo sana. Tuko na pendeleo ya kuhubiria watu . . . wenye kuishi mu hii dunia yenye mateso, kama mu siku zenye kuya mambo itakuwa muzuri.” Na ni vile ilikuwa, ule mwaka ulikuwa na mambo mingi yenye kutia moyo. Wanafunzi wa Biblia walifanya mabadiliko yenye kufurahisha kuhusu mikutano yao, mikusanyiko, na kazi yao ya kuhubiri. Na ile ilifanya wakuwe na umoja zaidi.

MIKUTANO ILITIA NGUVU UMOJA WAO

Kalenda yenye kuwa na maandiko na namba za nyimbo

Mu ule mwaka, tengenezo ilifanya mabadiliko yenye ilisaidia kutia nguvu umoja wa Wanafunzi wa Biblia. Mu Munara wa Mulinzi mulianza kutokea maelezo yenye kufasiria andiko yenye wangezungumuzia ku mukutano wao wa kila juma wa Sala, Sifa, na Ushuhuda. Zaidi ya ile Wanafunzi wa Biblia walitoa kalenda yenye ilikuwa na liste ya maandiko kwa ajili ya kila juma, na pia wimbo wenye wangeimba wakati wa funzo ya kipekee na ibada ya familia.

Ku ule mukutano, Wanafunzi wa Biblia walikuwa natoa ushuhuda juu ya mambo yenye walikutana nayo mu mahubiri, walikuwa nasema mambo fulani ili kumushukuru Yehova, walikuwa wanaimba, ao hata kusali. Eva Barney, mwenye alibatizwa mu 1923, wakati alikuwa na miaka 15, alikumbuka hivi: “Kama mutu alipenda kutoa ushuhuda angesimama na kuanza kusema maneno sawa vile, ‘Ninapenda kumushukuru Bwana kwa mambo yote ya muzuri yenye amenifanyia.’” Ndugu fulani walipenda sana kutoa ushuhuda. Dada Barney aliendelea kusema hivi: “Ndugu mupendwa Godwin, mwenye alikuwa amezeeka, alikuwa na mambo mingi ya kumushukuru Bwana. Lakini wakati bibi yake alikuwa naona kama ndugu mwenye kusimamia mikutano alishachoka kumusikiliza, alikuwa nakokota bwana yake kidogo ku koti, na kisha bwana yake alikuwa naikala.”

Mara moya ku mwezi, kila kutaniko ilikuwa na mukutano wa pekee wa Sala, Sifa, na Ushuhuda. Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 4, 1923, ulisema hivi juu ya ule mukutano: “Nusu ya mukutano unapaswa kutumiwa ili kutoa ushuhuda kuhusiana na kazi ya kuhubiri na kutia moyo wahubiri. . . . Tunaamini kama ule mukutano utasaidia ndugu wakaribiane zaidi.”

Charles Martin, muhubiri wa miaka 19 wa Vancouver, Kanada, alifaidika sana na ile mikutano. Alifikia kusema hivi: “Ni ku ile mikutano njo nilijifunza kwa mara ya kwanza mambo ya kusema ku milango ya watu. Mara mingi mutu alikuwa naeleza mambo yenye alikutana nayo mu mahubiri ya nyumba kwa nyumba. Ile ilinipatia mawazo juu ya mambo ya kusema na namna ya kujibia vizuia-mazungumuzo mbalimbali.”

KUHUBIRI KULITIA NGUVU UMOJA WAO

Bulletin ya tarehe 1, Mwezi wa 5, 1923

Kazi ya kuhubiri ilisaidia pia kukuwe umoja mu tengenezo. Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 4, 1923, ilitangaza hivi: “Ili kukuwe umoja mu kazi . . . , Siku ya Pili, tarehe 1, Mwezi wa 5, 1923, imechaguliwa kwa ajili ya kuhubiri fasi yote. Vilevile kuanzia hapa Siku ya Pili ya kwanza ya kila mwezi . . . kila mushiriki wa kutaniko anapaswa kuhubiri.”

Hata Wanafunzi wa Biblia vijana walifanya ile kazi. Hazel Burford, mwenye alikuwa tu na miaka 16 ile wakati, alisema hivi: “Mu Bulletin mulikuwa ushuhuda mbalimbali (yenye leo inafanana na sehemu namna ya kuanzisha mazungumuzo) yenye tulipaswa kuweka mu akili. a Miye na tate yangu mwanaume, tulitumika kwa bidii sana.” Lakini Dada Burford alipata upinzani fasi kwenye hakutazamia. Alisema hivi: “Ndugu fulani mupendwa mwenye kukomaa aliwaza kama sikupaswa kabisa kuzungumuza na watu. Ile wakati watu fulani hawakuelewa kama Wanafunzi wote wa Biblia kutia ndani ‘vijana wanaume na vijana wanamuke,’ walipaswa pia kumusifu Muumbaji wao Mukubwa.” (Zb. 148:​12, 13) Lakini Dada Burford aliendelea kuhubiri. Alifikia hata kuhuzuria darasa ya pili ya Masomo ya Gileadi na akakuwa misionere katika Panama. Kisha wakati, wale ndugu walibadilisha mawazo yao juu ya vijana kuhusiana na kazi ya kuhubiri.

MIKUSANYIKO ILITIA NGUVU UMOJA WAO

Mikusanyiko pia ilisaidia ndugu wakuwe na umoja zaidi. Mikusanyiko mingi ilikuwa na siku ya mahubiri. Mufano moya ni ya mukusanyiko wenye ulifanywa Winnipeg, Kanada. Tarehe 31, Mwezi wa 3, watu wote wenye walihuzuria ule mukusanyiko “walialikwa ku mahubiri ya pekee mu ule muji wa Winnipeg.” Siku za mahubiri sawa zile zilisaidia kukuwe ongezeko mu siku zenye kuya. Tarehe 5, Mwezi wa 8, watu karibu 7000 walihuzuria mukusanyiko mwingine wenye ulifanywa Winnipeg. Ile wakati, ile njo ilikuwa hesabu ya watu wengi zaidi kuhuzuria mukusanyiko katika Kanada.

Mukusanyiko wa maana sana wa watu wa Mungu wa mu 1923, ni ule wenye ulifanywa tarehe 18-26, Mwezi wa 8, katika Los Angeles, California. Mu majuma yenye ilitangulia ule mukusanyiko, magazeti ya kutangaza habari ilifanya matangazo kwa ajili ya ile tukio. Na Wanafunzi wa Biblia walitolea watu mialiko zaidi ya 500000. Nguo zenye kuwa na maneno ya kualika watu ku ule mukusanyiko ziliwekwa ku magari ya kusafirisha watu na magari ya kipekee.

Mukusanyiko wa Wanafunzi wa Biblia mu 1923 katika Los Angeles

Siku ya Sita, tarehe 25, Mwezi wa 8, Ndugu Rutherford alitoa hotuba yenye kichwa “Kondoo na Mbuzi.” Mu ile hotuba alifasiria waziwazi kama “kondoo” ni watu wenye kuwa na muelekeo wenye kufaa wenye wangeishi mu paradiso ku dunia. Pia alisoma azimio yenye kuitwa “Onyo.” Mu ile azimio alifunua wazi dini za uongo zenye kujiita kuwa za Kikristo, na alitia moyo watu wenye kuwa na moyo muzuri wajitenge na “Babiloni Mukubwa.” (Ufu. 18:​2, 4) Kisha, Wanafunzi wa Biblia wenye bidii wa mu dunia yote walifikia kugawanya mamilioni ya kopi za ile azimio.

“Ile mikutano itasaidia ndugu wakaribiane zaidi”

Siku ya mwisho ya mukusanyiko, watu zaidi ya 30000 wenye walihuzuria walisikiliza Ndugu Rutherford wakati alitoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Mataifa Yote Inaelekea Kwenye Armagedoni, Lakini Mamilioni ya Watu Wenye Wanaishi Sasa Hawatakufa Hata Kidogo.” Juu Wanafunzi wa Biblia walitazamia kama watu wengi sana watakuya, walilipia kiwanja ya michezo ya Los Angeles Coliseum yenye ilikuwa imetoka tu kujengwa. Ili kuhakikisha kama watu wote watasikia, ndugu walitumia vikuza-sauti vya ile kiwanja, vyenye ile wakati vilikuwa teknolojia ya mupya. Watu wengine wengi walisikia ile programu kupitia radio.

ONGEZEKO MU DUNIA YOTE

Mu mwaka wa 1923, kulikuwa ongezeko kubwa kuhusu kazi ya kuhubiri katika Afrika, Ulaya, India, na Amerika ya Kusini. Katika India, ndugu A. J. Joseph mwenye alikuwa nahangaikia bibi yake na watoto wake sita, alishugulikia kwa wakati uleule kutolewa kwa vichapo mu luga ya Hindi, Tamil, Telugu, na Urdu.

William R. Brown na familia yake

Mu Sierra Leone, Wanafunzi wa Biblia Alfred Joseph na Leonard Blackman waliandikia makao makubwa katika Brooklyn, New York, ili kuomba musaada. Tarehe 14, Mwezi wa 4, 1923, ombi yao ilijibiwa. Alfred alieleza hivi: “Usiku sana ya Siku ya Sita fulani, mutu fulani mwenye sikutazamia aliniita.” Alfred alisikia sauti ya buzito inamuuliza: “Weye njo uliandikia Societé Watch Tower juu ya kuomba wahubiri?” Alfred akajibia: “Ndiyo.” Ilikuwa sauti ya William R. Brown. alifika ile siku kutoka Karibea pamoya na bibi yake Antonia, na watoto wake wawili wanamuke, Louise na Lucy. Ndugu hawakungoja sana ili kukutana nao.

Alfred aliendelea kusema hivi: “Asubui ya siku yenye ilifuata wakati miye na Leonard tulikuwa nafanya funzo yetu ya kila juma, tuliona mwanaume murefu ku mulango. Ilikuwa Ndugu Brown. Alikuwa na bidii sana kwa ajili ya kweli mupaka alipenda kutoa hotuba ya watu wote siku yenye ilifuata.” Mbele hata mwezi moya ienee ndugu Brown aliachia wakati vichapo vyote vyenye alikuwa ameleta. Bila kukawia alipokea vitabu vingine zaidi ya 5000, na kisha watu kidogo tu kulikuwa na lazima ya vitabu zaidi. Lakini Ndugu Brown hakujulikana kuwa muuzisha-vitabu. Mu miaka mingi yenye alimutumikia Yehova kwa bidii, kila mara alitumia Maandiko mu hotuba zake, na ile ilifanya watu waanze kumuita Brown Biblia.

Beteli ya Magdeburg mu miaka ya 1920

Ileile wakati biro ya tawi yenye ilikuwa Barmen, katika Alemanye, ilikuwa ilishakuwa ya kidogo, na ndugu walikuwa wamepata habari kama karibuni maaskari wa Ufaransa watakamata ule muji. Wanafunzi wa Biblia walipata jengo fulani katika Magdeburg yenye ilionekana kuwa itakuwa ya muzuri kwa ajili ya kazi ya kuchapisha. Tarehe 19, Mwezi wa 6, ndugu walimaliza kufunga mashine za kuchapisha na vitu vingine na wakahamia ku ile Beteli ya mupya katika Magdeburg. Kisha tu siku yenye makao makubwa ilijulishwa kama ndugu wamemaliza kuhama, magazeti ya kutangaza habari ilitangaza kama Ufaransa umekamata muji wa Barmen. Ule uamuzi wa kuhama wenye ndugu walikamata ulihakikisha kama Yehova alikuwa anawabariki na kuwalinda.

George Young pamoya na Sarah Ferguson (kuume) na dada yake

Katika Brazili, Ndugu George Young, mwenye alisafiri sana ili kutangaza habari njema, alianzisha biro ya tawi ya mupya, na alianza kutoa Munara wa Mulinzi mu Kireno (Portugais). Mu miezi kidogo tu alitoa zaidi ya vichapo 7000. Kufika kwa ndugu George katika Brazili kulipatia pia Dada Sarah Ferguson nafasi ya pekee sana. Alikuwa anasoma Munara wa Mulinzi tangu mwaka wa 1899, lakini alikuwaka hayapata nafasi ya kubatizwa katika maji ili kuonyesha kama alikuwa amejitoa kwa Yehova. Kisha miezi kidogo Dada Ferguson na watoto wake ine walipata nafasi na kubatizwa.

“TUENDELEE KUMUTUMIKIA YEHOVA KWA BIDII NA FURAHA”

Ku mwisho wa mwaka, Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 12, 1923 ulionyesha matokeo ya muzuri ya mabadiliko yenye Wanafunzi wa Biblia walifanya. Ilisema hivi: “Ni mwepesi kuona kama makutaniko . . . iko mu hali ya muzuri ya kiroho . . . Tujitayarishe basi kwa ajili ya kazi kubwa, na tuendelee kumutumikia Yehova kwa bidii na kwa furaha mu mwaka wenye kufuata.”

Mwaka wenye ulifuata ungekuwa wa pekee sana kwa wanafunzi wa Biblia. Kwa miezi fulani ndugu wa Beteli walikuwa natumika ku kiwanja fulani katika Kisiwa ya Staten, yenye haikukuwa mbali sana na makao makubwa katika Brooklyn. Majengo yenye ilijengwa ku ile kiwanja ya mupya ilimalizika mwanzo-mwanzo wa 1924. Ile majengo ilisaidia ndugu wakuwe na umoja zaidi na ilisaidia pia habari njema itangazwe mu njia zenye hazikuwezekana mbele ya pale.

Kikundi ya wajenzi mu Kisiwa ya Staten

a Leo ni Buku ya Mukutano—Utumishi na Maisha ya Mukristo.