Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 42

Rĩ, Nwĩthagwĩrwa na Wendi bwa Kwathĩka?

Rĩ, Nwĩthagwĩrwa na Wendi bwa Kwathĩka?

“Ũũme bũrĩa bumaga ĩgũrũ . . . nĩ bwĩthagĩrwa na wendi bwa kwathĩka.”—JAK. 3:17, NWT.

RWĨMBO 101 Kufanya Kazi Pamoja kwa Umoja

MUHTASARI a

1. Nĩkĩ bũũmba kwĩthĩrwa bũrĩ ũntũ bũbũũmũ kwathĩka?

 JE, WAKATI mwingine ni vigumu kwako kutii? Mfalme Daudi alikabili changamoto hiyo naye alisali hivi kwa Mungu: “Chochea ndani yangu utayari wa kukutii.” (Zab. 51:12) Daudi alimpenda Yehova. Hata hivyo, wakati mwingine ilikuwa vigumu kwake kutii, na inakuwa hivyo pia kwetu. Kwa nini? Kwanza, tumerithi mwelekeo wa kutotii. Pili, sikuzote Shetani anajaribu kutuchochea tuasi, kama yeye alivyofanya. (2 Kor. 11:3) Tatu, tumezungukwa na ulimwengu huu wenye roho ya uasi, “roho ambayo sasa inafanya kazi katika wana wa kutotii.” (Efe. 2:2) Tunapaswa kujitahidi kushinda mwelekeo wetu wa kutenda dhambi na pia kupinga mkazo wa kutotii unaotoka kwa Ibilisi na ulimwengu huu. Tunapaswa kujitahidi kumtii Yehova na wale ambao amewapatia mamlaka.

2. Kwĩthĩrwa na “wendi bwa kwathĩka” nĩ kuuga atĩa? (Jakubu 3:17)

2 Soma Yakobo 3:17. Mwandikaji Yakobo ambaye aliongozwa na roho takatifu alisema watu wenye hekima wako “tayari kutii.” Fikiria maana ya jambo hilo. Tunapaswa kuwa tayari kabisa kuwatii wale ambao Yehova amewapatia mamlaka ya kadiri. Bila shaka, Yehova hatarajii kwamba tumtii mtu ambaye anatuambia tupuuze amri za Mungu.—Mdo. 4:​18-20.

3. Nĩkĩ Jehova onaga bũrĩ ũntũ bwa gĩtũmi kwathĩkĩra barĩa bagũtongeeria?

3 Huenda ikawa rahisi zaidi kwetu kumtii Yehova kuliko kumtii mwanadamu. Kwa sababu sikuzote Yehova hutoa mwongozo mkamilifu. (Zab. 19:7) Lakini wanadamu wenye mamlaka si wakamilifu. Hata hivyo, Baba yetu wa mbinguni amewapatia mamlaka ya kadiri wazazi, maofisa wa serikali, na wazee wa kutaniko. (Met. 6:20; 1 The. 5:12; 1 Pet. 2:​13, 14) Tunapowatii, kwa kweli tunamtii Yehova. Acheni tuchunguze jinsi tunavyoweza kuwatii wanadamu ambao Yehova amewapatia mamlaka, hata ingawa huenda wakati mwingine ikawa vigumu kwetu kukubali na kufuata mwongozo wao.

ATHĨKĨRA ACIARI BAAKU

4. Nĩkĩ aana babaingĩ batĩathĩkagĩra aciari baao?

4 Vijana wamezungukwa na vijana wenzao ambao wana mwelekeo wa ‘kutotii wazazi.’ (2 Tim. 3:​1, 2) Kwa nini wengi wao si watiifu? Baadhi yao wanafikiri kwamba wazazi wao ni wanafiki. Watoto wanatarajiwa kufanya mambo ambayo wazazi wao hawafanyi. Wengine wanaona kwamba ushauri wa wazazi wao umepitwa na wakati, hauwezi kuwasaidia, au unawabana sana. Ikiwa wewe ni kijana, je, wakati mwingine unahisi hivyo? Ni vigumu kwa wengi kutii amri hii ya Yehova: “Watiini wazazi wenu katika muungano na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la uadilifu.” (Efe. 6:1) Ni nini kinachoweza kukusaidia kutii?

5. O ta ũrĩa kwonanĩtue kĩrĩ Luka 2:​46-52, nĩkĩ tũkũringithua twamenya atĩ Jesũ naathĩkĩĩre aciari baawe?

5 Unaweza kujifunza kuwa mtiifu kutokana na mfano bora kabisa, yaani, Yesu. (1 Pet. 2:​21-24) Alikuwa mwanadamu mkamilifu aliyelelewa na wazazi wasio wakamilifu. Lakini Yesu aliwaheshimu wazazi wake hata walipofanya makosa au kukosa kumwelewa wakati fulani. (Kut. 20:12) Fikiria jambo lililotokea Yesu alipokuwa na umri wa miaka 12. (Soma Luka 2:​46-52.) Pindi moja Yesu alibaki Yerusalemu wazazi wake walipoondoka kurudi nyumbani. Yosefu na Maria walikuwa na jukumu la kuhakikisha kwamba watoto wao wote walikuwa miongoni mwa kikundi kilichokuwa kikisafiri kurudi nyumbani baada ya sherehe. Hatimaye, Yosefu na Maria walipompata Yesu, Maria alimlaumu Yesu kwa sababu ya usumbufu aliowasababishia! Huenda Yesu angesema kwamba hawakumtendea kwa haki. Badala yake, aliwajibu wazazi wake kwa maneno machache yenye heshima. Hata hivyo, Yosefu na Maria “hawakuelewa mambo aliyokuwa akiwaambia.” Ingawa hivyo, Yesu ‘aliendelea kuwatii.’

6-7. Nĩmbi biũmba gũtethia antũ babeethĩ kwathĩkĩra aciari baao?

6 Vijana, je, wakati mwingine ni vigumu kwenu kuwatii wazazi wenu wanapofanya makosa au wanapokosa kuwaelewa? Ni nini kinachoweza kuwasaidia? Kwanza, fikiria jinsi Yehova anavyohisi. Biblia inasema kwamba mnapowatii wazazi wenu, “hilo humpendeza Bwana.” (Kol. 3:20) Yehova anajua kwamba wakati fulani wazazi wenu wanakosa kuwaelewa au wanaweka sheria ambazo si rahisi kutii. Lakini mnapoamua kuwatii licha ya hali hizo, mnamfurahisha Yehova.

7 Pili, fikiria jinsi wazazi wako wanavyohisi. Unapowatii wazazi wako unawafurahisha, nao watakuamini zaidi. (Met. 23:​22-25) Inaelekea kwamba uhusiano wenu utakuwa wa karibu zaidi. Ndugu Alexandre anayeishi huko Ubelgiji, anasema hivi: “Nilipoanza kuwatii wazazi wangu mara nyingi zaidi, uhusiano wetu ulibadilika. Kukawa na uchangamfu na furaha zaidi kati yetu.” b Tatu, fikiria jinsi kuwa mtiifu sasa kutakavyokusaidia baadaye. Paulo, anayeishi nchini Brazili, anasema hivi: “Kujifunza kuwatii wazazi wangu kumenisaidia kumtii Yehova na wengine walio na mamlaka.” Neno la Mungu linatoa sababu muhimu ya kuwatii wazazi wako. Linasema: “Ili mambo yakuendee vema nawe ukae muda mrefu duniani.”—Efe. 6:​2, 3.

8. Nĩkĩ antũ babaingĩ babeethĩ bathuuraga kwathĩkĩra aciari baao?

8 Vijana wengi wameona jinsi wanavyopata matokeo mazuri kwa kutii. Luiza, anayeishi pia huko Brazili, hakuelewa kwa nini hakuruhusiwa kuwa na simu ya mkononi kwa kipindi fulani. Hakuelewa kwa sababu vijana wengine wenye umri kama wake walikuwa na simu. Kisha akatambua kwamba wazazi wake walikuwa wakimlinda. Sasa anasema hivi: “Ninaona kuwatii wazazi wangu si kama kufungwa pingu, bali kama kufunga mkanda kwenye gari ili kulinda uhai wangu.” Elizabeth, dada kijana anayeishi nchini Marekani, bado anahisi ni vigumu kuwatii wazazi wake pindi fulani. Anaeleza hivi: “Wakati ambapo sielewi kikamili kwa nini wazazi wangu wameweka sheria fulani, ninakumbuka pindi ambazo nilipata ulinzi kwa kutii sheria zao.” Monica, anayeishi nchini Armenia, anasema kwamba sikuzote amepata matokeo mazuri kwa kuwatii wazazi wake tofauti na wakati ambapo alikosa kuwatii.

ATHĨKĨRA “BARIA BATHANAGA”

9. Babaingĩ baigagua atĩa bwegie kwathĩkĩra mawatho?

9 Watu wengi wanakubali kwamba tunahitaji serikali za wanadamu na kwamba tunapaswa kutii angalau baadhi ya sheria zilizowekwa na “mamlaka [hizo] zilizo kubwa.” (Rom. 13:1) Lakini huenda watu haohao wakasita kutii sheria fulani wanayoona kwamba si ya haki au wanayohisi inawabana sana. Kwa mfano, fikiria kuhusu kulipa kodi. Asilimia 25 ya watu waliohojiwa katika nchi moja barani Ulaya, wanaamini kwamba “ni sawa kutolipa kodi ikiwa unahisi kwamba si ya haki.” Haishangazi kwamba raia katika nchi hiyo hulipa asilimia 65 hivi ya kodi wanazodaiwa na serikali.

Tunajifunza nini kuhusu kutii kutokana na Yosefu na Maria? (Tazama fungu la 10-12) c

10. Nĩkĩ twathĩkagĩra mawatho kinya jarĩa tũtĩendete?

10 Neno la Mungu linasema kwamba serikali za wanadamu zinasababisha mateso, zinaongozwa na Shetani, na hivi karibuni zitaangamizwa. (Zab. 110:​5, 6; Mhu. 8:9; Luka 4:​5, 6) Pia, linasema kwamba “yeyote anayepinga mamlaka amechukua msimamo dhidi ya mpango wa Mungu.” Tunajitiisha kwa kadiri fulani chini ya mamlaka zilizo kubwa kwa sababu ni mpango wa Yehova wa muda mfupi wa kudumisha utaratibu. Kwa hiyo, tunapaswa ‘kuwapa wote haki zao,’ kutia ndani kulipa kodi, kuwapa heshima, na kuwa watiifu. (Rom. 13:​1-7) Huenda tukaona sheria fulani kuwa yenye kubana, isiyo ya haki, au inatugharimu sana. Lakini tunamtii Yehova ambaye anatuambia tuzitii mamlaka hizo mradi tu hazituamuru kuvunja amri zake.—Mdo. 5:29.

11-12. O ta ũrĩa gũtaarĩĩrĩtue kĩrĩ Luka 2:​1-6, nĩatĩa Jusufu na Mariamu baathithĩrie nĩkenda baathĩkĩra waatho bũrĩa bwarĩ bũbũũmũ kwathĩkĩra, na maumĩĩra jaarĩ jarĩkũ? (Tega kinya mbica.)

11 Tunaweza kujifunza kutokana na mfano wa Yosefu na Maria, ambao walikuwa tayari kutii mamlaka zilizo kubwa hata ilipokuwa vigumu kufanya hivyo. (Soma Luka 2:​1-6.) Maria alipokuwa mjamzito kwa kipindi cha miezi tisa hivi, yeye na Yosefu walikabili jaribu la kutii. Augusto, ambaye alitawala Milki ya Roma, aliamuru watu wote waandikishwe. Yosefu na Maria walilazimika kusafiri kwenda Bethlehemu, safari ya kilomita 150 hivi wakipitia katika eneo lenye milima-milima. Safari hiyo haikuwa rahisi, hasa kwa Maria. Huenda wenzi hao walihofia usalama wao na wa mtoto wao ambaye bado hakuwa amezaliwa. Namna gani ikiwa Maria angepatwa na uchungu wa kuzaa wakiwa njiani? Tumboni mwake alikuwa amembeba Masihi wa wakati ujao. Je, wangetumia hali hiyo kuwa kisingizio cha kutotii serikali?

12 Yosefu na Maria hawakuruhusu mahangaiko hayo yaamue ikiwa watatii sheria. Yehova aliwabariki kwa kutii. Maria aliwasili salama Bethlehemu, akajifungua mtoto mwenye afya, na hata akasaidia kutimiza unabii wa Biblia!—Mika 5:2.

13. Kwathĩka gwetũ kwomba kwĩthĩrwa na maumĩĩra jarĩkũ kĩrĩ atana ba baaba?

13 Tunapotii mamlaka zilizo kubwa, tunajinufaisha sisi wenyewe na wengine. Jinsi gani? Jambo moja ni kwamba tunaepuka adhabu inayotolewa kwa wale wanaovunja sheria. (Rom. 13:4) Utiifu wetu tukiwa mtu mmojammoja unaweza kuathiri maoni ya wenye mamlaka kuhusu Mashahidi wa Yehova kwa ujumla. Kwa mfano, miaka mingi iliyopita nchini Nigeria, wanajeshi waliingia katika Jumba la Ufalme wakati wa mkutano wa kutaniko, wakiwatafuta waandamanaji ambao walikuwa wakipinga malipo ya kodi. Lakini ofisa aliyekuwa akiwasimamia aliwaambia wanajeshi hao waondoke, akisema hivi: “Sikuzote Mashahidi wa Yehova hulipa kodi.” Kila mara unapotii sheria, unadumisha sifa nzuri ya watu wa Yehova, sifa ambayo huenda siku moja ikawalinda waabudu wenzako.—Mt. 5:16.

14. Nĩmbi biatetherie mwarĩ wa baaba ũmwe kwĩthĩrwa na ‘wendi bwa kwathĩkĩra’ anene ba thirikarĩ?

14 Ingawa hivyo, huenda sikuzote isiwe rahisi kutii mamlaka zilizo kubwa. Dada anayeitwa Joanna, ambaye anaishi nchini Marekani, anasema hivi: “Ilikuwa vigumu sana kwangu kutii kwa sababu baadhi ya watu katika familia yangu walikuwa wametendewa isivyo haki na wenye mamlaka.” Lakini Joanna alijitahidi kubadili maoni yake. Kwanza, aliacha kusoma habari kwenye mitandao ya kijamii ambazo zilichochea hisia zisizofaa kuelekea wenye mamlaka. (Met. 20:3) Pili, alisali ili aweze kumtumaini Yehova badala ya kutumaini mabadiliko yanayoweza kuletwa na serikali mpya ya kibinadamu. (Zab. 9:​9, 10) Tatu, alisoma makala katika machapisho yetu kuhusu kutounga mkono upande wowote. (Yoh. 17:16) Sasa Joanna anasema kwamba kuheshimu na kutii mamlaka kumemletea “amani na utulivu mwingi ambao maneno hayatoshi kueleza.”

ATHĨKĨRA ŨTONGEERIA KUUMA KĨRĨ ŨTHURANĨRI BWA JEHOVA

15. Nĩkĩ no bwĩthĩrwe bũrĩ ũntũ bũbũũmũ kwathĩkĩra ũtongeeria kuuma kĩrĩ ũthuranĩri bwa Jehova?

15 Yehova anatuambia ‘tuwatii wale wanaoongoza’ kutanikoni. (Ebr. 13:17) Ingawa Kiongozi wetu Yesu ni mkamilifu, wale ambao anawatumia kuongoza hapa duniani si wakamilifu. Huenda ikawa vigumu kuwatii, hasa wanapotuambia tufanye jambo ambalo hatutaki kulifanya. Pindi fulani mtume Petro alisitasita kutii mwongozo aliopewa. Malaika alipomwagiza ale wanyama ambao walionwa kuwa wasio safi kulingana na Sheria ya Musa, Petro alikataa—si mara moja, bali mara tatu! (Mdo. 10:​9-16) Kwa nini? Kwa maoni yake, mwongozo huo mpya haukupatana na akili. Alikuwa amezoea kufanya mambo kwa njia tofauti. Ikiwa ilikuwa vigumu kwa Petro kutii mwongozo kutoka kwa malaika mkamilifu, inaweza kuwa vigumu hata zaidi kwetu kutii mwongozo kutoka kwa wanadamu wasio wakamilifu!

16. Nĩatĩa mũtũmwa Paũlũ aathithĩrie kinya kethĩra ũtongeeria bũrĩa aaerwe noonaga bũtĩagĩrĩte? (Mathithio 21:​23, 24, 26)

16 Mtume Paulo alikuwa “tayari kutii” hata alipopewa mwongozo ambao huenda angehisi kwamba haupatani na akili. Wakristo Wayahudi walikuwa wamesikia uvumi kumhusu Paulo—uvumi kwamba alikuwa akiwahubiria watu “kuiasi sheria ya Musa” na kutoiheshimu Sheria hiyo. (Mdo. 21:21) Wazee Wakristo huko Yerusalemu walimwagiza Paulo aende pamoja na wanaume wanne hekaluni na kujitakasa kisherehe ili kuonyesha kwamba alikuwa akitii Sheria. Lakini Paulo alijua kwamba Wakristo hawakuwa tena chini ya Sheria ya Musa. Naye hakuwa amefanya kosa lolote. Ingawa hivyo, Paulo alitii bila kukawia. “Akaenda pamoja na wanaume hao siku iliyofuata, akajitakasa kisherehe pamoja nao.” (Soma Matendo 21:​23, 24, 26.) Utii wa Paulo ulichangia umoja.—Rom. 14:​19, 21.

17. Nĩmbi ũkwiritana kuumania na ngerekano ya Stephanie?

17 Ilikuwa vigumu kwa dada anayeitwa Stephanie kukubali uamuzi uliofanywa na ndugu wanaoongoza katika nchi yao. Yeye na mume wake walikuwa wanafurahia kutumikia katika kikundi cha lugha ya kigeni. Kisha ofisi ya tawi ikavunja kikundi hicho, na wenzi hao wa ndoa wakapewa mgawo katika kutaniko la lugha yao ya asili. Stephanie anakiri hivi: “Sikufurahishwa na jambo hilo. Sikudhani kwamba kulikuwa na uhitaji mkubwa zaidi katika kutaniko la lugha yetu ya asili.” Hata hivyo, aliamua kuunga mkono mwongozo huo mpya. Anasema hivi: “Baada ya muda, niliona hekima ya uamuzi huo. Tumekuwa wazazi wa kiroho kwa baadhi ya watu kutanikoni ambao hawana watu wa familia zao katika kweli. Ninajifunza Biblia pamoja na dada ambaye ameanza kutenda tena hivi karibuni. Na sasa nina muda mwingi zaidi wa kujifunza kibinafsi.” Anaongezea hivi: “Nina dhamiri safi kwa sababu ninajua kwamba nimejitahidi kabisa kutii.”

18. Nĩatĩa tũgunĩkaga tontũ bwa kwĩthĩrwa tũrĩ aathĩki?

18 Tunaweza kujifunza kutii. Yesu “alijifunza kutii,” si akiwa katika hali nzuri kabisa, bali “kutokana na mateso yaliyompata.” (Ebr. 5:8) Kama Yesu, mara nyingi tunajifunza kutii tunapokabili hali ngumu. Kwa mfano, mwanzoni mwa janga la COVID-19 tulipoambiwa tuache kukutana katika Majumba ya Ufalme na tuache kuhubiri nyumba kwa nyumba, je, ilikuwa vigumu kwako kutii? Ingawa hivyo, kwa sababu ya kutii ulipata ulinzi, ulitenda kwa umoja pamoja na waabudu wenzako, na kumfurahisha Yehova. Sasa sisi sote tuko tayari zaidi kutii mwongozo wowote ambao tutapokea wakati wa dhiki kuu. Kutii mwongozo huo kutaokoa uhai wetu!—Ayu. 36:11.

19. Nĩkĩ bũrĩ ũntũ bwa gĩtũmi kĩrĩ o ũmwe weetũ kwathĩka?

19 Tumejifunza kwamba kutii huleta baraka nyingi sana. Lakini tunaamua kumtii Yehova hasa kwa sababu tunampenda na tunataka kumfurahisha. (1 Yoh. 5:3) Hatuwezi kamwe kumlipa Yehova kwa mambo yote ambayo ametufanyia. (Zab. 116:12) Lakini tunaweza kumtii yeye na pia wale walio na mamlaka juu yetu. Tunapotii, tunaonyesha kwamba sisi ni wenye hekima. Na watu wenye hekima huufanya moyo wa Yehova ushangilie.—Met. 27:11.

RWĨMBO 89 Sikiliza, Tii, Upate Baraka

a Kwa kuwa sisi si wakamilifu, ni vigumu kwetu sote kutii wakati mwingine, hata ikiwa mtu anayetupatia mwongozo ana mamlaka ya kufanya hivyo. Makala hii itazungumzia jinsi tunavyonufaika tunapowatii wazazi wetu, tunapotii “mamlaka zilizo kubwa,” na akina ndugu wanaoongoza katika kutaniko la Kikristo.

b Ili kupata madokezo ya jinsi ya kuzungumza na wazazi wako kuhusu sheria ambazo unahisi kwamba ni vigumu kutii, ona makala “Ninaweza Kuzungumzaje na Wazazi Wangu Kuhusu Sheria Walizoweka?” kwenye jw.org.

c MAELEZO YA PICHA: Yosefu na Maria walitii agizo la serikali la kuandikishwa huko Bethlehemu. Leo, Wakristo wanatii sheria za barabarani, wanalipa kodi, na kufuata miongozo ya afya inayotolewa na “mamlaka zilizo kubwa.”