Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 43

“Atawatia Nguvu”—⁠Namna Gani?

“Atawatia Nguvu”—⁠Namna Gani?

“[Yehova] atawafanya kuwa imara, atawatia nguvu, atawafanya ninyi musitikisike.”—1 PE. 5:10.

WIMBO 38 Atakupatia Nguvu

KIFUPI YA HABARI a

1. Waabudu wa zamani wa Mungu walipata wapi nguvu?

 MARA mingi wakati Neno ya Mungu inazungumuzia watu waaminifu wa zamani, inasema kama walikuwa wenye nguvu. Lakini wakati fulani hata wenye nguvu zaidi kati yao, hawakujisikia kuwa na nguvu. Kwa mufano, wakati fulani Mufalme Daudi alijisikia kuwa “imara kama mulima,” lakini wakati mwingine ‘aliogopa sana.’ (Zb. 30:7) Hata kama Samsoni alikuwa na nguvu mingi sana wakati alikuwa naongozwa na roho ya Mungu, alisema kama bila nguvu yenye kutoka kwa Mungu ‘atakuwa muzaifu na kuwa kama wanadamu wengine wote.’ (Amu. 14:5, 6; 16:17) Wale wanaume waaminifu walikuwa wenye nguvu kwa sababu tu Yehova aliwapatia nguvu.

2. Juu ya nini mutume Paulo alisema kama alikuwa muzaifu na wakati uleule mwenye nguvu? (2 Wakorinto 12:9, 10)

2 Mutume Paulo alikubali kama alikuwa na lazima ya nguvu kutoka kwa Yehova. (Soma 2 Wakorinto 12:9, 10.) Sawa vile wengi kati yetu, Paulo alipambana na magumu ya afya. (Gal. 4:13, 14) Wakati fulani, ilikuwa nguvu kwake kufanya mambo ya muzuri. (Ro. 7:18, 19) Na wakati ingine alikuwa na mahangaiko na hakujua ni nini itamufikia. (2 Ko. 1:8, 9) Hata vile, wakati Paulo alikuwa muzaifu, njo wakati alikuwa mwenye nguvu. Namna gani? Yehova alimupatia Paulo nguvu yenye alikuwa nayo lazima. Alimutia nguvu.

3. Tutajibia maulizo gani mu hii habari?

3 Yehova anaahidi kama atatutia nguvu siye pia. (1 Pe. 5:10) Lakini hatupaswe kutazamia kama tutapata ile nguvu bila kufanya kitu. Kwa mufano, motere inaweza kusaidia gari itembee, lakini mwenye kutembeza anapaswa kukanyanga ku accélérateur juu gari iende kwenye anapenda. Vilevile Yehova iko tayari kutupatia nguvu yenye tuko nayo lazima, lakini tunapaswa kukamata hatua fulani ili kupata ile nguvu. Yehova ametupatia nini ili kututia nguvu? Na tunaweza kufanya nini ili tupate ile nguvu? Tutapata majibu ya ile maulizo kwa kuchunguza namna Yehova alitia nguvu watu tatu wenye kuzungumuziwa mu Biblia, ni kusema nabii Yona, Maria mama ya Yesu, na mutume Paulo. Tutaona pia namna Yehova anaendelea kutia nguvu watumishi wake leo, sawa vile alifanya zamani.

PATA NGUVU KUPITIA SALA NA KUJIFUNZA

4. Namna gani tunaweza kupata nguvu kutoka kwa Yehova?

4 Njia moja yenye inaweza kutusaidia kupata nguvu kutoka kwa Yehova ni kumukaribia katika sala. Yehova anaweza kujibia sala zetu kwa kutupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida.” (2 Ko. 4:7) Tunaweza pia kupata nguvu kwa kusoma Neno yake na kwa kutafakari juu ya mambo yenye tunasoma. (Zb. 86:11) Mambo yenye aliandikisha mu Biblia kwa ajili yetu ‘iko na nguvu.’ (Ebr. 4:12) Wakati unasali kwa Yehova na unasoma Neno yake, utapata nguvu yenye uko nayo lazima ili kuvumilia, kuendelea kuwa na furaha, ao kutimiza mugao fulani wa nguvu. Ona namna Yehova alimutia nguvu nabii Yona.

5. Juu ya nini nabii Yona alikuwa na lazima ya uhodari?

5 Nabii Yona alikuwa na lazima ya uhodari. Alikimbia wakati Yehova alimupatia mugao wa nguvu. Matokeo ilikuwa nini? Alikaribia kupoteza uzima wake mu upepo mukali, na alitia mu hatari uzima wa wenye walikuwa nasafiri naye mu mashua. Wakati alitupwa mu maji, alijikuta fasi kwenye hayakuwaka, ni kusema mu tumbo yenye giza ya samaki mukubwa. Unawaza Yona alijisikia namna gani? Aliwaza kama atakufia mule? Alijiuliza ikiwa Yehova amemukatala? Bila shaka ile hali ilifanya Yona akuwe na mahangaiko sana.

Kama nabii Yona unaweza kufanya nini ili upate nguvu wakati uko na magumu? (Ona fungu ya 6-9)

6. Kulingana na Yona 2:1, 2, 7, nini njo ilitia Yona nguvu wakati alikuwa mu tumbo ya samaki?

6 Yona alifanya nini ili apate nguvu wakati alikuwa yeye peke mu tumbo ya samaki? Kwanza alisali. (Soma Yona 2:1, 2, 7.) Hata kama Yona hakumutii Yehova, alikuwa hakika kama Yehova atasikiliza sala yake ya kutubu yenye alitoa kwa unyenyekevu. Pia, Yona alitafakari juu ya Maandiko. Juu ya nini tunasema vile? Juu mu sala yake yenye kuwa mu Yona sura ya 2, anatumia maneno na misemwa ileile yenye kuwa mu Zaburi. (Kwa mufano, linganisha Yona 2:2, 5 na Zaburi 69:1; 86:7.) Ni wazi kama Yona alijua muzuri ile maandiko. Na wakati alifikiria ile maandiko mu ile hali ya magumu, ilimuhakikishia kama Yehova angemusaidia. Kisha Yona alirudishwa ku inchi kavu na alikuwa tayari kukubali na kutimiza mugao wenye Yehova alimupatia.—Yon. 2:10–3:4.

7-8. Namna gani ndugu moya wa Taiwan alipata nguvu wakati wa magumu?

7 Mufano wa Yona unaweza kutusaidia wakati tuko napambana na magumu mbalimbali. Kwa mufano, Zhiming, b ndugu wa Taiwan, iko na magonjwa ya nguvu sana. Zaidi ya ile anapambana na upinzani mukali wa watu wa familia yake kwa sababu ya imani yake kwa Yehova. Kusali na kujifunza kunamusaidia apate nguvu kutoka kwa Yehova. Alisema hivi. “Wakati fulani, wakati ninapata magumu, ninahangaikaka sana mupaka ninashindwa kutulia ili nifanye funzo ya kipekee.” Lakini ile haimuvunje moyo. Anasema tena hivi: “Kwanza ninatoaka sala kwa Yehova kisha ninasikiliza nyimbo zetu za Ufalme. Na hata wakati fulani, ninaimbaka kwa sauti ya chini mupaka wakati nitatulia. Kisha ninaanza kujifunza.”

8 Funzo ya kipekee imetia nguvu Zhiming mu njia zenye hakuwazia. Kwa mufano, kisha kufanyiwa upasuaji mukubwa, munganga alimuambia kama chembe zake nyekundu zilikuwa zimepunguka sana. Alimuambia kama iliomba atiwe damu mu mishipa. Usiku mbele ya ule upasuaji, Zhiming alikuwa amesoma habari kuhusu dada mwenye alifanyiwa uleule upasuaji. Chembe zake nyekundu zilikuwa pia zimepunguka sana kupita hata za Zhiming, lakini hakukubali kutiwa damu mu mishipa na alipona. Ile habari ilimutia nguvu Zhiming ili aendelee kuwa muaminifu.

9. Kama magumu inakufanya ukose nguvu, unaweza kufanya nini? (Ona pia picha.)

9 Wakati wa magumu unahangaikaka sana mupaka unashindwa kusali waziwazi? Ao unajisikiaka kama hauna nguvu ya kujifunza? Kumbuka kama Yehova anaelewa muzuri sana hali yako. Kwa hiyo, hata wakati unasali kwa kutumia maneno kidogo, unaweza kuwa hakika kama atakupatia mambo yenye uko nayo lazima. (Efe. 3:20) Kama maumivu ya kimwili ao ya kihisia inafanya ikuwe nguvu kwako kusoma na kujifunza, unaweza kusikiliza Biblia yenye kurekodiwa ao vichapo vyenye kutegemea Biblia vyenye kurekodiwa. Kusikiliza nyimbo zetu ao kuangalia video ku jw.org, kunaweza pia kukusaidia. Wakati unasali kwa Yehova na unatumia mambo ya kiroho yenye anatutolea, unamupatia nafasi ya kukutia nguvu.

PATA NGUVU KUPITIA WAABUDU WENZAKO

10. Ndugu na dada zetu Wakristo wanaweza kututia nguvu namna gani?

10 Yehova anaweza kutumia ndugu na dada zetu Wakristo ili kututia nguvu. Wanaweza kuwa “chanzo cha faraja nyingi” wakati tunapambana na magumu, ao wakati ni nguvu kwetu kutimiza mugao fulani wa nguvu. (Kol. 4:10, 11) Tuko na lazima ya marafiki, zaidi sana mu “nyakati za taabu.” (Mez. 17:17) Wakati tuko zaifu waabudu wenzetu wanaweza kutusaidia kimwili, kihisia, na kiroho. Tuone namna wengine walimutia nguvu Maria mama ya Yesu.

11. Juu ya nini Maria alikuwa na lazima ya kutiwa nguvu?

11 Maria alikuwa na lazima ya nguvu ya kufanya mapenzi ya Yehova. Wazia namna alipaswa kuwa na mahangaiko sana kisha Gabrieli kumuambia mugao muzito wenye alipaswa kutimiza. Hakukuwa na bwana lakini alipaswa kupata mimba. Hakukuwa alishakomalisha mutoto yeyote, lakini sasa alipaswa kuhangaikia mutoto mwenye angefikia kuwa Masiya. Na juu alikuwaka hayafanya ngono, namna gani angefasiria Yosefu, muchumba wake, ile mambo yote?—Lu. 1:26-33.

12. Kulingana na Luka 1:39-45, Maria alipata wapi nguvu?

12 Maria alipata wapi nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili kutimiza ule mugao muzito, wenye haukukuwa wa kawaida? Alitafuta musaada kwa Yehova. Kwa mufano, alimuomba Gabrieli amupatie mafasirio zaidi kuhusu mugao wake. (Lu. 1:34) Kisha wakati kidogo alisafiri kuenda mu eneo ya “inchi ya milima” ya Yuda ili kutembelea Elizabeti, mutu wa jamaa yake. Ile ilikuwa na matokeo ya muzuri. Elizabeti alimupongeza Maria na aliongozwa na Yehova ili kutoa unabii wenye kutia moyo kuhusu mwana wa Maria mwenye alikuwa hayazaliwa. (Soma Luka 1:39-45.) Maria alisema kama Yehova alikuwa “ametenda kwa nguvu kwa mukono wake.” (Lu. 1:46-51) Yehova alimutia nguvu Maria kupitia Gabrieli na Elizabeti.

13. Dada fulani wa Bolivia alipata faida gani juu alitafuta musaada wa waabudu wenzake?

13 Kama Maria, waabudu wenzetu wanaweza pia kututia nguvu. Dasuri dada mwenye kuishi Bolivia, alikuwa na lazima ya kutiwa nguvu. Wakati ilivumbuliwa kama baba yake alikuwa na ugonjwa wenye hauwezi kupona na iliomba abakie mu hopitali, Dasuri alikuwa tayari kumuhangaikia. (1 Ti. 5:4) Ile haikukuwa mwepesi kila wakati. Dasuri anasema hivi: “Mara mingi niliona kama sitaweza kuendelea.” Alitafuta musaada? Ku mwanzo hakufanya vile. Anasema hivi: “Sikupenda kusumbua ndugu zangu. Nilijiambia kama Yehova njo atanipatia musaada wenye niko nao lazima. Lakini nilitambua kama kwa kujitenga na wengine, nilikuwa najaribu kutatua magumu yangu miye peke.” (Mez. 18:1) Dasuri aliamua kuandikia marafiki fulani na kuwafasiria hali yake. Anasema: “Ninakosa maneno ya kufasiria namna nilitiwa moyo na Wakristo wenzangu. Walileta chakula ku hopitali na walinitia moyo kupitia maandiko ya Biblia yenye kufariji. Inagusa moyo sana kujua kama hatuko peke yetu. Tuko mu familia kubwa ya Yehova; familia yenye kuwa tayari kukusaidia, kulia pamoya na weye, na kupiganisha magumu pamoya na weye.”

14. Juu ya nini tunapaswa kukubali musaada wenye wazee wanatutolea?

14 Njia ingine yenye Yehova anatumia ili kututia nguvu ni kupitia wazee. Wazee ni zawadi yenye Yehova anatumia ili kututia nguvu na kututia moyo. (Isa. 32:1, 2) Kwa hiyo, wakati uko na mahangaiko, elezea wazee kuhusu mahangaiko yako. Wakati wanakutolea musaada, ukuwe tayari kuukubali. Kupitia wazee Yehova anaweza kukutia nguvu.

PATA NGUVU KUPITIA TUMAINI YAKO YA WAKATI WENYE KUYA

15. Wakristo wote wako na tumaini gani?

15 Tumaini yenye kuzungumuziwa mu Biblia yenye tuko nayo inaweza kututia nguvu. (Ro. 4:3, 18-20) Siye Wakristo tuko na tumaini ya muzuri sana ya kuishi milele, ikuwe mu dunia yenye kuwa paradiso ao mbinguni mu Ufalme wa Mungu. Inatupatia nguvu ya kuvumilia magumu, ya kuhubiri habari njema, na ya kutimiza migao mbalimbali mu kutaniko. (1 Te. 1:3) Ile tumaini njo ilipatiaka mutume Paulo nguvu.

16. Juu ya nini mutume Paulo alikuwa na lazima ya kutiwa nguvu?

16 Paulo alikuwa na lazima ya kutiwa nguvu. Mu barua yake kwa Wakorinto alijilinganisha na chombo cha udongo chenye kuwa zaifu. ‘Alikazwa,’ ‘alivurugika,’ ‘aliteswa,’ ‘aliangushwa chini,’ na hata maisha yake ilikuwa mu hatari. (2 Ko. 4:8-10) Paulo aliandika ile maneno wakati alikuwa mu safari yake ya tatu ya umisionere. Wakati aliandika ile maneno, pengine hakujua mambo yenye ilikuwa namungoya. Angepata magumu zaidi; angepambana na vikundi vya watu wenye kasirani, angekamatwa, angevunjikiwa na mashua, na kufungwa mu gereza.

17. Kulingana na 2 Wakorinto 4:16-18, nini njo ilisaidia Paulo akuwe na nguvu ya kuvumilia magumu?

17 Paulo alipata nguvu ya kuvumilia kwa kukazia akili tumaini yake. (Soma 2 Wakorinto 4:16-18.) Aliambia Wakorinto kuwa hata kama mwili wake ‘unaharibika,’ ile haingemuvunja moyo. Paulo alikazia akili wakati wake wenye kuya. Tumaini yake ya kuishi milele mbinguni ilikuwa ‘kubwa zaidi na zaidi.’ Njo maana alikuwa tayari kuvumilia magumu yoyote ili apate ile zawabu. Paulo alitafakari juu ya ile tumaini, na ile ilifanya ajisikie kuwa “anafanywa upya siku kwa siku.”

18. Namna gani tumaini ilimutia nguvu Tihomir na familia yake?

18 Tumaini yenye ndugu Tihomir wa Bulgaria iko nayo inamupatiaka nguvu. Miaka fulani yenye imepita, mudogo yake, Zdravko alikufa mu aksida. Kwa wakati fulani kisha pale, Tihomir alikuwa na huzuni mingi. Juu ya kupambana na ile hali, yeye na familia yake wanawazia namna ufufuo utakuwa. Anasema hivi: “Kwa mufano, tunazungumuzia fasi kwenye tutakutana na Zdravko, chakula yenye tutamutayarishia, nani njo tutaalika ku sherehe ya kwanza kisha kufufuliwa kwake, na mambo yenye tutamuambia kuhusu siku za mwisho.” Tihomir anasema kama kukazia akili tumaini yao, kulipatia familia yake nguvu ya kuendelea kuvumilia na kungoya siku yenye Yehova atafufua mudogo yake.

Wakati unawazia maisha yako mu dunia mupya, unaona itakuwa namna gani? (Ona fungu ya 19) c

19. Unaweza kufanya nini ili kutia nguvu tumaini yako? (Ona pia picha.)

19 Namna gani unaweza kutia nguvu tumaini yako? Kwa mufano, kama uko na tumaini ya kuishi milele ku dunia, usome na utafakari maandiko ya Biblia yenye kufasiria namna Paradiso itakuwa. (Isa. 25:8; 32:16-18) Fikiria namna maisha itakuwa mu dunia mupya. Ujiwazie uko pale, unasikia sauti gani? Unajisikia namna gani? Juu ya kuchochea uwezo wako wa kuwazia, angalia picha mu vichapo vyetu zenye kuonyesha namna Paradiso itakuwa. Ao uangalie video za muziki sawa vile Dunia Mupya Yenye Kuja, Iko Karibu Sana, ao Wazia ile Siku. Kama tunaendelea kukazia akili tumaini ya dunia mupya yenye tuko nayo, magumu yetu itakuwa ‘ya wakati kidogo na ya nyepesi.’ (2 Ko. 4:17) Yehova atatutia nguvu kupitia tumaini yenye ametupatia.

20. Hata wakati tuko wazaifu, namna gani tunaweza kupata nguvu?

20 Hata wakati tuko wazaifu, “kwa musaada wa Mungu tutapata nguvu.” (Zb. 108:13) Yehova amekupatia mambo yenye uko nayo lazima ili upate nguvu kutoka kwake, kwa hiyo wakati uko na lazima ya musaada ili kutimiza mugao fulani, kuvumilia magumu, ao kuendelea kuwa na furaha, usali kwa Yehova kwa moyo wote na utafute muongozo wake kupitia funzo ya kipekee. Ukubali vitia moyo vyenye ndugu na dada wanakutolea. Tafakari juu ya tumaini yako ya wakati wenye kuya. Kisha “utafanywa kuwa imara kwa nguvu zote kulingana na uwezo [wa Mungu] wenye utukufu ili uvumilie kwa ukamili kwa subira na furaha.”—Kol. 1: 11.

WIMBO 33 Umutupie Yehova Muzigo Wako

a Hii habari itasaidia wale wenye kuwa na mahangaiko kwa sababu ya magumu ao kwa sababu ya mugao wenye wanaona kuwa hawataweza kutimiza. Utajifunza namna Yehova anaweza kututia nguvu na mambo yenye tunaweza kufanya ili tupate musaada wake.

b Majina fulani imebadilishwa.

c MAFASIRIO YA PICHA: Dada mwenye kuwa kiziwi iko natafakari juu ya ahadi ya Biblia. Anaangalia video ya muziki ili imusaidie kuwazia namna maisha yake itakuwa mu dunia mupya.