Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Ulizo Yenye Siye Wote Tunajiulizaka

Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Ulizo Yenye Siye Wote Tunajiulizaka

Kama unapenda kuenda fasi kwenye hauyafikaka, unaweza kufanya nini?

  1. 1. Kuenda fasi kwenye mawazo yako inakutuma.

  2. 2. Kufuata wengine, kwa kutumainia kama wanajua njia.

  3. 3. Kutumia muongozo wenye kutumainika, sawa vile GPS, karte, ao kutafuta muongozo kwa rafiki fulani mwenye anajua njia muzuri.

Kama unachagula jibu ya kwanza ao ya pili, utafika fasi fulani, lakini pengine hautafika fasi kwenye ulipenda kuenda. Kama unachagula jibu ya tatu, ukuwe hakika kama utafika fasi kwenye uko naenda.

Maisha yetu iko sawa vile safari, yenye inaweza kutupeleka kwenye maisha ya furaha mu wakati wenye kuya. Kufika kule ao kutofika, itategemea kwenye tunatafutia muongozo mbele ya kukamata maamuzi.

Hata kama maamuzi mingi kati ya maamuzi yenye tunakamataka mu maisha inakuwaka mu mambo ya kidogo-kidogo, maamuzi fulani inakuwaka ya maana sana. Ile maamuzi yote inaonyeshaka mawazo yetu juu ya mambo ya muzuri na ya mubaya. Ile maamuzi itakuwa na matokeo ya muzuri ao ya mubaya kwa wakati murefu kwetu na kwa wale wenye tunapenda. Ile maamuzi inatia ndani mambo sawa vile:

  • Ngono na ndoa

  • Unyoofu, kazi, na makuta

  • Namna ya kukomalisha watoto

  • Namna ya kutendea wengine

Nini njo inaweza kutusaidia kuwa hakika kama maamuzi yenye tunakamata mu ile mambo itafanya siye na familia yetu tukuwe na furaha wakati wenye kuya?

Ulizo yenye kila mumoja wetu anajiulizaka njo hii: Nini njo inaweza kuniongoza juu nikamate maamuzi ya muzuri?

Hii gazeti itafasaria juu ya nini Biblia ni muogozo wenye kutumainika na namna inaweza kukusaidia.