Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 2

WIMBO 19 Chakula cha Mangaribi cha Bwana

Uko Tayari kwa Ajili ya Siku ya Maana Zaidi mu Mwaka?

Uko Tayari kwa Ajili ya Siku ya Maana Zaidi mu Mwaka?

“Muendelee kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”LU. 22:19.

WAZO KUBWA

Fikiria juu ya nini Ukumbusho ni tukio ya pekee sana, namna unaweza kujitayarisha, na namna unaweza kusaidia wengine wahuzurie.

1. Juu ya nini siku ya Ukumbusho njo siku ya maana zaidi mu mwaka? (Luka 22:19, 20)

 WATU wa Yehova wanaona siku ya Ukumbusho wa kifo ya Kristo kuwa siku ya maana zaidi mu mwaka. Ni ile tukio tu njo Yesu aliambia wanafunzi wake waendelee kukumbuka. (Soma Luka 22:19, 20.) Kuko sababu mingi zenye zinafanya tungoye Ukumbusho kwa hamu sana.

2. Juu ya nini tunangoyaka Ukumbusho kwa hamu sana?

2 Ukumbusho unatusaidia tufikiri juu ya samani ya bei ya ukombozi. Unatukumbusha njia mbalimbali za kuonyesha shukrani juu ya zabihu ya Yesu. (2 Ko. 5:14, 15) Unatupatia pia nafasi ya kufurahia “ubadilishanaji wa kitia-moyo” pamoja na ndugu na dada zetu. (Ro. 1:12) Kila mwaka, ndugu na dada wengi wenye hawatende tena wanahuzuria Ukumbusho. Wamoja wanachochewa hata kumurudilia Yehova kwa sababu ya namna wanakaribishwa kwa uchangamufu. Na watu wengi wenye kupendezwa wanachochewa kuingia mu barabara ya uzima kwa sababu ya mambo yenye wanaona na kusikia. Ile mambo yote inafanya Ukumbusho Ukuwe tukio ya pekee sana kwetu!

3. Namna gani Ukumbusho unaunganisha ndugu na dada wa mu dunia yote? (Ona pia picha.)

3 Fikiria pia namna Ukumbusho unaunganisha ndugu na dada wa mu dunia yote. Mashahidi wa Yehova mu dunia yote wanakusanyika pamoja wakati jua inashuka kulingana na fasi kwenye wanaishi. Siye wote tunasikiliza hotuba yenye inakazia faida ya bei ya ukombozi, tunaimba nyimbo mbili za kumusifu Yehova, tunapitisha mukate na divai, na kwa moyo wote tunasema “amina” ku sala ine zenye zinatolewa. Mu kipindi ya saa 24, makutaniko yote inafanya vile. Unaweza kuwazia furaha yenye Yehova na Yesu wanasikia wakati wanaona tunawatukuza pamoja?

Ukumbusho unaunganisha ndugu na dada mu dunia yote (Ona fungu ya 3) f


4. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

4 Mu hii habari tutazungumuzia hii maulizo: Namna gani tunaweza kutayarisha moyo wetu kwa ajili ya Ukumbusho? Namna gani tunaweza kusaidia wengine wafaidike na ile tukio? Na namna gani tunaweza kusaidia wale wenye hawatende tena? Majibu ya ile maulizo itatusaidia tukuwe tayari kwa ajili ya ile tukio yenye kuwa takatifu.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUTAYARISHA MOYO WETU KWA AJILI YA UKUMBUSHO?

5. (a) Juu ya nini tunapaswa kutafakari juu ya samani ya bei ya ukombozi? (Zaburi 49:7, 8) (b) Ulijifunza nini mu video Sababu Gani Yesu Alikufa?

5 Moja kati ya mambo ya maana sana yenye tunaweza kufanya ili kutayarisha moyo wetu kwa ajili ya Ukumbusho, ni kufikiri juu ya samani ya zabihu ya Yesu Kristo. Hatungeweza kujikomboa wenyewe kutoka katika zambi na kifo. (Soma Zaburi 49:7, 8; ona pia video Sababu Gani Yesu Alikufa?) a Kwa hiyo, Yehova na Mwana wake walijiima sana kwa ajili yetu. Yehova alifanya mupango ili Yesu atoe uzima wake kwa ajili yetu. (Ro. 6:23) Kadiri tunatafakari juu ya mambo yenye Yehova na Yesu walikuwa tayari kujiima kwa ajili yetu, ni vile tutaona bei ya ukombozi kuwa ya maana sana. Tutazungumuzia mambo fulani kati ya mambo yenye Yehova na Yesu walijiima ili zabihu ya ukombozi itolewe. Lakini, tuone kwanza bei ya ukombozi ilitia ndani nini

6. Bei ya ukombozi ilitia ndani nini?

6 Bei ya ukombozi ni bei yenye inalipwa ili kununua tena kitu fulani. Mutu wa kwanza Adamu alikuwa mukamilifu wakati aliumbwa. Wakati alifanya zambi alipoteza tumaini ya kuishi milele, haiko tu kwa ajili yake mwenyewe, lakini pia kwa ajili ya watoto wake wote. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, “hakufanya zambi, na udanganyifu haukupatikana katika kinywa chake.” (1 Pe. 2:22) Wakati wa kifo yake, uzima wake mukamilifu ulilingana kabisa na uzima wenye Adamu alipoteza.—1 Ko. 15:45; 1 Ti. 2:6.

7. Yesu alipambana na majaribu gani wakati alikuwa ku dunia?

7 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, aliendelea kuwa mutiifu kabisa kwa Baba yake wa mbinguni, hata wakati alipatwa na majaribu mingi. Wakati alikuwa mutoto alipaswa kutii wazazi wake, wanadamu wenye hawakukuwa wakamilifu, hata kama yeye alizaliwa mukamilifu. (Lu. 2:51) Wakati alikuwa kijana alipambana na vishawishi vyenye vingefanya akose kutii na apoteze uaminifu wake. Na wakati Yesu alikuwa mutu muzima, alipaswa kubakia muaminifu wakati Shetani Ibilisi alimujaribu, na hata wakati alimushawishi moja kwa moja avunje ushikamanifu wake kwa Mungu. (Mt. 4:1-11) Shetani aliazimia kabisa kumuchochea Yesu afanye zambi juu asiweze kulipa bei ya ukombozi.

8. Yesu alivumilia majaribu gani ingine?

8 Wakati wa utumishi wake ku dunia, Yesu alivumilia majaribu ingine. Maadui wake walimutesa na hata walitafuta kumuua. (Lu. 4:28, 29; 13:31) Alipaswa kupambana na uzaifu wa wafuasi wake. (Mk. 9:33, 34) Wakati alikuwa nasambishwa alitendewa mubaya na kuchekelewa. Kisha aliuawa mu njia yenye kuzaraulisha na yenye maumivu mingi sana. (Ebr. 12:1-3) Alipaswa kuvumilia yeye mwenyewe majaribu ya mwisho-mwisho ya mu maisha yake bila ulinzi wa Yehova. bMt. 27:46.

9. Tunachochewa kufanya nini wakati tunafikiria zabihu ya Yesu? (1 Petro 1:8)

9 Kwa kweli, Yesu alijizabihu sana juu ya kutoa bei ya ukombozi. Wakati tunafikiri sana juu ya namna Yesu alikuwa tayari kujitoa sana kwa ajili yetu, ile haifanye tumupende hata zaidi?—Soma 1 Petro 1:8.

10. Namna gani Yehova alijiima ili bei ya ukombozi itolewe?

10 Tuseme nini juu ya Yehova? Alikuwa tayari kujiima nini ili Yesu alipe bei ya ukombozi? Kati ya uhusiano wote wenye kuwa kati ya baba na mutoto, uhusiano kati ya Yehova na Yesu njo wa nguvu zaidi. (Mez. 8:30) Upime basi kuwazia namna Yehova alijisikia wakati aliona namna Yesu alikuwa navumilia majaribu mingi ku dunia. Bila shaka, Yehova aliumia sana kuona Mwana wake anatendewa mubaya, anakataliwa, na kujaribiwa.

11. Tumia mufano ili kuonyesha namna Yehova alijisikia wakati Yesu aliuawa.

11 Muzazi yeyote mwenye alishakafisha mutoto, anajua muzuri namna kifo ya mutoto inaumaka sana. Tuko na imani kabisa kama kutakuwa ufufuo. Lakini ile haitoshake maumivu yenye mutu anasikiaka wakati mupendwa wake anakufa. Ile mufano inatusaidia kuelewa namna Yehova alijisikia wakati aliona Mwana wake mupendwa anateseka na kufa ile siku ya mu mwezi wa Nisani, mwaka wa 33. cMt. 3:17.

12. Tunaweza kufanya nini mbele siku ya Ukumbusho ifike?

12 Kuanzia sasa mupaka siku ya Ukumbusho hauone kama ni muzuri mu funzo yako ya kipekee ao mu Ibada ya Familia, mujiwekee muradi wa kujifunza sana juu ya bei ya ukombozi? Tumia kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova (kama inapatikana mu luga yenu) ao vichapo vingine vya kusaidia kujifunza Biblia ili ujifunze kwa undani juu ya ile fundisho. d Pia ujikaze kufuata programu ya usomaji wa Biblia kwa Ajili ya Ukumbusho yenye inatolewa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo. Siku ya Ukumbusho, usisahau kuangalia programu ya Ibada ya Asubui. Kama tunatayarisha moyo wetu kwa ajili ya Ukumbusho, tutaweza kusaidia wengine ili wao pia wafaidike.—Ezr. 7:10.

NAMNA TUNAWEZA KUSAIDIA WENGINE ILI WAFAIDIKE

13. Ni jambo gani ya kwanza yenye tunaweza kufanya ili kusaidia wengine wafaidike na Ukumbusho?

13 Namna gani tunaweza kusaidia wengine ili wafaidike pia na Ukumbusho? Kwa kweli, jambo ya kwanza ya kufanya ni kuwaalika. Zaidi ya kualika watu wenye tunakutana nao mu mahubiri, tunaweza kufanya liste ya watu wengine wenye tutaalika. Mu ile liste munaweza kuwa watu wa familia yetu, wafanyakazi wenzetu, wanafunzi wenzetu, na watu wengine. Hata kama hatuna mialiko mingi yenye kuchapishwa, tunaweza kuwatumia mualiko wa kielektroniki. Siye tufanye tu sehemu yetu, hatuwezi kujua ni watu ngapi watakubali na kuja ku Ukumbusho!—Muh. 11:6.

14. Leta mufano wenye kuonyesha matokeo ya muzuri ya kualika mutu mwenye tunajua.

14 Usisahau kama kupatia mualiko mutu mwenye unajua, kunaweza kuwa na matokeo ya muzuri. Siku moya dada mwenye bwana yake haiko Shahidi, alishangaa wakati bwana yake alimuambia kama iko napanga kuhuzuria Ukumbusho pamoja naye. Juu ya nini alishangaa? Juu kwa miaka mingi alikuwa amealika bwana yake mara mingi, lakini hakuna siku alikubali kuhuzuria. Sasa nini njo ilifanya akubali? Bwana yake alimuambia hivi: “Kuko mutu mwenye alinipatia mualiko.” Alimufasiria kama muzee fulani wa mu ile eneo mwenye alijuana naye njo alimualika. Ule bwana alihuzuria Ukumbusho ile mwaka na miaka ingine mingi yenye ilifuata.

15. Wakati tunaalika watu ku Ukumbusho tunapaswa kukumbuka nini?

15 Kumbuka kama wale wenye tunaalika wanaweza kuwa na maulizo, zaidi sana ikiwa ni mara yao ya kwanza kukusanyika pamoja na siye. Ni muzuri kufikiria mbele ya wakati maulizo yenye wanaweza kuuliza na kufikiria majibu. (Kol. 4:6) Kwa mufano, wamoja wanaweza kujiuliza: ‘Nini njo itafanyika ku ile tukio?’ ‘Itakamata muda gani?’ ‘Inaomba kuvaa namna gani?’ ‘Inaomba kulipa mbele ya kuingia?’ ‘Wataomba sadaka?’ Wakati tunaalika mutu ku Ukumbusho tunaweza tu kumuuliza hivi: “Uko na maulizo fulani?” na kisha tunaweza kujibia maulizo yoyote yenye anaweza kuwa nayo. Tunaweza pia kutumia video Tukumbuke Kifo cha Yesu na video Kwa Kawaida Tunafanya Nini Kwenye Jumba la Ufalme? ili kusaidia mutu aelewe namna mikutano yetu inafanywa. Na mu somo ya 28 ya kitabu Furahia Maisha Milele! muko mambo mbalimbali yenye tunaweza kuzungumuzia na mutu.

16. Wale wenye kuhuzuria Ukumbusho wanaweza kuwa na maulizo gani ingine?

16 Kisha kuhuzuria Ukumbusho, wapya wenye kupendezwa wanaweza kuwa na maulizo ingine. Wanaweza kujiuliza juu ya nini watu kidogo tu njo walikula mukate na kunywa divai, ao juu ya nini hakuna mutu mwenye alikula ao kunywa. Wanaweza pia kuuliza Ukumbusho unafanywa mara ngapi. Na wanaweza pia kupenda kujua ikiwa mikutano yote ya Mashahidi wa Yehova inakuwaka tu vile. Hata kama karibu ile maulizo yote inajibiwa mu hotuba ya Ukumbusho, wapya wanaweza kuwa na lazima ya mafasirio zaidi. Habari “Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Wanafanyaka Meza ya Bwana Tofauti na Dini Zingine?” yenye kuwa ku jw.org, inaweza kutusaidia kujibia maulizo fulani yenye wako nayo. Tunapenda kufanya yetu yote mbele ya Ukumbusho, wakati wa Ukumbusho, na kisha Ukumbusho ili kusaidia wale wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa” wafaidike na ile tukio.—Mdo. 13:48.

SAIDIA WALE WENYE HAWATENDE TENA

17. Namna gani wazee wanaweza kusaidia wale wenye hawatende tena? (Ezekieli 34:12, 16)

17 Mu kipindi ya Ukumbusho, namna gani wazee wanaweza kusaidia wale wenye hawatende tena? Muwahangaikie kwa upendo. (Soma Ezekieli 34:12, 16.) Mbele ya Ukumbusho, muhakikishe kama munazungumuza na wengi wao kadiri inawezekana. Muwahakikishie kama munawapenda, na kama munapenda kufanya yenu yote ili kuwasaidia. Muwaalike wahuzurie Ukumbusho. Kama wanahuzuria, muwakaribishe kwa furaha. Kisha Ukumbusho, muendelee kupashana habari na wale ndugu na dada zetu wapendwa, na kuwatolea musaada wowote wa kiroho wenye wako nao lazima ili wamurudilie Yehova.—1 Pe. 2:25.

18. Namna gani kila mumoja wetu anaweza kusaidia wale wenye hawatende tena? (Waroma 12:10)

18 Watu wote mu kutaniko wanaweza kusaidia wale wenye hawatende tena wenye wanahuzuria Ukumbusho. Namna gani? Kwa kuwatendea kwa upendo, kwa wema, na kwa heshima. (Soma Waroma 12:10.) Kumbuka kama pengine wale kondoo wapendwa walikuwa na wasiwasi kuhusu kukusanyika tena. Pengine waliogopa kama hawatakaribishwa muzuri. e Kwa hiyo, epuka kuwafanya wajisikie mubaya kwa kuwauliza maulizo yenye inaweza kuwafanya wasikie haya ao kwa kusema mambo yenye inaweza kuwaumiza. (1 Te. 5:11) Wale ndugu na dada ni waamini wenzetu. Tunafurahi kumuabudu tena Yehova pamoja nao!—Zb. 119:176; Mdo. 20:35.

19. Kukumbuka kifo ya Yesu kuko na faida gani?

19 Bila shaka, Yesu alikuwa na sababu za muzuri za kutuamuru tukumbuke kifo yake kila mwaka. Wakati tunafanya vile, siye wenyewe tunapata faida mu njia za mingi, na tunasaidia pia wengine wapate zile faida. (Isa. 48:17, 18) Upendo wetu kwa Yehova na Yesu unaongezeka. Tunaonyesha kama tuko wenye shukrani sana juu ya mambo yenye wametufanyia. Upendo wetu kwa ajili ya waamini wenzetu unakuwa nguvu zaidi. Na tunasaidia wengine wajifunze namna wao pia wanaweza kupata baraka zenye bei ya ukombozi inaleta. Tufanye basi yetu yote ili tukuwe tayari kwa ajili ya Ukumbusho wa hii mwaka, siku ya maana zaidi mu mwaka!

NAMNA GANI TUNAWEZA . . .

  • kutayarisha moyo wetu kwa ajili ya Ukumbusho?

  • kusaidia wengine wafaidike na Ukumbusho?

  • kusaidia wale wenye hawatende tena?

WIMBO 18 Tuko na Shukrani juu ya Bei ya Ukombozi

a Tumia sehemu tafuta yenye kuwa ku jw.org ili kupata habari na video zenye kuwa mu hii habari.

b Ona habari “Maulizo ya Wasomaji Wetu” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 4, 2021.

e Ona picha na kisanduku “ Kutaniko Ilitenda Namna gani?” Ndugu mwenye hatende tena anasita kuingia mu Jumba ya Ufalme, lakini anajikaza tu. Anakaribishwa kwa furaha na anafurahia kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada.

f MAFASIRIO YA PICHA: Wakati Mashahidi wa Yehova wa mu sehemu fulani ya dunia wako nafanya Ukumbusho, Mashahidi wa Yehova wa mu sehemu ingine ya dunia wako najitayarisha kwa ajili ya ile tukio ya pekee.