Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unatendea Wanamuke Vile Yehova Anawatendea?

Unatendea Wanamuke Vile Yehova Anawatendea?

TUKO na pendeleo ya kutumika pamoja na wanamuke wengi waaminifu. Tunapenda kila mumoja wa wale dada zetu washikamanifu na wenye bidii, na tunawaona kuwa wa maana! a Kwa hiyo ndugu, mujikaze kuwatendea kwa upole, kwa haki, na kwa heshima. Lakini juu hatukamilike, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kufanya vile. Ndugu fulani wako na tatizo ingine yenye inafanya ikuwe nguvu kwao kufanya vile.

Wamoja walikomalia mu desturi yenye wanaume wengi wanaona wanamuke kuwa wa hali ya chini. Kwa mufano, Hans, mwangalizi wa muzunguko katika Bolivia anasema hivi: “Wanaume fulani walikomalia mu desturi yenye wanaume wanaonwa kuwa wa maana zaidi. Na ile inafanya wazo ya kwamba wanaume ni wa hali ya juu zaidi kuliko wanamuke iote kabisa mizizi ndani yao.” Shengxian, muzee katika Taiwan, anasema hivi: “Kwenye ninaishi wanaume wengi wanaona kama wanamuke hawapaswe kujiingiza mu mambo yao. Ikiwa mwanaume anazungumuzia mawazo ya mwanamuke, wenzake wanaweza kumuzarau.” Wanaume wengine wanabagua wanamuke mu njia ya chini-chini. Kwa mufano, wanatumia mizaha yenye kushushia wanamuke heshima.

Jambo ya kufurahisha ni kama hakuna mwanaume mwenye analazimika kuwa mutumwa wa desturi ya kwenye alikomalia. Anaweza kujikaza kuachana na mawazo ya kwamba wanaume ni wa maana kuliko wanamuke. (Efe. 4:22-24) Anaweza kufanya vile kwa kuiga mufano wa Yehova. Mu hii habari tutaona namna Yehova anatendea wanamuke, namna ndugu wanaweza kujifunza kutendea wanamuke namna Yehova anawatendea, na namna wazee wanaweza kuweka mufano kuhusu kuonyesha dada heshima.

YEHOVA ANATENDEA WANAMUKE NAMNA GANI?

Yehova ni mufano mukamilifu kuhusu namna ya kutendea wanamuke. Juu ni Baba mwenye huruma anapenda familia yote ya wanadamu. (Yoh. 3:16) Na anaona dada waaminifu kuwa watoto wake wanamuke wapendwa. Ona ni mu njia gani mbambali Yehova anaonyesha kama anapenda na anaheshimu wanamuke.

Anawatendea bila ubaguzi. Yehova aliumba wanaume na wanamuke kwa mufano wake. (Mwa. 1:27) Hakufanya wanaume wakuwe wenye akili ao wenye uwezo zaidi kuliko wanamuke; na hapendelee zaidi wanaume kupita wanamuke. (2 Ny. 19:7) Aliumba wanaume na wanamuke na uwezo uleule wa kuelewa kweli za Biblia na kuonyesha sifa zake. Pia, Yehova anasamini mu njia ileile imani ya wanaume na ya wanamuke, ikuwe wako na tumaini ya kuishi milele mu dunia paradiso ao ya kuwa wafalme na makuhani mbinguni. (2 Pe. 1:1, na maelezo ya chini) Ni wazi kama Yehova habague wanamuke.

Anawasikiliza. Yehova anahangaikia mawazo ya wanamuke na namna wanajisikia. Kwa mufano, alisikiliza na kutenda wakati Raheli na Hana walisali kwake. (Mwa. 30:22; 1 Sa. 1:10, 11, 19, 20) Kupitia roho yake, Yehova aliongoza pia waandikaji wa Biblia waandike habari kuhusu wanaume wenye walisikiliza wanamuke. Kwa mufano, Abrahamu alifuata muongozo wa Yehova wa kusikiliza bibi yake Sara. (Mwa. 21:12-14) Mufalme Daudi alimusikiliza Abigaili. Na hata aliona kama ni Yehova njo alimutuma ili azungumuze naye. (1 Sa. 25:32-35) Yesu, mwenye anaiga kwa ukamili sifa za Baba yake, alisikiliza mama yake Maria. (Yoh. 2:3-10) Ile mifano inaonyesha kama kusikiliza wanamuke ni njia moya kati ya njia zenye Yehova anatumia ili kuwaonyesha heshima.

Anawatumainia. Kwa mufano, Yehova alimutumainia Eva, njo maana alimupatia kazi ya kusaidia kutunza dunia yote. (Mwa. 1:28) Kwa kufanya vile, Yehova alionyesha kama hakumuona Eva kuwa wa hali ya chini kuliko bwana yake Adamu, lakini kuwa kikamilisho chake. Yehova alitumainia pia manabii Debora na Ulda, njo maana aliwapatia kazi ya kushauria watu wake kutia ndani mufalme na muamuzi. (Amu. 4:4-9; 2 Fa. 22:14-20) Leo, Yehova anatumainia dada Wakristo kwa kuwapatia mugao wa kufanya kazi yake. Wale dada waaminifu ni wahubiri, mapainia, na wamisionere. Wanasaidia kufanya plan, kujenga, na kutunza Majumba ya Ufalme na biro za tawi. Wamoja kati yao wanatumika ku Beteli; wengine ku biro za kutafsiri. Wale dada wako kama jeshi kubwa yenye Yehova anatumia ili kutimiza mapenzi yake. (Zb. 68:11) Ni wazi kama Yehova haone wanamuke kuwa watu zaifu ao wenye hawana uwezo.

NDUGU WANAWEZA KUJIFUNZA NAMNA GANI KUTENDEA WANAMUKE SAWA VILE YEHOVA ANAWATENDEA?

Ndugu, ili kujua ikiwa tunatendea dada Wakristo sawa vile Yehova anawatendea, tunapaswa kuchunguza kabisa mawazo yetu na matendo yetu. Ili kufanya vile tuko na lazima ya musaada. Sawa vile tu skanere inaweza kusaidia kujua magonjwa yenye kuwa mu moyo wa mutu, rafiki muzuri na Neno ya Mungu vinaweza kutusaidia tutambue mawazo yoyote yenye haifae yenye tuko nayo juu ya wanamuke, yenye pengine ilishaota mizizi ndani yetu. Tunaweza kufanya nini ili kupata ule musaada?

Uliza rafiki muzuri. (Mez. 18:17) Ni muzuri tutafute musaada wa rafiki mwenye tunatumainia, mwenye anatendeanaka muzuri, na mwenye kuwa na usawaziko. Na tumuulize maulizo sawa vile, “Unawaza ninatendeaka dada namna gani? Wanaweza kusema kama ninawaheshimiaka? Ninaweza kufanya maendeleo zaidi mu namna yangu ya kuwatendea?” Kama rafiki yako anakuambia mambo fulani yenye unaweza kufanyia maendeleo, uepuke kujitetea lakini ukuwe tayari kufanya mabadiliko yote yenye inaombwa.

Ujifunze Neno ya Mungu. Njia ya muzuri zaidi ya kujua ikiwa tunatendeaka dada zetu muzuri ni kutumia Neno ya Mungu ili kuchunguza muelekeo na matendo yetu. (Ebr. 4:12) Wakati tunajifunza Biblia, tunasoma kuhusu habari za wanaume wenye walitendea muzuri wanamuke na wengine wenye hawakufanya vile. Kisha tunaweza kulinganisha matendo yao na matendo yetu. Zaidi ya ile, kulinganisha maandiko ya Biblia kutatuzuia ili, bila kujua tusitumie mubaya maandiko juu ya kuunga mukono wazo fulani yenye haifae kuhusu wanamuke. Kwa mufano, kulingana na 1 Petro 3:7, wanamuke wanapaswa kupewa “heshima kama chombo kizaifu zaidi.” b Je, ile inamaanisha kama mwanamuke ni wa hali ya chini, iko na akili kidogo, na iko na uwezo kidogo kwa kulinganishwa na mwanaume? Hapana! Linganisha maneno ya Petro na maneno yenye kuwa mu Wagalatia 3:26-29. Ile andiko inaonyesha kama sawa tu vile Yehova alichagua wanaume, amechagua pia wanamuke ili watawale pamoya na Yesu mbinguni. Wakati tunajifunza Neno ya Mungu na kuuliza rafiki muzuri mawazo yake juu ya namna tunatendea wanamuke tunaweza kujifunza kuonyesha dada zetu heshima yenye wanastahili.

NAMNA GANI WAZEE WANAWEZA KUONYESHA DADA HESHIMA?

Ndugu mu kutaniko wanaweza kujifunza pia kutendea dada kwa heshima kwa kufuata mufano wa wazee wenye upendo. Namna gani wazee wanaonyesha mufano kuhusu kutendea dada kwa heshima? Tuone njia fulani.

Wanapongeza dada. Mutume Paulo aliachia wazee mufano muzuri wa kuiga. Alipongeza mbele ya watu wote dada mbalimbali mu barua yenye aliandikia kutaniko ya Roma. (Ro. 16:12) Wazia furaha yenye wale dada walipaswa kuwa nayo wakati barua ya Paulo ilikuwa inasomwa mbele ya kutaniko. Vilevile, wazee wanakuwaka tayari kupongeza dada kwa sababu ya sifa zao za muzuri na kwa sababu ya kazi yenye wanafanya kwa ajili ya Yehova. Ile inafanya dada waone kama wanaheshimiwa sana na wanapendwa sana. Pengine ni maneno yenye kutia moyo ya muzee njo yenye dada wako nayo lazima ili waendelee kumutumikia Yehova kwa uaminifu.—Mez. 15:23.

Pongeza

Wakati wanapongeza dada, wazee wanajikaza kusema maneno yenye kutoka mu moyo na wanataya juu ya nini wanawapongeza. Juu ya nini wazee wanafanya vile? Dada fulani mwenye kuitwa Jessica anasema hivi: “Inafurahishaka wakati ndugu wanaambia dada ‘aksanti kwa kazi.’ Lakini tanafurahiaka zaidi wakati ndugu wanataya juu ya nini wanatupongeza, kwa mufano kwa sababu tunasaidia watoto wetu wakae ku mikutano bila kufanya fujo, ao kwa sababu tunajitoa ili kuenda kukamata mwanafunzi wa Biblia na kuya naye ku mikutano.” Wakati wazee wanapongeza dada kwa sababu ya jambo fulani yenye wamefanya, ile inawafanya wajisikie kuwa wa maana mu kutaniko.

Wanasikiliza dada. Wazee wanyenyekevu wanajua kama haiko wao tu njo wanakuwaka na mawazo ya muzuri. Wale wazee wanaombaka dada mapendekezo, na wanasikiliza kwa uangalifu wakati dada wako nazungumuza. Kwa kufanya vile wazee wanatia dada moyo na wao pia wanapata faida. Juu ya nini? Muzee mwenye kuitwa Gerardo, mwenye kutumikia ku Beteli, anasema hivi: “Nimeona kama kuuliza dada mawazo yao kunanisaidia kufanya kazi yangu muzuri. Mara mingi ni wao njo wametumika kazi kwa muda murefu zaidi kuliko ndugu wengi.” Mu kutaniko dada wengi ni mapainia, kwa hiyo wanajua muzuri namna watu wa mu eneo ya kutaniko wanakuwaka. Muzee mumoja mwenye kuitwa Bryan anasema hivi: “Kuko mambo mingi yenye dada zetu wanaweza kutolea tengenezo. Kwa hiyo tufaidike na uzoefu wao!”

Sikiliza

Wazee wenye hekima hawakuwake haraka kukatala mapendekezo ya dada zetu. Juu ya nini? Muzee mwenye kuitwa Edward Anasema hivi: “Mawazo ya dada na uzoefu wao unaweza kusaidia ndugu aelewe muzuri zaidi mambo, na ajitie pa nafasi ya wengine.” (Mez. 1:5) Hata kama muzee hatatumia mapendekezo ya dada, anapaswa tu kumushukuru kwa maoni yake na kwa kuwa tayari kuchangia ujuzi na uelewaji wake.

Wanazoeza dada. Wazee wenye utambuzi wanatafuta nafasi za kuzoeza dada. Kwa mufano, wanaweza kufundisha dada namna ya kuongoza mukutano wa mahubiri ili wasaidie ikiwa hakuna ndugu mwenye kubatizwa. Wanaweza kuwazoeza kutumia vifaa na mashini mbalimbali ili waweze kusaidia mu kazi ya kutunza na kujenga majengo ya tengenezo. Ku Beteli, waangalizi wamezoeza dada kushugulikia migao mbalimbali sawa vile kutunza majengo, kununua vitu, kufanya hesabu, kutumia progamu za ordinatere na mambo ingine. Wakati wazee wanazoeza dada, wanaonyesha kama wanawaona kuwa wenye uwezo na wenye kutumainika.

Zoeza

Dada wengi wametumia mazoezi yenye wamepata kutoka kwa wazee ili kusaidia wengine. Kwa mufano dada wametumia mazoezi yenye wamepata mu ujenzi ili kusaidia wengine kujenga tena nyumba zao kisha musiba wa asili. Dada wengine wamezoezwa kuhubiri fasi kwenye kuwa watu wengi na wametumia ile ufundi ili kuzoeza dada wengine kufanya vile. Dada wanaona namna gani wazee wenye wanawazoeza? Dada mwenye kuitwa Jennifer anasema hivi: “Wakati nilitumika ku ujenzi wa Jumba fulani ya Ufalme, muzee fulani alichukua wakati wa kunizoeza. Aliona kazi yenye nilifanya na alinipongeza. Nilifurahia sana kutumika naye juu ile ilinisaidia nione kuwa wengine wananiona kuwa wa maana na wananitumainia.”

FAIDA YA KUTENDEA WANAMUKE SAWA WATU WA FAMILIA YETU

Tunapenda dada zetu sawa vile Yehova anawapenda! Kwa hiyo, tunawatendea sawa watu wa mu familia yetu. (1 Ti. 5:1, 2) Tunaona kuwa ni pendeleo na tunafurahi sana kutumika pamoya nao. Na tunafurahi sana wakati wanaona kuwa tunawapenda na kuwategemeza. Dada mwenye kuitwa Vanessa anasema hivi: “Namushukuru sana Yehova kwa sababu niko mu tengenezo yake yenye inajaa ndugu wenye wananitia moyo sana.” Dada mumoja wa Taiwan anasema hivi: “Namushukuru sana Yehova na tengenezo yake kwa sababu wanaona wanamuke kuwa wa maana na wanahangaikia namna wanajisikia. Ile inatia imani yangu nguvu na inanifanya nifurahie kabisa hata zaidi pendeleo yenye niko nayo ya kuwa mu tengenezo ya Yehova.”

Bila shaka, Yehova anafurahi sana wakati anaona wanaume Wakristo waaminifu wanajikaza kuona na kutendea wanamuke sawa vile yeye! (Mez. 27:11) Benjamin, muzee fulani wa Scotland, anasema hivi: “Mawazo ya ulimwengu juu ya wanamuke ni ya kuwashushia heshima. Kwa hiyo wakati wanakuja ku Jumba ya Ufalme tunapenda wajisikie mu njia tofauti.” Basi, siye wote tujikaze sana kumuiga Yehova kwa kutendea dada zetu wapendwa kwa upendo na kwa heshima yenye wanastahili.—Ro. 12:10.

a Mu hii habari, neno “dada” inatumiwa ili kuzungumuzia dada Wakristo hapana wenye mulizaliwa nao mu familia moya.

b Ili kupata mafasirio zaidi kuhusu maneno “chombo kizaifu zaidi,” ona habari yenye kichwa “Thamani ya ‘Chombo Dhaifu Zaidi’” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 5, 2006 na “Mwongozo Wenye Hekima kwa Wenzi wa Ndoa” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 3, 2005.