Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

Ĩta kĩrĩ birĩa birĩ ndeene

KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 5

RWĨMBO 27 Kufunuliwa kwa Wana wa Mungu

‘Ntĩkorokwĩrũkĩra’!

‘Ntĩkorokwĩrũkĩra’!

‘Mũrungu wengwa augĩte atĩrĩ, ntĩkorokwĩrũkĩra kana ngũtiga kinya-rĩ.’AHI. 13:5b.

JAMBO KUU

Kuwahakikishia watumishi wa Mungu duniani kwamba hawataachwa bila mwongozo wakati Wakristo watiwa-mafuta wote waliobaki watakapochukuliwa kwenda mbinguni.

1. Nĩrĩ etũrĩrua maguta bonthe bakethĩrwa ĩgũrũ?

 MIAKA mingi iliyopita, watu wa Yehova walijiuliza, ‘Wakristo watiwa-mafuta wa mwisho watachukuliwa lini kwenda mbinguni?’ Awali tulifikiri kuna uwezekano kwamba baadhi ya watiwa-mafuta wangebaki katika dunia Paradiso kwa muda fulani baada ya vita vya Har–​Magedoni. Lakini katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 15, 2013, tulijifunza kwamba watiwa-mafuta wote ambao bado wapo duniani watachukuliwa kwenda mbinguni kabla ya vita vya Har–​Magedoni.—Mt. 24:31.

2. Nĩ biũria birĩkũ biũmba gũciumĩria, na nĩmbi tũkaarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?

2 Hata hivyo, huenda swali hili likazuka: Ni nini kitakachowapata “kondoo wengine” wa Kristo ambao watakuwa wakimtumikia Yehova kwa uaminifu duniani wakati wa “dhiki kuu”? (Yoh. 10:16; Mt. 24:21) Huenda baadhi ya watu leo wakawa na wasiwasi kwamba watahisi wameachwa au watakosa mwongozo wakati ndugu na dada wapendwa watiwa-mafuta watakapochukuliwa kwenda mbinguni. Acheni tuchunguze masimulizi mawili katika Maandiko ambayo huenda yanaweza kuwafanya wahisi hivyo. Kisha tutazungumzia sababu zinazoonyesha kwa nini hatupaswi kuwa na wasiwasi.

NĨMBI BITĨKARĨKA?

3-4. Nĩatĩa antũ bamwe boomba gũciũria, na nĩkĩ?

3 Huenda watu wengine wakajiuliza ikiwa kondoo wengine wataiacha kweli wakati ndugu watiwa-mafuta wa Baraza Linaloongoza hawatakuwepo ili kuwaongoza. Labda wanahisi hivyo kwa sababu ya masimulizi fulani katika Maandiko. Acheni tuchunguze mifano miwili. Mfano wa kwanza ni kuhusu Kuhani Mkuu Yehoyada. Alikuwa mtumishi mwaminifu wa Mungu. Yeye na Yehoshabeathi, mke wake, walimlinda mvulana aliyeitwa Yehoashi na kumsaidia kuwa mfalme mwaminifu na mzuri. Kwa kipindi ambacho Yehoyada, ambaye alikuwa amezeeka alikuwa hai, Yehoashi alimtumikia Yehova na kutenda mema. Lakini muda mfupi baada ya kifo cha Yehoyada, Yehoashi alianza kufanya yaliyo mabaya. Aliwasikiliza wakuu waovu wa Yuda na kumwacha Yehova.—2 Nya. 24:​2, 15-19.

4 Mfano mwingine ni wa Wakristo wa karne ya pili. Mtume Yohana, ambaye alikuwa mtume wa mwisho aliyebaki, aliwachochea kwa njia nzuri Wakristo wengi, na kuwasaidia kuvumilia katika utumishi wa Yehova. (3 Yoh. 4) Kama mitume wengine waaminifu wa Yesu, Yohana alikuwa akijitahidi kwa muda mrefu kulilinda kutaniko dhidi ya uasi-imani uliokuwa ukienea. (1 Yoh. 2:18; 2 The. 2:7) Hata hivyo, baada ya Yohana kufa, uasi-imani ulienea haraka kama moto. Baada ya miaka kadhaa, kutaniko la Kikristo lilichafuliwa kabisa.

5. Nĩ mantũ jarĩkũ tũtĩbuĩrĩte gũciĩra jagakarĩka kuumania na tũrũgono tũu twĩrĩ?

5 Je, masimulizi hayo mawili katika Maandiko yanaonyesha kwamba jambo kama hilo litawapata kondoo wengine wa Kristo wakati watiwa-mafuta watakapochukuliwa kwenda mbinguni? Je, wakati huo Wakristo waaminifu duniani wataacha kufuata mambo waliyofundishwa, kama Yehoashi alivyofanya, au kuwa waasi-imani, kama Wakristo wengi katika karne ya pili W.K.? Bila shaka la! Tunaweza kuwa na uhakika kwamba watiwa-mafuta watakapoondoka duniani, kondoo wengine watatunzwa vizuri na kusitawi kiroho. Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika huo?

ŨTHATHAYIA BWA MMA BŨTĨTHŨŨKUA

6. Nĩ magiita jarĩkũ jathatũ tũkaarĩĩria na njĩra ĩnkuĩ?

6 Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba ibada safi haitachafuliwa, hata wakati wa kipindi kigumu kinachokuja? Tunaweza kuwa na uhakika huo kwa sababu ya mambo ambayo tumejifunza katika Biblia kuhusu nyakati tunazoishi. Kipindi hiki cha wakati kinatofautiana sana na nyakati za Israeli la kale na nyakati za Wakristo wa karne ya pili. Basi acheni tuchunguze kwa ukaribu zaidi nyakati hizi tatu: (1) Nyakati za Israeli la kale, (2) kipindi baada ya mitume kufa, na (3) nyakati zetu, “nyakati za kurudishwa kwa mambo yote.”—Mdo. 3:21.

7. Karaaja naarĩa Isiraeli, nĩkĩ antũ etĩkua bataunĩkĩre nkoro, rĩrĩa mũgongo jũu na anene baaju baathuurĩre kũthingata njĩra ĩnthũũku?

7 Nyakati za Israeli la kale. Muda mfupi kabla ya kifo chake, Musa aliwaambia hivi Waisraeli: “Najua vizuri kwamba baada ya kifo changu hakika mtatenda maovu na kuacha njia ambayo nimewaamuru ninyi.” (Kum. 31:29) Pia, Musa alilionya taifa la Israeli kwamba ikiwa wataasi, wangepelekwa uhamishoni. (Kum. 28:​35, 36) Je, maneno hayo yalitimia? Ndiyo. Kwa karne nyingi, wafalme wengi waliasi na kuwaongoza watu wa Mungu katika ibada ya uwongo. Kwa sababu hiyo, Yehova aliwaadhibu Waisraeli waovu na hakuruhusu wafalme Waisraeli waendelee kuwatawala. (Eze. 21:​25-27) Lakini Waisraeli waaminifu walitiwa moyo walipoona maneno ya Mungu yakitimia.—Isa. 55:​10, 11.

8. Rĩ, nĩtubuĩrĩte kũrigara twona atĩ Akristũ ba kĩũthũrano gĩa karine ya ijĩrĩ nĩbaatigĩre ũthathayia bwa mma? Tarĩĩria.

8 Kipindi baada ya mitume kufa. Je, tunapaswa kushangaa kwamba kutaniko la Kikristo la karne ya pili lilichafuliwa? Hapana. Yesu alitabiri kwamba uasi-imani mkubwa ungetukia. (Mt. 7:​21-23; 13:​24-30, 36-43) Mtume Paulo, Petro, na Yohana walikuwa wamethibitisha kwamba unabii wa Yesu tayari ulikuwa umeanza kutimizwa katika karne ya kwanza W.K. (2 The. 2:​3, 7; 2 Pet. 2:1; 1 Yoh. 2:18) Katika karne ya pili W.K., baada ya mtume wa mwisho kufa, kutaniko la Kikristo likachafuliwa. Wakristo waasi-imani wakawa sehemu ya Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwenguni pote ya dini za uwongo. Mambo ambayo Yesu alitabiri yalikuwa yakitimia.

9. Nĩatĩa magiita jaja tũgũtũũra jarĩ mwanya na ja Isiraeli ya karaaja, na ja Akristũ ba kĩũthũrano gĩa karine ya ijĩrĩ?

9 “Nyakati za kurudishwa kwa mambo yote.” Nyakati tunazoishi zinatofautiana na nyakati za Israeli la kale na kipindi cha uasi-imani mkubwa ulioanza wakati wa karne ya pili W.K. Kipindi cha wakati tunachoishi kinaitwaje? Kwa kawaida tunakirejelea kuwa “siku za mwisho” za mfumo huu mwovu wa mambo. (2 Tim. 3:1) Lakini Biblia inaonyesha kwamba kuna kipindi kingine cha wakati kilichoanza wakati uleule kipindi cha siku za mwisho kilipoanza. Kipindi hicho kitaendelea hadi Ufalme wa Kimasihi utakapowarudishia wanadamu ukamilifu na kuibadili dunia kuwa paradiso. Kipindi hicho kinaitwa “nyakati za kurudishwa kwa mambo yote.” (Mdo. 3:21) Kipindi hicho kilianza mwaka wa 1914. Ni nini kilichorudishwa wakati huo? Yesu aliwekwa rasmi kuwa Mfalme mbinguni. Hivyo, kwa mara nyingine tena, Yehova alikuwa na mtawala aliyemwakilisha, mrithi wa Mfalme Daudi. Hata hivyo, utawala huo si jambo pekee ambalo Yehova alirudisha. Muda mfupi baadaye, hatimaye ibada safi ilianza kurudishwa! (Isa. 2:​2-4; Eze. 11:​17-20) Je, itachafuliwa kwa mara nyingine tena?

10. (a) Nĩatĩa Bibiria ĩroretie bwegie ũthathayia bwa mma ntukũũne cietũ? (Isaya 54:17) (b) Nĩkĩ mororia ta jau jarĩ ja gwĩkĩra inya?

10 Soma Isaya 54:17. Fikiria kuhusu unabii huu: “Hakuna silaha yoyote itakayotokezwa dhidi yako itakayofanikiwa”! Maneno hayo yaliyoongozwa na roho yanatimia leo. Pia, maneno yafuatayo yenye kufariji yanahusu nyakati zetu: “Wana wako wote watafundishwa na Yehova, na amani ya wana wako itakuwa nyingi. Utaimarishwa kabisa katika uadilifu. . . . Hutaogopa chochote na hutakuwa na sababu yoyote ya kuhofu, kwa maana haitakukaribia.” (Isa. 54:​13, 14) Hata Shetani, “mungu wa mfumo huu wa mambo,” hana uwezo wa kuzuia kazi ya kutoa elimu inayofanywa na watu wa Yehova. (2 Kor. 4:4) Ibada safi imerudishwa, na haitachafuliwa tena kamwe. Itadumu kwa umilele wote. Hakuna silaha yoyote itakayotokezwa dhidi yetu itakayofanikiwa!

NĨATĨA GŨGAKARĨKA?

11. Nĩmbi bigũtũrikithĩria atĩ ntundu ĩrĩa nene ĩtĩtiganĩrua rĩrĩa etũrĩrua maguta bageeta ĩgũrũ?

11 Ni jambo gani litakalotukia watiwa-mafuta watakapochukuliwa kwenda mbinguni? Kumbuka kwamba Yesu ni Mchungaji wetu. Yeye ndiye kichwa cha kutaniko la Kikristo. Yesu alieleza hivi waziwazi: “Kiongozi wenu ni mmoja, Kristo.” (Mt. 23:10) Mfalme wetu anayetawala, hawezi kamwe kushindwa kufanya kazi yake. Kwa sababu Kristo anawaongoza wafuasi wake hapa duniani, hawatakuwa na lolote la kuogopa. Bila shaka, hatujui habari zote kuhusu jinsi Kristo atakavyowaongoza watu wake wakati huo. Hivyo, acheni tuchunguze baadhi ya mifano katika Biblia itakayotupatia uhakika.

12. Nĩatĩa Jehova aamenyereere antũ baawe (a) Musa arĩgũkua? (b) nyuma ya Elija kũthamĩrua gũntũ kũngĩ? (Tega kinya mbica.)

12 Musa alikufa kabla ya Waisraeli kuingia katika Nchi ya Ahadi. Ni nini kilichowapata watu wa Mungu? Je, walikosa mwongozo baada ya mwanamume huyo mwaminifu kufa? Hapana. Maadamu wangeendelea kuwa waaminifu, Yehova angewatunza. Kabla ya kifo cha Musa, Yehova alimwambia amkabidhi Yoshua mgawo wa kuwaongoza watu wake. Musa alikuwa akimzoeza Yoshua kwa miaka mingi. (Kut. 33:11; Kum. 34:9) Pia, kulikuwa na wanaume wengine wengi wenye uwezo waliokuwa wakiongoza, yaani, wakuu wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na hata wa makumi. (Kum. 1:15) Watu wa Mungu walitunzwa vizuri. Eliya ni mfano mwingine. Alikuwa akiongoza ibada safi katika Israeli kwa miaka mingi. Lakini wakati ulifika ambapo Yehova alimhamisha kwenda kwenye mgawo mwingine, upande wa kusini huko Yuda. (2 Fal. 2:1; 2 Nya. 21:12) Je, watu waaminifu katika ufalme wa kaskazini wa Israeli uliokuwa na makabila kumi walikuwa wameachwa? Hapana. Eliya alikuwa amemzoeza Elisha kwa miaka mingi. Pia, kulikuwa na ‘wana wa manabii’ ambao inaonekana walikuwa katika aina fulani za shule. (2 Fal. 2:​3, maelezo ya chini) Hivyo, kulikuwa na wanaume wengi waaminifu ambao wangesaidia katika kazi ya kuongoza watu wa Mungu. Naam, Yehova aliendelea kutimiza kusudi lake, na aliwatunza waabudu wake waaminifu.

Musa (picha ya kushoto) na Eliya (picha ya kulia) waliwazoeza watu wanaotegemeka ambao wangewakabidhi majukumu yao (Tazama fungu la 12)


13. Nĩ ũrikithia bũrĩkũ tũkwona kĩrĩ Ahibirania 13:5b? (Tega kinya mbica.)

13 Kwa kuzingatia mifano hiyo miwili, unafikiri ni nini kitakachotukia wakati watiwa-mafuta wa mwisho watakapochukuliwa kwenda mbinguni? Hatuhitaji kukisia. Biblia inafunua ukweli huu unaotutia moyo: Yehova hatawatupa kamwe watu wake walio duniani. (Soma Waebrania 13:5b.) Kama Musa na Eliya, kikundi kidogo cha Wakristo watiwa-mafuta kinachoongoza leo kinaelewa umuhimu wa kuwazoeza wengine. Kwa miaka mingi, akina ndugu katika Baraza Linaloongoza wamekuwa wakiwazoeza wanaume kutoka miongoni mwa kondoo wengine ili wawaongoze watu wa Mungu. Kwa mfano, wameandaa shule nyingi ili kuwazoeza wazee, waangalizi wanaosafiri, washiriki wa Halmashauri za Tawi, waangalizi walio Betheli, na wengine. Washiriki wa Baraza Linaloongoza wamekuwa wakiwazoeza kibinafsi wasaidizi katika halmashauri mbalimbali za Baraza Linaloongoza. Kwa sasa wasaidizi hao wanashughulikia majukumu mazito kwa uaminifu. Wako tayari kabisa kuendeleza kazi ya kuwatunza kondoo wa Kristo.

Baraza Linaloongoza linafanya kazi kwa bidii kuwazoeza wasaidizi wao na kupanga shule za kuwazoeza wazee wa makutaniko, waangalizi wanaosafiri, washiriki wa Halmashauri za Tawi, waangalizi walio Betheli, na wamishonari ulimwenguni pote (Tazama fungu la 13)


14. Nĩ ũntũ bũrĩkũ bũgũciumĩria kĩthoomone gĩkĩ?

14 Hili ndilo jambo kuu la mazungumzo yetu: Watiwa-mafuta wa mwisho watakapochukuliwa na kwenda mbinguni mwishoni mwa ile dhiki kuu, ibada safi itaendelea hapa duniani. Kwa sababu ya uongozi mzuri wa Yesu Kristo, waabudu wa Mungu hawatakosa chochote. Ni kweli kwamba wakati huo tutakuwa tukishambuliwa na Gogu wa Magogu, muungano wa mataifa yenye chuki. (Eze. 38:​18-20) Lakini shambulizi hilo fupi halitafaulu; halitawafanya watu wa Mungu waache kumwabudu Yehova. Bila shaka atawaokoa! Katika maono, mtume Yohana aliona “umati mkubwa” wa kondoo wengine wa Kristo. Yohana aliambiwa kwamba ‘umati huo mkubwa’ unatoka “katika ile dhiki kuu.” (Ufu. 7:​9, 14) Naam, tuna uhakika kwamba watakuwa salama!

15-16. Kũringana na Kugwurirwa 17:​14, nĩatĩa etũrĩrua maguta bakethĩrwa bakĩthithagia ĩgiita rĩa Armagedoni, na nĩkĩ bũu bũgũtwĩkĩra inya?

15 Hata hivyo, huenda bado wengine wakajiuliza: ‘Namna gani watiwa-mafuta? Watafanya nini baada ya kuondoka duniani?’ Biblia inajibu swali hilo moja kwa moja. Inafunua kwamba serikali za ulimwengu huu ‘zitapigana na Mwanakondoo.’ Ni wazi kwamba zitashindwa. Tunasoma hivi kwenye Biblia: “Mwanakondoo atawashinda.” Na ni nani watakaomsaidia? Biblia inatoa jibu; wale “walioitwa,” “waliochaguliwa,” na “waaminifu.” (Soma Ufunuo 17:14.) Ni nani hao? Watiwa-mafuta waliofufuliwa! Kwa hiyo, watiwa-mafuta wa mwisho watakapochukuliwa kwenda mbinguni mwishoni mwa dhiki kuu, mojawapo ya migawo yao ya kwanza ni kupigana. Huo ni mgawo wenye kusisimua sana! Baadhi ya Wakristo watiwa-mafuta walikuwa wapiganaji kabla ya kuwa Mashahidi wa Yehova. Baadhi yao hata walitumikia katika vikosi vya jeshi vya ulimwengu huu. Lakini baadaye wakawa Wakristo wa kweli na kujifunza njia ya amani. (Gal. 5:22; 2 The. 3:16) Waliacha kuunga mkono vita. Hata hivyo, baada ya kuchukuliwa kwenda mbinguni, watatumikia pamoja na Kristo na malaika wake watakatifu, katika vita vya mwisho dhidi ya maadui wa Mungu.

16 Fikiria jambo hili. Wakiwa duniani, baadhi ya Wakristo watiwa-mafuta wamezeeka, au hata ni dhaifu. Lakini watakapofufuliwa na kwenda mbinguni, watakuwa viumbe wa roho wenye nguvu na wasioweza kufa, ambao wamepewa mgawo wa kupigana pamoja na Mfalme-Shujaa, Yesu Kristo. Baada ya vita vya Har–​Magedoni kupiganwa, watashiriki katika kuwaongoza wanadamu kwenye ukamilifu. Bila shaka, wakati huo wakiwa mbinguni wataweza kuwasaidia hata zaidi ndugu na dada zao wapendwa walio duniani, kuliko walivyofanya walipokuwa wanadamu wasio wakamilifu!

17. Nĩatĩa tũkũmenya atĩ athathayia bonthe ba Jehova bakethĩrwa batĩ ũgwatine ĩgiita rĩa Armagedoni?

17 Je, wewe ni mmoja wa kondoo wengine? Ikiwa ndivyo, utahitaji kufanya nini vita muhimu vya Har–​Magedoni vitakapoanza? Jambo hili rahisi: Mtumaini Yehova, na ufuate mwongozo wake. Huenda hilo likatia ndani nini? Biblia inatoa faraja hii: “Ingieni katika vyumba vyenu vya ndani, na mfunge milango nyuma yenu. Jificheni kwa muda mfupi mpaka ghadhabu itakapopita.” (Isa. 26:20) Watumishi wote waaminifu wa Mungu, mbinguni na duniani, watakuwa salama wakati huo. Kama mtume Paulo, tunasadiki kwamba hakuna “serikali wala mambo yaliyopo sasa wala mambo yatakayokuja . . . [yatakayoweza] kututenga na upendo wa Mungu.” (Rom. 8:​38, 39) Sikuzote kumbuka jambo hili: Yehova anakupenda, na hatakutupa kamwe!

RĨRĨA AKRISTŨ ETŨRĨRUA MAGUTA BA MŨTHIA BAKAJŨKUA BAITIE ĨGŨRŨ,

  • nĩatĩa gũgakarĩka?

  • nĩkĩ tũtĩ na nkanja atĩ ũthathayia bwa mma bũtĩthũũkua?

  • nĩkĩ tũrĩ na mma atĩ Jehova akamenyeera antũ baawe?

RWĨMBO 8 Yehova Ni Kimbilio Letu